Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

nimekupata mkuu, ila bado nina tatizo, nalo ni je rais, na uongozi wa serikali ya muungano si jambo la muungano! kama jibu ni ndiyo, kwa nini wanapotekeleza wajibu wao inachukuliwa si kwa niaba ya wazanzibari, mpaka washirikishwe, na kama jibu ni hapana kwa nini wanapiga kura kumchagua raisi? nauliza hivyo kama layman wa constitutional law, japo natambua kwamba kutojua vifungu haitoshi kutokufanya uchambue mambo kimantiki.

uzuri umekubali kwamba muungano una matatizo, kama mimi ninavyoamini ndiyo maana napata shida ku-digest haya ninayojadili


Habari ndio hio Mkuu,


,"Without any question, the manner and the implications of the union between Tanganyika and Zanzibar is the most misunderstood aspect of Tanzania's political development. It may not matter very much when foreigners get confused, but unfortunately there are many times when Tanzanians themselves appear to misunderstand" - JK Nyerere.
 
Da hata mimi umenichanganya, nafika mwisho nimesahau mwanzo! Tukitengana ccm inapoteza wabunge kama 40 toka visiwani. Watakomaje?
 
Da hata mimi umenichanganya, nafika mwisho nimesahau mwanzo! Tukitengana ccm inapoteza wabunge kama 40 toka visiwani. Watakomaje?

Kumbee, nahisi na wao CCM unawachanganya akili ndio maana hadi leo hawajui wafanye nini wanaukingia kifua tu!
 
[quote="theophilius,

Mkuu.
Huyu rais ana kofia mbili ni rais wa Muungano, lakini wakati huo huo ni Rais wa Tanganyika.
Usijichanganye wala usikubali kuchakachuliwa. Kabla ya kutoa jibu la suali lako gumu, nikuchukue kabla ya Muungano.
Nani alikuwa rais wa Tanganyika? Nyerere
nani kwa upande wa Tanganyika aliingia mkataba na rais wa Zanzibar?...Nyerere.

Nani alitayarisha hati za muungano?...... Mwanasheria mkuu wa Tanganyika kwa idhini au amri ya Nyerere.

Je Tanganyika na Zanzibar waliunganisha kila kitu au kila jambo? Jawabu ni hapana. sasa kama ni hivyo yale mambo ya Tanganyika yaendeshwe na Nani? Rais wa Tanganyika au vipi? Hapa ndio unaipata dhana ya kuvaa kofia mbili.

Je Muungano una haki au mamlaka ya kuifuta serikali ya Tanganyika au Rais wake? muungano hauna mamlaka hiyo.
Muungano ni kiumbe wa Tanganyika na Zanzibar, bila ya hawa hakuna Muungano. sasa vipi tena baada ya Muungano mmoja apotee?....ukiwa na jibu la kitandawili hiki basi umeondoa utata wa muungano huu.

sasa wacha nichangie juu ya suali uliloliuliza.

Mkuu. Urais wa muungano ni taasisi ya muungano.
Lakini kwa bahati mbaya hakuna mipaka ya kueleweka baina ya mambo ya Tanganyika na mambo ya Muungano. Yote yamechanganywa katika kapu moja. na kwa hiyo, wanatenda mambo kwa kuboronga tu, ubabe na kubahatisha bahatisha. Vile mtu anavyotafsiri mwenyewe na kama hatapata kuulizwa au kuwekewa kipingamizi hujihisi ametenda sawa.

Lakini ugumu unaongezeka yanapokuja masuali ambayo moja kwa moja yanagusa ubia, mamlaka ya Zanzibar moja kwa moja. Kama katiba ya Muungano.

katiba ya Muungano ni zao la hati(mkataba) ya Muungano kwa hiyo inahitaji majadiliano ya Tanganyika na Zanzibar kwa pamoja. Muungano hauwezi kujiundia mamlaka ambayo haukupewa na Tanganyika na Zanzibar.

