Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.

Ndugu zangu watanzania;

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676

Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.

Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.

Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.

Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.

View attachment 1661678

Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.

Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.

Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.

Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.

View attachment 1661682

Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.

Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Asanye Serikali ya CCM kuongeza secondary kwa wingi!
 
Sasa hivi C mbili na D moja unaingia advance
Tena unaweza kuta C za civics na nutrition, D ya Bible/Islamic knowledge

Chuo E mbili

Akitoka hapo hataki kazi za bodaboda, eti anataka kazi za hadhi yake, hivi wana hadhi gani hawa mbwa!!!!
Kwa chuo kwa sasa lazima uwe na D mbili na kuendelea
 
Andika tena mkuu mimi bado sijakuelewa
Watu wa zamani,fresh from school au college. Walipokuwa wakiajiriwa,uwezo wao siku za mwanzo kazini ukilinganisha Na waliowatangulia kazini . Tofauti ya kiuwezo ilikuwaje?
 
Enzi zetu kwa Dar shule zilikuwa nne tu basi yaani Pugu,Minaki,Tambaza,Azania hakukuwapo na Benjamini Mkapa.
Mtoto wa kiume unatakiwa ukaze ili uende angalau hata Aza Boy.

Ila binafsi nilichaguliwa Ilboru kata nzima nilikuwa mwenyewe ila DsM nzima tulikuwa watatu tu.

Advance tukatupwa mzumbe pale kwa DsM tulikuwa wa tano mkoa mzima.
Jangwani na Zanaki,kisutu na Forodhani,Kibasila hazikua Secondary?,naanza kupata wasiwasi na wewe
 
Nilianzia kuruka kichura kwenye hiyo round about hadi bwenini, ni mwendo wa viwanja viwili vya mpira wa miguu,begi na jembe nimejitwisha kichwani.

Nilivyo fika getini akanisamehe, akanirudisha tena nilipoanzia kuruka kichura kwa lengo la kujitambulisha.
Kweli maisha ni hatua...
ulikuwa mzembe sana chief, au ndo ulikuwa mtoto wa mama sana
 
Mwaka 2001 mwezi wa 5 nilimaliza Advance kwa bahati nzuri tulifaulu wanafunzi karibu wote. Wale wachache waliobakia walienda kusoma TUMAINI UNIBERSITY. Wale watu tulikuwa tunawadharau sana kwakuwa wanasomeshwa na wazazi wao. Chuo hapakuwa na loan board.
Dah walikuja kusoma watoto wa masikini kwelikweli. Wengine tuliwasaidia kuwavusha barabara.
 
Hiyo haikuishia mwaka wa 1999, ilikwenda mpaka 2001/2 hivi, nakumbuka nilifaulu Mkolani Sekondari, ila kulikuwa mbali kipindi hiko na usafiri ulikuwa ni wa Taabu haswaa! Baba akanambia nihamie Thaqaafa nikakataa nikamjibu mimi nimefaulu siwezi kwenda shule ya waliofeli. Akanitizamaaa akaniacha kule kule. Kiukweli nilikuwa najisikia Furaha sana.
 
Umeandika kana kwamba ni jambo la kujivunia?

Unataka kusemaje? Kwamba ninyi ndio mlikuwa vipanga pekee hapa Tanganyika?

Excuse me, spare me the nonsense!

Ninachofahamu ni kuwa, shule zilikuwa chache sana. Wengi walikosa nafasi pamoja na kwamba walifaulu vizuri.

Halafu unakuja unajitapa hapa, ati ooohh tulienda sekondari wachache mno!

Kwamba ni swala la ujiko sana au wewe ulikuwa mtu spesheli sana kuliko wengine?
 
Umeandika kana kwamba ni jambo la kujivunia?

Unataka kusemaje? Kwamba ninyi ndio mlikuwa vipanga pekee hapa Tanganyika?

Excuse me, spare me the nonsense!

Ninachofahamu ni kuwa, shule zilikuwa chache sana. Wengi walikosa nafasi pamoja na kwamba walifaulu vizuri.

Halafu unakuja unajitapa hapa, ati ooohh tulienda sekondari wachache mno!

Kwamba ni swala la ujiko sana au wewe ulikuwa mtu spesheli sana kuliko wengine?
Kuna kauli moja Mh. Masaburi aliwahi kuitoa dhidi ya wabunge juu ya namna yao ya kufikiri ninaomba nisiiseme kwako.
 
Ndugu zangu waliosoma zamani kidogo itakuwa wanakumbuka vitu kama wali na maharage siku nne au tano ,wali nyama(nyama ya kuku,ng'ombe),maziwa,mikate mikubwa na siagi,uji uliochanganywa na maziwa,chai safi,madaftari na kalamu za bure,kuogelea bwawani,kula mboga za majani.........elimu imetoka mbali sana,sasa hiv ni balaa...
Umenikumbusha Masurufu na Gorvement warrant wakati kwenda likizo
 
siyo elimu tu wanaufahamu kuliko hao viongozi wenu serikalini
Punguza kuropoka maneno ya kashifa na dharau.
Hao viongozi wengi unaowasema ni member humu JF.

Pia humu JF kuna watu wana uelewa mdogo sana hadi unajiuliza huyu ana matatizo ya akili au ya elimu?
 
Tulipasua vibaya saana....nakumbuka wilaya nzima tulikiwa 15 tu tulijulikana!! Moshi Tech, Bihawana, Msalato, Weruweru; Tabora Boyz / Girls....

Wakati huo elimu under Mwalimu ilikuwa na hadhi...ukiwa form one ukirudi likizo kwenye msiba kijijini basi unakaa na wazee wa heshima eee wazee wastaafu na walimu na watumishi wa Serikali kama katibu kata / tarafa; Mratibu wa Elimu etc

Sasa hivi laah form one shule ya kata anachojua ni mauno ya nandi na singeli....
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Ni kweli ....kwa zamani shule za private secondary zilikua za wale ambao hawakufaulu sana kwenda shule za serikali
Duh unanikumbusha mbali. Shuleni kwetu tulifaulu watatu tu tena wavulana. Ukienda private unaonekana hauna kitu[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom