Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

warudishe tu, hii ni faida kwa wapinzani nina uhakika 100% wapo wanaCCM wengi wanaoguswa na Richmond moja kwa moja bila ubishi

walianzishe tu
 
Kwa hiyo CHADEMA ambao walikuwa hawana fursa ya kumuhoji Lowassa wakifanya ujinga wa kumuweka Lowassa kwenye list of shame bila kumpa wasaa wa kujieleza na ninyi CCM ambao mulikuwa na fursa ya kumpa wasaa wa kujieleza mnaiga ujinga wa CHADEMA?.

CCM walikopi ujinga wa chadema

kikubwa mwakyembe kasema wao hawakuwa mahakama, ni bunge
 
Waziri wa habari Harrison Mwakyembe amewambia wabunge wa chadema kama wanataka ukweli wa ufisadi wa Richmond warudishe hoja hiyo bungeni.

Haya sasa karibuni kukanyagana maana hii hoja ni mwiba ambao watu wengine hawatakaki hata kuuona!

Ivi tanzania hii. Kuna madaktari na maprofesa. Vilaza kumbe cau
 
Waziri wa habari Harrison Mwakyembe amewambia wabunge wa chadema kama wanataka ukweli wa ufisadi wa Richmond warudishe hoja hiyo bungeni.

Haya sasa karibuni kukanyagana maana hii hoja ni mwiba ambao watu wengine hawatakaki hata kuuona!

Huyu waziri nahisi ana mapungufu san. Yeye kama serikali anaseme mambo ya Richmond yalikwisha kitambo, alafu anasema naomba hilo swala liletwe bungeni alishughulikie kikamilifu tena hata ikibidi aache na uwaziri. Je! ina maana kuna jambo ambalo serikali haikulishughulikia kipindi kile na kama lipo kwa nini yeye na serikali kama wapinga ufisadi hadi kuanzisha mahakama maalumu wasilipeleke hilo swala huko???? Au anategea bunge limpe trip za USA tena???

Mh Askofu Gwajima naomba umfanyie maombi maalum akija kanisani kwako tena.
 
Angalau Umejitahidi kusaidia kujibu Mkuu. Wenzio wanachungulia swali lipo juu ya uwezo wa VYETI vyao.
Lakini nafasi ya kumhoji bado ipo. Akina TL watumie kanuni kurejesha hiyo hoja ili tuyamalize once and for all. Maana wengine tangu tuaminishwe na CHADEMA kuwa EL ndo FISADI number moja Tanzania bado tunaamini hivyo hadi leo.
Hahaha
 
Hivi nyie chadema mnaolilia bungeni kuwa kamati ya Richmond haikumpa fursa ya kusikilizwa nawauliza kwamba ilikuwaje mkamuweka kwenye "LIST OF SHAME" bila kumpa wasaa wa yeye kujielezea??
Wewe kweli hi JINGA LAO hata ulichokiandika hakisomeki
 
Usipende kuweka mawazo yako kwenye mawazo ya wengine.

Ukiniuliza kuhusu Urais nitakujibu hivi,Siyo JPM wala Lowassa wenye uwezo wa kutuongoza.Kama kukosa CDM pamoja na CCM mliingia mkenge.Ni bora CCM wangemweka Chikawe au Judge Ramadhani lakini kwa JPM hamna kitu kuanzia Uongozi mpaka kicwani kwani anafikiria kwa Chuki,visasi na ubaguzi. Hope umenielewa.

Kama ufisadi Lowassa na JPM wote ni mafisadi wametajirika kutumia madeal na wizi wa pesa za Serikali hakuna msafi hapo.
Hata mimi zamani kabla CHADEMA haijauzwa kwa hilo FISADI nilikuwa nafikiria hivo. Ila kwa kuwa niliaminishwa na CHADEMA kuwa EL ndo FISADI number moja, halafu ajabu ndo likabebwa nao na kupewa nafasi ya kugombea urais, nikaona ni Heri JPM maana yeye hata kwenye ile list hakuwemo. Nikampigia kura the less evil.
 
Hakuna mtu yeyote mwenye akili nzuri ambaye anamuunga mkono Lowassa ambaye anaweza kuthubutu hata ndotoni kuleta tena hoja ya Richmond; hii changamoto imetolewa mara nyingi na hakuna aliyethubutu kuichukua. Lowassa alipewa nafasi ya kujitetea mbele ya wabunge wote na mbele ya taifa lote lakini kwa hasira aliamua kuzira uwaziri mkuu kupitia ile hotuba yake maarufu ya "nimedhalilishwa sana".
Kwahiyo wale watanzania wooote qliokuwa naahaba nae hadi wakati wa kampeni wengine wakawa wanazimia kwa kukosa hewa kwa sababu tu ya kumuna na kumsikiliza Lowasa hawana akili? Na kama hakuna mtanzania mwenye akili anayemuunga mkono Lowasa mbona aliwasumbua sana mwaka 2005? Hizo asilimia 56 za kura alizopata ilikuwa ni miti iliyomuunga mkono na sio watu? Na pia kama nyinyi mnajiamini kuwa hakuna mtu mwenye akili anayemuunga mkono Lowasa, mwambie mkuu aruhusu mikutano ya vyama vya siasa just for one week then uone kati yako na watanzania wengi ni nani hana akili!!!
 
Hata mimi zamani kabla CHADEMA haijauzwa kwa hilo FISADI nilikuwa nafikiria hivo. Ila kwa kuwa niliaminishwa na CHADEMA kuwa EL ndo FISADI number moja, halafu ajabu ndo likabebwa nao na kupewa nafasi ya kugombea urais, nikaona ni Heri JPM maana yeye hata kwenye ile list hakuwemo. Nikampigia kura the less evil.

