Mwanamke kuolewa ni muhimu na ni mafanikio makubwa au mtindo wa maisha mtu anaouchagua tu?

Mwanamke kuolewa ni muhimu na ni mafanikio makubwa au mtindo wa maisha mtu anaouchagua tu?

Maisha yana "fakes" nyingi sana kama pesa, mali, majumba, starehe.

Lakini kiuhalisia utakuja kugundua maisha yanahitaji LOVE ( UPENDO ), AMANI na FURAHA.

Ukiwa na mtu anayeweza:

  • Kusimama na wewe katika nyakati ngumu,
  • Kukutia moyo
  • Kukupenda

Nakuhakikishia utahisi you have the world hata kama hujala siku 2

Ukitaka kujua hili, siku ukiwa very stressed au deppressed, hebu chukua simu yako mpigie mtu unayempenda, eithet awe:

  • Mama
  • Baba
  • Mwanao
  • Mpenzi
  • Mjomba
  • Rafiki

Utajihisi moyo unapoa tuliiii

Ndio maana hata wagonjwa, huko hospitalini akioneshwa upendo anakuwa poa mnooo.

Hii siri ya upendo, hamasa na matumaini inatumiwa sana na:

  • Viongozi wa dini
  • Motivational speakers

Hakuna jambo zuri kama kuambiwa Nakupenda, kutoka kwa mtu umpendae.

Ukiwa bado kijana, una nguvu mbwembwe zinakuwa nyingi. Ila itafikia stage hata kukaa mjini utaona kelele, hata ukiwa na majumba 600 utalala kwenye chumba kimoja. Na wakati huo utahitaji kuwa na mtu wa karibu siyo tena kampani za Bar na Night clubs.

Family! family! family! Is irreplaceable.

Vitu vingine kama midegree, sijui vyeo ni vitu artificial vya kutengeneza tu.
Kuna upande una ukweli ktk hii message yako, lakini ni ngumu sana kupata mwanamke mwenye upendo kwa mwanaume. Mwanaume kwa asilimia kubwa ndio mwenye upendo wa Kweli ktk hii dunia, kwa hio ni bora Kuwa na uchumi mzuri kwani unaweza kuajiri wafanyakazi au kupata familia ya hiari
 
Ni fikra au itikadi za kiimani ambayo imeshaweka tangia enzi na enzi na inatuathiri mpaka leo.

Ndoa ni makubaliano ,kihalalisho au kithibitisho katika jamii kwamba wawili hawa wapo pamoja officially.

Ndoa ni muhimu ijengwe na msingi wa upendo,vingenevyo inakuwa pambo tu na inapoteza mantiki na ladha ya ndoa.So umri haupaswi kuwa kigezo katika ndoa ndo maana wapo wanaofunga ndoa za uzeeni.
Ndoa nyingi hazidumu kwasababu zinafungwa kwa minadhiri potofu aidha umri umekwenda au kufata mkumbo.


Ndoa sio ya kila mtu.Naweza kusema ni fani ambayo si kila mja anaimudu ndo maana ndoa nyingi hazidumu.Kuna watu walivyoumbwa ipo katika asili yao hawezi kudumu na mtu mmoja sasa hapo kutakuwa na ndoa? labda ya mitala!

Tuwe na uelewa sio watu sote wanaipa ndoa kipaumbele au wanataka ndoa.Hii inaweza kutokana na sababu tofauti mfano mtu ameexperience ndoa alofunga mwanzo haikuenda vizuri na baada ya hapo hataki kabisa kusikia habari hio.Au ameona wazazi wake au watu wanaomzunguka wanavyohenyeka katika ndoa so haoni umuhimu!

