Muujiza wa Kwanza alioufanya Yesu ni kubadili maji kuwa divai. Kwanini Makanisa mengi yanahubiri kuwa pombe ni dhambi?

Ili USIWE mlevi unatakiwa unywe bia kuanzia ngapi?
Au alcohol ngapi imewekwa Kama kipimo yaani ukifika hyo alcohol inakuwa umekuwa mlevi.
Si nimekuandikia hapo juu au unasoma juu juu.

Usinywe pombe kuzidi UWEZO WAKO WA MWILI.

Kunywa ILIYORUHUSIWA NA SERIKALI.

Kunywa MUDA WA MAPUMZIKO baada ya kazi zako

Usinyweee BAJETI YA MAMBO MENGINE KAMA ada, matibabu, ujenzi, Akiba yako, chakula cha nyumbani nk.
 
Hawa jamaa wajanja wajanja Sana.[emoji16][emoji16].
Yaani haiingii akilini kweli nabii wa Mungu.
Au Mungu au mtoto wa Mungu Kama wao wanavyomuita
AKATENGENEZA POMBE
Hapo watakwambia hilo ni agano la kale na ni sheria kipindi cha Musa, ila alipokuja Yesu alitengua kwa yeye mwenyewe kiyageuza maji kua divai katika sherehe kisha waumini wakapombeka.
 
Mimi muislam naamini mitume na manabii wa Mungu hawawezi kuwa walevi.
Ila Kama wakristo mnaamini yesu alikuwa mlevi.
MIMI SIMOOOOOOOOOOOO
Nuhu alilewa mvinyo akakaa uchi watoto wake wakamsitiri isipokuwa mdogo alimcheka
 
Ndo nimekuuliza ili ujue umekunywa pombe ndani ya uwezo wako.
Unatakiwa unywe bia kuanzia ngapi?
au Kuna maandiko yanafundisha jinsi ya kunywa pombe ?
Kwamba unatakiwa unywe kiasi kadhaa ndio kipo ndani ya uwezo wako
 
Hayo maji yenu mmetengeneza wenyewe mmeweka matakataka ya chemical zinazo haribu akili yenu
Sio ile divai aliyo ibariki Yesu
 
Yesu alikuwa anashtua glass ngapi?[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ndio ila hakuwa Mlevi.
Na alikuwa anakula chakula ila hakuwa Mlafi

Ndio maana ya hilo Andiko

Iko tofauti kati ya Kula chakula, na kuwa Mlafi.
Na Kunywa Pombe, na kuwa Mlevi.
 
Hata biblia inasema
" kuleni majani ya mkunde maana yana baraka ndani yake"
Katika utafiti wetu wa kutafuta majani ya mkunde tukagundua majani ya mkunde ni mirungi
 
Hawa jamaa wajanja wajanja Sana.[emoji16][emoji16].
Yaani haiingii akilini kweli nabii wa Mungu.
Au Mungu au mtoto wa Mungu Kama wao wanavyomuita
AKATENGENEZA POMBE
Kwani Pombe iliumbwa na nani?

Nyie Mbinguni si mmetengenezewa Mito ya Pombe kabisa.
Mito kama Nile na Rufiji ya Pombe.
Katengeneza nani hiyo?
 
Na vipi Mambo ya Paulo?Aya ya 10
MWANZO:9/20

Nuhu akaanza kuwa mukulima, akapanda mzabibu: AKANYWA DIVAI AKALEWA;

HAYO NI MAMBO YA WALAWI!

NA SISI WACHAGA TUNA MAMBO YETU!!!
 
Ushasema mbinguni.
Lakini duniani tumekatazwa.
Kutokana na maandiko yetu.
Ila kwenye BIBLIA pia pombe imekatazwa.
Aya ya 10.
Kwanini unabishana na maandiko?
Kwani Pombe iliumbwa na nani?

Nyie Mbinguni si mmetengenezewa Mito ya Pombe kabisa.
Mito kama Nile na Rufiji ya Pombe.
Katengeneza nani hiyo?
 
Ila alikumbuka kuwatengenezea POMBE.[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787].
Yesu alishuka duniani kwa lengo moja tu.

Kuwatangazia walimwengu Habari Njema ya Ufalme wa Mbingu.

Alipo maliza alipaa Mbinguni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…