Chadema iliuzwa ulikuwa shahidi number ngapi??Ongea hoja na si viroja.
 
Waziri wa habari Harrison Mwakyembe amewambia wabunge wa chadema kama wanataka ukweli wa ufisadi wa Richmond warudishe hoja hiyo bungeni.

Haya sasa karibuni kukanyagana maana hii hoja ni mwiba ambao watu wengine hawatakaki hata kuuona!


Mimi natka sana kuona mbivu na mbichi lakini Bungeni siyo Mahakamani apeleke mahakamani.Issue amekuwa mkali kama mbogo sababu ameapa kumtetea lile Jambazi lililovamia Clouds
 
Issue ya Richmond irudi Bungeni kufanya nini? hapo Mmwakyembe kamtega Magufuli na sio CHADEMA. Issue hiyo ilipaswa kuwa kwenye the so called ''Mahakama ya Mafisadi'' kitambo sana kama wana grounds za kufanya hivyo na hawaogopi kuwavua nguo wote walioshiriki, akiwamo JK.
 
Tumia akili mangi, mbege imekuharibu - Mamvi ni jizi bobezi

Wewe umeharibiwa na nini?Viroba au MAsogange??Hivi kuna FISADI zaidi ya Paul Makonda?Aliyekwapua Bilion nane za kivuko kibovu ni Lowassa au ni JPM??

Wa barabara mbovu je?Aliyejengewa hotel maneo fulani kama asante toka kwa mkandarasi ni Lowassa??

Kama umelewa Masogange ni juu yako
 
Mkuu katika siasa hakuna pumbu,kuna vitu vinaitwa "destructions". Prof. Mwakyembe amejibu kwa mantinki kwamba ikiwa kesi ya RICHMOND kulikua na "injustice" ya kutokuhoji upande mmoja na maamuzi bado yakatolewa. Hivyo hilo sakata lifufuliwe tena upande wa pili(EL) uhojiwe "which this is inevitable",halafu muda huo awe ameshaachia uwaziri katika harakati. Mwishowe nani wa kudhani suala la mkuu wa mkoa mtalikumbuka ikiwa mnarumbana kuhusu mapapa?

Wana sheria wamemwelewa kwa jinsi yao. "Two wrongs never makes a right", mapungufu ya "RICHMOND" hayamaanishi "negligence" sakata la Bashite. Simtetei Mwakyembe ila kuna jinsi "his logical reasoning" akili za mtanzania wa wastani hawezi kuzielewa.
Huwa anatumia hisia zaidi kuliko akili ndio maana hu panic vibaya

He can only fool wachache sana, sakata la Richmond atake asitake alichemka, hayo maneno ya kusema yafufuliwe ya nyuma there is no need of that

Kutamka kwake kuwa awekwe pembeni kwenye uwaziri ni dhahiri kabisa kakubali uozo wake Wa nyuma
 
Wewe umeharibiwa na nini?Viroba au MAsogange??Hivi kuna FISADI zaidi ya Paul Makonda?Aliyekwapua Bilion nane za kivuko kibovu ni Lowassa au ni JPM??

Wa barabara mbovu je?Aliyejengewa hotel maneo fulani kama asante toka kwa mkandarasi ni Lowassa??

Kama umelewa Masogange ni juu yako
Uko sawa bwashee mangi, hudumia wateja kwanza hapo dukani - matusi ya mitandaoni hayasaidii
 
Huwa anatumia hisia zaidi kuliko akili ndio maana hu panic vibaya

He can only fool wachache sana, sakata la Richmond atake asitake alichemka, hayo maneno ya kusema yafufuliwe ya nyuma there is no need of that

Kutamka kwake kuwa awekwe pembeni kwenye uwaziri ni dhahiri kabisa kakubali uozo wake Wa nyuma
Kufufuliwa kwa RICHMOND kwake ni ahueni, atakimbia majanga mawili kwa mpigo. Mzigo wa ofisi ya uwaziri pili kufanya kazi na Mkuu. Kuna malalamiko mengi kuhusu mahusiano kazini kutoka kwa Mkuu, pia itakua nafasi kwake kutotoa dukuduku alilonalo moyoni kuhusu EL.
 
Mwakyembe ajibu hoja siyo kwakuwa ana platform ya kusemea ndiyo aitumie negately!Ajibu maswali haya Clouds Media ilivamiwa au haikuvamiwa ,Je mamlaka hiyo ilikuwa na uhalali wa kufanya hivyo?Nani kimamlaka yupo juu ya mwenzake kati ya RC na Waziri?RC ni kweli hakupewa wasaa akaimbia timu iliyotakiwa kuongea naye?Kuhusu Edward maamuzi Yale ya Richmond aliyafanya yeye peke yake au yalifanyika ndani ya baraza la mawaziri ambalo lina m/kiti na wajumbe?Kama anatuaminisha kuwa watamnyoa kwa vipande vya chupa kuna sheria inayoruhusu hayo kutendeka au anapiga propaganda?Vipi kuhusu watuhumiwa wengine?Halafu huyu Mwakyembe mbona akitajiwa Edward huwa anapandwa na 'mzuka'?
 
Uko sawa bwashee mangi, hudumia wateja kwanza hapo dukani - matusi ya mitandaoni hayasaidii

Nimemtukana nani??Mie duka langu linaendelea vizuri,nalipa kodi na ninapata chakula kwa watoto na familia yangu
 
Mnaojua mnijuze maana naona ni kama hili jambo linafanywa "kimazingaombwe".Mods naomba msiunganishe huu uzi ili tufahamishane kinaga ubaga!
 
Back
Top Bottom