Kuna baadhi ya nchi za magharibi kutokufunga ndoa ni jambo la kawaida yaani watu wanaishi pamoja kama mke na mume miaka nenda miaka rudi lkn hamna ndoa.Kama kujijenga wanajijenga na kuzaa wanazaa ila wanaandikiana contract ili wakiachana wanagawana mali n.k
 
Ndoa nyingi hazina furaha! Simaanishi ndoa zisizo na changamoto ila kuna ndoa nyingi hazina tu furaha completely!
Lete ushahidi na wenye ndoa wakubaliane na ushahidi wako la sivyo! itakuwa ni nginjera za vijiwe vya wazaramo tu.

Mi binafsi nilikuwa mwembamba kabla sijavuta jiko, lakini hivi sasa nimenenepa balaa kama kitimoto.

Sina maana kuwa sikutani na changamoto la hasha! lakini namshukuru Mungu 85% ya maisha yangu ya sasa ni furaha, amani na upendo.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Dah hili gumu sana kwa maisha ya leo, umejaribu kuzungumza na tabibu kuona kwanini hali hii inakupata! Unajua kuna kutopenda na kuna kutofurahia kitu! Can you make it clear hapo? Hupendi ama hufurahii? Do you have bad memories with it?
Vidonge vya uzazi wa mpango ndivyo vinawasabisha hao Ke wawe hivyo na vyakula wanavyokula visivyo na virutubisho vya afya zaidi ya kujaza matumbo tu.


Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Wapo. Tupo.

They say kama wewe kitu haujawahi kukiona au kukisikia haimaanishi kwamba hakipo au hakijawahi kutokea! Binafsi silipendi hilo tendo na sijawahi kulichukulia kama starehe!
Pamoja na hilo je unatoa papuchi?
 
Kuoa au kuolewa sio mafanikio ktk maisha, bali ni jamii imejenga hizo fikira potofu na zinaathiri maisha ya watu Wengi sana, kwani wanatumia muda mwingi na rasilimali ktk eneo hilo. kama kijana kuanzia miaka 18 - 30 atatumia muda na rasilimali zaidi kwenye kuwekeza anakua na uchumi na Afya Nzuri zaidi, kwa umri kama huo ukitumia 10% ya muda wako na rasilimali ktk mahusiano na ndoa unakua na hasara Kubwa sana.
Hiyo ni roho mbaya ya ubinafsi/umimi.

Hizo mali unazo/unazofuta ni kwajili ya nini?

Ebu toka huko haraka ktk fikra chafu za matumizi mabaya ya ubongo wako.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Wapo. Tupo.

They say kama wewe kitu haujawahi kukiona au kukisikia haimaanishi kwamba hakipo au hakijawahi kutokea! Binafsi silipendi hilo tendo na sijawahi kulichukulia kama starehe!
Ebu achana na hizo stories za kusadikika.

Mungu mwenyewe kaumba viumbe vyote hai kwa jinsia 2(Ke na Me) na ikiwa kwa viumbe vingine hai kama nyani, kuku hawana hayo matatizo ktk sex, iweje kwetu sisi Binadamu ndiyo iwe?

Si sisi Binadamu ndiyo tumependelewa haswa kuumbwa ktk uzuri, utimamu wa akili na hata maarifa kuliko hivyo viumbe vingine na ndiyomaana tukapewa mamlaka ya kuvitawala, Sasa hizi hadithi zenu za njoo utamu kolea mnazitolea wapi tena?

We una tatizo la kuathirika kiakili kwa kijijengea imani potofu juu ya hilo/psychological problem ambalo no jepesi sana kutatulika ukimkabidhi Mungu njia zako kiimani.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Siko hapa kumuaminisha mtu na wala sina haja ya kukuletea ushahidi wewe ili uamini kuwa kuna ndoa ambazo hazina furaha! Wewe kutokuamini au wewe kunenepa kwa sababu ndoa yako ina furaha haibadilishi ukweli kuwa kuna ndoa nyingi ambazo hazina furaha!

