Pre GE2025 Mwana JF, Be The First to Know CCM Ndie The Overall Winner wa Uchaguzi Mkuu wa 2025 Kufuatia Ushindi Serikali za Mitaa。CCM Amekomba Almost Everything!

Pre GE2025 Mwana JF, Be The First to Know CCM Ndie The Overall Winner wa Uchaguzi Mkuu wa 2025 Kufuatia Ushindi Serikali za Mitaa。CCM Amekomba Almost Everything!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wana JF,

Maadam JF ni ukumbi wetu, na sisi humu JF, tuko members wengi, na tumefanya mengi, hivyo mimi member mwenzenu Pascal Mayalla, naomba niwe wa kwanza, kuwajulisha wana JF wenzangu, ili kuwapa ile JF advantage ya wewe kama Mwana JF, be the first to know kuwa CCM ndio mshindi wa jumla wa Uchaguzi Mkuu wa 2025 kufuatia ushindi wa kishindo wa uchaguzi huu wa Serikali za mitaa kwa a landslide victory ya ushindi wa kishindo, kwa kwa kukomba almost everything,kila mtaa,kila kata,kila kitongoji na kila kijiji, hivyo mshindi wa serikali ya mtaa mwaka huu, ndie mshindi wa uchaguzi mkuu wa 2025!。

Ushindi huu ni kufuatia mimi mwana JF mwenzenu, Pasco Mayalla, nimesikia sauti ndani ya moyo wangu, yaani ile "voices from within", kuwa katika uchaguzi huu, wa serikali za mitaa, mshindi wa jumla ni CCM!, ndie anayekwenda kushinda uchaguzi wa 2025!。

Hii voices from within yangu is never wrong, maana ni sauti yake YEYE mwenyewe!,aliye ndani yangu!。

Lengo la uzi huu sio kutangaza ushindi wa CCM uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu 2024, bali kuutangaza kinachokwenda kutokea uchaguzi Mkuu wa 2025!, kwasababu kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa tulishauri Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana! haya sasa ni matokeo!

