Muungano wetu: Mgao wa Fedha za IMF na Zanzibar kupewa asilimia 18, ni sahihi?

Muungano wetu: Mgao wa Fedha za IMF na Zanzibar kupewa asilimia 18, ni sahihi?

Weka hapa huo mkataba wa Muungano.Pili unaelewa maana ya kero za Muungano? Na je mkataba ni biblia au msahafu?

Mwisho Zanzibar sio Mkoa ni Nchi na pia ni sehemu ya JMT kwa hiyo ina haki zote na tena haki zaidi ya Mkoa.
Haki zipi sasa? Mtaalamu amesema 21% na 30% sio halali yenu, nyie ni 4.5%, je ni kweli?
(230/1300)×100 = ???
 
Hivi karibuni, kuna taarifa zilizowekwa wazi kwenye baadi ya vyombo vya habari, juu ya mgawanyo wa mikopo ya nje, kati ya Tanzania bara na Zanzibar.

Mkopo wa pesa ya Uviko 19, tunaambiwa Zanzibar ilipata 21%. Mkopo wa kutoka Japan, tunaambiwa Zanzibar imepata 30%.

Mkataba wa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, umeweka wazi kanuni ya mgawanyo wa mikopo na misaada kutoka nje, ambapo Zanzibar inastahili kupewa 4.5%.

Kama ni kweli Zanzibar ilipata 21% badala ya 4.5%, na pia ilipata 30% badala ya 4.5%, waliohusika wote, wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Katibu Mkuu Wizara ya fedha, walistahili wasimamishwe mara moja, na kama tungekuwa na Bunge, lilistahili kuunda kamati kuchunguza ukweli wa jambo hili, na kuchunguza uhusika wa Rais katika ukiukaji huu wa kanuni za Muungano.

Jambo la kujiuliza:

1) kwa hali hii ya sasa, ambapo nchi haina bunge linalowakilisha wananchi, nani ataihoji serikali?

2) kama trend itaendelea hivi, mpaka kufikia 2025, hali itakuwaje?

3) kama hiki ndicho kinachoendelea, hatuoni kuna njama za kuitumia Tanganyika kuijenga Zanzibar, na kuifanya Tanganyika kuwa 'kubwa jinga?'

4) Hali ikiendelea hivi, na bunge hatuna, nani ataweza kuhoji juu ya jambo hili?

5) Je, hatuoni kuwa kama hali hii ni kweli, mikopo hii inailenga Zanzibar, na Tanzania bara inatumika tu kama daraja, huku kisheria deni likiwa la kwake?

6) Japo hatuombei, kama kukiwa na njama ambazo zikafanya siku moja Muungano ufe, hatuoni hasara itakayokuwepo kwa Tanzania bara kwa sababu madeni haya yote mkopaji ni yeye, na hivyo ndiye atakayewajibika kulipa?
Wazanzibari waliokuwa Tanganyika wameanza kurudi makwao,mizunguko yahela ipo safi, watumishi wa umma huko Zanzibar wanaishi maisha ya peponi huku tanganyika maisha ni magumu mno,mfumuko wa bei chakula,vifaa vya ujenz n.k ni juu.Zanzibar hawalimi lakin maisha kwa sasa ni murua.Acha tupigwe wajinga wengi mno.
 
Zanzibar sio Mkoa ni Nchi na pia ni sehemu ya JMT kwa hiyo ina haki zote na tena haki zaidi ya Mkoa.
Hakuna aliyesema Znz haina haki, ila kuhusu mikopo na misaada kutoka nje haki ya Znz ni 4,5%.
Huwezi kuwapa 30% watu 1m na 70% watu 60m. Huo ni wizi na unyang'anyi jamani.
 
Iwe pasi kwa pasu, si mna upenda muunga o??
 
Hakuna aliyesema Znz haina haki, ila kuhusu mikopo na misaada kutoka nje haki ya Znz ni 4,5%.
Huwezi kuwapa 30% watu 1m na 70% watu 60m. Huo ni wizi na unyang'anyi jamani.
Hakika, kinachofanyika sasa ni kutafuta hasira za Watanganyika, na huenda inafanywa makusudi.
 
Kwani Tanganyika iko wapi? Mbona siioni kwenye Atlas, siioni kwenye ramani ya dunia, siioni Google Maps. Iko wapi hiyo Tanganyika inayozungumziwa kila siku humu ndani?
 
