Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Mzee Mwanakijiji umenikuna! Hawa Wazanzibari wanaota ndoto za mchana za utajiri, sasa wameipata. Ooh Mafuta ya Zanzibar ni ya Zanzibar; mara Ooh zama za kutishana zimeisha, Ooh mafuta ya Zanzibar hayaendi bara mpaka dhahabu ya Mwanza igawiwe Zanzibar! Hawa wala tende wana matatizo kweli kweli! Wanasema hayo huku bara tukilipia starehe zao zote kwa fedha itokanayo na pamba, mpunga, chai n.k. Zama za kuwabeba Wazanzibari zimekwisha - tuwaachie Zanzibar yao ndogo kama wilaya ya Pangani lakini yenye Rais, Waziri Kiongozi, Naibu WK, mawaziri na manaibu wao 40, wakurugenzi na makatibu wakuu zaidi ya 100, viongozi wa siasa zaidi ya 5,000! Kisiwa cha viongozi! Kalagha bhao!


Kwa mwenye akili na kama ungekuwa nawe unazo basi ungeuliza kwanini hilo pendekezo lako linanawashindeni kulitimiza.
 
nafikiri hapa kwa hali ya sasa tatizo lilopo ni wanasiasa wa bara (tanzania bara) kwani utaona kabisa wazanzibar including karume hawataki muungano, sasa kwa nini tunawang'ang'ania? Mtu hataki kuishi na wewe tatizo ni nini? Kama mafuta wanayo si basi na sisi tutaendelea kuishi bila shida. Vikao vikubwa vya chama hawa jamaa wanatishia kuvunja muungano, kule butiama swala la muafaka kati ya ccm-zanzibar na cuf, karume kaongea kwa jaziba mpaka analia anamwambia coton man (muungwana) kama anataka muafaka basi yeye anarudi zanzibar na nchi yake. Sasa kweli hapo kuna muungano? Na wajumbe wote wa zanzibar wakawa wanafoka kama nguruwe kapigwa mkuki. It's time tufanye referendum zanzibar, kama wanataka kuwa nasi au lah



isipokuwa pana jambo sisi wa kawaida hatulijuwi.
 
Enzi zile nchi yetu ikiwa na viongozi wenye vision!

Immediately ingetafutwa kampuni la wazungu na waarabu lingine... lije lidhibitishe kwamba Zanzibar sorry Pemba hakuna mafuta... maana hawa lazima uwahakikishie tena kwa kudhibitishwa na watu wengi kwamba hiyo kitu ilikuwa hadithi tamu za wakati huo.

You know what?

Muafaka ungepatikana haraka sana... maana kiburi cha wapemba na chokochoko zao pia ni hiyo hadithi kwamba kuna mafuta Pemba.

Wakati wananchi wa Comoro wanatamani wangekuwa sehemu ya Jamhuri ya Tanzania, wenzetu wao wanatamani kuwa na Jamhuri yao.

Mungu ibariki Tanzania



Harakati za kudai haki mnazibatiza kuwa ni kuvunja Muungano. Kwa hilo ni hiari yenu lakini haki si mafuta tu na taratibu tutafanya hivyo kwa vitu vyengine . Hizi lugha za kututisha na Muungano ni hollow, hollow hollow. tunataka haki ndani ya Muungano na mnapohisi kuwa haki hiyo mtaitowa kwa kuvunja Muungano you can do this instant bila ya kungoja kesho na mambo mnayotutisha eti kuuwana na kufa njaa haya yapo hadi sasa. Hili la kuuwana tunafanyiwa na wenzetu kwa kutuletea majeshi kufanya hayo mauwaji na suala la njaa linafanywa na nyie wenzetu kwa kutubana hata kwa rasilimali zetu.
 
Nilipojiunga elimu ya Upili pale Dabanga Camp (kwa wanaoijua) miaka ya 1980 mwishoni nilipokelewa na SWALI hili
" Kuna utumwa na utumwa; kuna utumwa wa mwili na utumwa wa akili: Kuna utumwa wa kutumwa na utumwa wa kujituma. Mradi kuna utumwa na utumwa. Jadili.

