Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!


Ndio hivyo mkuu watanzania tulitaka spika CCM wakatuletea "Mwanamke" na bado wanataka kuuendeleza huu Upuuzi.
 
Sasa si ndio tunataka kuwasaidia mtoke vizuri; najua tukianza kudai serikali moja Zanzibar hawatokubali.. tukidai serikali tatu bado tutakuwa tunajaribu kuwaappease Zanzibar...


Wewe endelea na madharau yako! Kwani mnajali nini tunachosema? Hatuhitaji msaada wenu kwani hamjui mnataka nini wala msilolitaka.
 
USIPITE BILA KUSOMA!
Hautojuta, (ni mtzamo wangu, ila
nimeuchambua kwa kias chake)
Sikia ww, hakuna mwananch wa kawaida
wa
tanganyka anayewang'ang'ania znz, kwa
7bu hakuna cha ajab znz,
wanaong'ang'ania
ni viongoz, wote wa znz na bara ndo maana
wao hawabshan kama cc.
Mi sion faida ya muungano. Tena nazd
kuwa
na ujasir huo kwa kitendo cha kupunguzwa
kwa mambo ya muungano, inaonesha
hakuna cha msing kinachopatkana na hz
pand 2, kitakachokosekana bila muungano,
ila wanashkilia na hzo nyuz 7 ila ucvunjke.
Kuna faida gan ya muungano (inayotosha
kufumbia macho matakwa ya weng?) Kama
ni biashara, znz na tanganyka ztakuwa ktk
soko huru la afrka mashark xo hakuna
tofaut.
Kamwe waznz weng hawakubal serkal 1,
wanataka ikishndkana kuvunja muungano
bas kila k2 kwe nus kwa nus na wabara
weng hawatak serkal 2, wanaona hawawez
gawana nus kwa nus na nch iliyo ndogo
kama dar, kwan wao watapata kdogo
kischotosha na znz watapata na zaid.
So kilichobak ni muungano uvunjwe kwa
aman.
Kitu kingne., baada ya muungano Karume
alwaambia waznz wachofu coz c hatuwez
kwenda kene baraza lao ila wao kwetu
wanakuja. Hi inanitia mashaka kama
Nyerere
na Karume walkuwa na lengo jema la muda
murefu. Mi naona waliungana ili wakolon
wakiamua kurud tuwe na nguvu(hao
wawili
wasipoteze uhai na vyeo vyao, ila Nyerere
alikuwa desperate kulko Karume had
akakubal serkal 2, zinazotusumbua na
kupoteza uhuru wa tanganyka huku znz
wakbak nao wakwao kwa kias kikubwa.
Tofaut na weng wafikiriavyo Karume
alkuwa
mjanja kulko Nyerere. Karume aliona faida
ya
muungano kwake binafsi wakat ule, kama
nilivyoeleza hapo ju, ila akajua tena
muungano hautadumu milele coz
watanganyka wakijaznduka namna Nyerere
alvyosacrifice sovereignity ya tanganyka
kijanja, hawatovutiwa. Na waznz
wakishanyonya vya kutosha watataka
uhuru, kama sasa. Ahaaa kumbe! Kwa hyo
akaamua awekeze kwa ajil yake na znz.
Akakubal kuwa makam ili muungano
uwepo,
kwa wakat wake, aweze kujilinda na baadae
muungano uvunjke, znz wakiwa
wameshatunyonya, znz iwe nch huru).
NB: ni mtazamo wangu! Ila fikiri, hata hayo
mambo meng ya muungano yaliyopo sasa,
je
isingekuwa hvyo kungekuwa na tofaut
kubwa? Je yanatosha kuwa 7bu za Karume
na Nyerere kutuunganisha? Kila nch
ingeendelea kivyake!
Viongoz wa sasa nao wanaona faida ya
muungano, ni kuongeza uwanja wa
utawala,
nafasi za uongoz, kodi, ...(etc, jaza
mwenyewe)...
Hv fikiria vyama (ccm, cdm, cuf) kila moja
ikishka serkal moja au, hata hz 2 zilzopo
zkishkwa na vyama tofaut tena vyenye
sera
tofaut tofaut, itakuwaje?(k2 chenye
uwezekano mkubwa kutokea)!
Cuf hawatak muungano, xo wakshka znz,
watapiagania kuuvunja.
Mi naomba muungano tuuvunje kwa aman
ili
tuendelee kuwa marafik huru, kuna
uwezekano upand fulan ukahamasishwa na
walioshka madaraka kwa upand huo,
wavunje muungano kwa vurugu.
Sikulazmish kuwa na mtzamo kama wangu!
Ila...
Tafakar chukua hatua!
 
