Muziki kutoka nchini Zaire (sasa ni D.R.C) uliwezaje kutamalaki na kupendwa sana hapa Tanzania ilhali tumepakana na jirani wengine takribani 6?

Muziki kutoka nchini Zaire (sasa ni D.R.C) uliwezaje kutamalaki na kupendwa sana hapa Tanzania ilhali tumepakana na jirani wengine takribani 6?

Muziki kutoka nchini Zaire (sasa ni D.R.C) uliwezaje kutamalaki na kupendwa sana hapa Tanzania ilhali tumepakana na jirani wengine takribani 6?
1. Walijua mapema kwamba muziki ni kazi na siyo starehe tu.
2. Walichanganya vionjo vya kongo na vile vyenye asili ya Cuba ambavyo zama hizo asili yake ilikuwa kongo basin
3. Walijenga mapema zaidi matumizi ya lugha yao kimuziki na kwa nguvu kubwa
4. Mabepari wa kigiriki walifungua "nyumba" za muziki na kuajiri session musicians kutoka DRC, Brazza, Angola etc na kujenga mashindano makali. Santuri zilitengenezwa na kuuzwa nje. Bendi zote kuu African Jazz, Rock A Mambo pamoja na OK Jazz etc zinahusika hapa.
5. Gitaa za umeme ziliingia mapema zaidi fuatilia midundo ya Orch. Watam na ilivyobadilika hadi OK Jazz miaka ya hamsini
6.Kuwa na wanamuziki wachache ambao walikuwa na ubunifu wa hali ya juu sana mmoja wapo akiwa Franco the Genius aliyejaribu kujiongeza kila idara, alihahakisha ngoma zake zinaendana na midundo ya kiafrica. African Jazz ilikuwa ya kisomi zaidi na OK Jazz ilikuwa ya mtaani. Kwa mfano OK Jazz na baadae TP OK Jazz ingawapo wengi wetu wanamjua Franco tu, lakini ilikuwa na nguzo kali kama Vicky Longomba (Baba yake Awilo) na huyu ndiye alikuwa sauti ya OK Jazz 1956-1971 na mtunzi mahiri (Co-president wa OK Jazz), Simaro Masiya Lutumba (1961-1993), Chef d'Orchestre, mpiga rythm mashuhuri, mtunzi bora wa OK Jazz na TP OK Jazz (The Poet),Vice President na President wa bendi baada ya Luambo kufariki na bila kumsahau Kiambukuta Londa Josky (1973-1993) mtungaji bora, muimbaji bora kabisa wa TP OK Jazz-kama Vicky alikua sauti ya OK Jazz basi Josky ndiye sauti ya TP OK Jazz (Comandant du Bord) alikuwa Vice President wa TP OK Jazz baada ya kufariki Luambo.
7. Nidhamu ya hali ya juu na mazoezi ya kufa mtu ili kutoa kitu kinachoeleweka.
8. Mobutu alisaidia lakini kikubwa zaidi ni wanamuziki wenyewe kujituma.
9. Bendi za DRC zilisafiri sana ndani na nje ya nchi na hivyo kueneza muziki wao
10.Baada ya wagiriki kuachana na muziki wazawa kama Verckys wa Maison Veve na Luambo waliingia sana kwenye biashara ya santuri na kufanya Kenya kwa Afrika mashariki kuwa kituo kikuu cha kutolea santuri zao (ASL) na hivyo kupatikana muziki wao wkwa urahisi zaidi.
11. Mpangilio wao wa mziki: mfano mzuri ni matumizi ya magitaa manne kwa wakati mmoja ambayo nafikiri ni Afican Jazz/Fiesta ndio walianza lakini Franco aliposhika hii kitu akaipaisha kwa namna ambayo haijatokea na kila gitaa likisikika kikamilifu na kwa kiwango bora zaidi na ndio maana haitarajiwi tena kutokea bendi kama TP OK Jazz.
12. Mwisho wa yote-hizo ni sababu zilizochangia wenzetu hao kuja na mirindimo bora ya kiafrica na kuisambaza kwa hamasa kubwa na kukubalika na waafrica wengi.
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu JamiiForums.

Ndugu zangu watanzania;

Muziki kutoka nchini Zaire (sasa ni D.R.C) uliwezaje kutamalaki na kupendwa sana hapa Tanzania ilhali tumepakana na jirani wengine takribani 6?

