Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais

Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais

Jikite kwenye hoja, Je kuchoma picha ni kosa kisheria?

Halafu huo ujinga wa kuona kila anayepinga serikali katumwa ni dharau sana, yaani unataka kusema Watanzania ni mbumbumbu na kwamba hawawezi kuamua mambo wenyewe na kutafakari hadi watumwe?

Hakika utalipwa kwa dharau zako hizo, Wallah tena!
Kama sio kosa mrekodi mwanao akichoma picha ya Mbowe halafu post. Hata Mbowe na Lissu sio mbumbumbu ndo maana huwezi kuona watoto wao kwenye mambo ya kipumbavu kama kuchoma picha ya Rais. Ni kweli ninadharau mno mtu mpumbavu anayeona hili sio sawa ila analeta ujuaji.
 
Akifutiwa uwakili maana yake hana hadi ya usomi kwa hiyo hastahili kuendelea kusimamia kesi mahakamani! Mbumbumbu kama wewe ndiyo mtaendelea kumwita msomi lakini siyo wasomi wa sheria! Wao mawakili wasomi watamwita mwanasheria!
Sawa , mbumbumbu mwenzio aliyechoma picha ya mh rais keshahukumiwa miaka miwili jela au faini milioni tano. Nakushauri andamaneni au mumlipie faini asalimike na kifungo , la sivyo jela inamhusu.
 
Hujapangua hoja ya mleta mada hata kidogo. Mleta mada anasema kuchoma picha yenye sura ya rais (lkn siyo mali ya rais), hakuna kosa kisheria. Wewe chawa wa rais unasemaje??
Jamaa yenu keshahukumiwa miaka 2 je au faini milioni 5, je mnamsaidiaje?!
 
Je vipi Kama kijana huyo angechimba kaburi na kuizika hiyo picha kwa heshima zote za kiislam hapo pasingekuwa na kosa?
Kosa vilevile. Tafsiri yake ingekuwa kwamba anamuombea kifo muhusika wa picha hiyo
 
Kwamba hata yule kijana aliyekamatwa Rungwe kwa kosa la kuipiga kiberiti picha ya Rais Samia, hana kosa lolote na hata wakamataji hawajui wampachike kesi gani, maana kwa katiba ya Tanzania kitendo kile ni sawa na mtu kuokota makaratasi ili awashie mkaa kwenye jiko lake.

Inadaiwa kukamatwa kwake kumesababishwa na mihemko tu na fikra duni za viongozi wa Mbeya

=========

Ni siku tatu tangu Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limkamate Shadrack Chaula (24), kijana anayetuhumiwa kuchoma moto picha ya Rais Samia Suluhu Hassan, suala hilo limeibua mvutano wa kisheria, ikielezwa hakuna sheria iliyovunjwa.

Akizungumza na Mwananchi jana Julai 3, 2024 kuhusu kosa la kijana huyo na lini atafikishwa mahakamani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema jukumu lao liliishia kumkamata suala la kupelekwa mahakamani linabaki kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

“Siwezi kusema ni lini atapelekwa mahakamani, kazi yetu ilikuwa ni kumkamata, Ofisi ya Mashtaka ndiyo itaandaa mashtaka kwa kuangalia ushahidi na kuonyesha ni vifungu gani vya sheria mtuhumiwa amekiuka,” amesema.

Suala hilo pia limeibua mjadala kwenye mitando ya kijamii na miongoni mwa waliolijadili ni Wakili Peter Kibatala aliyeandika ujumbe kupitia ukurasa wake, na baadaye alipotafutwa na Mwananachi kuufafanua, amesema amewaelekeza mawakili wiwili kwenda kutoa msaada wa kisheria kwa kijana huyo.

“Hatutaingilia maamuzi ya mkuu wa mkoa aliyetaka kijana huyo ahojiwe, lakini atakapopelekwa mahakamani ana haki ya kupata msaada wa kisheria, ndiyo maana niliwagiza mawakili wenzangu wawili kwenda kumsaidia kijana huyo,” amesema.