Nani anatoa mamlaka kwa Muungano? Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar. Hawa kupitia majadiliano wanaweza kuongeza au kupunguza mamlaka ya Muungano wa Tanzania....sasa kazi ipo hapa..serikali ya Tanganyika inapokuwa imeji-dissolve kienyeji nani watakaa kujadiliana? ndio tunaishia kuwa huu si muungano...ni "Changa la Macho", "mazingombwe" ausanii at its best!
 
mkuu maswali yako ni mazuri sana-cha ajabu viongozi wetu hawataki kuiachia zanzibar-yaan mi ni moja ya vitu ambavyo sivipendi na vina nishangaza sana-sijui kwa nini wa-zenji tunawahusisha kwenye mambo yetu-
kuna baazi ya viongozi wanadai eti kwa sababu za kiusalama ndo maana zenji wanaikumbatia-hivi jamani kwani Kenya na Uganda zipo mbali na Tanzania? Kweli hii nchi haina viongozi
 
Hakuna kosa kubwa nyerere alilofanya kama kuleta huu mungano, kuliko hata siasa za ujamaa, kwa sababu moja kubwa ni kuwa Tanganyika imetoka kwenye ukoloni halafu ikawa mkoloni.
Sasa kitu kingine ni kuwa tunafanya makosa makubwa kuona kuwa wazanzibari wanafaidika na huu muungano, ukweli ni wachache ambao ni wafanya biashara na wanasiasa, sasa hao ndio wanaofanya muungano uendelee.
Tunaitaji kiongozi mwendawazimu kuuvunja, sio wanafiki
 
mhhhh .sijui kama wapemba walio jenga huku bara na biashara zao itakuwaje, pili umeme,vyakula nk vinatoka bara,tukiwakatia itakuwaje?wale kule hawana jeshi na hawa viongozi walio huku watafanyaje? itabidi pia zanzibar ife kuwe na pemba na unguja sijui dr shein wa pemba atakuwa rais wa wapi na unguja atatawala nani.ni ngumu lakini kuvunja muungano wkt CCM inamuandaa DR Mwinyi kugombea 2015.hbr ndio hiyo.

Mkuu.
Unaongea kama vile Zanzibar haikuwepo kabla ya Muungano.
Kama Zanzibar haikuwepo au haikuwa ikijiendesha yenyewe kabla ya muungano utakuwa uko sahihi katika usemayo.

Kama Zanzibar ilikuwepo na ilikuwa inafanya biashara na nchi nyengine basi sioni kama itakuwa ni tatizo ikitokea Muungano kuvunjika.

Unakumbuka soviet Union....nchi nyingi zimeibuka baada ya umoja huu kuvunjika. zenyewe zinajiendesha na zina mahusiano na Russia mpya. Wengine wananunua gesi kutoka Russia kukidhi mahitaji ya nishati katika nchi zao.

Wapo watanzania wana majumba UK, US, Dubai, wengine wazee wa vijisenti wana fedha katika benki za nje. Kwa hiyo hii pia si issue ya kuogopesha watu.

Kama unafuatilia Dubai investments wao wanajenga properties na kuziuza kwa wageni,katika nchi nyingi wanakaribisha wageni kununua makaazi katika nchi zao...ni biashara. na hao wenye majumba au biashara nyengine watakuwa na uamuzi wa kuendelea na bishara au kufunga biashara zao kulingana na mazingira. wakiamua watauza majengo yao na kuelekea kule wanakoona kunafaa, au naturalisation ya uraia pia ni jambo ambalo linaweza kufanyika.

Hapa ndio inakuwa ni muhimu na jambo bora muungano kama utavunjika, uvunjike kwa salama na sio kwa vita. Kura ya maoni ndio njia ya salama zaidi. Mambo huwa yanajadiliwa kabla kulingana na kura ya yes au no. na kunakuwa na mipango ya utekelezaji kulingana na matokeo ya kura hiyo ya maoni.

Tatizo lipo kwa hao viongozi ambao hawaoni mbali.
 
huyu aliyeleta hii ramani Unimaps.com - Tanganyika & Zanzibar, 1886 sikubaliani nayo. kama muungano ukivunjika & i pray for that nchi zitarudi kama ilivyukuwa kabla ya muungano.

binafsi mimi ni mzaliwa wa tanga tena kwetu ni vile vijiji vilivyo katika pwani ya bahari ya hindi kuelekea mombasa barabara ya horohoro ukisimama pwani ya kijiji chetu pemba unaiona ileee!... na sidhani kama tukiletewa kura ya maoni ati tangayika au znz! kamwe hatuwezi tukachaguwa znz. wazee wangu wengi wa pale kijijini wanayemfahamu ni nyerere hawana historia wala ufahamu wowote kuhusu znz.. iweje leo hii mje muwaambie kwamba wao ni wa znz! this must be JOKE!
 