Kufuatia wengi hawana muda kusoma makitu marefu,wale wa short and clear mnaweza kuishia hapa na ku jump kwenye conclusion
Mjue Pasco
Sasa kwa faida ya wasionijua, mimi Pasco Mayalla, ili muweze kuamini ninachowaambia ni kitu cha kweli na ndio kinatokea, naomba niwape ushuhuda mdogo wa nimewahi kuwa wa kwanza kwenye mambo mengi tu, ambayo wana jf hamjui, je wewe mwana JF mwenzangu, wajua mimi Mwana JF mwenzako Pasco Mayalla, nimewahi kuwa Mtanzania wa kwanza kwenye mambo mengi tuu, ikiwemo humu JF, mimi ndiye Mwana JF wa kwanza kuwa kada wa Chama Cha Siasa? Tuanzie hapa
  1. Tangu kuanzishwa kwake, japo JF ina members wengi wa fani tofauti tofauti, lakini Pascal Mayalla, ndiye member wa kwanza kuwa recognized na modes wa JF kuwa ni kada wa chama fulani cha siasa, hivyo kuna wakati nilikuwa nikipost chochote humu JF, chini kuna maandishi hutokea automatically yameandikwa "Pasco Mayalla sasa ni Kada wa Chama cha Mapinduzi, CCM", hii haina maana humu JF, kada wa chama cha siasa ni mimi tuu peke yangu, but it just happened, mimi ndie the first member wa JF, kuwa kada wa chama cha siasa!. Japo najua tuna makada wengi humu wa vyama vya siasa, na sijawahi kuona kada yoyote mwingine akiandikwa so and so ni kada wa chama fulani, then this means, mimi ndiye the first JF member to be kada wa chama cha siasa!
  2. Tangu Primary, na sekondari, somo la siasa, nilipata A, hivyo nilikuwa wa kwanza kwenye siasa, hata Chuo Kikuu, UDSM, kitivo cha sheria, somo la Katiba, lilifundishwa na Prof. Shivji, mimi somo lake nilipata A, na hata degree yangu ya sheria LL.B ya UDSM ni (hons), na iko tuu kabatini, mimi nikiendelea kuwa mwandishi wa habari, na inawezekana mimi ndie mwandishi wa habari wa kwanza, mwenye LL.B Hons, ambaye pia ni wakili, ambaye pia ni wakili lakini naendeleo na kuandika na kutangaza and get nothing, badala ya kwenda mahakamani na kupiga pesa ndefu za uwakili!.
  3. Nilipokuwa JKT Makotupora kwa mujibu wa sheria, mimi ndiye niliongoza somo la range, na parade, kwenye kupiga parade mwendo wa haraka, wakati wa kutoa heshima, mguu wangu huku umenyooka, ulipiga heshima kwa 90 degrees! hivyo kumaliza JKT, niliunganishwa moja kwa moja kujiunga na JWTZ, kule tukapigishwa depo mpya, kwa vile wito wangu haukuwa kuwa mjeda, niliaga rasmi JWTZ, nikajiunga na TSJ kusomea uandishi wa habari badala ya kwend Monduli kuvaa nyota!。
  4. Baada ya kuhitimu TSJ, nikajinga na RTD, kule nikashauriwa niende newsroom, kwasababu enzi hizo, utangazaji ni kipaji tuu, nikawa ni mtangazaji wa kwanza wa RTD kuingia utangazaji na Diploma, enzi hizo watangazaji wengi ni form IV tuu,mimi form VI wa Ilboru na diploma ya TSJ juu!。
  5. Nikiwa RTD, enzi hizo tukilipwa mshahara dirishani, kuna mtu moyo wangu ulimdondokea mtu, hivyo siku ya mshahara, baada tuu ya kupokea bahasha ya mshahara, nilimkabidhi mtu, bahasha hiyo hivyo ilivyo!, hivyo kuwa mtangazaji mpya wa kwanza aliye ...mshahara wake wote shauri ya kupenda!。
  6. Nilijiunga Televisheni ya DTV mwaka 1995, na mimi ndie mtangazaji wa kwanza wa TV Tanzania kuhost TV Talk Show, ikiitwa "Mada Moto" kuzungumzia uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi. Kipindi hicho, kiliandaliwa na Mjerumani mmoja akiitwa Wolfgang Baraniek akishirikiana na Mtanzania, Beatrice Mugishagwe na kilidhaminiwa na wafadhili mbalimbali wa kimataifa, nilikuwa navuta 6figure mwaka 1995!, naomba msiniulize nilifanyia nini hizo pesa, ila mwaka huo ndio nilioa, na honeymoon yangu ni London nchini Uingereza!.
  7. Mimi ndio mwandishi wa Kwanza kutangaza matokeo yasiyo rasmi ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar ile 1995 kulikopelekea sheria kutungwa ni marufuku media kufanya tallying na kutangaza matokeo ya urais yasiyo rasmi
  8. Baada ya uchaguzi, ndipo Nikachukuliwa na Masai Studios, kuendesha kipindi cha Kiti Moto, nikiwa tena pioneer host wa talk shows za ukumbini, reality show nchini Tanzania。
