Uchaguzi 2020 Mwana JF, be the first to know kuwa CCM ndio mshindi wa jumla wa Uchaguzi huu

Uchaguzi 2020 Mwana JF, be the first to know kuwa CCM ndio mshindi wa jumla wa Uchaguzi huu

Mshindi ni Lisu na CHADEMA, ccm hatuitaki.

Tumechoshwa matusi, manyanyaso, masimango, dhulma, kunyimwa haki ndani ya nchi yetu wenyewe.

Mwenye shibe hamjui mwenyewe njaa, bora tusiwe na fly over tuwe na HAKI, usawa na amani.

Tumechoshwa na unyanyasaji wa vyombo vya Magufuli.

Mahakama zake zimegoma kutoa haki, polisi wake wamegoma kutoa HAKI, TAKUKURU ndio kabisa badala kuzuia rushwa ndio wamekuwa wala rushwa na kutishia watu,ili wapate rushwa.

No piece no justice.
 
Mtitiririko wako wamatukio umekaa vizuri sana nakupongeza kwa hayo yote na kwa Utumishi wako wa muda mrefu, lakini conclusion yako inaukakasi na imenipa mashaka makubwa sana sikutegemea kwa mtu mwenye weledi wako na LL.B Hons from UDSM utasupport upumbavu unaoendelea katika nchi yetu.

Ni kweli huenda Degree ya LL.B haikuweza kuwa na manufaa kwako ndo maana hata watu wa Kawe wakaliona hilo na hawakusita kukuonyesha hilo kwa kukupiga chini.

Endelea tu na uandishi wa habari kwani nahisi ndicho alichokupangia Mungu uku kwingine unakurupuka kurupuka tu sio siri. Yaani kwa kujisifu na kwa mtiririko wa matukio nilidhani wewe ndo utakuwa kifua mbele kuwahimiza watu katika kujua, kupinga ukiukwaji wa sheria na kuhimiza kusimamia haki na pia kupinga ukiukwaji wa katiba yetu au hata kuwa kifua mbele katika mapendekezo ya katiba mpya katika nchi yetu kwa “Maslahi mapana ya Taifa” kama unavyodai katika kila thread zako nilizokuwa nikifatilia kwetu sisi na kwa vizazi vinavyokuwa ila imekuwa tofauti sana kwani umeshindwa kuficha hisia zako na nimesikitishwa kwa jambo hilo mno kwani umekuwa ni limbukeni wa mabarababara na Fly over kwa Miaka 5 na kusahau kwa Miaka yote hakukuwa na chama chochote madarakani zaidi ya chama unachojinadi kuwa kada kwa Miaka takribani 50 iliyopita na phase ya kujenga na kuleta vitu hivyo ilipaswa tuwe tumeshapita huko.

I was wondering why you had to be selected and to come first at everything and also to be a representative journalist wa Nchi katika shughuli mbalimbali kama ulivyotaja hapo juu ila baada ya kuevalute the system inapenda kuwa praised then nikapata majibu ya maswali yangu kwanini uliweza ulifit in. Na sikushangai kwa kupigania tumbo lako pia huenda ukaonekana ili uweze kutimiza hazma yako yakuwa mbunge [emoji23] hata kwenye vile viti kumi endapo Mgombea wako akishinda. Hivyo pambana.

Eti “ Nawatakia maandalizi mema ya October 28, sio kwenda kuchagua, bali tuu kuthibisha kukamilisha mchakato”.

And you still brag to hold a Honorable degree of LLB this is a disgrace and embarassment to the intellectual proffesion.
 
CV yako haiondoi ukweli kuwa uko biased!

Isitoshe,hatuna chombo huru cha kusimamia na kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki hivyo huna uhalali wa kusema kuwa CCM atashinda.

Kazi yako kubwa hapa JF ni kufanya propaganda kwa lengo la kutaka kuwaaminisha watu(kuwaanda kisaikolojia) kuwa CCM itashinda kihalali wakati ukweli unaujua.

Mtu anayeopgopa ushindani ndani ya chama chake ndio unakuja kutuambia atashinda?
Huyu jamaa pamoja na kuwa na umri mkubwa lakini bado hajaelimika na busara kwake ni mtihani mgumu sana. Haki huinua taifa
 
Mshindi ni Lisu na CHADEMA, ccm hatuitaki.