huyu aliyeleta hii ramani Unimaps.com - Tanganyika & Zanzibar, 1886 sikubaliani nayo. kama muungano ukivunjika & i pray for that nchi zitarudi kama ilivyukuwa kabla ya muungano.

binafsi mimi ni mzaliwa wa tanga tena kwetu ni vile vijiji vilivyo katika pwani ya bahari ya hindi kuelekea mombasa barabara ya horohoro ukisimama pwani ya kijiji chetu pemba unaiona ileee!... na sidhani kama tukiletewa kura ya maoni ati tangayika au znz! kamwe hatuwezi tukachaguwa znz. wazee wangu wengi wa pale kijijini wanayemfahamu ni nyerere hawana historia wala ufahamu wowote kuhusu znz.. iweje leo hii mje muwaambie kwamba wao ni wa znz! this must be JOKE!
hio ramani ni ya zamani sana-then naamini tanganyika hawawezi kukubali kuwaachia zenji pande hizo zote-naamini hata kwa vita tutapigania ardhi yetu
 
mkuu maswali yako ni mazuri sana-cha ajabu viongozi wetu hawataki kuiachia zanzibar-yaan mi ni moja ya vitu ambavyo sivipendi na vina nishangaza sana-sijui kwa nini wa-zenji tunawahusisha kwenye mambo yetu-
kuna baazi ya viongozi wanadai eti kwa sababu za kiusalama ndo maana zenji wanaikumbatia-hivi jamani kwani Kenya na Uganda zipo mbali na TZ?Kweli hii nchi haina viongozi

Binafsi naona kuna sababu nyingine labda za msingi ambazo may be viongozu wa CCM wanazilinda ndio maana wanakumbatia huu muungano, hata kudiriki kutaka suala lake lisijadiliwe kwenye katiba mpya!

Watu hatuuongei tu huu muungano is a pain in the ass!
 
Hakuna kosa kubwa nyerere alilofanya kama kuleta huu mungano, kuliko hata siasa za ujamaa, kwa sababu moja kubwa ni kuwa Tanganyika imetoka kwenye ukoloni halafu ikawa mkoloni.
Sasa kitu kingine ni kuwa tunafanya makosa makubwa kuona kuwa wazanzibari wanafaidika na huu muungano, ukweli ni wachache ambao ni wafanya biashara na wanasiasa, sasa hao ndio wanaofanya muungano uendelee.
Tunaitaji kiongozi mwendawazimu kuuvunja, sio wanafiki

Mkuu naunga mkono, na sisemi kwamba naona wanzanzibar ndio wanaofaidika hapana, ila naona kwamba Zanzibar wanapewa VETO kwenye mambo ya bara (sio Tanzania) wakati bara hatupewi, hapo natatizika.
 
Hata wakati wa uhuru wa Marekani 04/07/1776 State zilizo kusini mwa USA ambazo zilikuwa zinajihusisha na shughuli za Kilimo wakati huo hazikutaka kuwa ndani ya USA, zilitaka uhuru wa kwao nje ya USA lakini zililazimishwa na watawala waliokuwepo kipindi hicho.
Chanzo tafadhali.
 
Binafsi naona kuna sababu nyingine labda za msingi ambazo may be viongozu wa CCM wanazilinda ndio maana wanakumbatia huu muungano, hata kudiriki kutaka suala lake lisijadiliwe kwenye katiba mpya!

Watu hatuuongei tu huu muungano is a pain in the ass!
naomba hii nchi ipate kiongozi ambaye atakuwa tofauti na wengine ili hili swala la muungano aje alifanyie kazi-ili huu muungano ufe
 
naomba hii nchi ipate kiongozi ambaye atakuwa tofauti na wengine ili hili swala la muungano aje alifanyie kazi-ili huu muungano ufe

Halafu Swali ni kwamba; Sasa kama tuna wawakilishi/ wabunge kutoka Zanzibar kwenye bunge letu la Muungano, kuna haja gani tena kutaka Bunge la Zanzibar lihusishwe tena katika maamuzi....wakati bunge letu halihusishwi katika bunge (baraza la wawakilishi) la Zanzibar!
 
Majibu ya maswali yote yatapatikana iwapo Tanganyika Italivua Koti la Muungano.

Matatizo ya muungano huu nimefuatilia kwa kina na mijadala yake,kitu ambacho nimekiona mkanganyiko wa mambo ulianzia pale Tanganyika ilipo jufuta kimnya kimnya na kujigeuza kua Tanzania.