Tatizo wewe Mwanakijiji una akili sana lakini ujue jamaa wanapanua mianya ya ufisadi na uwingi wa maofisi ili kuajiri watoto wao, mashemeji na wajomba. Hivi nchi imeliwa mpaka imetoboka sasa ndio tuwe na mafastjet watatu tukione cha moto bora tuunde majimbo, Zanzibar iwe jimbo, bara pawepo majimbo kwa idadi ya jimbo moja sawa na idadi ya wazanzibari kisha tuwe na Raisi mmoja. Hakua haja kuongeza urasimu mpya na ubwerere wa matumizi hebu watupe mfano marais watatu au wanne wanatawala nchi gani duniani kama sio watu waliochanganyikiwa hawa.
 

Mkuu hawa Ma-CCM tatizo wanauzunguka mbuyu , lakini mwisho huu Muungano utawafia Mikononi!
Kama ulivyodokeza Raisi wa JM Tanzania Nchi yenye kutegemea kuuza kahawa,pamba,tanzanite,mafuta/gesi(mali ghafi) hautakuwa na maana yoyote zaidi ya kuwa Bendera fuata upepeo na mtu wa kula maraha kwa Jasho la Watanganyika na Wazanzibari maana hata kuwa na Nguvu ya Kisiasa na Kiutawala.

Raisi wa Tanganyika na Zanzibar kwa maana nyingine Nchi mbili kwa mlango wa Nyuma
.
 
Mpango mzima n kauli za nyerere 2 kuelekea kweny one serikali bhaaaanaaah
 

Katika swala la bunge umekosea, wabunge hawatokuwa 400, watakua 75. Majimbo yatapunguzwa!
 

Tehee , Nitafurahi kuona Gavana Slaa na Gavana Seif wakifanyakazi pamoja na Rais Lowassa!
 

Hakika tusidhani kwamba kwa kuunda serikali tatu tumeimarisha Muungano la hasha tumeupa kisogo Muungano wetu. Na hiyo ndiyo step nambari moja kuua Muungano. Niungane na Mzee Mwanakijiji katika harakati za kuunga mkono serikali MOJA.

Serikali tatu maana yake tumekubaliana na matwakwa ya wanaotaka tuuvunje muungano. Hapa ndipo ninapoona serikali imekosea. Kumbuka Mwanzo wa Ngoma ni LELE!!!

Hivi huyu Rais asiye na nchi Maalum ataishi wapi???
 
Vuteni Hisia ikitokea hivi kwenye serikali tatu: Rais wa Muungano CCM,Rais Tanganyika Chadema,Rais wa Zanzibar CUF! Hii itakuaje? Itakua vuta nikuvute!
 
Kitu cha kijinga zaidi ni uwepo wa mawaziri zaidi ya kumi wakishughulikia mambo saba. Mambo saba wizara 15? Haiwezekani.
 
Mbona rasimu haijasema pesa za kuendesha hizo serikali zitachangiwa katika mfumo gani ?
 
Kuhusu wabunge, tuache kupondana kisiasa.
Tufikirie nje ya box! Everything has a
begining! Nyie mnataka kuiga 2, sio kutoa
vyenv viigwe? Kama utaratbu huu haupo
kwngne kote bas, mi nawapa hongera
kwa uvumbuz. Swala hili halina shda. Logic
ni hii
Tunataka tuwe na uwiano wa kijinsia
bungeni, hiyo ni njia safi.
Tunataka kupunguza idadi yd wabunge,
tunaondoa viti maalum.
Wanawake watatetewa na nani?
(mwanamme hawez kumtetea mwanamke
kama anavyoweza kujitetea yeye)
tutatumia utaratbu huo.
Hatimaye, tuna wabunge wachache bila
kupoteza vitu kama watetez wa
wanawake, na huku tumekuwa mfano ktk
usawa wa kijinsia ktk uongoz.
Pia, wabunge wawil wanaeza gawana
mjukumu ya kufuatilia na ufanisi
ukaongezeka. Wakafikia wananch moja
kwa moja na kwa umdn katka nyanja
tofaut tofaut.
Tusipinge vitu kisa ni vipya, tutathibitisha
kuwa kufikiri kwetu kuna ukomo!
 