Swali hilo sikuwahi kulielewa hadi yalipoanza mambo haya mara UFISADI mara ZENJ ni nchi mara;mara; mara.
Ila yote ni ubatili na kujilisha upepo kwa wazenj; wanachokitaka wakiseme na kukitekeleza upesi

Hata mimi nilifundishwa shule kuwa bazazi huwa anaelewa ukweli wa jambo lakini akajizunguusha.
 
Mkuu Pakacha punguza munkari.
Kubishana na mtaalam hakuonyeshi ukomavu wa hao wawakilishi. Unless wangekuja na ripoti ya kitaalam kupinga utafiti wa bwana reading. Hakuna mbara anayeshikilia la mafuta tu, suala la mafuta limekuwa ni kete ya wazanizbrai, ndilo wanalolitumia kila siku. Ukisoma bandiko la mwanzo kabisa utaona wawakilishi wameonyesha mawazo yao kuhusu suala la mafuta.
Kujadiliwa Muungano! Mbona hilo linafanyika, tatizo baadhi wanaujadili kwa jazba kwa kupenyeza mambo mengine yasiyokuwepo ili kukwepesha hoja kuu-kama wanavyotaka kulifanya suala la mafuta lionekane kuwa nalo ni tatizo.

Bottom line ni kuwa WAZANZIBARI WANAJADILI KILICHO NDANI YA ZANZIBAR> SIFIKIRI TUNAHITAJI KUWA MAPROFESA KUNGAMUA HILO>
 
sisi kina nani? u mean CCM bara ndo wanataka muungano zaidi? as far as am concerned wananchi wa kawaida hatuna mshawasha wowote na muungano.

Tulio wengi humu ndio sie wananchi wa kawaida na wenngi wetu si CCM lakini tunaotukanana na kukebeheana humu ndani ni sie
 
Nani kakwambia Wabara wanalishikilia la Mafuta? Kwenye hiyo semina kulikuwa na Mbara hata mmoja? Au huyo Reading ni mzanaki? Kinachowahangaisha nyie akina Ami sasa hivi hata hamkijui! Kusema mwasema lakini chenga mwaliwa! Hayo mafuta mnayotafuta mtayaweka kwenye Mapakacha? Au mnamsubiri Okello aje tena kuwasaidia kuifukuza hii 'mijitu ya bara' kama alivyofanya kwa ZNP+ZPPP=CUF? Habari za mitaani zinasema ndani ya serikali yenu hiyo ya nchi yenu kuna harufu kali ya Abdulrahman Babu!! Ya kweli hayo???


kwani almasi na dhahbu zenu mnazitia kwenye vikapu? Si mnagawa tu? Tuachieni nasi iwe zamu yetu kugawa. Towa boriti kwenye jicho lako ndio utaweza kutowa kibanzi kwa mwenzako.
 
Unde_age,
Hivi nani anatawaliwa na mwingine? Kelel za mafuta kwa JK ni sawa na macho ya chura yasivyomzuia Ng'ombe kunywa maji. Baada ya Karume mkubwa tuambie ni rais gani au mwenyekiti gani wa baraza la mapinduzi amepita bila ridhaa ya bara? Leo hii hamlii mnaomba bara iwasaidie kumaliza tofauti? Nafikiri hukijui unachoongea ni kheri unyamaze, na kwa kukufahamisha tu kwa mfumo wa sasa wa CCM wa kumpata mgombea sahau rais kuja kutoka Zanzibar

Inashangaza kuwaambia wenzako wanaongelea wasichokijuwa na wakati kama kufanya hivyo ni ujinga basi wewe umeupita.
Umesahau kuwa huyo JK angekuwa ameshamaliza muda wake zamani kama si hiyo Zanzibar? Umesahau kuwa huyo Jk asingekuwa madarakani hivi sasa kama si Zanzibar kumwangusha Salim. Ni tabu kujifanya unajuwa bali ni raha kukubali kuwa hujui jambo.
 
