ngoja ngoja
JF-Expert Member
- Jun 20, 2024
- 673
- 1,526
Chief ni nani anae oa je kuoa ni nini?Badala utoe hoja ñàona umejiunga na weñye uwezo Mdogo.
Embu jitutumue basi angalau wale wanaotumia Akili wakisoma waone umeandika kitu,
Wewe utakubali úwe Mume WA pili yaani Wanaume wawili muoe Mke mmoja?
Kama sivyo, Kwa nini hutokubali?
Kipi kinakufanya usikubali?
Karibu
Lakutisha linakuaje na sio la kutisha lainakuaje,hakika leo umeandika pumba.Wanawake wasiojitambua ndîo huambiwa maneno hayo ili kuwatisha na kuwapumbaza Kisha Wanaume hutumia propaganda hiyo kuwatumia Wanawake dhaifu wasiojiamini.
Ndîo maana nikasema, Kwa Binti za Tibeli hiyi desturi ya kuwa mchepuko au kuolewa Mke WA pili wawaachie Wengine No matter what.
Gap la idadi ya Watu Baina ya Wanawake na Wanaume siô la kutisha kiasi kwamba mwanamke anayejitambua aolewe Mke WA pili au awe mchepuko.
Hiyo ni mitazamo na falsafa za Watibeli Mkûu siô Kwa Watu wote
Chief ni nani anae oa je kuoa ni nini?
Lakutisha linakuaje na sio la kutisha lainakuaje,hakika leo umeandika pumba.
Unatusagia kunguni tulio na chance ya kugombea majimbo manne
Mwanaume kumchukua mwanamke kumuoa na sio mwanamke kumchukua mwanaume bali mwanamke huchukuliwa na mwaume na kua mke anae oa ndie anae chukuliwa sio anae olewa .Mwanaume anao Mwanamke anaolewa.
Kuoa NI kitendo cha Mwanaume kuchukua Mwanamke na kumfanya Mkewe
Kuolewa na kitendo cha Mwanamke kumchukua Mwanaume na kumfanya kuwa Mumewe.
Wewe unatafsiri Ipi ya Kuoa?
Hii nakupinga mkuu. Kuwa mke wa pili sio laana wala kutokujitambua labda kwako tu hili ndo kutokujitambua!!
Jamii za kifugaji ni kawaida sana na ni Baraka kabisa na mahali hutolewa sawasawa na Wa kwanza.
Pili umeingilia dini za watu wenye Imani ya kuoa Hadi wake4 na nikawaida kabisaa.
Uzungu umekuingia sana usijione uko sawa Kila Wakati muda mwingine unapuyanga vibaya.
Aliyekuambia nataka kukubalika NI Nani?Unakuwa unajitahidi sana kuandika kifalsafa ila huwezi na bado una safari ndefu mno kuweza kuandika ipasavyo ukakubalika. Fanya vitu vingine tu jamaa
Hakuna kujitambua kwa mwanamke mbele ya mwanaume mwenye akili timamu, ni jambo la asili, ni mwanamke kwa ajili ya mwanaume na si mwanaume kwa ajili ya mwanamke.MWANAMKE ANAYEJITAMBUA HAWEZI KUWA MCHEPUKO AU MKE WA PILI.
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli
Binti yàngu, kwetu Watibeli ni mwiko Kwa Binti zetu kuolewa Mke wa Pili au Uke Wenza au Kuwa mchepuko.
Huko ni kutojitambua, kujidhalilisha na dalili ya umaskini na uvivu.
Wewe siô mzuri mpaka úwe Mke WA pili au úwe mchepuko?
Wewe siô mchapakazi na mwenye uwezo wa kujitegemea mpaka úwe Mke WA pili au mchepuko.
Mwanamke mwenye mzuri kwelikweli hawezi kuwa Mchepuko au Mke WA pili. Hakunaga huyo Mwanamke.
Mwanamke anayefanya Kazi na kujitegemea hawezi kuwa Mke WA pili au mchepuko.
Kama nilivyokufunza Binti yàngu, kuwa Sisi Watibeli kufanya Kazi ni Dini. Lazima ufanye Kazi uweze kujitegemea mwenyewe.
Ndoa pia ni Dini lakini haimaanishi úwe Mke wa Pili au mchepuko.
Ukijitegemea Huwezi kuwa Mke WA pili Daima dawamu.
Kitu kizuri huwa chaguo la Kwanza. Kitu kinachopendwa huwa chaguo la Kwanza Binti yàngu. Usikubali kuwa na kuitwa wa ziada au nyongeza. Wewe siô wanyonyeza. Wewe NI wathamani.
Úkiwa mvivu na mwenye kumtegemea Mwanaume, hutaki kufanya Kazi na kujitegemea unavunja utu wako na Kwa hakika Watu watakudharau ikiwemo kuwekwa mchepuko au Mke wa Pili.
Kuolewa Mke WA pili au mchepuko NI kukosa Soko, haiwezeniki Wanawake wenzako Kila Siku wanaolewa na kupata Wanaume waô wènyewe alafu wewe úwe mpàngo wa kando au Mke WA Pili.
Huo ni Mkosi
Huko ni kujichafulia Ñyota yako. Kuizim.
Kuitwa Mke mdogo Binti yàngu siô Sifa Njema. Wewe siô Bi. Mdogo. Nilikuzaa úwe Mke Mkubwa Kwa Mwanaume atakayekupa First priority. Sikukuzaa uitwe Bi. Mdogo au Nyumba ndogo.
Wewes siô Bi. Mdogo.
Nyumba yako Kamwe isiitwe Nyumba ndogo.
