Mwana FA: Kuendesha timu Kabla ya kukamilisha taratibu za kisheria za uwekezaji chanzo cha Mgogoro Simba

Mwana FA: Kuendesha timu Kabla ya kukamilisha taratibu za kisheria za uwekezaji chanzo cha Mgogoro Simba

Sasa huyo mwana Fa km alijua yote hayo mbona hakusema hapo kabla, na kwann hakushauri kuwa mchakato ukamilike afu ndo mengine yaendelee?

Tukio la Yanga yeye anaisemea Simba, inahusuuu? Hata km aliongea akiwa Naibu waziri bado hakukua na haja. Aache unafiki huyu rafiki wa tajiri mtata.

Mxxxxiiiiiieeeew.
Yeye ni Naibu Waziri kanena kama serikali. Na kasema Wazi wao kama serikali walinyamaza ili kupisha viongozi na wanachama kumaliza Mambo Yao wenyewe lakini si kama hawaoni. Akaongeza kama Hali itaendelea wataingilia Kati kama regulator. Unafiki wake uko wapi?
 
Serikali itoe tamko kwamba kinachoendelea kufanyika Simba siyo sahihi na iamuru utaratibu ufuatwe na ikiwezekana mchakato uanze upya chini ya katiba inayotambuliwa na serikali pamoja na TFF,haiwezekani serikali itoe maelekezo halafu muda unaenda bila maelekezo yake kufanyiwa kazi halafu yenyewe nayo iseme inasubiri tu! Hadi lini? Na tayari mvurugano ushaanza kutokea kwahiyo ni wakati sasa serikali ichukue jukumu lake kama baba mlezi wa kila kitu hapa nchini.
Namuunga mkono.
 
Yeye ni Naibu Waziri kanena kama serikali. Na kasema Wazi wao kama serikali walinyamaza ili kupisha viongozi na wanachama kumaliza Mambo Yao wenyewe lakini si kama hawaoni. Akaongeza kama Hali itaendelea wataingilia Kati kama regulator. Unafiki wake uko wapi?
Hii serikali inachochea fujo tayari wanajua tatizo lipo wapi Ila wamekata kimya
 
Sio kweli, Yanga wameanza mchakato ila bado tu kukamilika.

Yanga wao walianza na kufanya tathimini ya mfumo sahihi wa uendeshaji wa klabu kupitia La Liga.
Mchakato huo ukakamilika kwa kupewa mapendekezo na wakaanza kuyafanyia kazi kwa kuanza na katiba mpya. Ikaandaliwa katiba mpya kisha wakaiwasilisha ili ipitiwe na kisha ipitishwe. Katiba ikapitishwa na serikali na pia wanachama wa Yanga.

Hersi Saidi aliwahi kuzungumzia kuhusu mabadiliko ya kimfumo na kiutendaji kuwawameweka muundo bora wa uongozi ili kuhakikisha wawekezaji wanaokuja kuwekeza kwenye klabu hiyo wanapata manufaa wanayoyataka badala kufanyiwa ujanja ujanja.

"Tunajenga mfumo ambao mwekezaji akija anakuta muundo bora wa utawala, kimapato. Malengo yetu ni kuhakikisha kuwa na timu imara kiuchumi ili yule anayekuja awe na uhakika wa kile anachowekeza kwenye timu.

"Hivyo tumezingatia sana usalama wa biashara kwa kila ambaye ana nia ya kuwekeza kwenye Klabu yetu." Mwisho wa kumnukuu.

Tarehe 1 mwezi wa 4 Hersi akaja kuzungumzia kuwa wanaanza mchakato wa kuifanya Yanga kuwa kampuni na aliongea vyema sana kwa kutoa ufafanuzi juu ya hiyo hatua. Ila sijajua hiyo hatua imefikia wapi

Yanga walikuwa wawazi wawekezaji wanakuja hawatagusa Mali za yanga Ila mo hata hdjakamilisha uwekezaji alitaka hati ya jengo la Msimbazi,, uwanja wa Bunju anataka uitwe jina lake.
 
Yeye ni Naibu Waziri kanena kama serikali. Na kasema Wazi wao kama serikali walinyamaza ili kupisha viongozi na wanachama kumaliza Mambo Yao wenyewe lakini si kama hawaoni. Akaongeza kama Hali itaendelea wataingilia Kati kama regulator. Unafiki wake uko wapi?
Em soma vizuri nilicho kiandika, kwakua wee ni uto huwezi elewa.
 