  9. Mimi ndiye mwandishi wa kwanza wa Tanzania kuripotia Local TV, mikutano ya UNGA from New York kwa miaka 10 mfulululizo. miaka 5 na Mkapa na 5 JK。
  10. Mimi ndiye mwandishi wa mwisho kufanya mahojiano na Baba wa Taifa kabla hajaugua, ambayo tuliyafanya The Bundes House, nchini Uswisi, na mimi ndiye mwandishi pekee wa Tanzania aliyekwenda kumtembelea Mwalimu hospitali ya St. Thomas inchini Uingereza, na kisha kuja kumzika kijijini Mwitongo pale Butiama。
  11. Mimi ndie the first journalist kutumia big bike kukusanyia habari, bike yangu ilikuwa kubwa na haina kiti cha abiria bali ina sanduku lenye digital video camera na digital still camera。
  12. Mimi ndie mwandishi wa kwanza nchini Tanzani kutumia digital media, enzi hizo media zetu zote ni analogues, I was the fastest journalist kufika eneo la tukio。
  13. Ni mimi ndie mwandishi wa kwanza kuripoti vurugu za Mwembe Chai.
  14. Mimi ndio mwandishi wa kwanza kuripoti vurugu za uchaguzi wa Zanzibar na kutiwa ndani kituo cha Mwembe Madema na Ali Saleh wa BBC na Khalfan Saidi wa Nipashe。
  15. Mimi ndiye mwandishi wa kwanza wa Tanzania kufanya VJ, yaani video journalist, unaandika mwenyewe, unapiga picha mwenyewe, unajirekodi mwenyewe, una edit mwenyewe, na unatuma story yenye piece to camera huku kila kitu umefanya mwenyewe
  16. Mimi ndiye mwandishi wa kwanza wa private media, kuandamana na misafara ya ziara za rais nje ya nchi, hivyo nimeandamana na rais Mkapa, na JK katika ziara kibao, kutokana na uwezo wa multi task.
  17. As a freelance journalist, mimi ndiye freelance wa kwanza nchini Tanzania kualikwa press conference za Ikulu, na kuuliza swali kwa rais.
  18. Mimi ndio mwandishi wa kwanza wa habari nchini Tanzania, kuitwa na Kamati ya Bunge na kuhojiwa kutokana na Makala Zangu。
  19. Mimi ndie mwandishi wa kwanza kuwahoji marais 5 wa Tanzania,Nyerere,Mwinyi,Mkapa,Kikwete,na JPM,barua yakuomba kumhoji Rais,iko mezani kwenye kurugenzi yake ya habari,ikisubiri kupangiwa siku。
Mambo ambayo Pasco ni wa kwanza humu jf
  1. Hata humu JF, mimi ndiye mtu wa kwanza kuwaeleza watu humu kuwa Magufuli ndio atakuwa rais 2015!. Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli
  2. Mimi ndio the 1st kuwaeleza watu humu Makonda atakuwa RC wa DSM. Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
  3. Mimi ndio the first kuwaeleza watu humu kuwa Mwanasheria mkuu wa Zanzibar atafutwa kazi. Dr. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii
  4. Mimi ndie mtu wa kwanza kumtangaza Dr Tulia atakuwa Spika Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...
  5. Kwenye siasa, mimi ndiye mwandishi wa kwanza kuaga rasmi fani ya uandishi na kusema nitajiunga na siasa. Nimeamua Kustaafu Rasmi JF, Utangazaji na Uandishi wa Habari Baada ya Kuhudumu Miaka 30. Niko Free Kujiunga Siasa, Nimejiunga CCM na Nitagombea Ubunge
  6. Siku naanga rasmi media, mimi ni mwandishi wa kwanza kuaga rasmi from studio nikiwa live.
  7. Kumbe kuwa the 1st, pia kuna faida zake na hasara zake, kufuatia kuwa the 1st kwenye mengi, nilipojitokeza kutangaza nia Kawe, baada ya kupata the 1 vote, ikagomea hapo hapo!。
  8. Kuna mambo mengi nimeyaeleza humu na yakatokea,
  9. Hivyo leo ninapowaeleza humu mshindi wa jimla wa uchaguzi huu wa serikali za mitaa naombeni mniamini, na kwa msio amini, endeleeni kusubiria matokeo rasmi ndipo mtaamini.
  10. Mpaka sasa wengi wanaamini mgombea wa urais wa CCM 2025 ni huyu anayetajwa tajwa, be the first to know mgombea urais wa CCM 2025 sio lazima awe yeye huyu kama HII sauti ni sauti ya kweli 。
  11. Hivyo uchukulie uzi huu kama uzi wa an info pack ya mshindi wa uchaguzi mkuu wa 2025 ni CCM, Wapinzani labda 2030 Uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM! Wajinga karibu wote watakuwa wamemalizika!