!

In short.. Tusikubali serikali tatu za nchi; bali serikali moja, nchi moja, taifa moja na watu wamoja.. Mapendekezo ya Tume ya Warioba kuwabebesha Watanzania mizigo hii ni ya kupingwa, kukataliwa na kupuuzwa.

What do you mean by "nchi moja, taifa moja na watu wamoja'? Kwa maoni ya wengine wengi hii "nchi moja' imekuwa na tofauti kubwa za kimsingi na ndio sababu kuna sauti kubwa ina yo tutaka kutafakari upya huu muungano. Zipo tofauti wazi za kijamii na kihistoria ambazo zimetufanya tukatofautiana kimitazamo (mfano mahusiano na taasisi na mataifa ya nje, nk). Tuwe wakweli Mkuu Watanzania tukubaliane kupata serikali zetu mbili.
 
Tumejaribu Muungano, umetushinda...na tuachane nao...Ndoa gani hii, watu hamuelewani lakini kila siku mnalazimishana kulala kitanda kimoja?
 
Mbona rasimu haijasema pesa za kuendesha hizo serikali zitachangiwa katika mfumo gani ?

Sijapata kuisoma, ila kama haijasema, ajabu! Labda kene sheria itaainishwa, ila hapana, watu watabishana sana bila hitimisho na huku katba ndo ishapita! Tena na hyo serikal ya tanganyika itaundwa lin akat katba inakamilika 2014?
 
Tunapozungumzia Muungano wa
Serikali Moja ni aina ya Muungano
ambayo mataifa ya asili yanayoungana
yanapotea kabisa na kuwa na mfumo
mmoja wa kiserikali na nchi. Si aina ya
Muungano unaopendelewa hasa kwa
nchi zilizo na tofauti kubwa kama
Zanzibar na Tanganyika.


Muundo wa Serikali mbili ndio uliopo hivi
sasa ambao umekuwa ndio chanzo cha
migogoro karibu yote ya Muungano huu.
Watanzania wote ni mashahidi wa jinsi
muundo huu ulivyoshindwa kuweka
utulivu na maridhiano katika mahusiano
ya Muungano. Zaidi ya yote umeshapitwa
na wakati na hauwezi kuhimili mageuzi
ya kikanda na kimataifa yanayotokea.
Mbali na kero kadhaa za humu humu
ndani, lakini tuchukulie mfano mdogo
wa kuwepo kwa Jumuiya ya Afrika
Mashariki na ushiriki wa Tanzania.
Zanzibar haimo kama mwanachama
katika Jumuiya hii bali iliyomo ni
Tanzania. Kati ya mambo 18
yanayoshughulikiwa na Jumuiya hii, ni
mambo 4 tu ambayo ni ya Muungano na
ambayo Tanzania ina mamlaka ya
kisheria kuiwakilisha Zanzibar. Kwa
yaliyobakia 14 Tanzania kuiwakilisha
Zanzibar ni kwenda kinyume na Katiba.
Hata suala la Zanzibar kujiunga na
Jumuiya ya Nchi za Kiislamu Duniania
(OIC) lilikwamishwa kutokana na mfumo
wa muundo huu na Tanzania ikadai
ingejiunga kwa vile ndio yenye mamlaka.
Takriban inakaribia miaka 20 tokea
kutolewa kwa ahadi hio lakini umma
haujaelezwa maombi yalikwama wapi.
Hata hivyo, hili la OIC ni utashi wa kisiasa
au kidini tu ndio uliokwamisha; lakini
muundo wa Muungano huu unasutwa
hata na maumbile ya mataifa haya
yaliyoungana. Kwa mfano upo umoja wa
visiwa vya Bahari ya Hindi ambao
Zanzibar kama kisiwa wanastahiki
kujiunga, lakini haina mamlaka, na hio
Tanzania iliyojipa mamlaka haiwezi
kujiunga kwa vile sio kisiwa – hii
imepelekea Zanzibar kukosa haki zake
mbali mbali za kimaendeleo.
Muungano mwengine ni ule wa Serikali
Tatu. Hii ni aina ya Muungano wa
Shirikisho. Nchi zilizoungana hubaki na
serikali zao na Serikali ya Shirikisho
hubaki na yale mambo ya Muungano tu.
Aina hii ya Muungano inadai kuwepo na
Serikali ya Tanganyika, ya Zanzibar na ya
Muungano. Hapa zitakuwepo nchi mbili,
mamlaka tatu na serikali tatu.
Kwa kuangalia uendeshaji wa mambo ya
ndani ya nchi, huu unaweza kuwa
muundo unaoweza kuondoa kidogo
mtafaruku uliopo; lakini ukiangalia
uwakilishi wa nchi hizi na Serikali zao
katika mambo ya nje, muundo huu nao
umeshapitwa na wakati. Tujiulize kwa
mfano, kwa kuangalia mfano ule ule wa
karibu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ni
ipi kati ya Serikali tatu hizo itajiunga na
EAC?
Kama ni serikali hizi 2 za Zanzibar na
Tanganyika suali linakuja jee ni nani
atawakilisha kuhusiana na masuala
yaliyo chini ya Serikali ya Muungano/
Shirikisho ambayo Serikali mbili hizi
hawatakuwa na mamlaka nayo? Na vivyo
hivyo endapo itayojiunga ni Serikali ya
Muungano nayo itawakilishaje
kuhusiana na yale mambo yaliyo chini ya
Serikali ya Zanzibar na Tanganyika
ambayo haina mamlaka nayo? Huu ni
muundo ambao umeshapitwa na wakati.