Tumechoshwa matusi, manyanyaso, masimango, dhulma, kunyimwa haki ndani ya nchi yetu wenyewe.

Mwenye shibe hamjui mwenyewe njaa, bora tusiwe na fly over tuwe na HAKI, usawa na amani.

Tumechoshwa na unyanyasaji wa vyombo vya Magufuli.

Mahakama zake zimegoma kutoa haki, polisi wake wamegoma kutoa HAKI, TAKUKURU ndio kabisa badala kuzuia rushwa ndio wamekuwa wala rushwa na kutishia watu,ili wapate rushwa.

No piece no justice.

Haki ipi unayoitaka ambayo sasa hivi umenyimwa? Kwa maana umelitaja neno haki mara nyingi na kwenye maandishi yako
 
#LogicalArgument-Paschal Mayalla amejieleza vizuri sana na anaufahamu yakinifu wa masuala ya habari, historia na sheria. I fully concur with his healthy and constructive narration.

Itikadi za vyama mbadala zisiwe kikwazo cha kumtia moyo mtu mwenye maono ya kujenga nchi kwa ujumla bila ubaguzi, chuki na upendeleo. Katika mfumo wa maisha ili kila kitu kiende ipasavyo ni sharti pawe na utaratibu uliokubalika, pawepo na utulivu na amani ya moyo na akili (peace of heart and mind) miongoni mwa jamii, kikundi au mtu ili haki na maendeleo chanya yatokee. No justice will take course if there is no tranquility among the community.
 
Isitoshe,hatuna chombo huru cha kusimamia na kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki hivyo huna uhalali wa kusema kuwa CCM atashinda.
Ila Diwani wa Chadema akishinda Tume itakuwa huru! Hamueleweki mjue?? Sasa kama huna imani na tume kwa nini umemsimamisha diwani agombee!? Akili 'kubwa' hizi zina tia mashaka!
 
Haki ipi unayoitaka ambayo sasa hivi umenyimwa? Kwa maana umelitaja neno haki mara nyingi na kwenye maandishi yako, ...
Haki ya kuchagua ni mtakaye sio kuchaguliwa na vyombo vya dola, niende polisi nipate, haki badala ya kutupwa mahabusu kwa kutishwa nisidai haki yangu.

Nisilazimishwe kuwamwaba CCM na nisitishwe kwa kuwakosoa CCM na serikali yao.

Mahakama isiingiliwe na serikali na CCM, na isiwe kichaka cha CCM kunyamazisha watu.

Mahakama zitende HAKI kwa watuhumiwa wote badala kutumika kisiasa, kulazimisha watu kufanya wasiyoyataka na kwa kutishiwa vifungo.

Waliokaa Mahabusu miaka 10 wafikishwe mahakamani na wapewe dhamana na kesi ziendelee wakiwa nje wakiendelea na maisha yao.

Takukuru wazuie rushwa badala kugeuka kututisha na kutubambikia kesi za rushwa tunapopeleka madai ya msingi.

Haki ya kuishi huru na kuongea kwa uhuru bila kutishwa na maccm na vyombo vya dola vinavyotetea maslahi ya ccm badala ya wananchi.

We have laws but no justice.

No justice no peace.
 
Haki ya kuchagua ni mtakaye sio kuchaguliwa na vyombo vya dola, niende polisi nipate, haki badala ya kutupwa mahabusu kwa kutishwa nisidai haki yangu.

Nisilazimishwe kuwamwaba ccm na nisitishwe kwa kuwakosoa ccm na serikali yao.

Mahakama isiingiliwe na serikali na ccm, na isiwe kichaka cha ccm kunyamazisha watu.
Mahakama zitende HAKI kwa watuhumiwa wote badala kutumika kisiasa, kulazimisha watu kufanya wasiyoyataka na kwa kutishiwa vifungo.

Waliokaa Mahabusu miaka 10 wafikishwe mahakamani na wapewe dhamana na kesi ziendelee wakiwa nje wakiendelea na maisha yao.

Takukuru wazuie rushwa badala kugeuka kututisha na kutubambikia kesi za rushwa tunapopeleka madai ya msingi.