Hebu ndugu muuliza masuali Jaribu kujaalia kua Tanganyika ipo leo na zanzibar ipo halafu tukawa na kitu cha muungano yani Tanzania,halafu Tanganyika ikafanya mambo yake binafsi kama ilivyo Zanzibar leo,na Tanzania ikashuhulika na Mambo ya muungano tu,Je ungali jiuliza maswali hayo leo?

Na huo mfumo niliokueleza ndio mkataba wa muungano ulivyoelekeza,haukusema kabisa kua baada ya muungano Tanganyika au na pia Watu wanapaswa kufahamu kua Muungano haukua wa mambo yote bali ni baadhi tu ya mambo.

Hapa ndio Maana wazanzibari hadi hii leo wanachojua nikua Tanzania ni Tunda la Muungano,Ndio maana wanataka kilichomo ndani ta tunda wakigawe sawa sawa.
Ama kosa lililofanywa na watanganyika wenyewe lakijiingiza ndani ya KOTI (MUUNGANO) na kujigeuza jina na kijifanya wao(Tanganyika) ndio Muungano na muungano ndio wao(Tanganyika),hili wazanzibari hatutaki kulijua tunachojua ni makubaliano yetu tu yaliomo ndani ya mkataba wa muungano.

Nikisema makubaliano ninamaana ya liokubaliwa na nchi mbili yani Tanganyika na Zanzibar sio yaliobadilishwa na Bunge la Tanganyika lililojibadilisha jina na kujiita Bunge la Muungano.

Wito wangu kwa Watanganyika waanze harakati za kuidai nchi yao kwanza halafu ndio tufikire tena kama iko haja ya kuungana au tukakutane Muungno wa Af.Mashariki.
 
Wana JF, nakwazika na saa zingine nasikia kupata wehu na mambo kadhaa ya Jamuhuri yetu ya Muungano. Naomba mnisaidie majibu au kutoa hoja na mwelekeo katika haya yafuatayo:
1. Tangayika na Zanzibar (nchi mbili) ziliungana na kutengeneza nchi mbili, Tanzania na Zanzaibarhii inawezekanaje??? marais wawili?? Katiba Mbili? tena kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar iliyofanyiwa marekebisho mwaka jana, Zanzibar ni nchi huru yenye mipaka yake?
Tangu 1964 hapajawahi kuwa na nchi moja kwenye huu Muungano. Wazanzibari tukijuwa kuwa kuna zanzibar na Tanganyika na kiongozi wetu mkuu Karume alishakataa Azimio la Arusha na kusema mwisho chumbe! Wimbo wetu wa Taifa tukiutambua kuwa ndio wimbo wa Taifa, na viongozi wa nje tukiwapokea kwa heshima zote za kitaifa. Tulikuwa tukitumia bendera yenye jembe kila sehemu ya serikali. Hapo nafikiri utaelewa kuwa nchi ni mbili na hivyo ndivyo tulivyokubaliana!