Wakili wa kujitegemea, Philip Mwakilima akizungumza na Mwananchi amesema hakuna sheria wala kifungu kinachoonyesha kuchoma au kutochoma picha ya kiongozi huyo ni kosa na hakuna athari yoyote kwa jamii.

(Imeandikwa na Waandishi Wetu)

Mwananchi
Mwambieni huyo mwendawazimu , huo ujinga apeleke Kenya
 
Nimecheka wakili anauliza maswali, kachoma picha iliyopigwa au kuchorwa na nani ambae sasa analalamika? Na mnajuaje picha iliyochomwa inafanana na Samia hadi mseme kachoma picha ya Samia, toa ushahidi😀😀😀

Halafu nimemwona Kamanda wa Polisi Mbeya ni mtupu aliposema, sie tumemkamata tunasubiri DPP atuambie tumemkamata kwa kuvunja sheria ipi! Yaani Polisi wa Tanzania bwana, ovyo sana. Sasa kwa nini Mkuu wa Mkoa aliposema kamkamate hamkuuliza haya maswali? Kuna siku Kamanda wa Polisi ataambiwa amkamate mwanamke kwa sababu kamkataa mkuu wa mkoa. Wawe na ujasiri wa kuuliza unatutuma tumkamate huyu mtu kwa kuvunja sheria gani na kushauri kama ni sawa kumkamata au la. Polisi wasiwe wanaamrishwa na wanasiasa kama hawana akili kichwani, ni roboti tu.

Hivi kama mimi ni msanii, nikachora picha ya Samia, lakini watu wakasema nimekosea macho sijayafanya marembo kama yalivyo ya Samia, na kidevu sijaweka cha mfuto kama chake, nikaamua kuichoma ili nichore picha nyingine, nitashitakiwa kwa kosa la kuchoma picha ya Samia?
Mkuu wa mkoa ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama katika mkoa wake. Na sheria ya majeshi Dunia nzima ni kwamba mwanajeshi anapopewa amri na mkuu wake hawaruhusiwi kuhoji zaidi ya kufanya alichoamrishwa na kungoja maelezo baadae. Sasa kulingana na kanuni za kijeshi ni polisi asiyejipenda atakaethubutu kumuuliza mkuu wa mkoa mtu aliyeamrisha akamatwe kafanya kosa gani!!
 
Kwamba hata yule kijana aliyekamatwa Rungwe kwa kosa la kuipiga kiberiti picha ya Rais Samia, hana kosa lolote na hata wakamataji hawajui wampachike kesi gani, maana kwa katiba ya Tanzania kitendo kile ni sawa na mtu kuokota makaratasi ili awashie mkaa kwenye jiko lake.

Inadaiwa kukamatwa kwake kumesababishwa na mihemko tu na fikra duni za viongozi wa Mbeya

=========

Ni siku tatu tangu Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limkamate Shadrack Chaula (24), kijana anayetuhumiwa kuchoma moto picha ya Rais Samia Suluhu Hassan, suala hilo limeibua mvutano wa kisheria, ikielezwa hakuna sheria iliyovunjwa.

Akizungumza na Mwananchi jana Julai 3, 2024 kuhusu kosa la kijana huyo na lini atafikishwa mahakamani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema jukumu lao liliishia kumkamata suala la kupelekwa mahakamani linabaki kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

“Siwezi kusema ni lini atapelekwa mahakamani, kazi yetu ilikuwa ni kumkamata, Ofisi ya Mashtaka ndiyo itaandaa mashtaka kwa kuangalia ushahidi na kuonyesha ni vifungu gani vya sheria mtuhumiwa amekiuka,” amesema.

Suala hilo pia limeibua mjadala kwenye mitando ya kijamii na miongoni mwa waliolijadili ni Wakili Peter Kibatala aliyeandika ujumbe kupitia ukurasa wake, na baadaye alipotafutwa na Mwananachi kuufafanua, amesema amewaelekeza mawakili wiwili kwenda kutoa msaada wa kisheria kwa kijana huyo.

