i ONCE dated a woman from JF, sikumpata JF na kipindi hicho nilishajiunga na JF ila siku nimepevuka kiasi cha kujali kuficha identity yangu.
Nilikua na Account JF yenye FULL NAME yangu kama kitambulisho ya NIDA,Huyu mdada niseme tu anaonyesha alikua expert wa JF haswaa, (sikua nimejua hilo) siku katika mambo yetu story story kuna kitu tulikua tunabishana akasema tu google.
suggestion sites zikaletwa na malink kibao toka nyuzi zilizofunguliwa JF,kwakua wote tulikua tunaperuzi (nilishika simu yeye akawa ana scroll) hapo tumejilaza.
akagusa link ya JF akasema "tuingie JF" tukawa tumeingia,tukasoma soma mada yetu tulokua tunabshana nayo,baada ya hapo akaniambia mwenyewe "Nina account ya JF nipogo huku kwahyo najuaaa"
nikamuuliza Unatumia jina gani? akaaanza nchekea chekea ila akantajia tukasearch nikamuona,hakuweka profile yake wala jina lake ila ni kweli ilikua account yake.
Hapo sasa mimi nishajifanya siijui JF wala nini nikawa natafuta Upenyo sasa niende "internet cafe" nikamchungulie,maana ile smartphone ilikua n YAKE,mimi nlikua na kitochi tu.
Mambo yakawa mengi nilichelewa kwenda m search nimpekue,siku nikakumbuka,Kuja search Jina lile lile SILIPATI nakutana tu na "no user found", search search nikawa nahisi au nakosea spelling,ila wapiiiiii...nikawa ndo nishakosa chance ya kumjua yule mtoto (tukajaga break up)
nikiwa humu humu nikajaga hisi ni yeye kwa account flani ya MAKISEO Uyo mdada wakujiita makiseo aliweka profile ya mdada copy copy na mtuhumiwa wangu.
nikaanza mfatilia bana,anzisha urafiki na MAKISEO lengo langu najua ni huyo bi shost,kweli makiseo akawa rafiki hatmae mpk tukajuana kwa picha,Siku namuona OG makiseo nikasema Aaaaaaaaah (huyu sio yeye)...
ila ki ukweli Hamna member wa JF anajitaja nnje ya JF sijui n kwann?