2.Tanganyika iko wapi katika Muungano au Watanganyika (kama sehemu mojawapo ya muungano) tunatambulika au kuji-identify wapi katika Muungano?
Tanganyika mliamuwa kujiita Tanzania na majina yote mliyabadilisha na kuwa Tanzania. Zaidi ya mabadiliko ya jina hakuna kilichobadilika. Rais, Waziri Mkuu, Bunge, mahakama,jeshi na kila kitu hakijawahi kubadilika. Hata Mzanzibari (kwa jina) alipopewa urais alipewa urais wa Tanganyika. Hapo mwanzo Makamo wa Rais alikuwa akishughulikia mambo ya Zanzibar lakini Tanganyika mkaona hata yeye awe Makamo wa Rais wa Tanganyika. Kimipaka nafikiri bado ni ile ile na ndio sehemu inayoshughulikiwa na Rais na Taasisi zake na Bunge!
3. Je kipi ni sahihi kutamka au kutambulika kati Tanganyika na Tanzania bara??
Sahihi kutamka ni Tanzania na wala sio Tanganyika au Tanzania Bara kwani Tanganyika ilishabadili jina na kuitwa Tanzania bara ingekuwa sahihi kama kungekuwa na Tanzania mbili. Kuna Zanzibar na Tanzania tu.
4. Najua kwenye hesabu inawezekana 1 + 1 = 2 lakini huwezi kuunganisha nchi mbili ukapata nchi mbili, hapa si hakuna muungano??? Au sisi ni shirikisho?
Kwa hesabu za Kitanzania na muungano wao ni sahihi kwa 1+1= 2 kwani tumezoelea utopian (nadharia).
5. Katika kuandika katiba, katiba ya WAZANZIBAR iliandikwa na wao wenyewe tena na referendum yao wenyewe bila kuhusishwa Tanzania bara. Sasa sisi wa bara tunapotaka kuandika katiba kwanini iwe ndio katiba ya Muungano pia???
Sababu ni kuwa bado hamjakuwa tayari kujivua Gamba na kusema wazi kuwa nyie ni Tanganyika ndani ya Gamba la Tanzania. Sasa unapovaa gamba inbidi ushirikiane na wale uliowavalia gamba lao. Lengo la Muungano wa Tanzania lilikuwa usawa kwa nchi zote lakini hili la kujitwallia madaraka yote ni uvaaji wa Gamba!
6. Watanganyika tuna haki gani katika muungano kuandika katiba yetu wenyewe kwanza (inayotuhusu sisi na watu wetu hao zaidi ya Million 40) kabla ya waZanzibari kuhusishwa??? NAONA TANGANYIKA TUNAINGILIWA NA KUNYIMWA HAKI YA KUTAMBULIKA (KAMA SEHEMU MOJAWAPO YA MUUNGANO) KULIKO HATA MNAVYOFIKIRIA?
Watanganyika hamuingiliwi bali mnajipendekeza kwa Muungano. Kama mliweza kuwafanya CCM wajivue magamba kwanini gamba hili nalo hamlilazimishi kuvuliwa. Naomba ujiulize kwenye makelele haya mengi ya Katiba nani (labda Mbatia) anaesema kuwa Katiba kwanza iwepo ya Tanganyika kabla ya Muungano? Kelele ni ohh wawakilishi wa Zanzibar wasiwe sawa na wa Tanganyika, hii inaonyesha mtizamo wa kuidai Tanganyika? Halafu hamkosi kitu kwa kujibadilisha jina.
7.Kwanini ya ZANZIBARI yawahusu ZANZIBARI TU na ya Hayatuhusu WABARA,wakati ya BARA yawahusu WANZANZIBARI??? au ndio mambo ya chako changu, changu changu??
Hivyo sivyo hata kidogo. Toka lini Zanzibar ikahoji mambo mnayofanya? Mbona mnahoji na mnataka kuidhamini Zanzibar katika mikopo? Halafu kule bungeni mbona mambo yote yanayozungumzwa ni ya huko tu? Na hata hotuba ya Rais hata zile za mwisho wa mwezi huwa zinahusu huko tu?/ Kiko wapi hicho cha ya bara kuwahusu Wazanzibari?
8. Inakuaje Rais wa Muungano ndio rais wa Bara (Tanganyika - ambayo haipo) tena ni Rais wa Zanzibar pia?? hapohapo eti Wazanzibar Wana Rais wao tena????
Bwana mdogo Rais wa Zanzibar ni mmoja tu na Rais wa Tanzania si Rais wa Zanzibar bali Rais wa Tanzania ni Rais wa Tanganyika. Kihesabu Tanganyika kama kawaida ndio wanaonufaika kutumia Tanzania na sio wazanzibari hata katika hili la urais.
9. Inakuaje Tanzania ndio Tanganyika pia???? yaani hata sijui nauliza nini nahisi naanza kuchanganyikiwa???
Hapo juu ulishasema hiyo ndiyo changu changu chetu changu! Kama hali hii bado inawaridhisha basi hizo ni silka.

