Mwalimu ajinyonga huko Moshi kisa riba kubwa ya mkopo

Mwalimu ajinyonga huko Moshi kisa riba kubwa ya mkopo

Mwalimu wa shule ya sekondari ya Ebenezer iliyopo Sango mkoanikilimanjaro, Anthony Sulle amefariki dunia kwa kujinyonga.

Habari kutoka Moshi zinadai kuwa kabla ya kujinyonga marehemu aliandika ujumbe unaoelezea kisa cha yeye kuchukua maamuzi hayo magumu.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, ujumbe huo unadai kisa cha marehemu kuchukua maamuzi hayo ni kitendo cha Mwajiri wao kuwapa mikopo walimu yenye riba kibwa (kaushadamu)

Ujumbe huo unadai kuwa riba hiyo kubwa imemfanya kuishi kwa shida kwani kila mwisho wa mwezi amekiwa akijikuta hana chochote.

Hata hivyo mmoja wa wakurugenzi wa shule hiyo, Doreen makundi hakuwa tayari kuzungumzia tukio hilo kwa kile alichodai hahusiki Kwa namna yoyote.

Kazi kwenu waalimu na mikopo kausha damu.
Watumishi wote wenye kipato duni kukopa nikama tabia, hata kama hana haja muhimu atakopa tu hysusani waalimu,......waalimu wangesitisha kukopa kwa miaka 10 tu benki nyingi zitafungwa na matajiri wengi watafirisika kabisa
 
Mwalimu mjinga na amejaa tamaa alivyochukua mkopo hakuona kama riba ni kubwa??je alilazimishwa? Mwalimu anapigwa maisha anakimbilia kujiua napata mashaka na quality ya alichokuwa anafudhisha watoto wetu.
Una umri gani? Waswahili walisema kua uyaone. Miaka ya nyuma kuna dada mmoja alijinyonga na tulipokuwa kwenye mazishi yake kuna jamaa mmoja alitoa maneno makali kuliko ya kwako. Alikuwa anakashifu na akawa anacheka kama yuko kwenye sherehe. Haikupita miezi sita tukasikia jamaa naye kanywa sumu. Siyo kwamba nakutisha wala nasema na wewe utafikwa na jambo baya, la hasha. Nataka kukujulisha kuwa mtu anayejinyonga anakuwa hayuko kwenye mental state yake ya kawaida. Wengi wanaweza kuwa wanaugua depression hivyo akili zinabadilika kabisa na kuona hakuna faida ya kuishi. Kwa kifupi elewa tu kuwa siyo yeye anafanya maamuzi bali kuna nguvu ambayo inamuongoza.
 
Pole sana,nadhani marehemu kuna sehemu kaficha,salary slip yangu haipumui ila sina mpango wa kujinyonga na wala sijawahi hlkuwaza huu upuuzi,yeye kakwama wapi?

Mimi nikisikia habari za taasisi kukopesha fedha lazima nitie mguu,poor and coward teacher kafa na kuacha huzuni kwa ndugu
Una roho ngumu sana🤣
 
Waalimu wakiambiwa waikatae CCM kwani inahusika na madhila yote wanayopitia kikokotoo, mshashara duni, inapelekea kujiingiza ktk mikopo ya riba kubwa lakini hawa waalimu wanakataa siyo CCM inayosababisha haya yote kwa uchache hapo juu.
 
Pole sana,nadhani marehemu kuna sehemu kaficha,salary slip yangu haipumui ila sina mpango wa kujinyonga na wala sijawahi hlkuwaza huu upuuzi,yeye kakwama wapi?

Mimi nikisikia habari za taasisi kukopesha fedha lazima nitie mguu,poor and coward teacher kafa na kuacha huzuni kwa ndugu
Inawezekana kuchukua mikopo mingi kama hivyo?


Hadi Platinum inaonekana kwenye salary slip?
 
Back
Top Bottom