Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nawafanyaga hvo hvo wakinipigiaga....
Wanawake wengne wajnga sana...
hao uwasemao wewe wanajifunza kupiga mizinga, wataalam halisi hawapigi mizinga kwenye msg au sim. Mzinga unapigwa live bila kupepesa macho .... utatoa tu penda usipende!
Sasa mnataka tuwaombe hela kina nani?
sasa kama huna msaada unauliza ya nini?" si ufunge kinywa chako....... unajichetua na maswali ya mtego nikwambie mazuri wakati kiuhalisia ni mabaya hapana kwa kweli......''Maisha yanasemaje kipenzi changu'' nitakujibu maisha yanataka hela na sina hela embu nitumie laki 5 hapo mar moja......
Ukiona umemtumia mpenzi wako/mchumba wako/mchepuko wako/mke wako au hata rafiki wa kike wakati mwingine SMS ya kawaida tu kwaajili ya kumsalimia lakini yeye akakujibu moja kati ya majibu yafuatayo, tafadhali sana usiendelee kuchat nae maana kinachofuata hapo ni majanga tu.
KWA MFANO:
1. Ukimtumia sms ''Mambo mpenzi wangu?'' akikujibu ''mambo mabaya'', usimuulize kwanini mambo mabaya, ukimuuliza atakwambia kuwa ''sina hela dear''
2. Ukimtumia sms ''Maisha yanasemaje kipenzi changu'' akikujibu ''maisha magumu hubby wangu we acha tu'' usimuulize kwanini, ukimuuliza kwanini atakwambia ''nimefulia mwenzio kama nini sijui''
3. Ukimtumia sms ''Mbona kimya sana mchumba wangu, umenitupa kiasi hicho'' akikujibu ''sijakutupa wangu yaani mambo hata hayaendi'' usimuulize kwanini mambo hayaendi, ukimuuliza atakwambia kuwa ''yaani sina kitu mpenzi wangu, simu ilikuwa haina hata hela ya kubeep''
4. Au ukiona mwanamke anaanza kwa kukwambia nikwambie kitu? We mkatalie kiutani utani tu, mwambie usiniambie, hata akikomaa vipi akwambie mwambie sitaki uniambie huku unafanya kama utani lakini moyoni unakuwa upo serious.
Ni mara chache sana mwanamke akikwambia kuwa mambo mabaya, maisha magumu au mambo hayaendi huwa na matatizo mengine kama kuumwa, misiba.... n.k lakini THE REST ni wapigaji mizinga tu. Akikwambia maisha magumu mjibu ''pole wangu, mambo mengine vipi?''
Ukipewa majibu kama hayo, chagua moja, either usiendelee kuchat nae mpaka badae kidogo au mbadilishie maada ili kukwepa huo mzinga ambao unakuja mbele yako.
Dr. MCHUNGUZI HURU (PhD)

sasa kama huna msaada unauliza ya nini?" si ufunge kinywa chako....... unajichetua na maswali ya mtego nikwambie mazuri wakati kiuhalisia ni mabaya hapana kwa kweli......''Maisha yanasemaje kipenzi changu'' nitakujibu maisha yanataka hela na sina hela embu nitumie laki 5 hapo mar moja......
Proffesor anasema ... sio ATM
Binamu upo?
Wanawake bwana..!
..mtu ana kipato kizuri lakini kila kukicha ni kama ombaomba..!
hapa nadhan ni kwa wale ambao kupiga mizinga ndo profession zao.
Nywele gani laki moja kusuka nywele gan izo
Wazazi wenu ndugu zenu
Yaani mzigo ule wewe na hela tukaombe kwa wazazi? Inahusu?