Mwanamke lazima Abadili Dini na Imani Ili ifanane na yako ndipo umuoe.

Mwanamke lazima Abadili Dini na Imani Ili ifanane na yako ndipo umuoe.

Ni kweli sana

Mtoto wa mama mkwe aliponikamata sawasawa niliswitch kutoka RC kwenda KKKT chap bila kuombwa, na niko vizuri kuzidi na yeye mwenyewe mzawa, hisia na imani vinaenda pamoja ni ngumu kumuombea mtu ambae hamko imani moja hamuongei lugha moja

Ila PM na mkewe wamewezaje kuishi hivyo mpaka kufikia level hiyo na bado kila mmoja akiwa na dini yake na jamaa hajaongeza mke mwingine wala
High level of maturity, kama una akili ndogo kama pilitoni huwezi kutoboa
 
Watu kuwa tofauti hakuyafanyi Kanuni za mapenzi kuwa Tofauti,
Mapenzi bila kujali Watu wapo tofauti yanahitaji, Kujali, kuthamini, kuvutiwa, kujitoa n.k. mapenzi yanaongozwa na Kanuni kinzani ya Wivu. Wanadamu wote wanawivu linapokuja suala la mapenzi licha ya kuwa Binadamu kuna baadhi ya ishu tunatofautiana.
Hapa tutazunguka mpaka kesho... Mtu anaposema maisha hayana formula / au mapenzi hayana formula haimaanishi kwamba Mapenzi hayana uhusiano na attraction wala haibadilishi uhusiano wa kudumu kwa ndoa na uvumilivu... zile variables zipo ila sababu reaction ni tofauti kati ya mtu na mtu basi majibu yatakuwa tofauti...

Unaongelea binadamu wana wivu linapokuja suala la Mapenzi ? Je wale wanaoshare wake / waume Au yule anayempenda sana mwenza wake sababu anajua hamtimizii kitu fulani akaamua kumuacha achukuliwe na mwingine sababu kwake yeye furaha ya mwenza wake ndio furaha yake utasemaje Yaani yule ambaye yupo radhi yeye aumie ili mwenza wake afurahie utasemaje hapo kwamba hayo sio mapenzi.... au Haujaona mtu anajua kabisa kwa tabia zake sio perfect kwa mtu fulani anaamua ku-sacfrice his/her happiness kwa kumuacha aende.... (au undhani msemo wa if you love someone set him/her free..., ulikuja bila precedent ?) kwahio hata unachosema mapenzi yanaongozwa na wivu as I have just shown does not hold water in all cases.... (Ni myopic thinking na kuwa possisive kwa mwadamu anakodhani anaweza kummiliki binadamu mwenzake) na hizi nyingi mwisho wake huwa ni dissapointments na msongo wa mawazo....

Ingawa kwangu mimi hii hapo chini huenda ndio ikawa true love (na hapo true nasema perfect / ideal) lakini does not mean sababu dunia sio ideal haimaanishi kinachoendelea sio upendo....
 

Attachments

  • 1690196182918.png
    1690196182918.png
    85.3 KB · Views: 5
Watu kuwa tofauti hakuyafanyi Kanuni za mapenzi kuwa Tofauti,
Mapenzi bila kujali Watu wapo tofauti yanahitaji, Kujali, kuthamini, kuvutiwa, kujitoa n.k. mapenzi yanaongozwa na Kanuni kinzani ya Wivu. Wanadamu wote wanawivu linapokuja suala la mapenzi licha ya kuwa Binadamu kuna baadhi ya ishu tunatofautiana.

Kuhusu hizo Kanuni za mapenzi, sasa itategemea na tamaduni husika jinsi ya kuzitekeleza.
Mfano, Mwanamke wa Kikurya ili ajue unamjali basi sharti umpige. Wakati Mwanamke wa jamii zingine ukimpiga atajua haumpendi.
Sasa wewe unajadili hiyo tofauti ya mchakato wa kujali badala kuangalia dhamira ya mchakato ni kuonyesha Kujali. Nafikiri wewe unajadili zaidi Reactions kuliko lengo au chanzo cha hiyo reaction.

Mfano mwingine, MTU anaweza akafumania Mkewe au mumewe lakini mmoja akaua na mwingine asiue. Lakini Wote Wataumia(Wivu) lakini reaction zao zitakuwa tofauti Kutokana na sababu zingine ambazo zipo katika vipengele vingine labda vya Afya ya Akili, vyakula MTU anavyopendekea Kula au unywaji ambavyo huathiri tezi na homoni zinazozalishwa mwilini.

Utofauti wa Watu hauvunji Kanuni au formula.
Ila unaweza kuathiri mchakato(reactions) wa kudhihirisha Kanuni au formula Fulani.

Kwa mfano, Ukichukua Watu Wawili ambao wanapenda Gari Aina ya V8 nyeusi kama wapendavyo au kama walivyochagua, ukawaletea Kwa pamoja, mmoja anaweza kushangilia huku akikukumbatia, mwingine anaweza akalia huku akiwa haamini. Wote wamefurahi lakini reactions ni tofauti.

Ukimfanyia MTU Jambo zuri na analolipenda lazima atafurahi. Lakini kwenye kuonyesha furaha ndipo Watu wanapishana, ndio hizo reactions unazozisema.

Ndio maana Sheria za nchi hutungwa Kwa kuangalia Kanuni za vitu mahususi na sio reactions za Watu Kutokana na utofauti wao.
Wataangalia zaidi intention, dhamiri kulingana na reactions MTU alizofanya.

Kwa mfano, Mtu ameua. Hapo watataka vithibitisho vya kuonyesha Fulani ameua, kisha wataangalia sababu ya yeye kuua, hapo ndio itakuja kaua bila kukusudia au kakusudia. Kote Huko wanaendeshwa na formula au Kanuni Fulani.

Chukua MKE au Mpenzi wa mtu uone nini kitatokea, jibu ni kuwa Wivu na maumivu ya mapenzi lazima yatokee, hiyo ni Kwa binadamu wote. Kuhusu reactions ndio huwa tofauti lakini Kanuni na formula ni Ileile.
Nakupata sana that is to say sheria au kanuni hazitaangalia Emotions za wahusika sio
 
😀😀
Hamna Mkuu.
Nimetoa tuu ushauri Kwa Vijana. Leo na kesho Dada zetu mkianza kuwanyima unyumba na kuwapigisha jaramba wasijesema Kaka zao hatukusema

80% ya vijana wa leo wanalilia haki sawa, tena wanasema kizungu hakina kuoa na kuolewa ila kuoana....hovyo kabisaa

Ila mimi dada yao anawaambia sisi wanawake waafrika na waswahili wa Tanzania tumebarikiwa kwamba tunaolewa tena wasituletee habari za haki sawa.
Kikwetu Mwanaume anaoa na Mwanamke anaolewa! Mwenye maono ya kuoa ni mwanaume na sio mwanamke
 
MWANAMKE LAZIMA ABADILI DINI NA IMANI ILI IFANANE NA YAKO NDIPO UMUOE.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Moja ya ishara za awali Kwa Mwanamke anayekupenda na anayeweza kuwa Mkeo ni kukuamini, na kuamini Kwa kile ukifanyacho na kile unachokiamini. Kwa Mwanamke Hisia na Imani vinaenda sambamba. Mwanamke akishakuwa na hisia za upendo na wewe hapo moja Kwa moja atakuwa na Imani na wewe. Atakuamini. Kila unachomwambia Mwanamke anakiamini. Weka akilini hiyo.

Mwanamke akikupenda, atapenda unayoyapenda. Mtazamo wake utabadilika utakuwa Sawa na wako. Ndio maana ni rahisi kumbadilisha Mwanamke hata kama alikuwa ni kahaba lakini akishakupenda atauacha ukahaba wake. Ishu hapo ni hivi, Kwenye Moyo WA Mwanamke kuna Hisia na Imani. Wakati Sisi wanaume Imani Ipo kwenye Ubongo. Yaani hatuwezi kuamini Jambo bila kulitafakari Kutumia ubongo Akili.
Wakati Wanawake hawawezi kukuamini Jambo pasipo kuwa na hisia nalo, yaani kulipenda.