Kwani Tanganyika iko wapi? Mbona siioni kwenye Atlas, siioni kwenye ramani ya dunia, siioni Google Maps. Iko wapi hiyo Tanganyika inayozungumziwa kila siku humu ndani?
Tanganyika ndiyo Tanzania. Na hilo limekuwa sababu mojawapo ya malalamiko ya Wazanzibari kuwa Tanganyika imevaa koti la Muungano.

Kiuhalisia, Tanganyika ndiyo Tanzania lakini ndani ya hiyo inayoitwa Tanzania, imetoa sehemu ya mamlaka yake kwa Zanzibar, na yenyewe kuendelea kusimamia yale ya Tanganyika.

Kwa ujumla, hata kwa logic ndogo kabisa, huu Mwungano ni utata mtupu. Hata tukichelewesha vipi, kuna siku ama utavunjika au utaboreshwa ili kuleta mantiki.
 
Kumbukeni hili limepata baraka za mkuu wa awamu ya 6 kwa ushirikiano na yule wa zenji
Ndugai kuna kitu alitaka kufikishia umma kuhusu mgawanyo uliopita wa fedha za covd lkn 'akapotea njia'
Wakipata nafasi ya kuongea akina ndugai, polepole na wengine hali itakuwa mbaya sana
 
Kiukweli hivi sasa zanzibar inajengeka asee tuache utani, mfano dr. Mwinyi ameamua waunguja wawe wafanyabiashara na anajenga masoko matatu makubwa yote kwa mkupuo tena yenye kiwango kama lile la Kisutu, magomeni au zaidi ya hayo.

Kuna soko linajengwa Mwanakwelekwe, Kwa nyanya na lingine Jumbi njia ya kwenda tunguu, ukiachilia mbali yale maduka pale darajani ukiangalia ujenzi huu wa mkupuo unaweza usielewe ila kwa ndani unawaza je, fedha za miradi hii inatoka wapi?.

Unaweza sema kuna bandari na ile peaa ya mrahaba wa wawekezaji wa mahoteli ila, kiukweli ile pesa ni tone tu katika maendeleo yoyote ya nchi inayoamua kujenga na kuwekeza miradi mikubwa kwa mara moja.

Pesa za uviko 19 je?.
usilolijua ni bora uulize masoko yote hayo ni PPP ambapo wawekezaji binafsi wanafanya. Miradi ya bandari Mamngapwani na Malindi pia inajengwa kwa PPP na Mamlaka ya Uwekezaji ya Oman. Mradi wa Darajani ni uwekezaji wa Kampuni ya AFRICAB ya wazawa. Ni kweli kwa sasa Zanzibar kuna miradi mingi ipo katika Planning Stage lakini asilimia kubwa ni ya uwekezaji binafsi wa ndani na nje ya nchi. Miradi hiyo mchango wa Serikali ni mdogo sana
 
Hili swala ndio lililomtoa Ndugai kwenye Uspika...CCM mlifurahi sana kubaki na bunge la ndio Mzee ona sasa maumivu tunayaonja wote.
 
Tanganyika ndiyo Tanzania. Na hilo limekuwa sababu mojawapo ya malalamiko ya Wazanzibari kuwa Tanganyika imevaa koti la Muungano.

Kiuhalisia, Tanganyika ndiyo Tanzania lakini ndani ya hiyo inayoitwa Tanzania, imetoa sehemu ya mamlaka yake kwa Zanzibar, na yenyewe kuendelea kusimamia yale ya Tanganyika.

Kwa ujumla, hata kwa logic ndogo kabisa, huu Mwungano ni utata mtupu. Hata tukichelewesha vipi, kuna siku ama utavunjika au utaboreshwa ili kuleta mantiki.
Ramani gani hiyo inaonyesha Tanganyika ndiyo Tanzania? Au ni wapi Tanganyika inatambulika kama Tanzania? Tanganyika siioni kwenye ramani popote pale.
 
