TANZIA Mwana JamiiForums Miguu ya Kuku/ Mpauko afariki dunia

TANZIA Mwana JamiiForums Miguu ya Kuku/ Mpauko afariki dunia

Pole sana ila mshukuru Mungu kwa yote. Hukutimiza ahadi lakini dhamira yako ilikua njema.
Mwenyewe sikutimiza nilichomuahidi 2018 sababu mtu tuliekua tunamtegemea atusaidie alitolewa nafasi aliyokuwepo ambayo ingekua rahisi Robin kusaidika.

Early January alinicheck sikumjibu kwa wakati mpaka message zikafutika kwenye simu na namba ikapotelea huko. Labda ningejibu message yake that day ningeweza kumuokoa na hatua aliyoichukua.

Bwana ametoa na bwana ametwaa apumzike kwa amani Robin [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120] Avriel,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu ,nimeletwa kwenye uzi husika. uzi wa Mshana umeunganishwa .
uziwa wa Mshana jr ulianza ba kivhwa kisemacho Tumetanzika halafu ,kwenye maelezo yake bi lawama tu..
Binafsi nyuzi zenye lawama tu huelewi zimeanzia wapi ,huwa nakuwa ba wasiwasi , ndiyo maana nikataka kufahamu zaidi. Ahsante.
Ooh sawa mzee...
kumbe wame ku redirect.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umasikini kitu kibaya sana, kwangu huyu ndio anakua adui namba moja, namba mbili na namba tatu. 1.6M imehangaisha mtu namna hii?

Sitaki nipate pesa nyingi na mali nikufuru lakini niwe na uwezo wa kukidhi mahitaji yangu na kusaidia wahitaji, ntakua nimeishi maisha ya amani na kufanikisha kitu kikubwa sana maishani mwangu.

Avriel usife moyo, ulifanya ulichoweza, nafasi bado zipo. Tuombe uzima. Barikiwa sana
 
Tumepoteza watu wawili ndani ya muda mfupi ambao walihitaji msaada kwetu ambao ni fasi dwasi na mpauko. Tunatakiwa tujitafakari, tunakwama wapi. Halafu pia wale ambao tumezoea kukejeli kwenye nyuzi za wahitaji tuache hiyo tabia, tunaongeza maumivu kwa wahitaji.

Kama unaona huna uwezo wa kumsaidia kifedha au kwa namna yoyote inayohusisha matumizi ya kile ulichonacho basi msaidie hata ushauri. Kama unaona hata kumpa ushauri huwezi basi ni vyema ukapita kimya.

Dunia inazunguka, inaweza kutokea siku na wewe ukalazimika kuomba msaada humu, na utaweza kuona maumivu ya mtu kukejeli tatizo lako yanavyouma kuliko tatizo lenyewe. Jf ina deni.
 
Daaahhh kwa hakika Dunia sio makazi yetu.

Kijana aliwah nifata PM kwa msaada wa Afya, kutokana na Umbali wa eneo alilokuwepo namm nilipo ,nikaplan kumuunga na Rafiki angu Daktar pia yupo Eneo hilo.


Kwa Bahati mbaya Huyu Rafiki akawa naye kasafiri , hivo nikamwambia kijana asubiri.


Ujumbe wa mwisho alisema " Nisaidie kaka kuniunga nao kama wanaweza kunisaidia".



Pumzika kwa Amani Ndugu, nyuma yako tupo !!.
 
Mkuu eti inawezekana mdogo wa marehemu atumie simu ya aliyekufa kwa muda wote huo, bila hata kubadili sim card. Sasa ana lengo gani nayo. Hatujui.
Mimi nilipewa simu ya babu yangu nikae nayo alipokufa baada ya miezi miwili nikaizima.
Kumbe baada ya miezi miwili ukaizima na huyo mdogo wake kaiacha kwa mwezi mmoja sasa labda ikifika wa pili ataizima kama wewe ulivyoizima ya babu yako.

Mnaacha kuongelea mambo ya maana mnaongelea habari za kuzima simu mpaka mnajiumbua wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana Jr,
Mimi niliwahi kuandika huu uzi.....


Nimeandika thread hii baada ya kuona ongezeko la thread za members wa JF wakitishia au wakitoa thread zenye mawazo ya muelekeo wa kujiua/ kukata tamaa ya maisha.

Pia, naelewa kuwa hiki nitakachosema kinaweza kisiwe kilifikiriwa mwanzoni na waanzishaji wa JF. Lakini ni kitu kizuri kama watafiikiria kukifanya.

Kwa social medias za nchi za wenzetu, kwa mfano Facebook, wana njia ambazo mtumiaji wa Facebook anaweza kuripoti post ambayo imekaa kiuelekeo wa mtu kuwa na suicidal thoughts, then kuna taratibu wanafanya nadhani kupitia 'hot lines' kwa wataalamu wa saikolojia kuweza kuwasiliana na mhusika na kumpa msaada wa counselling (sifahamu the exact procedure wanafanyeje, lakini najua kuna kitu wanafanya kwa watu wanaopost post za aina hiyo).

Sasa challenge kwa waanzilishi wa JF, je, hawaoni kama kuna umuhimu pia wa kuweza kuweka mechanism ya aina hiyo? Watu ambao wanapost thread za kutaka kujiua au kukata tamaa ya maisha, post zao zinakua identified, na ID zao, then wanakua contacted (na wanasaikolojia) kwa maongezi kupitia PM... kama wakiafiki na wakawa tayari kutoa mawasiliano yao ya simu, wanaweza kufikiwa pia kwa njia ya simu kwa kupigiwa kupitia a 'hot line' ambayo itakua imekua established.

Hii inaweza kusaidia sana pia hata wale wenye msongo wa mawazo tu na matatizo ya kisaikolojia (wako wengi sana humu, kwa kuangalia tu post watu wengi wametingwa sana, vichwa vyao vimejaa misongo).

JF inaweza ikawa link ya muhimu kati ya hawa watu na wanasaikolojia kupitia utaratibu maalum ambao utaruhusu anonymity ya mtu kuwa preserved if they wish so.

Kama waanzilishi wa JF mtakuwa tayari, mimi niko tayari kuandika a write-up ya kuombea fund hii idea BURE KABISA, ambayo mnaweza kuipeleka kwa potential NGOs ambazo ziko interested na mental and social health they might be interested.

Au, mnaweza kufanya hata kama ni kwa scope kidogo kwanza kwa kadri ya uwezo wenu bila kuhitaji a lot of funds.

What do you think guys?
Maxence Melo Moderator Invisible

Ila wadau wengi hawakunielewa kabisa, na wengine walinituhumu nina multiple IDs, natafuta kiki.
Nadhani ni muda wa kufanya kitu sasa.
Mshana Jr
 
Back
Top Bottom