Wewe kutokuona au kutokusikia kitu haimaanishi kuwa hakipo au hakijawahi kutokea! Mimi na wengine wote tunaoziona na tunaozisikia hizo ndoa tunatosha kujua hilo bila kuthibitishiwa na mtu na ukweli hauhitaji ushahidi wala kuungwa mkono ili eti ndiyo uwe ukweli!
Pole sana, endelea kujiokotea hizo stories za huko unakozitoa ukiamini ndiyo uhalisia wa maisha kumbe no tango pori

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Haya na wewe unaweza ukatupa ushahidi kuwa wanawake wote wa hivyo wako hivyo kwa sababu ya hivyo vidonge na hivyo vyakula? Au umeamua tu kuandika kwa mihemko?
Njoo inbox uwekewe ushahidi ili ukitoka hapo unishukuru na uzidi kuniombea maisha marefu ili nizidi kuwaokoa wengine kwa elimu nitoayo bure.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Chief mbona unahemka? Unajua maana ya feminist bro?
Mi nakuelewa kuliko we unavyojielewa, hivyo nakuomba unielewe tu kwa wema ya kuwa we ni nguli wa feminism hata kama kishingo upande Dada.

Ni siku nyingi sana niko humu na nilikuwa nabishana sana na ninyi na wengine kama akina Rebecca.

Hili ni jina langu la 3 kama sikosei kwa sababu za kutoka na kurudi mara kwa mara hapa JF.

Nakukumbusha majina mengine niliyokuwa nikiyatumia hapa ni "Fulfilled Truth na Strongest Belief Secret"

Nisamehe kwa hilo maana nakupenda sana na nahitaji nikutoe huko uliko ili uendane na matendo mazuri yanayompendeza Mungu.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu mie wala sijaja kuomba ushauri kuhusu hii hali yangu kwa sababu naifurahia au wewe unaumia mimi nikiwa hivi? Hata haya mashairi yako hayatanibadilisha chochote wewe ukiwa sex addict inatosha kabisa!

Halafu we na wewe unamjua Mungu? Ungekuwa unamjua Mungu usingekuwaga unachepuka kaka!
Nina zaidi ya miaka mitatu sijui nini maana ya kuchepuka.

Afu kumjua Mungu hakumaanishi kuwa we ni malaika yani hautendi/hautatenda dhambi milele "METHALI 24:16" bali maisha utayoishi ni dhahiri yataakisi uwepo wa Mungu kiimani na kivitendo.

Unadhani kwanini Mungu alimuita Nabii Daudi "MTAKATIFU WANGU" ilihali alimuasi Mungu kwa kulala na Ke mjane ambaye mumewe aliuawa na Daudi vitani?

Hakuna aliye mkamilifu lakini kwa rehema na neema za Mungu tunaishi na tunaakisi tabia za Mungu ndiyomaana yatupasa tuungame dhambi zetu kila tunapoomba au kusali.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Swali ni umejuaje kama hizo ndiyo sababu kwa wanawake WOTE wenye hilo tatizo? Acha kurukaruka kama bisi!
Nilishafanya uchunguzi tangu 2011 na ni Ke wengi sana wamebadilika na kumshukuru kwa jinsi nilivyowaelimisha na kuwasaidia kurudi katika hali zao za kawaida kabla ya kuanza kutumia vidonge vya uzazi wa mpango na kuathirika kwa kutokujisikia hamu kimatamanio ya kujaamiana na kupata raha wakati wa tendo la ndoa.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Haukuwa na haja ya kujitambulisha maana tangu kitambo tu najua kuwa wewe ndiye strongest belief secret! Sasa sijui maelezo yote haya yalikuwa ya nini badala ya kujibu swali langu kuwa unajua maana ya feminist?
Yani nisijue ilihali uasisi wenyewe ulikuwa pale China?

Pole sana rafiki, ebu leta maswali mengine yenye akili kuliko hayo ya kitoto ili tuonekane kidogo tunajitambua ndugu.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom