Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais

Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais

Endeleeni kuwapotosha vijana kutoka familia maskini huku wa kwenu mkiwahimiza kuwa makini na kujiepusha na siasa za kipumbavu. Huwezi kukuta mtoto wa kiongozi wa ngazi za juu CHADEMA anafanya harakati za kipumbavu au kuropoka hovyo. Watoto wa maskini kama kina Mdude ndo hutolewa kafara ili kupata political mileage. Wewe mleta uzi nina uhakika huwezi ruhusu mwanao achukue picha ya Rais na kuichoma huku akirekodi video.

lkn kama mnajua kwamba watoto masikini “wanapotoshwa” kwa nini mnawakamata masikini na msikamate hao wanaowapotosha hao watoto wa masikini kama ni kweli ni watenda haki ?
 
my friend, republic hawajawahi kukosa kosa la kushitaki.

kitu nawashauri vijana, siasa sio fujo, nasema hivi kwasababu huwezi kushindana kwenye fujo na mtu mwenye dola na pesa. ccm wana dola na pesa. wewe huna polisi, huna TISS huna jeshi utashindana nao kwa manguvu? si utaumia tu.

Pili, harakati zenu fanyeni kwa busara, hekima na maarifa. Hoja dhidi ya hoja, acheni matusi. Kijana wetu sativa tunamwonea huruma sana, ni mdogo, hana hata career, anatafutiza tu chumba cha kupanga, ila mdomoni alikuwa na matusi mazito sana sana, hafanani na alivyo. sababu hiyo alijitengenezea maadui wengi, hakwenda kwa hekima na busara, hata Mungu kuamwokoa basi tu kwasababu yeye hana Mungu, ni mtu mwenye mdomo mchafu, tujifunze, na yeye ajifunze, jenga hoja, acha matusi.

someni mazingira, Tanzania sio kenya, na sio marekani ambako uhuru wako wa kujieleza upo asilimia mia. marekani unaweza kuchoma ramani ya nchi, au picha ya rais, hawakufanyi kitu. hapa ukichoma utakamatwa na utafungwa. kwa akili tu, badilisheni tactic za mapambano yenu kulingan ana mazingira. huyo dogo amechoma picha ya rais, kwa bongo icho kitu hakikubaliki.

kenya waliandamana, waliharibu vitu, waliwachezea polisi, walifanya yote wapendavyo, na hawakufanywa kitu sana. Tanzania chezea polisi utajua mwenyewe, ndio maana tunasema cheza mziki kulingana na rythm yake.

chadema acheni matusi, chadema acheni matusi, chadema acheni matusi, nimewataja mara tatu. jengeni hoja, mjibiwe kwa hoja, maguvu hamtaweza kwasababu watanzania ni waoga na pia ninyi hamna dola, mnaumiza vijana wetu bure kwa maslahi ya matumbo yenu.
Sasa ndugu Yesu hapo Chadema imehusikaje?
 
kitendo kile ni sawa na mtu kuokota makaratasi ili awashie mkaa kwenye jiko lake.

Hahahaa ,kama lingekuwa kosa wangefungwa watu wengi sana ,magazeti kibao yana picha ya rais na watu wanayachoma.

Msingi ni kwamba RC alisema akamatwe kwa kosa la kuchoma picha ya rais na kama siyo kosa basi aachiwe kisha akamatwe tena wamfungulie kesi nyingine labda ya kutukana ambayo ina dhamana.
 
Kwamba hata yule kijana aliyekamatwa Rungwe kwa kosa la kuipiga kiberiti picha ya Rais Samia, hana kosa lolote na hata wakamataji hawajui wampachike kesi gani, maana kwa katiba ya Tanzania kitendo kile ni sawa na mtu kuokota makaratasi ili awashie mkaa kwenye jiko lake.

Inadaiwa kukamatwa kwake kumesababishwa na mihemko tu na fikra duni za viongozi wa Mbeya

=========

Ni siku tatu tangu Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limkamate Shadrack Chaula (24), kijana anayetuhumiwa kuchoma moto picha ya Rais Samia Suluhu Hassan, suala hilo limeibua mvutano wa kisheria, ikielezwa hakuna sheria iliyovunjwa.

Akizungumza na Mwananchi jana Julai 3, 2024 kuhusu kosa la kijana huyo na lini atafikishwa mahakamani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema jukumu lao liliishia kumkamata suala la kupelekwa mahakamani linabaki kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

“Siwezi kusema ni lini atapelekwa mahakamani, kazi yetu ilikuwa ni kumkamata, Ofisi ya Mashtaka ndiyo itaandaa mashtaka kwa kuangalia ushahidi na kuonyesha ni vifungu gani vya sheria mtuhumiwa amekiuka,” amesema.

Suala hilo pia limeibua mjadala kwenye mitando ya kijamii na miongoni mwa waliolijadili ni Wakili Peter Kibatala aliyeandika ujumbe kupitia ukurasa wake, na baadaye alipotafutwa na Mwananachi kuufafanua, amesema amewaelekeza mawakili wiwili kwenda kutoa msaada wa kisheria kwa kijana huyo.