Sasa ili Mwanamke apende Jambo kuna michakato kadha wa kadha. Na yote lazima itimize imagination zake.

Ukiona umemtongoza Mwanamke mkaingia kwenye mahusiano alafu mpaka mnamaliza miezi sita hajataka Kubadili Imani na dini, jua huyo hujamkamata, yaani hujauteka moyo wake. Huyo hakufai. Hakuna mahali mtaenda.

Tena akikuambia wewe ndio umfuate ndio kabisa. Sisi Watibeli na wataalamu WA hayo mambo tunajua kuwa huyo Mwanamke Hakupendi, lakini pia atakupelekesha tuu.
Kingine ni lazima utashindwa kwenye ishu ya malezi. Yaani Watoto lazima wakushinde Kwa sababu tayari ulimshindwa Mama Yao.

Kubaniwa papuchi na kupewa chakula cha Usiku Kwa vipimo litakuwa ni Jambo la kawaida kwako na hautakuwa na chakufanya. Kiufupi utakuwa Dume-jike ambalo limeoa.

Asije akakudanganya MTU kuwa ndoa ya MKE na Mume WA Imani tofauti zinadumu au zinakuwa na Amani, hakuna kitu kama hicho.

Kingine cha muhimu zaidi ni kuwaz kamwe usimwambie Mwanamke abadili dini ili UMUOE. Hilo ni kosa la kiufundi. Mwanamke akishakupenda hatasubiri umwambie abadili Dini. Atabadili mwenyewe tuu Kwa mapenzi na uelewa wake kuhusu dini yako.

Kama hataki Kubadili dini yake Kwa hiyari jua huyo moyo wake haukupendi. Na kamwe hatakutii wala kukusikiliza Ila wewe ndiye utamtii na kumsikiliza. Atakupelekesha vile atakavyo.

Kesi nyingi za wanaowasiliana na Mimi nyingi zipo Kwa wanandoa ambao ni Aidha Mume alibadili dini na kufuata dini ya MKE. Au kila MTU alibaki na Dini yake wakafunga ndoa za bomani(serikalini).
Au mwanaume alitumia nguvu kumbadilisha Mwanamke Imani na Dini.

Elewa kuwa, kwenye mapenzi sio lazima uwe na MTU Fulani hasa kama hakupendi.
Elewa kuwa , mapenzi hayalazimishwi.
Elewa kuwa, kila mtu anauhuru wa Kutumia mwili wake. Hivyo usimpangie mkeo au mumeo matumizi ya mwili wake. Bali jipangie mwenyewe. Kama anakupenda basi ataji-commit kwako na sio wewe umlazimishe aji-commit kwako. Ila unaweza kujipangia kuwa huwezi ishi na Mwanamke au Mwanaume aliyeamua kuutumia mwili wake kufanya uasherati na uzinzi.
Hivyo katika mkataba wenu wa mahusiano ya ndoa, uwepo sheria iliyosainiwa au kukubaliana kuwa Kila MTU anauhuru wa Kutumia mwili wake atakavyo pasipo kuingiliwa na mwingine lakini Mimi(unaweza kuwa MKE au Mume) hutoweza kuishi na mtu mchafu (mzinzi na muasherati) hivyo Talaka itatoka ili kumpa MKE/mume Uhuru wa kuutumia mwili wake katika uchafu kadiri ya atakavyo.
Na hakutakuwa na Mijadala wala usuluhishi Kwa sababu ni Jambo lililojulikana mapema.

Hakutakuwa na hiyo nafasi ya kumshauri, kumfundisha mtu mzima aliyeko kwenye ndoa namna ya kuutumia mwili wake. Ila kila litakalofanyika litahesabika kama uamuzi wa Makusudi uliodhamiriwa na Mhusika.

