Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,768
- 2,361
Tee..hee.. hii yanikumbusha kwenye ndoa - hivi nani anatakiwa afungashe na kuondoka ? Anayeona hapendwi (anaonewa, hathaminiwi) au yule ambaye bado anapenda. Nafikiri hapa hakuna cha kuondoka mtu bali kuna wivu tu wa kutaka apendwe zaidi - wivu wa kike ? Nani tena huyu anataka kulitia doa penzi kati ya Tanganyika na kisiwa cha karafuu ?
wabara ndio wanaoungangania huu muungano Zanzibar hawautaki
wabara ndio wanaoungangania huu muungano Zanzibar hawautaki
Wanaotakiwa kudai serikali ya Tanganyika ni Watanganyika wenyewe na si Wazanzibar.
he! Mbona hivyo wewe...hakuna haja ya kuanzisha serikali ya tanganyika.
..masuala ya tanganyika yanashughulikiwa na serikali ya muungano.
..kama zanzibar hawako tayari kuvunja smz na masuala yote yashughulikiwe na serikali ya muungano basi wachukue hatua za kujitoa ktk muungano.
Nb:
..msimamo wangu mimi huu muungano uvunjwe tu.
kama hawautaki si waondoke sisi tujiunge na visiwa vya Comoro?
kazi zenyewe zipo? nyinyi mkiletwa huku kuja kupiga kura na chama chenu cha Mafisadi hamrudi makwenu mnahamia kila pahala mnajipachika tu...........aaaaagh.Taabu kubwa Visiwani ni watu wavivu ktk kazi!!!
Kubwa Visiwani wanalojua ni Kulalamika tu na kuomba msaada!!!
Moja ya matatizo makubwa sana nchini ni kwamba we are not informed. Tuliambiwa kwamba wahusika, mawaziri wa muungano, wanasheria wakuu n.k, wameagizwa wakae watatue kero za muungano. (Kwa wamazo ya kina Pinda, that blowhard Shamhuna na Idi Pandu na Mwanyika, wanaweza wakakaa waka solve huu Muungano.)
Walifikia tamati gani, hakuna kiongozi aliyetuhabarisha, hakuna mwandishi aliyeuliza, hatujui, we don't know nothing. Imekuwaje hili swala la Muungano limeibuka tena, si walisema wamekaa kulisuluhisha?
Naomba kuuliza wana wa Jamii,
Kama tunaweza kuita Zanzibar Zanzibar, wakati Tanganyika na Zanzibar ndio zinazofanya Tanzania, je itakuwa sahihi kutamka Tanzania Bara Na Tanzania Visiwani?
Kama tunaweza kutamka Tanzania na Zanzibar; Kwa mantiki hiyo hakuna Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Wakati sasa hivi nchi nyingi zimeungana kwa mfano, EU sisi huku bado tu tunamawazo ya kujitenga.
Vunjeni tu huo Muungano mkae mjadiliane! Who is the loser? Saa nyingine kuvunja uhusiano ndio inakuwa njia mbadala ya kuujenga uhusino huo, Vunjeni!
..kama CUF wako serious hawataki Muungano basi ni vizuri hizi hoja zao wakazizungumzia ndani ya Bunge la Muungano.
..sasa hivi kuna kikao cha Bunge kinaendelea sasa tunasubiri kusikia CUF wakileta hoja ya kuvunja Muungano, au kuunda serikali ya Tanganyika.
Mwiba,
..kikao cha Bunge kinaendelea Dodoma wiki ijayo.
..tusubiri kama Mzanzibari yoyote na atatamka kwamba Watanganyika wanawanyonya wa-Zanzibari.
..tuone kama kuna Mzanzibari atarudia kile alichosema Juma Duni kwamba wa-Tanganyika wanaharibu utamaduni wa wa-Zanzibari.
Wanaotakiwa kudai serikali ya Tanganyika ni Watanganyika wenyewe na si Wazanzibar.
Wazanzibar wana haki ya kudai mambo mengine yote, hili la kudai serikali ya Tanganyika si lao wala hawatakiwi kuwa na uchungu nalo.
Mimi kama Mtanzania kutoka ilokuwa Tanganyika sijawahi kumwomba hata mzanzibari mmoja kunisemea ili kudai serikali ya Tanganyika.
Hoja hii ya baadhi ya Wazanzibari ni hoja ya kukemewa vikali, kwa sababu lengo lake ni kurudisha nyuma hoja nzima ya kujadiri kero za muungano ambazo wote tunajua zipo na kamwe hazitakaa ziondoke mpaka sisi Watanzania wenyewe tuweke makalio yetu chini na kuzijadiri kwa kina na kuzitolea ufumbuzi wa kisheria.
Wote tumechoka kukoromewa na watu wanaojifanya kutetea muungano kwa misuli yao bila kuweka akili zao katika utetezi.
Lakini hatuwezi vumilia vitendo vya kuvuruga mambo na kuingilia haki za watu wengine na kuleta madai ambayo kisheria wasemaji hawana uwezo wa kuajadiri.
Kama hoja ya kudai Zanzibar hruru isiyokuwa mshiriki wa Muungano wa Tanzania haiwezi simama kwa miguu yake yenyewe mpaka hoja ya kudai Tanganyika iwekwe mezani, basi hoja ya kudai Zanzibar haina nguvu na pengine itakufa kwa kujikaba yenyewe kuliko kuuawa na watu.
Labda tu kama kuna maana nyingine ambayo mtoa hoja anaweza kuianisha, Sivyo "Shut Up and Drive".