“Hatutaingilia maamuzi ya mkuu wa mkoa aliyetaka kijana huyo ahojiwe, lakini atakapopelekwa mahakamani ana haki ya kupata msaada wa kisheria, ndiyo maana niliwagiza mawakili wenzangu wawili kwenda kumsaidia kijana huyo,” amesema.

Wakili wa kujitegemea, Philip Mwakilima akizungumza na Mwananchi amesema hakuna sheria wala kifungu kinachoonyesha kuchoma au kutochoma picha ya kiongozi huyo ni kosa na hakuna athari yoyote kwa jamii.

(Imeandikwa na Waandishi Wetu)

Mwananchi
Wizara ya Afya taarifa yake inasema kati ya watu 4 hapo ulipo Kwa idadi hiyo mmoja wenu atakuwa na tatizo la Afya ya akili
 
penal code ni kubwa sana ndugu yangu. kwa tuliokaa mahakamani mda mrefu, kosa lipo.
Ila wee unachekesha kweli, lete hivyo vifungu vya penal code hapa sisi tujionee na tuhakiki, lete uthibitisho hapaa.

Wee c umekaa mda mrefu mahakamanii? Haya lete hapa watu tujisomee hiyo sheria.

Hatutaki porojo na vijisababu vya kutunga au kuokoteza ili mfurahishe nafsi zenuu, Lol
 
Ila wee unachekesha kweli, lete hivyo vifungu vya penal code hapa sisi tujionee na tuhakiki, lete uthibitisho hapaa.

Wee c umekaa mda mrefu mahakamanii? Haya lete hapa watu tujisomee hiyo sheria.

Hatutaki porojo na vijisababu vya kutunga au kuokoteza ili mfurahishe nafsi zenuu, Lol
Huyu chizi naye anajiita wakili
 
Kwamba hata yule kijana aliyekamatwa Rungwe kwa kosa la kuipiga kiberiti picha ya Rais Samia, hana kosa lolote na hata wakamataji hawajui wampachike kesi gani, maana kwa katiba ya Tanzania kitendo kile ni sawa na mtu kuokota makaratasi ili awashie mkaa kwenye jiko lake.

Inadaiwa kukamatwa kwake kumesababishwa na mihemko tu na fikra duni za viongozi wa Mbeya

=========

Ni siku tatu tangu Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limkamate Shadrack Chaula (24), kijana anayetuhumiwa kuchoma moto picha ya Rais Samia Suluhu Hassan, suala hilo limeibua mvutano wa kisheria, ikielezwa hakuna sheria iliyovunjwa.

Akizungumza na Mwananchi jana Julai 3, 2024 kuhusu kosa la kijana huyo na lini atafikishwa mahakamani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema jukumu lao liliishia kumkamata suala la kupelekwa mahakamani linabaki kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

“Siwezi kusema ni lini atapelekwa mahakamani, kazi yetu ilikuwa ni kumkamata, Ofisi ya Mashtaka ndiyo itaandaa mashtaka kwa kuangalia ushahidi na kuonyesha ni vifungu gani vya sheria mtuhumiwa amekiuka,” amesema.

Suala hilo pia limeibua mjadala kwenye mitando ya kijamii na miongoni mwa waliolijadili ni Wakili Peter Kibatala aliyeandika ujumbe kupitia ukurasa wake, na baadaye alipotafutwa na Mwananachi kuufafanua, amesema amewaelekeza mawakili wiwili kwenda kutoa msaada wa kisheria kwa kijana huyo.

“Hatutaingilia maamuzi ya mkuu wa mkoa aliyetaka kijana huyo ahojiwe, lakini atakapopelekwa mahakamani ana haki ya kupata msaada wa kisheria, ndiyo maana niliwagiza mawakili wenzangu wawili kwenda kumsaidia kijana huyo,” amesema.

Wakili wa kujitegemea, Philip Mwakilima akizungumza na Mwananchi amesema hakuna sheria wala kifungu kinachoonyesha kuchoma au kutochoma picha ya kiongozi huyo ni kosa na hakuna athari yoyote kwa jamii.

(Imeandikwa na Waandishi Wetu)

Mwananchi
Lakini Kosa la Dogo ni la kimaadili zaidi kuliko kijinai.

Ni utovu wa nidhamu kuchukua picha ya mtu na kuichoma hadharani tena mtu huyo akiwa ni Rais wa Nchi.

Mtu kama humpendi na chumbani kwako kuna picha zake unachukua unazitia kiberiti kimya kimya.
 
Kwenye penal code kuna kosa linaitwa ARSON i.e kuchoma Mali moto, swali ni vitu vinavyoitwa Mali ni vipi?
Mbona mimi jana tuu nimetoka kuchoma picha kibao zikiwepo za Magufuli, Samia, Mbowe, Msigwa, Lissu, etc. Waje wanikamate
 
Back
Top Bottom