Watu wanazunguka Sana, tatizo la Simba ni mo, kabla ya kuja Simba mo alimiliki timu mbili na zote zikamshinda. African Lyon na mto Singida.
Mo alipotaka kuingia Simba alikuja na thamani yake apewe kwa bilioni 20, awe na hisa 51 lakini baada ya malumbano serikali. Ikaingilia Kati na kutunga kanuni kuwa vilabu vya wanachama Kama Simba na yanga vinatakiwa kuwa na wawekezaji wasiopungua watatu na wapewe hisa zisizozidi 49.
Mo bado alitumia ushawishi wake hizo hisa 49 awe mmiliki pekee na alianza kutoa pesa kabla mchakato haujaanza ili mradi yeye mwenyewe apitishwe. Lakini imebainika hata hizo bilioni 20 hajatoa badala yake anataka kugeuza misaada aliyotoa ndio iwe hisa zake.
Nia ya Simba kutafuta mwekezaji ilikuwa kufanya klabu ijitegemee na kuwa klabu kubwa zaidi Afrika . Swali la kujiuliza tangia mo ajishigulishe na Simba Nini kimeongezeka kwani rasilimali Kama jengo la msimbazi na uwanja wa Bunju alivikuta.

Alipinga mkataba wa Simba na Azam ambao wangeingia kwa miaka 10 na Simba kupata bilioni 40 kuwa hauendani na thamani ya Simba wakati yeye ametaka apewe asilimia 49 kwa pesa ambayo ni nusu ya thamani ya mkataba.
Amewazuia Simba kuingia mkataba na NIC ili atangaze kampuni zake ambazo zinatoa pesa kiduchu.
Simba wakubali walifanya makosa wake chini na kuanza upya.
 
Kuna mambo yanashangaza sana! Serikali kupitia vyombo vyake kama FCC na BMT tayari wameshaweka muongozo kwamba uwekezaji unaotakiwa ni wanachama wamiliki hisa 51% na mwekezaji awe na hisa 49% tena mwekezaji asiwe mmoja lakini kinatokea kikundi cha watu wachache kwa sababu ya maslahi yao binafsi wanapindisha pindisha halafu tena serikali hiyo hiyo inasema eti inawaachia wenyewe kwanza wamalizane wakishindwa ndipo serikali iingilie kati sasa sijui inasubiri timu ivurugike kiasi cha kukosekana amani ndipo watajua wameshindwa! Wakati ndiyo huu serikali iingilie kati kuinusuru Simba kwa maslahi ya walio wengi.
Kweli tunataka timu ifanye vizuri sisi mashabiki ndiyo raha yetu lakini siyo kwa mtu mmoja kuipora timu kwa sababu ya fedha zake.
Ikumbukwe kwa kanuni za FIFA serekali haipaswi kuingilia maswala ya ndani kuanzia TFF na Vilabu vyake, Serekali inasimamia sheria na kutoa ushauri tu.
 
Ikumbukwe kwa kanuni za FIFA serekali haipaswi kuingilia maswala ya ndani kuanzia TFF na Vilabu vyake, Serekali inasimamia sheria na kutoa ushauri tu.
Simba Sports Club ni zaidi ya mpira wa miguu ambao unasimamiwa na FIFA. Ni club ya michezo mingi. FIFA wanadeal na sehemu ya mpira wa miguu tu. Sasa serikali lazima ihakikishe hii club inayotaka kuwa kampuni kuwa inafuata taratibu.
 
Simba Sports Club ni zaidi ya mpira wa miguu ambao unasimamiwa na FIFA. Ni club ya michezo mingi. FIFA wanadeal na sehemu ya mpira wa miguu tu. Sasa serikali lazima ihakikishe hii club inayotaka kuwa kampuni kuwa inafuata taratibu.
Kuna Mambo serikali haiingilii Ila mengine wanaingilia ndio maana fbi waliweza kuingilia na kumtoa Blater.
Kama serikali ndio ilitunga kanuni kwanini ishindwe kusimamia.
 
Mtindo ni uleule ukikosa hoja unamwamishia Mtu upande wa pili. Ignored.
Nimekuambia soma vizuri andiko langu, sasa huo msuso unahusu nn hapa? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ikumbukwe kwa kanuni za FIFA serekali haipaswi kuingilia maswala ya ndani kuanzia TFF na Vilabu vyake, Serekali inasimamia sheria na kutoa ushauri tu.
Serikali hairuhusiwi kuingilia sheria na kanuni za uendeshaji soka lakini suala usajili na usimamizi wa vyama na vilabu na kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa ni jukumu la serikali, hakuna chama cha soka wala klabu isiyo sajiliwa na mamlaka ya nchi husika ikaruhusiwa kufanya kazi katika nchi hiyo.
 
Serikali hairuhusiwi kuingilia sheria na kanuni za uendeshaji soka lakini suala usajili na usimamizi wa vyama na vilabu na kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa ni jukumu la serikali, hakuna chama cha soka wala klabu isiyo sajiliwa na mamlaka ya nchi husika ikaruhusiwa kufanya kazi katika nchi hiyo.
Issue iliyobaki kwenye mchakoto wa simba inapaswa kumalizwa na wanasimba wenyewe ndani, kwa mujibu wa katiba yao.
 
Wewe na mjumbe wa Bodi wa Simba upande wa wanachama Tena ana cpa nani anajua zaidi
mbona mjumbe yuko wazi pesa ipo imewekwa equity na simba wanapata gawio lao la 200M kila mwezi, Haya ni maneno ya mwenyekiti wa Simba Mangungu
 
Back
Top Bottom