Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais

Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais

Endeleeni kuwapotosha vijana kutoka familia maskini huku wa kwenu mkiwahimiza kuwa makini na kujiepusha na siasa za kipumbavu. Huwezi kukuta mtoto wa kiongozi wa ngazi za juu CHADEMA anafanya harakati za kipumbavu au kuropoka hovyo. Watoto wa maskini kama kina Mdude ndo hutolewa kafara ili kupata political mileage. Wewe mleta uzi nina uhakika huwezi ruhusu mwanao achukue picha ya Rais na kuichoma huku akirekodi video.
Nimeipenda hii
 
Kwa hio nini kifanyike
Dr. Samia Suluhu sio tu ni mkuu wa nchi bali pia ni mama.

Tuwaheshimu wakubwa, TUWAPINGE KWA HOJA, na siyo kuwakosea adabu.

Wote wanaofanya vitendo vya utovu wa nidhamu wapewe onyo kali
 
Dr. Samia Suluhu sio tu ni mkuu wa nchi bali pia ni mama.

Tuwaheshimu wakubwa, TUWAPINGE KWA HOJA, na siyo kuwakosea adabu.

Wote wanaofanya vitendo vya utovu wa nidhamu wapewe onyo kali
Tujikite kwenye Kikomo cha kisheria . Kama anataka kofia ya umama ibaki kwenye familia yake . Samia ni kiongozi wa Tanzania sio kiongozi wa familia za watanzania.
 
Je vipi Kama kijana huyo angechimba kaburi na kuizika hiyo picha kwa heshima zote za kiislam hapo pasingekuwa na kosa?
Huo ungekuwa ni umwehu.

Unazika vipi picha kwa heshima ya kiislamu ili hali aliyepo kwny picha yuko hai?
 
Tujikite kwenye Kikomo cha kisheria . Kama anataka kofia ya umama ibaki kwenye familia yake . Samia ni kiongozi wa Tanzania sio kiongozi wa familia za watanzania.
Kwa hiyo ni sahihi kumkosea adabu kiongozi wa watanzania?
 
Nim
Sure, picha yake nna matumizi nayo maalum geto kwangu...usiniulize matumizi gani!!.
Nimecheka ...umenikumbusha tukiwa Boarding school ya wanaume tupu halafu mtu Mmoja anaitwa Ally yupo bafuni anapiga kelele akiita "Mwajuma wangu njoo" kumbe ingekuwa Leo angefunguliwa mashitaka?
 
Jikite kwenye hoja, Je kuchoma picha ni kosa kisheria?

Halafu huo ujinga wa kuona kila anayepinga serikali katumwa ni dharau sana, yaani unataka kusema Watanzania ni mbumbumbu na kwamba hawawezo kuamua mambo wenyewe na kutafakari hadi watumwe?

Hakika utalipwa kwa dharau zako hizo, Wallah tena!
Ungefafanua kwanza kwanini watoto wa viongozi wa vyama vya upinzani hawaonekani kufanya uhuni wa aina hiyo na kurekodi video na kutuma mitandaoni.?! Tunaweza kusema labda kisheria kuchoma picha ya rais ni kama kuchoma karatasi yoyote!! Lakini ukiulizwa , kurekodi video wakati unachoma picha ya rais na Kisha kuirusha video hiyo mitandaoni unalenga kufikisha ujumbe gani kwa jamii , utasemaje?!
 
hapo sasa ngoja tuone Dpp ataandikaje kuhusu hiyo mali picha
Uchochezi na kuamsha chuki, hasira na taharuki katika jamii!, kosa linaweza lisiwe kuchoma picha husika, lakini kosa ikawa ni kurekodi video ya kitendo hicho na kuiweka mitandaoni. Unakumbuka yule mfanyakazi wa serikali kule kirosa enzi za magufuli aliyerekodiwa akichana na kukanyaga kitabu kitukufu Cha Quran waziri jafo akamsimamisha kazi na magufuli akasema afukuzwe kazi Moja kwa Moja? Si na yeye angejitetea kuwa kitabu ni Mali yake kanunua Dukani kwa pesa zake.?! Kwa kanuni za nchi picha ya rais pia ni kitu kitukufu na kinachoheshimika ndoa maana ukiingia ofisi mbalimbali za serikali na hata ofisi binafsi unakuta imebandikwa ukutani mahala pananapoheshimika.
 
Lakini vijana wengi hatuielewi vyema siasa.

Hizi ni biashara za watu,wanawekeza pesa,nguvu,muda nk.
Wewe mfuasi unawekeza hisia peke yake,hapo ndipo unapoweka rehani ustawi wako na jamii yako.
 
Kuichambia je?
Huko kuchamba hadharani peke yake ni kosa hata bila kutumia picha ya rais itakuwaje uchambie picha ya rais hadharani na kurekodi video na kutuma mitandaoni! Nia yako ni kufikisha ujumbe gani kwa jamii inayoangalia video hiyo?!
 
Mali lazima iwe na mwenyewe, sasa ile karatasi yenye picha ni mali ya nani? Na je mwenye karatasi amelalamika?
Karatasi ni mali yake picha ni ya mheshimiwa kiongozi mkuu wa nchi.
 
Back
Top Bottom