Kamwe Usiitwe Mpàngo wa kando au mchepuko. Wewe ni Njia kuu, Mke Mkubwa. Nyumba kûbwa.
Wewe ni Highway, michepuko itoke kwako hiyo siô kesi lakini siô wewe ati úwe mchepuko Kutoka Njia kuu. Huko ni kujidhalilisha. Binti za Tibeli Kamwe na haitokuja kutokea wakawa na sîfa hiyo.
Kwani unaharaka gàni?
Wanaume wa kukuoa wàpo anakimbilia kuwa Mke WA pili au mchepuko ili kushusha hadhi na Ñyota yako Maisha yako yôte Kisa nini?
Fanya Kazi wewe NI Mwanamke unayeweza kujitegemea.
Elewa, Mwanamke mzuri anayefanya Kazi akajitegemea hawezi kuwa Mke WA pili au mchepuko Kwa sababu Wanaume weñye Akili hujua thamani yake na watamuoa akiwa nafasi ya Kwanza.
Fanya Kazi, linda heshima yako na thamani yako kama Mwanamke.
Masuala ya kusema mbona Zamani Bibi zako walikuwa wanaolewa Wake Wenza au Michepuko hiyo ilikuwa Zamani Wakati Wanawake wakiwa watumwa.
Tenà hata hizô Zamani Binti za Tibeli na Wanawake wa Tibeli hawakuwahi kuolewa Mke wa Pili Wala kuwa michepuko.
Hiyo siô desturi ya Wanawake Bora wanaojitambua.
Hilo la Mke WA pili au mchepuko Acha Wengine wafanye lakini siô wewe Binti yàngu. .
Baadhi ya Mapokeo ya Dini àmbayo hayakufuata HAKI Bali yalifuata matamanio ya Wanadamu na matamanio ya waandishi wa Wakati huo usiyafuate.
Mimi Baba yako, na Mama yako ndivyo tulivyokuagiza hayo. Yasikilize maneno yàngu
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Eeee, hata namba moja hujui kama ni mke wa 2. Jisemee mwenyewe, wako wasomi na wanaruhusu kabisa waume wao waongeze mke. Kila mtu ana maamuzi yake na afanye anachopenda.
Ndoa zenyewe nyingi zimejifia ,watu wanaishi kama roommate huku kila mmoja akiwa na mtu mwingine. Watu wanaishi kiunafiki na maneno yao usiyaamini. Hata mleta mada si qjabu anachangamsha jukwaa tu.
Soma tena ulichokiandika na nilichoandika ulinganisheAliyekuambia nataka kukubalika NI Nani?
Au wewe unafanya vitu ili ukubalike?
Yàani niandike ili wewe unikubali ili Mimi nipate nini? Wewe kunikubali au kunikataa inaniongezea kitu gàni?
Hakuna kujitambua kwa mwanamke mbele ya mwanaume mwenye akili timamu, ni jambo la asili, ni mwanamke kwa ajili ya mwanaume na si mwanaume kwa ajili ya mwanamke.
Soma tena ulichokiandika na nilichoandika ulinganishe
Isaya 4 : 1 Na siku hiyo wanawake saba watamshika mtu mume mmoja wakisema, Tutakula chakula chetu, na kuvaa nguo zetu wenyewe, lakini tuitwe tu kwa jina lako; utuondolee aibu yetu.
Bible ina kila kitu, sijasema mmWasiojitambua.
Mwanamke mwenye viwango hawezi jidhalilisha namna hiyo
Bible ina kila kitu, sijasema mm
Mbona namba moja anaendelea na ndoa yake? Si atoke huko kama amejitambua. Watu wasipangiane maisha, kama wewe hupendi kitu it is fine , na wao pia . Kila mtu achague au afanye anachoona kinafaa.Aliolewa akiwa Namba Moja?
Mwambie Sasa hivi kama atakubali.
NI Sawa na Christina Shusho unaweza ukamuoa Mwanamke akiwa hajajitambua au Kwa sababu ya umaskini wake Akakubali kuwa hata Mke WA Saba Huko lakini Siku akijitambua au kujipata Hawezi kukubali tenà huo ujinga
Mbona namba moja anaendelea na ndoa yake? Si atoke huko kama amejitambua. Watu wasipangiane maisha, kama wewe hupendi kitu it is fine , na wao pia . Kila mtu achague au afanye anachoona kinafaa.
Hapa duniani kila mtu ana ujinga wake. Kwa mfano, kwa wazungu , mitala hairuhusiwi lakini ushoga au ndoa za jinsi moja ni halali na zinalindwa na sheria .
Nimesema ulaya hawaruhusu mitala na haipo kisheria, sijakataa kama hakuna wazungu wanapenda mitala. Tunarudi pale pale, kila binadamu ana mtazamo wake kuhusu jambo fulani. Mitazamo ya watu na iheshimiwe. Hatuwezi kuwa na mitazamo inayofanana hata siku moja.Hapa hamna aliyechaguliwa.
Kutojitambua nako NI uchaguzi Mkûu.
Kuhusu Namba Moja nimeshakuambia kuwa hata yeye ukimuuliza Sasa hivi hawezi kukubali.
Wazungu wanatoka Wapi?
Hata wazungu wàpo weñye mitazamo ya Ndoa za mitala.
Hapa Afrika zîpo familia nyingi Ambazo hawataki Ndoa za mitala
Huko arabuni zîpo familia pia Ambazo hazitaki Ndoa za mitala
Ushoga ni Dhambi
Kuoa wake wengi au kuolewa wake wengi Siô dhambi Ila NI kutojitambua.