Haki ya kuishi huru na kuongea kwa uhuru bila kutishwa na maccm na vyombo vya dola vinavyotetea maslahi ya ccm badala ya wananchi.

We have laws but no justice.

No justice no peace.

Mimi nina hizo haki zote hapa Tanzania ulizoziorodhesha na sijui mtu yoyote kwenye familia, rafiki au jirani yoyote ambaye anasema hana haki hapa Tanzania, hivyo labda ni shida binafsi zaidi na ungeanza na wewe labda una matatizo makubwa zaidi ya kibinafsi, acha kunyooshea wengine vidole, jaribu kutatua matatizo yako binafsi kwanza, ...
 
Uko sawa sana Pasco ! Ajae in JPM wala hapana Shaka! Huo ndio ukweli hata kama n mchungu kwa wengine. Alunta continua
 
Hongera Mh.DC Mtarajiwa...

Baba Yako Alikuwa JIKONI..
Mama Yako Alikuwa JIKONI...

Iweje Leo JIKO lililokulisha na kukukuza ULIKATAE kama ilivyotokea KULIKATAA kipindi kile RTD na kusababisha MOSHI WAKE ukutoe machozi?!!!😂😂

JPM hoyeeeeee

Kada wa kweli NISIYETAKA UDC
Tandale Kwa Mtogole.
 
Seems to me you only remember that “Karma is a bitch” when it suits what you are alleging at the moment mkuu Pascal.
 
Mimi nina hizo haki zote hapa Tanzania ulizoziorodhesha na sijui mtu yoyote kwenye familia, rafiki au jirani yoyote ambaye anasema hana haki hapa Tanzania, hivyo labda ni shida binafsi zaidi na ungeanza na wewe labda una matatizo makubwa zaidi ya kibinafsi, acha kunyooshea wengine vidole, jaribu kutatua matatizo yako binafsi kwanza, ...
Na sikukuongelea wewe nilijiongelea mimi na ninao wawakilisha tunaokosa Haki hizo nchini kwetu Tanzania.

Ukiona unapata hizo haki ndio ujue wewe ni ccm au baba yako au mama yako au wazazi wako wote ni watawala wa ccm, ndio wako privileged kupata kila kitu bila shida yoyote hata wanapovunja sheria, na hata wasipostahili.

Mimi na ninao wawakilisha tunaipigania haki na usawa nchini mwetu Tanzania.

Tumedhulumiwa mahakamani, tukaombwa rushwa mahakamani, tukaenda takukuru tukataka kupewa kesi ya rushwa, kwa nadai eti sisi ndio tunaichafua nchi.

Hivyo tunalazimishwa kuinunya HAKI , ukiitafuta unaambiwa unaichafua nchi, kwamba mambo madogo mpaka twende takukuru , sasa takukuru ina kazi gani kama sio kuzuia rushwa?!

Vyombo vya kutoa haki vinatuona wasumbufu, wajinga, na tusioelewa utaratibu, tukiombwa rushwa mahakamani ni sahihi kabisa kwao.

We have laws but no justice.

No justice no peace.

Chagua Lisu na CHADEMA.
 
Na sikukuongelea wewe nilijiongelea mimi na ninao wawakilisha tunaokosa Haki hizo nchini kwetu Tanzania.

Ukiona unapata hizo haki ndio ujue wewe ni ccm au baba yako au mama yako au wazazi wako wote ni watawala wa ccm, ndio wako privileged kupata kila kitu bila shida yoyote hata wanapovunja sheria, na hata wasipostahili.

Mimi na ninao wawakilisha tunaipigania haki na usawa nchini mwetu Tanzania.

Tumedhulumiwa mahakamani, tukaombwa rushwa mahakamani, tukaenda takukuru tukataka kupewa kesi ya rushwa, kwa nadai eti sisi ndio tunaichafua nchi.

Hivyo tunalazimishwa kuinunya HAKI , ukiitafuta unaambiwa unaichafua nchi, kwamba mambo madogo mpaka twende takukuru , sasa takukuru ina kazi gani kama sio kuzuia rushwa?!

