Fall Army Worm
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 19,355
- 14,408
Ndio uonezi huo.Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ndio uonezi huo.Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake.
Wenye maisha mazuri hawaandiki hiviKumbuka huyu mwalimu alikuwa na madeni lukuki, kabla ya adhabu hiyo alikuwa na makato mengi.
Kazi ya ualimu ina laana, maana Walimu wengi wanaishi maisha magumu.
Labda aje mwenyewe atueleze yaliyomkuta. Sad storyNi elfu thelathini na nne(34000).Mr.Ban huyu mwalimu ni graduate, ana degree kutoka UDSM.
Nusu mshahara 34000!!!!
Naamini kuna zaidi ya haya uliyoandika. Umewahoji waajiri wake au viongozi wake shuleni alikokuwa akifundisha? Umemhoji yeye mwenyewe akakupa uhalisia wa maswahibu yake? Umemhoji hata mtu wake wa karibu?Nimesikitishwa kupata habari kuhusu mwalimu anayefundisha shule ya sekondari Dunda iliyopo Bagamoyo mkoa wa Pwani kukimbia kazi ya ualimu baada ya kulipwa 34000 kwa mwezi.
Hii inatokana na adhabu ya kushushwa cheo na kulipwa nusu mshahara na Tume ya Utumishi wa Walimu kwa kosa la utoro kazini.
Mwalimu huyo wa kike aliishi maisha magumu sana hapo hapo shuleni ,alikosa mpaka hela ya kula ilimlazimu auze miwa na maembe aliyoyaokota hapo shuleni ili apate pesa ya kula.
Uzalendo ukamshinda baada ya mazingira magumu ya kazi aliamua kuondoka kazini bila ya taarifa kwa muajiri.
Habari nilizozipata mwalimu huyo yupo Mlandizi akifanya kazi ya kuhudumia wateja bar.
TSC mnapotoa adhabu ya kupunguza mishahara kwa walimu mzingatie iwapo kama mtuhumiwa ana mikopo benki, isitoshe adhabu ya kupunguza mshahara ni ya kikatili maana mshahara wenyewe hautoshi hapo hapo mnaupunguza.
Habari nilizozipata huyu mwalimu alikuwa na madeni benki na taasisi za fedha hapo Bagamoyo.
Kutokana na mazingira magumu ya kazi mwalimu huyo kaamua kutelekeza kazi yake.
Walimu Wenzake wanaishijeKumbuka huyu mwalimu alikuwa na madeni lukuki, kabla ya adhabu hiyo alikuwa na makato mengi.
Kazi ya ualimu ina laana, maana Walimu wengi wanaishi maisha magumu.
Kima cha chini kwa mwl mwenye certificate ni sh ngapiWalimu waboreshewe maslahi kama wabunge.
Nilisikia report ya katibu mkuu wa tume ya Utumishi wa Walimu kwamba asilimia 50 ya Walimu wamefukuzwa kazi kwa utoro baada ya kuishi ktk mazingira magumu.
Mbona hatusikii idadi hiyo kuacha kazi Benki Kuu, TRA, Uhamiaji, Bandari, Jeshi?
Ndio alipwe 34000 kwa mwezi?Wanawake wanapitia mengi, huendi alimnyima mtu uchi, kwa hiyo kosa dogo anaadhibiwa pakubwa angalau alegeze sketi
Umeifafanua vzr, nadhani mlalamikaji ana mikopo mingi, kupanga ni kuchaguaWa zamani sio siku hizi.
Graduate anavuta sio chini ya laki 8 akiwa na masters anavuta 1.8.
Ukipata Kazi ya ualimu omba vijijini life is simple Hakuna kufatiliana baada ya Kazi piga ujasilimali.
Timiza wajibu wako wasome wasisome shauri yao na wazazi wao ukijifanya unawafatilia fatilia Ili wasome watakuroga.
Anaetaka kusoma mpe ushirikiano.
Wikiendi kuwa bize kwenye mishe zako.
Usiingize siasa kwenye Kila mjadalaLaana ya Walimu wa Tanzania kutumika na CCM kuiba kura
Nini maana ya net payLet’s say alikuwa na netpay ya 468,000 na jumla ya makato yalikuwa 200,000.
Ukiigawa nusu na bank wakakata chao unabaki na 34,000 ikutunze kwa siku 30 zijazo. Mmmmae naacha kazi.
Mwajiriwa na madeni ni pete na kidole, pengine ukute huo utoro kazini chanzo ni kujiongeza kutafuta kipato cha ziada baada ya maisha kuwa magumu pale unapokopa na kuwekeza kwenye ujenzi na pesa ikakata kwenye renta.
Kuwafungulia code wanaodharau Kazi ya ualimu, walimu wengi wamejenga nyumba za kisasa nzuri tu.True pia fursa nyingi mjini.
Maisha ni akili
390000 mkononi basic ni 419000Kima cha chini kwa mwl mwenye certificate ni sh ngapi
Mkuu umeshawahi pitia maisha ya kipato cha chini kama ya walimu wa msingi na hata sekondari? Unadhani kwa huo mshahara wake anaweza hata kukopa milioni kumi au anaenda kukopa ili anunue gari au afanyie biashara kubwa? Ukiwa na kipato kama cha hawa walimu, mkopo wenyewe hata haufiki milioni 5, halafu unakuta amekopa pesa hiyo labda aweke sawa mambo ya familia kama kulipa ada, kujenga choo, n.k.Sijauliza anadaiwa na taasisi ipi, nimeuliza peza za mikopo ziko wapi?
Mi nimeuliza mkopo aliokopa uko wapi? Wewe unaleta risala? What for? Kama kachinmba choo tupewe jibu, kama kaenda kulipa ada tupewe jibu, simple.Mkuu umeshawahi pitia maisha ya kipato cha chini kama ya walimu wa msingi na hata sekondari? Unadhani kwa huo mshahara wake anaweza hata kukopa milioni kumi au anaenda kukopa ili anunue gari au afanyie biashara kubwa? Ukiwa na kipato kama cha hawa walimu, mkopo wenyewe hata haufiki milioni 5, halafu unakuta amekopa pesa hiyo labda aweke sawa mambo ya familia kama kulipa ada, kujenga choo, n.k.
Pia tukumbuke si kila mkopo unaenda kuzalisha na si kila mkopo uliochukuliwa ukazalishe utafanikiwa kwa hizi riba zetu Tanzania. Wanaofanikiwa kirahisi ni wale wanaokopa, huku pembeni wanakula kwa urefu wa kamba zao. Sasa mwalimu wa watu hawezi kula chaki.
Yeye ndio laana,hakuna mshahara wa hivyoKumbuka huyu mwalimu alikuwa na madeni lukuki, kabla ya adhabu hiyo alikuwa na makato mengi.
Kazi ya ualimu ina laana, maana Walimu wengi wanaishi maisha magumu.
Hata mimi nashangaa sana.Nusu mshahara 34000!!!!