leo ninapowaeleza humu mshindi wa jumla wa uchaguzi huu wa serikali za mitaa ni CCM,na mshindi wa uchaguzi Mkuu wa 2025 ni CCM, naombeni tuu mniamini, na kwa msio amini, endeleeni kusubiria matokeo rasmi ndipo mtaamini.

Hii predictability ya mshindi wa uchaguzi kabla hujafanyika,inamaana chaguzi zetu ni very predictable,uchaguzi haujafanyika,huku watu wanajua matokeo,hii inaweza kumaanisha sio kuwa tunafanya uchaguzi,bali ni tunafanya igizo tuu la uchaguzi!。
Maoni yangu Kuhusu uchaguzi huu wa serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu wa 2025
  1. Kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa,mimi binafsi nimeshauri sana tuu Kuelekea 2025 - LGE2024 - Ombi Maalum, Kwa Mtu Maalum Achana na Hizi Mutatis Mutandis Kwenye Chaguzi za SM2024 & U/Mkuu2025, Tumia Ceteris Peribus, Utabarikiwa, Tutabarikiwa!
  2. Ombi kama hili kwanza nililitoa mwaka 2019 Ombi Maalum, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Uendeshwe kwa Ceteris Peribus, Sio Kwa Mutatis Mutandis. Tutabarikiwa!
  3. Nikashauri Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!
  4. Nikashauri Mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi: Je Tupige Ndege Wawili kwa Jiwe Moja kwa Uchaguzi Serikali za Mitaa/Mkuu, Ufanyike Siku Moja au Tuendeleze Mazoea?
  5. Nikaulizia Madudu ya ajabu ya ubatili wa Katiba yetu, mabadiliko "fake" ya sheria na Tume ya Uchaguzi. Rais Samia asilaumiwe kwasababu yeye sio mwanasheria!
  6. Nikazungumzia Kuelekea 2025 - Kwa kauli ya Nape kuhusu chaguzi zetu, anastahili kulaumiwa au kupongezwa kwa kuusema ukweli?
  7. Nikasisitiza Kuelekea 2025 - Baada ya Mtu Kusema Ukweli Kuhusu Uchaguzi Kuendeshwa kwa Mutatis Mutandis, Tunaomba Uchaguzi Mkuu wa 2025 Uendeshwe kwa Ceteris Peribus!
  8. Nikaomba sana Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
  9. Na。kuhusu uchaguzi wa 2025
    Mpaka sasa wengi wanaamini mgombea wa urais wa CCM 2025 ni huyu anayetajwa tajwa, be the first to know mgombea urais wa CCM 2025 sio lazima awe yeye huyu kama HII sauti ni sauti ya kweli 。Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?. Ombi kwa Rais Samia: Sheria Mpya ya Uchaguzi Bado ina Ubatili. Haki ya Kuchagua na Kuchaguliwa imeporwa! Irejeshwe kwa Mujibu wa Katiba! Kuelekea 2025 - Kufanya kosa si kosa, kosa kurudia kosa! Sheria ya Uchaguzi ni kosa. Kwanini tunarudia kosa? Haki si hisani, ni stahiki. Bunge tutendeeni haki!
Conclusion
Tanzania sio nchi ya watu fulani tuu au chama fulani tuu, Tanzania ni nchi ya Watanzania wote, wa vyama vyote, dini zote, makabila yote, jamii zote, jinsia zote, rangi zote, hali zote za maisha, matajiri na masikini na Watanzania wa circumstances zote.

Nimesikia sauti, "voices from within" ikiniambia kuwa tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis, hizi, kuna jambo fulani litatokea tena kama lilivyotokea baada ya mutatis mutandis ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu wa 2020.
Sijui ni wangapi humu wanaojua, kile kilichotokea ile 2021, kilichangiwa na matokeo ya uchaguzi wa 2019 na uchaguzi wa 2020, tusiporekebisha makosa, kinaweza kujirudia!.

Hivyo uchukulie uzi huu kama uzi wa an info pack ya mshindi wa uchaguzi mkuu wa 2025 ni CCM, Wapinzani labda 2030 Uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM! Wajinga karibu wote watakuwa wamemalizika!

Hongera sana CCM kwa ushindi wa kishindo baada ya Watanzania kutekeleza kwa vitendo wito huu Ukipokea Ujumbe Huu wa Rais Samia Kuhusu Kesho, Usikae Nao, Sambazia na Wengine!. Kesho Kazi ni Moja Tuu!, ni Unachukua...Unaweka...!.

Hata baada ya uchaguzi huu wa serikali za mitaa, fursa to make it right kwa uchaguzi wa 2025 bado ipo!.
Rais Samia ni fursa ya kutenda haki 2025, Ombi kwa Rais Samia: Japo wengi wape, wachache pia wasikilizwe, Hoja ya kufanya minimum reforms za Katiba ni hoja ya msingi sana kuliko hata Sheria! Hongera Sana Rais Samia kwa Miaka Miwili Madarakani. Japo Umefanya Mengi, Makubwa, Mazuri, Lakini Bado! Linalowezekana Leo, Lisingoje Kesho!

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
 
Mtu utunge mtihani mwenyewe, usimamie mwenyewe, unyime wenzio peni za kufanyia mtihani, usahihishe mwenyewe halafu ukose kupass kwa alama zote basi utakuwa mjinga wa mwisho.

