Mwaka 1983 Lowassa alinunua suti pair 10 wakati Nyerere na Sokoine wakiwa na kaunda suti zaidi ya pair tano

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Mwaka 1983, Lowassa akiwa na miaka 30 akiwa ofisa wa CCM, walikwenda UK kwa training, alinunua suti jozi 10 kwa mpigo, kumbuka kipindi hicho nchi ilikuwa na makovu ya vita ya Uganda, Nyerere akiwa Rais, Sokoine akiwa Waziri Mkuu walikuwa na viatu jozi mbili na suti jozi nne au tatu.
Tuliokuwepo miaka hiyo mtanielewa,wale wadogo zangu hamuwezi kuelewa,maisha ya 1973 yalikuwa mazuri kwa wananchi kuliko ya 1983,tulivaa midabwada ,viraka,mtu mzima matako nje....,sigara,sabuni ,sukari,ungekamatwa navyo ni jela miezi sita
 

hapo shida iko wapi? kumbuka kuwa wamasai wana ng'ombe wengi.na inategemea na hulka ya mtu.mimi hapa nina jirani ana ghorofa.mimi nyumba ya kawaida kabisa.but MUNGU amenijaria kufungua ng'ombe . huyu jirani yangu huwa ananunua nusu ya lita ya maziwa kwangu.sasa kuwa nacheka sana.mimi mwenye kipato cha chini nakunywaga lita nzima ya maziwa ,tajiri anakunywa nusu lita .hahahaha.so staili ya mtu inamtuma kuishi anavyotaka.
 
Masai wa miaka ile auze mifugo anunue suti,?unadhani Sokoine hakuwa na ngombe kwao?
 
Kipindi hicho kumiliki baiskeli tu ilikuwa ni fahari kubwa,kumbuka ni 1983 tulikuwa gizani tunanuka umasikin
 
Nachukia sana umaskini - Edward Ngoyai Lowassa

Huyo Mzee Mchonga aliuendekeza umaskini na mpaka leo nchi imetawaliwa na mentality ya umaskini
 
Mmasai akizaliwa, wazazi humpa kundi lake la ngombe, mpaka anafikia utu uzima ni mamia ya ngombe, suti kumi inakutoa udenda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…