Unde_age,
Hivi nani anatawaliwa na mwingine? Kelel za mafuta kwa JK ni sawa na macho ya chura yasivyomzuia Ng'ombe kunywa maji. Baada ya Karume mkubwa tuambie ni rais gani au mwenyekiti gani wa baraza la mapinduzi amepita bila ridhaa ya bara? Leo hii hamlii mnaomba bara iwasaidie kumaliza tofauti? Nafikiri hukijui unachoongea ni kheri unyamaze, na kwa kukufahamisha tu kwa mfumo wa sasa wa CCM wa kumpata mgombea sahau rais kuja kutoka Zanzibar

Inashangaza kuwaambia wenzako wanaongelea wasichokijuwa na wakati kama kufanya hivyo ni ujinga basi wewe umeupita.
Umesahau kuwa huyo JK angekuwa ameshamaliza muda wake zamani kama si hiyo Zanzibar? Umesahau kuwa huyo Jk asingekuwa madarakani hivi sasa kama si Zanzibar kumwangusha Salim. Ni tabu kujifanya unajuwa bali ni raha kukubali kuwa hujui jambo.
 
kuna mtu aliwahi kusema na mimi naona kuna mantiki flani katika usemi huo kwamba muungano umewasaidia wazanzibari kuwa na mshikamano kwa sababu umewapa kisingizio cha kuelekeza malalamiko yao. Usingekuwepo mwungano hawa wangekuwa wameshapinduana sijui mara ngapi mfano wa comoro. Na aliyesema haya alikuwa mzanzibari.




usiandikie mamate........
 
wazanzibar wanataka tuwaache na matuta hewa..watakoma baada ya kuvunja muungano...pemba nao wakajitenga na mafuta yao....alafu nao mwisho wa siku wakashindwa kuyapata...

watanganyika msijali ...mafuta tanganyika yameshapatikana kwa wingi.........

Kama ilivyokuwa kwa Almasi , dhahabu, gesi na madini mengine mafuta yenu hayatawasaidia Wazanzibari kwani sasa ukiondowa hayo mafuta si mnayo madini na mnatumia wenyewe?
 
zanzibar pia hakuna upinzani ...kuna mgawanyiko..pemba ..CUF,unguja ..CCM...

huwezi kuiita hiyo kuwa ni hali huru ya kisiasa.....ningeita hivyo kama pemba ccm na cuf wangegawana nusu..na unguja vile vile..lakini sasa hatuchekani...


Buisara ingetumika kujadili kitu unachokijuwa kuliko kusikia masikioni tu.
 
Tatizo la Muungano linakuwa linafichwa. Kinachoendelea huko Zanzibar kwa hao wawakilishi na hasa viongozi wa CCM Zanzibar (Afro Shiraz) ni kuutafuta umaarufu tu wa kisiasa. CCM Zanzibar wanajua kabisa hawawezi kubakia madarakani bila ya sapoti ya serikali ya JMT. Hivi nani ambaye hajui matokeo ya uchaguzi Zanzibar yamekuwa yakipikwa kwa kutumia nguvu za Bara? Hao Mawaziri wa Karume wanaopiga kelele kwamba Zanzibar ni Nchi, wana malengo makubwa ya kutafuta umarufu wa kisiasa.

Nina imani ukimuuliza mwananchi wa kawaida wa Zanzibar khs Muungano atakwambia hautaki. Hautaki sio kwa 'vijisababu' wanavyotoa akina Shamhuna. Nani ambaye hajui ubabe unaofanywa na Serikali ya JMT kwa wananchi wa Zanzibar ambao ambao haiungi mkono Afro Shiraz? Wanawake wangapi wamebakwa na Polisi waliotoka Bara kwenda kumlinda Karume na wenzake? Wanaume wangapi wamekimbia familia zao kwa sababu ya undava wa Mahita na wenzake? Wapemba wangapi waliuwawa na Serikali ya Mkapa? Wazanzibari wangapi wamekosa ajira kwa kutomshabikia Karume tu. Sasa nani atataka Muungano au ataupenda huo Muungano kwa matlaba niliyoyataja hapo juu. Karume na wenzake wanapiga kelele ili kuonesha kwa wazanzibari kuwa nao wamechoka na Muungano wakati wanajua ndio kwanza wanauhitaji kuliko wakati mwingine wowote.