Njia pekee kwa sasa ambayo itakata
mzizi wa fitina ni kuwa na Mashirikiano/
Muungano wa Mkataba. Huu ni
muungano ambao kila nchi inajitegemea
na inabaki na Serikali yake, na
uendeshaji wa mambo yake, utaifa wake
nk na huingia katika mashirikiano kwa
njia ya Mkataba (Treaty) juu ya mambo
na kwa utaratibu wanaokubaliana hizo
pande mbili au zaidi zinazoungana.
Mifano ya miungano ya aina hii ni kama
EAC (Kenya, Uganda, Tanzania Rwanda
na Burundi) na European Union ulio na
nchi wanachama 27.
Uzuri wa muundo huu ni kuwa unatoa
fursa kwa nchi zilizoungana kuweza
kuuagalia kila inapobidi ule mkataba
wao bila vikwazo vya Kikatiba na hivyo
kusukuma mbele maslahi yao bila
kumezana, kubebana au kuoneana.


Serikali zetu hazina haja ya kuogopa
mawazo mapya kutoka kwa wananchi
wake ya kutaka kuirudisha Jamhuri ya
Watu wa Zanzibar itakayokuwa na
mamlaka kitaifa na kimataifa na
kufuatiwa na ‘Mikataba ya Mashirikiano
mema’ na Tanganyika na nchi
nyenginezo.
Na kwa kweli tunahitaji kugundua njia
mpya za mashirikiano badala ya
‘Miungano ya Kikatiba’ iliyopitwa na
wakati. Ni kazi ya Serikali zetu kuzitafuta
njia hizi mpya za ‘Mashirikiano ya
Mikataba’ badala ya ‘Miungano ya
Kikatiba’. Serikali zetu zisione aibu wala
ugumu kuzipokea njia hizo
zinapotolewa na wengine.
Kwa upande wa Zanzibar, Serikali ya
Umoja wa Kitaifa inaweza tu kuthibitisha
umuhimu wake katika dunia ya leo kwa
kutenda yale wanayoyahitajia Wananchi
wakiwa ndio ‘wadhamini na wamiliki’
wa Katiba.


Katiba ya Zanzibar, Toleo la 2010, ibara
ya 9 inaeleza kuwa nguvu, uwezo na
mamlaka yote ya kuendesha nchi
yatatoka kwa wananchi wenyewe.


Itaendelea............
 
ngojea anakuja mda huu yupo kwenye foleni ya magari anatokea unguja alikoenda kuwaulizia kama wanataka serikali ya muungano ama la!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…