Hizo sio voices from within mzee, ni sad reality ya ubaradhuli wa CCM.
 
Kama umefanya mambo yote hayo je hawa akina salumu kikeke na Wengineo walikuacha wapi.

Kuna faida kubwa ya kuwa na weledi kuliko kusifu , kuabudu siasa ambazo hazina tija. Ile reputation Kama journalist haipo.

Japokuwa umebarikiwa uwezo mzuri wa kuchambua mambo Ila bado hauna legacy katika habari.

Ungetenganisha siasa na Kazi yako ungefika mbali japo hata ulipo sio padogo.
 
Ni mbumbumbu pekee ndiye atashangilia ushindi huo. Kabla hata ya uchaguzi kufanyika CCM ilikuwa imeshashinda 65% kwa figisu za waziwazi za wasimamizi wa uchaguzi.

Mchakato mzima ni doa kubwa kwa uhai wa demokrasia yetu.
Chaguzi kama hizi zina akisi namna sisi waafrica tusivyoweza kujisimamia wenyewe kwa mambo madodo madogo kama haya.
 
Wana JF,

Maadam JF ni ukumbi wetu, na sisi humu JF, tuko members wengi, na tumefanya mengi, hivyo mimi member mwenzenu Pascal Mayalla, naomba niwe wa kwanza, kuwajulisha wana JF wenzangu, ili kuwapa ile JF advantage ya wewe kama Mwana JF, be the first to know kuwa CCM ndio mshindi wa jumla wa Uchaguzi Mkuu wa 2025 kufuatia ushindi wa kishindo wa uchaguzi huu wa Serikali za mitaa kwa a landslide victory ya ushindi wa kishindo, kwa kwa kukomba almost everything,kila mtaa,kila kata,kila kitongoji na kila kijiji, hivyo mshindi wa serikali ya mtaa mwaka huu, ndie mshindi wa uchaguzi mkuu wa 2025!。

Ushindi huu ni kufuatia mimi mwana JF mwenzenu, Pasco Mayalla, nimesikia sauti ndani ya moyo wangu, yaani ile "voices from within", kuwa katika uchaguzi huu, wa serikali za mitaa, mshindi wa jumla ni CCM!, ndie anayekwenda kushinda uchaguzi wa 2025!。

Hii voices from within yangu is never wrong, maana ni sauti yake YEYE mwenyewe!,aliye ndani yangu!。

Sasa kwa faida ya wasionijua, mimi Pasco Mayalla, ili muweze kuamini ninachowaambia ni kitu cha kweli na ndio kinatokea, naomba niwape ushuhuda mdogo wa nimewahi kuwa wa kwanza kwenye mambo mengi tu, ambayo wana jf hamjui, je wewe mwana JF mwenzangu, wajua mimi Mwana JF mwenzako Pasco Mayalla, nimewahi kuwa Mtanzania wa kwanza kwenye mambo mengi tuu, ikiwemo humu JF, mimi ndiye Mwana JF wa kwanza kuwa kada wa Chama Cha Siasa?
kufuatia wengi hawana muda kusoma makitu marefu,wale wa short and clear mnaweza kuishia hapa na ku jump kwenye conclusion


Mambo ambayo Pasco ni wa kwanza humu jf

hapo!。
  1. Kuna mambo mengi nimeyaeleza humu na yakatokea,
  2. Hivyo leo ninapowaeleza humu mshindi wa jimla wa uchaguzi huu wa serikali za mitaa naombeni mniamini, na kwa msio amini, endeleeni kusubiria matokeo rasmi ndipo mtaamini.
  3. Mpaka sasa wengi wanaamini mgombea wa urais wa CCM 2025 ni huyu anayetajwa tajwa, be the first to know mgombea urais wa CCM 2025 sio lazima awe yeye huyu kama HII sauti ni sauti ya kweli 。
  4. Hivyo uchukulie uzi huu kama uzi wa an info pack ya mshindi wa uchaguzi mkuu wa 2025 ni CCM, Wapinzani labda 2030 Uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM! Wajinga karibu wote watakuwa wamemalizika!
Hongera sana CCM kwa ushindi wa kishindo baada ya Watanzania kutekeleza kwa vitendo wito huu

Paskali
The First
P this is extreme shame kuandika mada kama hii wakati unajua wazi huu haukuwa uchaguzi bali UCHAFUZI
 
Back
Top Bottom