Muwekezaji kutoka Tanzania bara apigwa stop kuanzia January

Muwekezaji kutoka Tanzania bara apigwa stop kuanzia January

Kabla ya mtoto kujiunga na shule kuna sheria za shule anapewa na anasign yeye pamoja na mzazi kukubaliana nazo, sasa kama sheria huziwezi si unamuhamisha mtoto wako shule nyingine, iweje ukubaliane na sheria, halafu baadae uje kugeuka?
 
Necta wanaratibu mitihani tu na si kuwapangia sheria za uendeshaji shule zao na tamaduni zao
Kwenye Hilo la kufungia hiyo Shule wamechemka tena mno wanaanzisha mgogoro usio na sababu uliohitaji hekima ndogo TU kumwambia mzazi peleka mwanao kwingine atakakuwa anashida anatiririka Aya za kurani na kuwrweseka Kwa kuongea kutwa lughaya kiarabu na kushinda msikitini akiswali swala tano
 
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, imeifutia usajili Skuli ya Eden inayomilikiwa na Shirika la Afrika Agape Association kuanzia Januri 3 mwakani.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Wizara kubaini mmiliki wa Skuli hiyo kuendesha Skuli kinyume na sheria, miongozo na kanuni za Wizara.

Akizungumza na wamiliki wa Skuli hiyo huko Shakani Kaimu Mrajis wa Elimu na Katibu wa Baraza la Elimu Zuwena Mataka Hafidh, amesema kumekuwepo malalamiko mbalimbali yaliyowasilishwa na wazazi hali iliyopelekea Wizara kuchukua maamuzi hayo.

Ameyataja baadhi ya malalamiko hayo ni pamoja na Wanafunzi wa kislam kutosomeshwa somo la dini ya kislaam na kiarabu, kulazimishwa kujifunza dini ya kikiristo, kutotakiwa kufunga katika mwezi mtukufu wa Ramadhan na Wanafunzi kutoruhusiwa kuvaa hijabu.

Malalamiko mengine amesema kupandishwa ada bila ya utaratibu, kutokuwa na mashirikiano mazuri baina ya wazazi, walimu na mmiliki wa skuli na mmiliki huyo kuendesha skuli kwa hisia zake binafsi.

Aidha amebainisha kuwa malengo ya Wizara sio kuifutia leseni Skuli hiyo bali ni kuhakikisha inafuata sheria na miongozo ya Serikali katika kuendesha Skuli yao.

Kaimu Zuwena, amebainisha kuwa mmiliki wa Skuli hiyo amekuwa mgumu kufuata sheria na miongozo ya Wizara na kuendesha Skuli yake anavyotaka yeye jambo ambalo halivumiliki.

“Haiwezekani Skuli kuendeshwa bila ya kufuata miongozo ya Wizara kwani tuna skuli 590 hatutakuwa tayari kuona mmiliki yoyote wa skuli binafsi anakwenda kinyume na utaratibu na hatutasita kuchukua hatua,” amesisitiza.

Hata hivyo, amesema Skuli hiyo imekuwa ikifatiliwa mara kwa mara na kupewa maagizo ya kurekebisha kasoro hizo lakini haizingatii maagizo anayopewa na badala yake kuendelea kuendesha skuli kinyume na sheria.

Amesisitiza kuwa skuli yoyote ya binafsi inatakiwa kufuata sheria, miongozo na mambo mbalimbali yanayotolewa na wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar.

Nae Afisa Elimu Taaluma Mkoa wa Mjini Magharibi, Amosi John Henock, amesema toka skuli hiyo kusajiliwa mwaka 2010 imekuwa ikijitokeza migogoro baina ya mmiliki na jamii pamoja na kushindwa kujirekebisha baadhi ya kasoro ambazo alitakiwa kuzifanyia kazi.

Aidha amesema Skuli hiyo imeshawahi kufungiwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahmoud na kutakiwa kurekebisha kasoro zilizoonekana lakini aliendelea kukaidi.