Vyombo vya kutoa haki vinatuona wasumbufu, wajinga, na tusioelewa utaratibu, tukiombwa rushwa mahakamani ni sahihi kabisa kwao.

We have laws but no justice.

No justice no peace.

Chagua Lisu na CHADEMA.

Siyo kweli, kwanza familia yangi mimi wala hawajihusishi na Siasa, na majirani na marafiki wengi ni CUF na hawaipendi CCM kabisa, lkn sijawahi kusikia wakisema hawana haki hapa Tanzania, ...
 
Mimi sijawahi kuona ukiandikwa kada wa CCM, leo ndiyo kwanza ninakusikia wewe na ndiyo kwanza kusikia huwa inaandikwa Fulani ni kada wa CCM.

Shukurani zikufikie kada wa CCM (sifa nyingine ya ziada) mkazi wa eneo lenye elites na hakuna watu wenye simple minds.
 
Hakuna wapiga mil 6 hewa ila tatizo ni uelewa mdogo wako juu ya suala dogo tu. Kila kituo kinatakiwa kiaccomodate wapiga kura wasiozidi 400-450. Hii haimanishi kila kituo kina idado ya wapiga kura 450. Dafatali la kudumu kila chama kimepewa hao mil 6 wanatoka wapi?
 
Nina uhakika hata mke wako anajutia ni kwa nini kaolewa na mwanaume aliye mke wa wengine. Wee jamaa umeolewa mazima kabisa!!!!!
 
Siyo kweli, kwanza familia yangi mimi wala hawajihusishi na Siasa, na majirani na marafiki wengi ni CUF na hawaipendi CCM kabisa, lkn sijawahi kusikia wakisema hawana haki hapa Tanzania, ...
Sasa hayo matatizo yako, kwanza CUF iliiisha kufa haipo, CUF kabaki Lipumba.
Nimekueleza mimi madhila niyapatayo na dola la ccm, na niyaonayo kwa macho.

Sio kweli nini tena, nikupe matatizo yangu ndio ujue ukweli?!

Mimi ni mtumishi wa umma muda mrefu nafasi tofauti, na ni mtaaluma pia, lakini siyo mwana ccm, na sitaki kulazimushwa hilo.

Nasitaki haki niipate kwa mgongo wa ccm au influences zao, nataka haki iwe haki kweli.

Ndugu yangu anashutumiwa wao wanadai kafanya kosa wakati ushahidi hawana, unauliza matokeo ya uchunguzi hayapo, na hawana ushahidi wowote, naye no mtumishi wa umma lakini wanataka wamuweke mahabusu, kwa kudhani atatoroka, na hiyo kesi ipo tangu 2016 na hajatoroka,leo ndio atoroke, au wanatafuta kumuumiza akae mahabusu tuwape hongo kumtoa?!

Kwamba yuko nje ya mahabusu hawafurahii kila siku anatokea nyumbani kwenda mahakamani, wanataja wambinye familia yake ipate taabu, na hawana ushahidi zaidi ya hear say, na kutafuta rushwa.

Tangu 2016 hawana hata ukurasa mmoja wa taarifa ya uchunguzi, wanadai uchunguzi unaendelea, ukikamilika kesi itasikilizwa, sasa kwanini wamuweke mahabusu kama hawana taarifa yoyote ya uchunguzi, naye hajawazuia kufanya uchunguzi.

Walimsimamisha kazi miezi 8 kupisha uchunguzi hawakuleta taarifa za uchunguzi kwa miezi yote hiyo, hakimu akasema, kama haingilii ucgunguzi basi arudishwe kazini. Akarudi kazini, wale mahasimu wanalazimisha awekwe mahabusu eti atatoroka.

Kupinga hilo la mahabusu, tunaambiwa tunaichafua mahakama, mara tunaisema vibaya mahakama, sisi sio wazalendo na manemo mengi ya kijinga, kwamba sisi ni wapinzani, kwanini tusikubali kisha tukate rufaa, mahabusu ukate rufaa?!.

Sasa kwanini niiendelee kuipenda serikali ya ccm, inayolazimisha kwa assumptions za kijinga.
Na hii ni single incident.

Achana na ccm, bora ni chague tumaini la HAKI, Lisu tu.
 
Back
Top Bottom