“Hatutaingilia maamuzi ya mkuu wa mkoa aliyetaka kijana huyo ahojiwe, lakini atakapopelekwa mahakamani ana haki ya kupata msaada wa kisheria, ndiyo maana niliwagiza mawakili wenzangu wawili kwenda kumsaidia kijana huyo,” amesema.

Wakili wa kujitegemea, Philip Mwakilima akizungumza na Mwananchi amesema hakuna sheria wala kifungu kinachoonyesha kuchoma au kutochoma picha ya kiongozi huyo ni kosa na hakuna athari yoyote kwa jamii.

(Imeandikwa na Waandishi Wetu)

Mwananchi
Haya mchagieni hiyo 5m asiende jela miaka 2
 
Kwamba hata yule kijana aliyekamatwa Rungwe kwa kosa la kuipiga kiberiti picha ya Rais Samia, hana kosa lolote na hata wakamataji hawajui wampachike kesi gani, maana kwa katiba ya Tanzania kitendo kile ni sawa na mtu kuokota makaratasi ili awashie mkaa kwenye jiko lake.

Inadaiwa kukamatwa kwake kumesababishwa na mihemko tu na fikra duni za viongozi wa Mbeya

=========

Ni siku tatu tangu Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limkamate Shadrack Chaula (24), kijana anayetuhumiwa kuchoma moto picha ya Rais Samia Suluhu Hassan, suala hilo limeibua mvutano wa kisheria, ikielezwa hakuna sheria iliyovunjwa.

Akizungumza na Mwananchi jana Julai 3, 2024 kuhusu kosa la kijana huyo na lini atafikishwa mahakamani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema jukumu lao liliishia kumkamata suala la kupelekwa mahakamani linabaki kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

“Siwezi kusema ni lini atapelekwa mahakamani, kazi yetu ilikuwa ni kumkamata, Ofisi ya Mashtaka ndiyo itaandaa mashtaka kwa kuangalia ushahidi na kuonyesha ni vifungu gani vya sheria mtuhumiwa amekiuka,” amesema.

Suala hilo pia limeibua mjadala kwenye mitando ya kijamii na miongoni mwa waliolijadili ni Wakili Peter Kibatala aliyeandika ujumbe kupitia ukurasa wake, na baadaye alipotafutwa na Mwananachi kuufafanua, amesema amewaelekeza mawakili wiwili kwenda kutoa msaada wa kisheria kwa kijana huyo.

“Hatutaingilia maamuzi ya mkuu wa mkoa aliyetaka kijana huyo ahojiwe, lakini atakapopelekwa mahakamani ana haki ya kupata msaada wa kisheria, ndiyo maana niliwagiza mawakili wenzangu wawili kwenda kumsaidia kijana huyo,” amesema.

Wakili wa kujitegemea, Philip Mwakilima akizungumza na Mwananchi amesema hakuna sheria wala kifungu kinachoonyesha kuchoma au kutochoma picha ya kiongozi huyo ni kosa na hakuna athari yoyote kwa jamii.

(Imeandikwa na Waandishi Wetu)

Mwananchi
Kama picha hiyo ingekuwa iko kwenye noti ya pesa za Kitanzania hapo ndio ingekuwa kosa, lakini karatasi la kuchora mwenyewe lisilo na ithibati ya vipimo vya sura halisi sio kosa.
Mbona picha za mabango ya JPM ya kampeni yaliyokuwa yamebandikwa sehemu mbalimbali, alipokufa tu manispaa ziliagiza zishushwe na kuchanwa au kuchomwa moto na watumishi wa umma waliotumwa na viongozi wao mchana kweupe lakini hakuni hawakukamatwa kamwe hadi leo hii.

Kuchomwa kwa picha ya kuchora ya mfano isiyo halisi ilileta athari gani ya kimwili, kiafya, kisaikolojia na kiusalama wakati ikiteketea na moto?

Kwani huyo kijana alifanya kosa gani kusema ushoga umetamalaki na kufanyika wazi wazi kwa sasa?

*Huyo kijana aachiliwe mara moja ni uonevu tu wa kisiasa
 
Back
Top Bottom