Tatizo lililopo ni kwamba Karume na wenzake WAMEDEKEZWA na CCM Bara. Na hili linatokana na namna Karume alivyompa sapoti kubwa JK kuingia madarakani. Angalia Karume na wenzake walivyomchafua SAS kwa lengo la kumfanya asiingie madarakani. Karume mdogo alipandikizwa ili avuruge kura za SAS.

kihistoria Wazazibari ndio wamekuwa wakipandikiza Marais wa JMT. Mkatae msikatae marais wote wa Tanzania wamepatikana kutokana na nguvu za Wazanzibar. Kuanzia Nyerere. Karume alipokubali kuwa Makamu wa Rais ina maana aliamua kwa makusudi kumpa Nyerere Urais. Karume hakuwa na ubavu wa kuongoza Zanzibar kwa sababu yeye alikaribishwa tu kwenye serikali ya mapinduzi kwa kuwa yeye hakushiriki. Mwalimu alipeleka wanajeshi kumlinda na alipomwambia mwanzoni kuhusu kuunganisha nchi Karume alikataa. Mwalimu kwa kusaidiwa na Marekani walitishia kuyaondoa majeshi ya Tanganyika na Karume akajua kuwa hana ujanja ila kusalimu amri na kumuuzia Mwalimu nchi kwa bei poa.

Mwinyi hakuwa chaguo la Nyerere. Chaguo la Nyerere alikuwa ni SAS. Kwa msingi huo Mwalimu kumchagua SAS alikuwa anawakilisha mawazo ya watanganyika wengi lakini tunakumbuka akina Natepe walivyokuja kumzima Mwalimu na kuteletea Mwinyi JMT. Wazanzibari tena wakatuchagulia Rais.

Wazanzibari tena wakatuletea Mkapa. Kumbuka Salmini mwanzoni hakuwataka Mkapa na JK hivyo kura zake na wenzake walimpa Msuya. Walipokuja kugombanishwa Ben na JK kura za 'kujazia' za Salmini na wenzake akapewa Ben. Salmini hawakuwa na mahusiano mazuri na JK hasa pale walipokuwa watumishi wa CCM. Wazanzibar tena wakatutafutia Rais.

Akaja JK. Naye akaletwa na Wazanzibari. JK akijua namna Karume alivyokuwa hawaivi na Salmini aliamua kumpiga tafu kubwa kwenye vikao vya juu vya CCM. Kumbuka kwenye uchaguzi wa Rais wa Zanzibar Karume alikuwa ni wa tatu kwenye mapendekezo ya Kamati Maalum ya CCM Zanzibar akitanguliwa na Bilal na Amina Salum Ali. Kwenye vikao vya Dodoma Karume aliibuka kidedea kwa nguvu za kina JK. Hapo ndipo sasa uswahiba wa JK na Karume ukakolea na ndio kama mlivyoona walivyoamua kummaliza SAS.

Kwa mtizamo huo hapo juu. CCM Zanzibar haina ubavu wa kuongoza Zanzibar bila kuwa na nguvu za Bara. Kelele za kina Karume kama nilivyosema awali ni KUDEKA tu. Sasa hivi CUF na CCM Zanzibar wameungana kupiga kelele kwamba Zanzibar ni nchi na ina Rais. Nataka nimuulize Seif Hamad Rais wa Zanzibar ni nani? Na amechaguliwa lini? Na yeye Hamad na CUF wametambua lini kwamba Karume ni Rais wa Zanzibar?

Kama nilivyosema hapo awali, wananchi wa kawaida wa Zanzibar hawautaki Muungano kwa madhila waliyofanyiwa na wenzao wa Bara, kuanzia kupelekewa Polisi na Wanajeshi kuwapa kibano, kuongezewa wapiga kura kutoka Bara ili wapandikiziwe utawala wasioutaka, Kwa upande wa wananchi wa wa kawaida wa Bara, Muungano ndio hata hawauelewi. Kimsingi huku Bara Rais wa TFF Leodgar Tenga ni maarufu sana kuliko Rais wa Zanzibar Karume. Huku Bara Laila Odinga ni maarufu sana kuliko Rais wa Zanzibar Karume. Huku Bara Zanzibar ni 'kamkoa kadogo sana' kuliko Wilaya ya Kahama. Huku Bara Nadir Haroub Kanavaro ni maarufu sana kuliko kiongozi yoyote yule wa Zanzibar. Kwa maana hiyo kwa wananchi wa kawaida wa Bara kuvunja Muungano hakuna tofauti yoyote na kutovunja Muungano.

