Mwaka mmoja bila Magufuli: Jimbo Kuu Katoliki Mwanza kuongoza Misa ya maombezi yake

Mwaka mmoja bila Magufuli: Jimbo Kuu Katoliki Mwanza kuongoza Misa ya maombezi yake

Sang'udi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2016
Posts
9,138
Reaction score
22,236
Mhashamu Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema katika adhimisho la Misa Takatifu ya kumuombea pumziko la milele mbinguni Hayati John Pombe Joseph Magufuli.

Misa hii takatifu itafanyika Jumapili ya Machi 20 katika viwanja vya madhabahu ya Bikira Maria Malkia wa Kawekamo kuanzia saa nne kamili asubuhi.

Aidha, Mhashamu Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande anatukumbusha kumuenzi Hayati Magufuli kwa kuwa wazalendo wa kweli, kudumisha amani, undugu na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Hayati Magufuli apumzike kwa amani mbinguni, Amina.

Screenshot_20220311-201913_Adobe Acrobat.jpg
 
Hilo jizi halistahili kuombewa, ni la kuchomwa moto wa milele! Alituletea wahuni akina Bashite, Sabaya na akawalinda kwa nguvu zote! akawafanyia unyama wapinzani as if siyo watanzania, hafai, hafai, na hastahili kuombewa
Pole sana mkuu,
Unatakiwa ku-move on.

Karibu Jumapili ya tarehe 20 Machi tumuombee Rais wetu bora kabisa wa wakati wote pale Kawekamo, Mwanza.
 
Mhashamu Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema katika adhimisho la Misa Takatifu ya kumuombea pumziko la milele mbinguni Hayati John Pombe Joseph Magufuli...
kuombea/ibaza za wafu ni chukizo kwa Mungu. baada ya kifo ni hukumu, hata uombe namna gani mtu aliyekufa kama hakutengeneza maisha yake kabla ya kufa huwezi kumtakasa. acheni kupoteza watu, acheni ibada za wafu. kanisa katoliki lina imani ya kupeleka watu motoni moja kwa moja.
 
Back
Top Bottom