View attachment 1644761

Mbali na D.R.C nchi yetu ya Tanzania pia imepakana na jirani zake kama vile Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi na Msumbiji.

Ninakumbuka enzi zile nipo mtoto baba yangu alikuwa anawapenda sana wanamuziki kama akina M'bilia Bel, Madilu Système, Sam Mangwana, Pepe Kalle and Empire Bakuba, Diblo Dibala, Bozi Boziana pamoja na Awilo Longomba.

Kwanini ni muziki wa Zaire tu na sio hizo nchi zingine zilizopakana na Tanzania? Waliwezaje kuwa "the best"? Ipi ni siri ya mafanikio yao?

View attachment 1646545

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Swali zuri sana;

Utamaduni wa ndugu zetu wa kongo unaendana sana na Muziki pamoja na kucheza Muziki. Wakiwa wanalima watafanya hivyo iwapo kuna watumbuizaji wa muziki na hata kwenye mazishi huwa wana watumbuizaji wa muziki; na lolote wnalofanya kama jumuia lazima kuwe na muziki. Hii ni tofauti sana na kwetu huku ambako muziki ni burudani tu. Sasa wanamuziki wa Kongo waliamua kuchukua muziki wao kwa next level ili ujulikane ni muziki wa Kongo, na wakafanikiwa sana. Kwa hiyo muziki ni sehemu ya maisha yao na nyimbo nyingi unazojua za kikongo zina asiili muziki wa makabila yao. Tanzania na Uganda hatujawahi kuwa na muziki ambao ni brand ya Tanzania au ya Uganda, huwa tunakopi Kongo tu labda ukitoa ukitoa taarabu. Kenya walijaribu Benga kidogo lakini nadhani nao walifeli.

Nimeangalia kuwa kila mara Diamond akishirikiana na wakongo, muziki wake huwa unatazamwa sana kuliko akishirikiana na wengine ambayo ni zaidi sana kuliko akiimba bila kumshirikisha mtu mwingine yeyote. Ni kwa sababu hiyo kuwa muziki wa Kongo umeshajiimarisha masikioni mwa waskilizaji wengi. Dr. Khalid alijaribu kupromote muziki wa kimakonde wakati akiwa na makondeko, lakini hakufika popote.
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu JamiiForums.

Ndugu zangu watanzania;

Muziki kutoka nchini Zaire (sasa ni D.R.C) uliwezaje kutamalaki na kupendwa sana hapa Tanzania ilhali tumepakana na jirani wengine takribani 6?

View attachment 1644761

Mbali na D.R.C nchi yetu ya Tanzania pia imepakana na jirani zake kama vile Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi na Msumbiji.

Ninakumbuka enzi zile nipo mtoto baba yangu alikuwa anawapenda sana wanamuziki kama akina M'bilia Bel, Madilu Système, Sam Mangwana, Pepe Kalle and Empire Bakuba, Diblo Dibala, Bozi Boziana pamoja na Awilo Longomba.

Kwanini ni muziki wa Zaire tu na sio hizo nchi zingine zilizopakana na Tanzania? Waliwezaje kuwa "the best"? Ipi ni siri ya mafanikio yao?

View attachment 1646545

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Sikiza kibao Cha Grande Kalle kiitwacho "Felicity" tangu miaka ya 1950 fan Anisha na chochote kati ya nchi hizo miaka yote
 
Naona siku hizi umekua huamkii tena, ila kama baba’ko alipenda wasanii uliwataja hapo basi ni rika langu... nami niliwapenda sana enzi hizo.

Hivyo basi, nakusihi kijana uendelee kuniamkia.
 
Kulikuwa na nyimbo nyingi sana za mtindo wa twist za akina Fadhili William, Edward Masengo, Mwenda John Bosco, Haji Fundi Konde, Equator Sound Boys na wengine wengi.
Edward Masengo na Mwenda John Bosco wa Bayeke ambao wana undugu fulani (cousins) ni wakongomani-sikilza ucharazaji wao wa box guitar. Hao ni kati ya generation ya kwanza ya wanamuziki toka Kongo kabla ya kuingia kizazi cha pili Grand Kalle, Grand Maitre Franco etc.
 
Edward Masengo na Mwenda John Bosco wa Bayeke ambao wana undugu fulani (cousins) ni wakongomani-sikilza ucharazaji wao wa box guitar.
Upo vizuri sana mkuu. Hakika wewe sio rika langu...
 
Back
Top Bottom