Mwaka huu kutakuwa na njaa, heri ukose hela ila uwe na chakula ndani

Mwaka huu kutakuwa na njaa, heri ukose hela ila uwe na chakula ndani

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Chukua hii nakupa; japo hatupangiani maisha kila mtu anajua jinsi anavyoyaendesha ila kiukweli life ni gumu ndugu zangu na mwaka huu huku mashambani hali sio hali hasa Kwa upande wa zao la mahindi.

Mikoa ambayo sio wazalishaji wakubwa wa chakula tumepata pata ila sio ya kuuza ni kwa ajili ya kula tu mahindi yalinyauka pia mvua Ilikuwa nyingi ikaathiri kiasi fulani.

Mpunga kidogo mwaka huu maeneo mengi wametoboa. All in all maisha tu ni magumu pesa ngumu kupatikana na bado haikaliki inapepea yaani laki ukienda sokoni kununua vitu hivyo vitu ukiviona ni vichache kama utani laki inakata ila kuipata laki yenyewe ni mtiti.

So kama unaishi ki bachelor au una familia aisee ni heri ukajiandaa mapema ukipata pesa weka stock kabisa ya vyakula hata kama gunia bora uweke mapema, mkaa weka, gas jaza,Maharage weka, mpunga weka, mafuta ya kutosha weka n. k.. UOGA PIA NI AKILI SOMETIMES

Ukiwa huna hela wala chakula ndani unaweza kudata ukajikuta unageuka omba omba majumbani mwa watu.

Hakuna kitu kibaya kama njaa inatisha aisee kweli wahenga walisema ADUI YAKO MUOMBEE NJAA.

images.jpeg
images (7).jpeg
 
Tafuta Hela mkuu ,unga si AKIBA pesa ndio akiba ya Kila kitu,,mfano mtt akiumwa hapo uwezi mpelekea docta unga na Mchele ampe mtt huduma ,Bali atataka pesa..narudiaa tafutaa pesaaaa sanaaaaa..
Mkuu tatizo la pesa wengi wetu ku save tumeshindwa labda uizungushe tofauti na hapo lazima tu itakwisha
 
Back
Top Bottom