Amesisitiza kuwa Skuli hiyo haitaendelea kufundisha mpaka pale itakapokubali kwenda sambamba na maagizo ya Serikali katika kuwapatia watoto elimu.

Amesema hata katiba ya Zanzibar imeeleza wazi kwamba mtu yoyote hapaswi kufanya jambo lolote kwa lengo la ubaguzi wa moja kwa moja ama kwa taathira yake.

Kwa upande wake Sheha wa Shehia ya Shakani bi Mwanaisha Khamis Rashid amebainisha kuwa mara nyingi amekuwa akikaa na uongozi wa Skuli hiyo katika uendeshaji elimu kwa kufuata miongozo na mitaala ya Wizara lakini hakuifuata.

Nae mmiliki wa skuli hiyo bwana Youung Am Kim ameahidi kuheshimu maamuzi ya Wizara ya Elimu ya kutofungua Skuli na hiyo na kuwajuillisha wazazi juu ya suala hilo.

Aidha amesema atahakikisha anafuata sheria ya elimu ya Zanzibar na kuondoa changamoto ambazo zinalalamikiwa kupitia Skuli yake.

Akizungumza kwa niaba ya walimu wenzake Mwalimu Ummy Aga amesema wameweka jitihada binafsi kwa wanafunzi wao kuona wanafanya vizuri katika mitihani yao na kujipima katika ufundishaji lakini kufutwa kwa Skuli hiyo imeondosha ndoto yao kwa Wanafunzi wao.
Mwishoe wataanzisha sheria kuwa ukitaka kufanya kazi au biashara yoyote Zanzibar lazima ufanyiwe interviews ya kiarabu na dini ya kiislamu!
 
Kwenye Hilo la kugungia hiyo wamechemka tena mno wanaanzisha mgogoro usio na sababu uliohitaji hekima ndogo TU kumwambia mzazi peleka mwanao kwingine atakakuwa anashida anatiririka Aya za kurani na kuwrweseka Kwa kuongea kutwa lughaya kiarabu na kushinda msikitini akiswali swala tano
Wangekuwa hawana sheria za kuendesha skuli kungekuwa na tatizo hapo suala ni kufuata sheria tu au kama mmezichoka mzibadili utaratibu wake unafahamika pia
 
Kuna siku lazima Tanganyika ijitegemee tu, Wazanzibar bara wamejaa sehemu zote na hatuna ubaguzi wowote kwa sababu tunaona ni waTanzania wote!

Inakuwaje Raisi wa Tanzania anatoka sehemu zote lakini wa Zanzibar anatoka Zanzibar tu?

Makamu vile vile na mawaziri pia.
Nini manufaa ya haya?
Watu 58ml wanataka usawa na watu 1.4ml?

Hawa watu wametuvaa sawa sawa, huko tuendako lazima kila mmoja abebe fito zake.
Hicho ndo wazanzibar wanachotaka maana muungano unawachelewesha kufikia maendeleo
 
Kwenye Hilo la kugungia hiyo wamechemka tena mno wanaanzisha mgogoro usio na sababu uliohitaji hekima ndogo TU kumwambia mzazi peleka mwanao kwingine atakakuwa anashida anatiririka Aya za kurani na kuwrweseka Kwa kuongea kutwa lughaya kiarabu na kushinda msikitini akiswali swala tano
Tatizo ni kuwa unakuta hizo shule za kukesha msikitini wanafunzi wanafeli kinoma kasoro somo la dini tu,,,, lakini shule za makafiri ndio zina ufaulu mkubwa. kwahiyo wanataka kupeleka watoto kwenye shule zenye ufaulu mkubwa lakini hawataki kufata mambo ya kikafiri
 
Nyinyi watanganyika hemu acheni tabia zenu za kibishi bishi mnavokuja kuweleza huku visiwani. Zanzibar tuna ustaarabu wetu kwaio mkija huku muwe mnakuja na adabu zenu
Afukuzwe tu, huwezi kufanya anavyotaka yeye.. Eboo
 
Huu ni udinibulivuka mipaka. Yani shule ya Kikristo anataka ifuate misingi ya dini ya kiislamu.
 
Back
Top Bottom