Tunapozungumzia Muungano wa Tanzania huwa tunamsahau Mdau mmoja muhimu sana katika Muungano huu. Serikali ya Marekani. Kwa sasa ni wazi kabisa Marekani ilihusika kwa kiwango kikubwa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar. Nadhani kwa sasa makabrasha ya namna Marekani ilivyohusika na Muungano yako wazi kwenye tovuti za serikali ya Marekani. Siku 10 kabla ya Muungano Mwalimu Nyerere alimtuma Kambona kwenda Kenya kuongea na Jommo Kenyata namna ya kuziunganisha Nchi za Afrka Mashariki. Siku 10 kabla ya Muungano hakuna aliyekuwa ametamka hadharani kwamba kulikuwa na maongezi ya kuziunganisha Tanganyika na Zanzibar. Marekani ambao walikuwa wakimhofia Mohamed Abdulrahman Babu kama mkomunisti hatari na mwenye nguvu kubwa na ushawishi angeweza kuifanya Zanzibar kuwa Cuba ya Afrika. Mwalimu ambaye alikuwa anaogopa kukaribishwa Zanzibar maadui zake na kwa maneno yake mwenyewe aliwahi kutamka kuwa angeweza angevisukumia Visiwa hivyo mbali zaidi baharini. Ilikuwa ni Rais kwa Marekani kumtumia Mwalumu kumlazimisha Karume akubali kuunanisha Nchi ukizingatia Wanajeshi waliokuwa wakimlinda walitoka Bara na Mwalimu akatishia kuwaondoa.

Nimelisema hili la Marekani. Je Marekani kwa sasa iko tayari kuruhusu Muungano wa Tanzania uvunjike. Kwa dunia ya sasa ya Marekani adui yake mkubwa ni Al Qaeda. Je hatuoni kwamba bado Marekani anautaka Muungano kwa gharama yeyote kwa hili la Zanzibar kuwa kituo cha Al Qaeda? Hivi Marekani hajui mchezo mchafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na JMT katika kucheza faulo kwa uchaguzi wa Zanzibar? Nina imani Marekani yu radhi Afro Shiraza iendelee kutawala Zenji kuliko CUF. Ukijumlisha na hayo Mafuta kiduchu na Migodi ile ya Buzwagi ambayo naambiwa familia ya Bush ina nasaba nayo ukiachilia mbali na Marekani yenyewe kuna kuvunjwa Muungano hapa kweli? AU TUNAZUGANA na VIJIKELELE vya kitoto vya kina SHAMHUNA?

Post yako yako naikubali na ina viashiria vilivyo sahihi lakini umesahau kuwa hata hao viongozi wa CCM Visiwani wameshachoka na kubanwa sana na Muungano kwa vile watu wanaowaongoza wanazidi kudidimia kihali kila siku.
Si kweli kuwa mwananchi wa kawaida haupendi muungano lakini Muungano unamsukuma mwanannchi kwenye kona na hivyo juu ya udhaifu wake atapigana na Muungano.
CCM haiwatoshelezi viongozi wote wa Zanzibar na badala yake vijisenti vinabidi vigawiwe miongoni mwao. Unaonaje iwapo donge nono litakuja directly mikononi mwao? Wanafahamu kuwa kwa mfdumo wa sasa unawanyima fursa ya kutekeleza njia za kupata kipato kikubwa. Hivyo ndani ya hiyo unayofikiriunkuwa ni kujitafutia umaarufu kuna element ya kutaka kupata uhuru wa kujitafutia kipato kwa ajili ya Zanzibar directly kwani wanajuwa kuwa kipato hicho kitawapa fungu kubwa zaidi kama ilivyo kwa wenzao wa Bara.
Kelele unazozifikiri kuwa za kujigamba zinaweza zikawa ni harakati za kweli za kuondokana na hali ya sasa hivi iliyozingirwa na kunyimwa fursa na njia zile zile zinazotumiwa na wenzao Bara kujipatia kipato cha Zanzibar ambapo wao watakuwa na mgao mkubwa.
 
kama hamuamini wazanzibari wamechoka kutawaliwa na Muungano here is the litmus paper, just wapeni fursa wafanye uchaguzi huru wa viongozi wanaowataka, naaapa kwa dini jina la Mungu mmoja, kitu CCM kitakuwa history zanzibar.
 
kama hamuamini wazanzibari wamechoka kutawaliwa na Muungano here is the litmus paper, just wapeni fursa wafanye uchaguzi huru wa viongozi wanaowataka, naaapa kwa dini jina la Mungu mmoja, kitu CCM kitakuwa history zanzibar.

