Mwalimu aliyeshtakiwa kwa kumbaka Mwanafunzi ahukumiwa miaka 30 jela. Mwanafunzi afukuzwa shule

Mwalimu aliyeshtakiwa kwa kumbaka Mwanafunzi ahukumiwa miaka 30 jela. Mwanafunzi afukuzwa shule

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Habari wanaJamiiForums,

Mwalimu George Ngallu wa Mahiwa Sekondari aliyekuwa na kesi mahakamani ya kufanya ngono na mwanafunzi wake wa kidato cha tano 2019/20 katika mchepuo wa History, Geography na Kiswahili (HGK) amakutwa na hatia na amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kuanzia tarehe 14/08/2020.

Hata hivyo Mwanafunzi naye alifukuzwa Shule na Bodi ya Shule na hata alipokata rufaa, bado Bodi ya rufaa ya Mkoa iliona bodi ya Shule ilikuwa sahihi na adhabu ya kufukuzwa Shule iliendelea.

=======

Taarifa husika iliripotiwa kama ifuatavyo;


Mwalimu kizimbani kwa tuhuma ya kumbaka mwanafunzi wake

Mwalimu wa Shule ya Sekondari Mahiwa, wilaya na mkoa wa Lindi, John Ngalu (38) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya mkoa wa Lindi kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake anayesoma kidato cha tano.

Hayo yalielezwa jana na wakili wa serikali, Juma Maige alipozungumza na Muungwana Blog, ofisini mwake mjini Lindi.

Maige alisema Ngalu alipandishwa kizimbani tarehe 5 mwezi huu baada ya kufunguliwa kesi ya jinai yenye namba za jalada 4/2020, na kuongeza kuwa kitendo hicho kilifanyika kwenye nyumba anayoishi mwalimu huyo. Ambayo ipo katika eneo la shule hiyo.

Alisema mshitakiwa huyo alikutwa usiku baada baadhi ya wananchi ambao ni raia wema kutoa taarifa,kwa wananchi wenzao ambao walipokwenda eneo la tukio walimkuta akifanya mapenzi na mwanafunzi wake huyo.

Maige alisema inadaiwa kuwa kitendo cha namna hiyo kwa mwalimu huyo na mwanafunzi wake ni cha muda mrefu. Hali iliyo sababisha wananchi hao wamchoke na kuamua kumkamata.

Kesi hiyo itaendelea tena tarehe 13 Februari 2020. Huku Ngalu akirudishwa mahabusu baada kushindwa kutekeleza vigezo na masharti ya dhamana.

Chanzo: muhabarishaji.com
 
Hata mtendwa anahukumiwa? Ama kulikua na viashiria vya mwanafunzi kumtega mwalimu ila ishu ikavuja kuwa kalalwa na mwalimu wazazi wakafungua mashtaka ya mtoto wao kubakwa
 
ukipita
Shule nyingi za mikoani mabinti wengi ni wakubwa na wanakua na mitego sana kwa walimu, bila umakini unaishia jela huku unajiona

Ukipita stend jioni unakutana na mtoto wa kike amejichubua...amenyoa sijui kiduku..kisket kifupii na kapaka wanja...Bora sikuwa mwalimu..ningefukuza shule aisee!sijui watoto wahivyo wanatokea familia yenye baba na mama kweli?
 
serikali wangeruhusu tu kama ulaya ruhusa kutembea na msichana miaka 16-17 kama tuu amekukubalia kwa ridhaa yake bila kumhonga hela sigara, bangi ama pombe. Ila kwa walimu na wakufunzi akitembea na hawa 16-17 adhabu inamfaa lakini isizidi miaka 6.
Kwa mazingira ya yetu haiwezekani,mtu ana mke anamrubuni mwanafunzi kwa ajili ya ngono unategemea asimhonge?nani atamkubalia,tutaishia kuharibu maisha yao tu

Na wakiruhusu mpaka wenye 13 au 14 watachenjuliwa tu,kisa wamekubali, wabongo sio watu!
 
faulo kama hizo zinapigwa mbali...na surveillances ya kutosha

*wale wa kula kimasihara wanalo la kuongezea,karibuni mtiririke inakuwaje ticha amedakwa na mvua30 juu
 
Atatoka akiwa na miaka 68. Wanafunzi munipitie mbali, tena mbali sana .
 
watetezi wa haki za wanawake mbona mko kimya hapa, simamieni na hili sasa..

Mama kafukuzwa shule, Baba wa mtoto jela 30yrs.
Mtoto akizaliwa baba yake yuko jela na mama yake kafukuzwa shule, what a future for this innocent kid..
 
Hizi sheria ziangaliwe upya na hawa mabinti itafutwe namna nyingine ya kuwalinda, kifupi hapa hakuna haki na kiumbe kitakachozaliwa kinaweza kufungua kesi na kudai fidia kubwa kwa kuharibiwa future na waliomfukuza mama na kumfunga jela baba..
 
Back
Top Bottom