Ni bora tutengane tu,kwenye masuala ya ulinzi kama itakuwa lazima basi ndio tuwe na makubaliano!
50/50 wakati mdanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar na mzanzibar anaweza kumiliki ardhi Bara!
Kichekesho nyinyi watu wa maajabu sana. kitu usichokijuwa ni bora kufanya uchunguzi ili kuwa na uhakika na unachokisema. Mmeimbishwa uongo na nyinyi mmekuwa mkiurudia mpaka mnauamini kuwa ni ukweli. Zanzibar ardhi yote ni ya Serikali. Mzanzibari anapatiwa hati ya matumizi ya ardhi ya kulima, kujenga na shughuli za uzalishaji wa kawaida. Uwekezaji mkubwa inabidi aombe kukodishwa ardhi ambayo atalipa kodi kila mwaka Serikalini. Hivyo hivyo kwa mgeni anaekuja kuwekeza nakodishwa ardhi kwa malipo kwa muda aliokubaliwa kwa kujibu wa sheria zilizopo. Halafu mnajiwa kuwa Mtanzania yoyete anaweza kuwa Mzanzibar akiamua kufanya hivyo? anachotakiwa aishi Zanzibar miaka 5 na kuomba ndio maana Mhe. Ali Hassan Mwinyi amekuwa Mzanizbari na Rais wa Zanzibar. Kwa hiyo kama hoja ni ardhi nenda kaishi Zanzibar ili upate hiyo ardhi inayokutoa roho.
 
Hivi karibuni, kuna taarifa zilizowekwa wazi kwenye baadi ya vyombo vya habari, juu ya mgawanyo wa mikopo ya nje, kati ya Tanzania bara na Zanzibar.

Mkopo wa pesa ya Uviko 19, tunaambiwa Zanzibar ilipata 21%. Mkopo wa kutoka Japan, tunaambiwa Zanzibar imepata 30%.

Mkataba wa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, umeweka wazi kanuni ya mgawanyo wa mikopo na misaada kutoka nje, ambapo Zanzibar inastahili kupewa 4.5%.

Kama ni kweli Zanzibar ilipata 21% badala ya 4.5%, na pia ilipata 30% badala ya 4.5%, waliohusika wote, wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Katibu Mkuu Wizara ya fedha, walistahili wasimamishwe mara moja, na kama tungekuwa na Bunge, lilistahili kuunda kamati kuchunguza ukweli wa jambo hili, na kuchunguza uhusika wa Rais katika ukiukaji huu wa kanuni za Muungano.

Jambo la kujiuliza:

1) kwa hali hii ya sasa, ambapo nchi haina bunge linalowakilisha wananchi, nani ataihoji serikali?

2) kama trend itaendelea hivi, mpaka kufikia 2025, hali itakuwaje?

3) kama hiki ndicho kinachoendelea, hatuoni kuna njama za kuitumia Tanganyika kuijenga Zanzibar, na kuifanya Tanganyika kuwa 'kubwa jinga?'

4) Hali ikiendelea hivi, na bunge hatuna, nani ataweza kuhoji juu ya jambo hili?

5) Je, hatuoni kuwa kama hali hii ni kweli, mikopo hii inailenga Zanzibar, na Tanzania bara inatumika tu kama daraja, huku kisheria deni likiwa la kwake?

6) Japo hatuombei, kama kukiwa na njama ambazo zikafanya siku moja Muungano ufe, hatuoni hasara itakayokuwepo kwa Tanzania bara kwa sababu madeni haya yote mkopaji ni yeye, na hivyo ndiye atakayewajibika kulipa?
Hivi vitu ndio vilishababisha Ndugai kulazimishwa kujiuzulu Kwa lazima. Ndugai alipojaribu kuhoji ishu za mikopo alionekana ni msaliti. Alionekana msaliti namba moja kwenye chama
 
Weka hapa huo mkataba wa Muungano.Pili unaelewa maana ya kero za Muungano? Na je mkataba ni biblia au msahafu?

Mwisho Zanzibar sio Mkoa ni Nchi na pia ni sehemu ya JMT kwa hiyo ina haki zote na tena haki zaidi ya Mkoa.
Pamoja na haki zote hata ingekuepo ni nchi huru haingeweza kupewa hela nyingi kiasi hicho kwasababu pesa hutolewa kulingana na GDP ya mkoa husika. Kwahiyo Znz isingeweza kupewa kiasi chote hicho cha pesa kwasababu haina uwezo wa kuzilipa
 
Back
Top Bottom