Hapo umawakanyaga kwenye donda ndugu 😀 watapita wakilalamika njia nzima.
 
Nafurahi kuwa unakubali kurudi nyuma na kutafakari hiyo kadhia. Sasa nakutaka pia dondoo za kadhia hiyo pia ziwe hadidu rejea yako katika kulijadili suala la mafuta hivi sasa. Nakubaliana na vugu vugu jipya la kudai yote hayo watu wanayodai sasa katika Muungano. Lakini nashindwa kuvumilia kuona wachezaji ambao walikuwemo uwanjani wakati huo unaosema wewe Mwalimu aliendesha hiyo game yake, wanaibuka sasa na kutoa kauli kuhusu kadhia hiyo. Na wakae pembeni kama vile walivyokaa hao wachezajji wengine wakuu (Jumbe , Ramadhan Haji na kadhalika). Wasilitumie suala hili kuendelea kutubabaisha. Lakini mimi na wewe na wenzetu na tuendelee kudai hivi sasa mafuta na yabaki Zanzibar.


Pakacha, uhali gani gani? Kwa hadidu rejea hizo hizo unazotaka wewe hebu fikiria kwa Zanzibar ukiondowa huu umri wetu nani hakufanya makosa katika hali hii tuliyomo sasa ya Muungano? Karume Mkubwa ndiye alieiuza nchi kwa kuhofia kuondoshwa madarakani. Watu kama Seif Bakari waliwauwa wenzao kwa kupinga muungano huu na baadae wao wenyewe walipotanabahi na kuidai haki wakafungwa. Aboud Jumbe aliiuwa ASP na kuipeleka Zanzibar Tanganyika na alipotanabahi akataka kujitowa kwenye muungano nae akaangamizwa.Wazanzibari wenyewe walishangiria kuuliwa ASP baada ya kuona inawabana Kidemokrasia na wakiwaonea choyo Watanganyika, sasa kweli imedhihirii wanaitaka ASP irejee, Seif Sharifu na kundi lake walimsaliti Aboud Jumbe nao walipotanabahi wakapigwa na chini. Marehemu Dr Ali Juma aliwasaliti Wazanzibari kwa nafasi ya Umakamo wa Rais na mungu amempenda hakuwahi kuvuna usaliti wake. Salmini aliwatia uhaini wenzake kwa kudai hadhi na haki ya Zanzibar nae aliishia kivyake. Na hata Karume Mdogo (Amani) alipopewa madaraka akaipeleka Zanzibar Tanganyika na sasa anarudi kiguu nyuma.
SASA nieleze kati ya Wazanzibari ukiondowa Generation hii mpya nani hana mkono wake katika kuifisadi Zanzibar kwa kisingizio cha Muungano na nani mwenye haki na asie na haki katika kuitetea nchi yake? Pakacha mrengu wako pengine ndio waliokosa sifa za kutetea haki za Zanzibar kwa hili la mafuta kwani ni nyie mnaofadhiliwa na hao mnaowaambia kuwa waachane na mafuta yenu. Nina hofu kuwa mrengu wako hamko serious na hili jambo kwani ni nyie mnaowapa uwezo wa kuwa na sauti kwa kitu kisicho chao. Kauli yako ya kubaguwa wapiganaji wa haki hiyo inathibitisha kuwa mnafanya kiini macho kwa Wazanzibari wenzenu. Kinyume cha hayo hebu wachieni Wazanzibari waamue kwa haki katika uchaguzi unaofuata na muweke nguvu ya pamoja katika kudai haki yenu.
 