10. Kama sisi ni muungano kwanini Wazanzibar wampigie kura Rais Wetu (wa bara) na sisi hatumpigii kura kumchagua Rais wao (zenji)????? Huu ni muungano wa aina gani huu???? muungano nusu (partial) au????
Bado unarudu kule kule mdogo mpe pipi ili alale mkubwa afanye atakavyo.
11. Hivi sasa naambiwa KATIBA YA ZANZIBAR NI KINYUME NA KATIBA MAMA YA MUUNGANO na ETI pia kutokana na marekebisho ya KATIBA YA ZANZIBAR ya Mwaka jana HUU MUSWADA wetu wa katiba ni batili HIYO PIA ni kwa mujibu wa KATIBA YA JAMUHURI YA MUUNGANO kwa kuwa haujahusisha Baraza la wawakilishi la Zanzibar na Rais na Mwanasheria wau sijui......Hapa nahisi haya mambo yanazunguka katika duara la kizungu zungu (in cycles) na yaani inakua ni kama ile ishu ya nani alianza kati ya kuku na yai na ndipo hunifanya nijione kama akili yangu imefika mwisho wa kufikiria...which is which jamani????
Kwani kilichoanza ni kipi? kuwepo kwa Zanzibar na baadae ndio kuja Muungano au kulianza Muungano na baadae kukazaliwa Zanzibar? Jawabu ni kuwa Zanzibar ilianza na hapo ndipo neno mama linapokuja. Mtoto hawezi kumzaa mwana. Nionavyo mimi kama Tanganyika kwa jina jipya mlilolichukuwa ndio utaifa wenu ulianza hapo basi hiyo Katiba ya Muungano itakuwa Katiba mama kwenu kwani utaifa wenu ulikuja kwa Katiba hiyo. Hali ni tafauti kwa Zanzibar kwani kwao Katiba ya Zanzibar ni Katiba mama kwa vile utaifa wao haukufutika. Kufanya mabadiliko ni sawasawa na mtindo wa dada zetu kutafuta wigi kuondowa nywele wanazozioneya haya!
12. Haya yote ya muungano ambayo na Zanzibar inahusika yananichanganya akili sana naweza kuchanganyikiwa mwenzenu! Je sisi (Tanzania Bara) tunaweza kutumia utaratibu gani utakao tuwezesha kuandika katiba yetu wenyewe kwanza kabla na waZanzibar kuhusika?
Watanganyika hamjawahi kufanya kitu na Wazanzibari wakakuzuieni. 55 haikuzuiwa na Wazanzibari bali aliezuia ni Baba wenu wa Taifa. Isitoshe Wazanzibari mbona wameshaanza harakati za kutaka mjivue Magamba lakini kwa hili si CCM si CHADEMA nyote mnalingangania gamba!
13. Nashindwa hata kuendelea sijui hata niulize nini, yaani sijui????

14. Wakati hapo hapo kuna ANGALIZO hili hapa chini (alilolisema Nyerere) nalinukuu...
"....On april 26, 1964, two independent African states surrendered their sovereignty to one New country - the United Republic of Tanzania......"
Pengine alikuwa sahihi kuwa nchi mbili zilitowa sovereignity kwa nchi moja mpya (Tanganyika ilijibadilisha jina. Nikifikiri naona hakukosea kwani nchi mbili hizi kilichotolewa muhanga ni sovereignity basi lakini nchi ziliendelea kuwepo. Katika kupoteza sovereignity Zanzibar ndiyo ilipata hasara kwani Tanganyika ilivaa Gamba na kujinyakulia hiyo sovereignity iliyoacha na Zanzibar na Tanganyika. Ni kizungumkuti kikubwa mmoja anapojidai kujilsha kitu kwa kutumia Gamba!
......naona kwa mujibu wa marekebisho ya katiba (ya Zanzibar - 2010) Zanzibar washajichululia 'SOVEREIGNTY' yao Sisi Bara tunasubiri nini????
Hadi sasa bado hawajaipata bali walichofanya ni kuwakumbusha waliovaa Gamba kuwa Zanzibar bado ni nchi na waliovaa Gamba hawataki kutoka kwenye Gamba kwani kufanya hivyo hiyo sovereignity wanayotumia peke yao itabidi apewe Tanzania ya kweli na iwe inagawiwa sawa kwa wote. Hilo wavaa Magamba hawataki!
15. Yaani hata sijui, hivi naruhusiwa kujadili muungano au siruhusiwi???...

Msaada wenu jamani!......

Wew wakikluruhusu au wasikuruhusu ujadili tu ama kwa Wazanzibari kwao ni ruhusa kuujadili.
 
Halafu Swali ni kwamba; Sasa kama tuna wawakilishi/ wabunge kutoka Zanzibar kwenye bunge letu la Muungano, kuna haja gani tena kutaka Bunge la Zanzibar lihusishwe tena katika maamuzi....wakati bunge letu halihusishwi katika bunge (baraza la wawakilishi) la Zanzibar!

Kama unakusudia kwenye Katibahii inayojadiliwa mtalazimika iwe hivyo hadi pale mtakapojivua Gamba la Tanzania na kusema tunaunda katiba ya Tanganyika na hilo ndugu yangu hamko tayari hata siku moja.
 
Back
Top Bottom