Pakacha, uhali gani gani? Kauli yako ya kubaguwa wapiganaji wa haki hiyo inathibitisha kuwa mnafanya kiini macho kwa Wazanzibari wenzenu. Kinyume cha hayo hebu wachieni Wazanzibari waamue kwa haki katika uchaguzi unaofuata na muweke nguvu ya pamoja katika kudai haki yenu.
Nakupongeza swahib kwa bandiko lina mengi ya kutukumbusha na kuwaeleza wachangaaji wengine wasiyoijua kadhia ya Zanzibar. Sawa na tuwaachie Wazanzibari waamue kwa haki katika uchaguzi ujao- lakini hiyo ni pamoja na kutotutumia opinion leaders (wazee) kuwatisha na kuwashurutisha watu(hasa vijana- new generation) kule Pemba waipigie CUF. na waachwe huru kabisa. Jengine hao viongozi waliowahi kufanya makosa ndio ninasema tuachane nao - tena kwa mirengu yote. Kwani hivi CUF hawana wengine zaidi ya Seif? au hawapewi nafasi tu. Huo mrengu mwengine wanabadilika kila mara au huoni? Wafanyao makosa hawarudi (Dk. Bilali hakurudi!!!!!!)-ingawa makosa hayakuwa yake ya moja kwa moja.
 
Nakupongeza swahib kwa bandiko lina mengi ya kutukumbusha na kuwaeleza wachangaaji wengine wasiyoijua kadhia ya Zanzibar. Sawa na tuwaachie Wazanzibari waamue kwa haki katika uchaguzi ujao- lakini hiyo ni pamoja na kutotutumia opinion leaders (wazee) kuwatisha na kuwashurutisha watu(hasa vijana- new generation) kule Pemba waipigie CUF. na waachwe huru kabisa. Jengine hao viongozi waliowahi kufanya makosa ndio ninasema tuachane nao - tena kwa mirengu yote. Kwani hivi CUF hawana wengine zaidi ya Seif? au hawapewi nafasi tu. Huo mrengu mwengine wanabadilika kila mara au huoni? Wafanyao makosa hawarudi (Dk. Bilali hakurudi!!!!!!)-ingawa makosa hayakuwa yake ya moja kwa moja.

PAKACHAjamaa yangu usiwe rahisi hivyo wa kujitia mitegoni. Nini kosa la Dr. Bilali? kufuata mkondo wa demokrasia? Hivyo huoni kuwa unapalilia kile unachowakosoa wenzako? Kwa hatuwa ya mwanzo nani alikuwa chaguo la Wazanzibari kwa mujibu wa katiba yenu? La pili kwanini mlikubali kuteuliwa mtu aliekuwa si ridhaa yenu? La tatu nyinyi ni chama chenye demokrasi kubwa,iweje mumuone Dr Bilali kuwa ni mkosa kwa kufuata taratibu mlizojiwekea? Na kama mmeshampa mtu miaka mitano na akashindwa kuiongoza nchi kwa nini mkazanie abaki tu eti amalize miaka kumi? Hii si sawa na watani wenu CUF wanaomweka mtu huyohuyo kwenye chaguzi zote?
Kuhusu suala la kubadilisha viongozi naona bado hamjafanya hivyo na kinachofanyika ni kuwa mtu akishapewa urais miaka kumi katiba inamzuia kuendelea kinyume cha hivyo mgekuwa mkiendelea na hao hao. Hebu niambie kina Ali Ameir, Mohammed seif khatib na wengine mnawangojea wafe madarakani kwa vile hamna wengine wa kuchukua nafasi zao?
Nakushauri jamaa yangu muache kupanga nani ni mzanzibari zaidi ya mwengine ili mfanikiwe katika harakati za kudai haki zenu.
 
Tatizo la Zanzibar ni kuwa ile jamii yenyewe bado haijajikomboa. Uchaguzi ni kweli hauwi huru -kwa maana ya huru- Wengi wa wapiga kura hawapigi kura kwa mujibu wa ridhaa zao. Hii kwa pande zote wanaoipigia CUF na wanaoipigia CCM. Wapiga kura wanapiga kura kutekeleza misimamo inayowekwa na hao "opinion leaders" (wazee) Na ndiyo maana ya CUF kushinda siku zote Pemba- na CUF hiyo kushindwa kuambulia kitu Kaskazini Unguja na Kusini Unguja. Sasa nafikiri tuwe na system ambayo itafanya wapiga kuira(hasa hao new generation) kuwa huru kweli. Lile suala la nguvu ya Dola si la kweli Bwana. CUF hawana nguvu ya Dola -kwa nini wanashinda Pemba?
 
Back
Top Bottom