Msamaha WA pekee utatolewa Baada ya Talaka kukabidhiwa. Kila MTU aishi Maisha yake lakini tukiwa tumesameheana. Hizo ni Kanuni za Watibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Utumwa wa fikra;
 
Hii kitu ya dini kwenye ndoa staki hata kuiskia ilinifanya nipitie wakati mgumu sana pamoja na baby mama wangu alafu kipindi hicho ndokatoka kujifungua daah depression is really mzee wanasemaga ugali moto mboga moto hakuna pakushika kwake wazazi wamewaka awataki kuelewa kitu upande wangu wazazi wamewaka hawataki kuskia kitu vikako havikaliki vumbi linatimka mwanamke muda wote kulia tu kutengana na mimi hataki nikiwaza kumchukua niondoke nae kimya kimya nikaishinae mbali nikiwaza je likitokea lakutokea maana sisi nibinadami unafikiri nani atakuelewa daah kile kipindi nilichopita sitokisahau
 
Hapa tutazunguka mpaka kesho... Mtu anaposema maisha hayana formula / au mapenzi hayana formula haimaanishi kwamba Mapenzi hayana uhusiano na attraction wala haibadilishi uhusiano wa kudumu kwa ndoa na uvumilivu... zile variables zipo ila sababu reaction ni tofauti kati ya mtu na mtu basi majibu yatakuwa tofauti...

Unaongelea binadamu wana wivu linapokuja suala la Mapenzi ? Je wale wanaoshare wake / waume Au yule anayempenda sana mwenza wake sababu anajua hamtimizii kitu fulani akaamua kumuacha achukuliwe na mwingine sababu kwake yeye furaha ya mwenza wake ndio furaha yake utasemaje Yaani yule ambaye yupo radhi yeye aumie ili mwenza wake afurahie utasemaje hapo kwamba hayo sio mapenzi.... au Haujaona mtu anajua kabisa kwa tabia zake sio perfect kwa mtu fulani anaamua ku-sacfrice his/her happiness kwa kumuacha aende.... (au undhani msemo wa if you love someone set him/her free..., ulikuja bila precedent ?) kwahio hata unachosema mapenzi yanaongozwa na wivu as I have just shown does not hold water in all cases.... (Ni myopic thinking na kuwa possisive kwa mwadamu anakodhani anaweza kummiliki binadamu mwenzake) na hizi nyingi mwisho wake huwa ni dissapointments na msongo wa mawazo....

Ingawa kwangu mimi hii hapo chini huenda ndio ikawa true love (na hapo true nasema perfect / ideal) lakini does not mean sababu dunia sio ideal haimaanishi kinachoendelea sio upendo....

Hakuna Mwanamke ambaye anakubali kuwa Uke Wenza, huo ni ukweli.
Kwa sababu penye mapenzi lazima Wivu uwepo.

Wewe unacholeta sasa ni ubishi, hiyo kuongea mpaka kesho labda utafute MTU mwingine WA kuongea naye.

Kama Kwa Akili yako unaona Watu kuolewa Wawili unadhani Hawana Wivu basi utakuwa huna unachoelewa kuhusu kile ninachozungumzia.
 
Ni kweli sana

Mtoto wa mama mkwe aliponikamata sawasawa niliswitch kutoka RC kwenda KKKT chap bila kuombwa, na niko vizuri kuzidi na yeye mwenyewe mzawa, hisia na imani vinaenda pamoja ni ngumu kumuombea mtu ambae hamko imani moja hamuongei lugha moja

Ila PM na mkewe wamewezaje kuishi hivyo mpaka kufikia level hiyo na bado kila mmoja akiwa na dini yake na jamaa hajaongeza mke mwingine wala
"Aliponikamata sawasawa" maelezo tafadhali[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Hii kitu ya dini kwenye ndoa staki hata kuiskia ilinifanya nipitie wakati mgumu sana pamoja na baby mama wangu alafu kipindi hicho ndokatoka kujifungua daah depression is really mzee wanasemaga ugali moto mboga moto hakuna pakushika kwake wazazi wamewaka awataki kuelewa kitu upande wangu wazazi wamewaka hawataki kuskia kitu vikako havikaliki vumbi linatimka mwanamke muda wote kulia tu kutengana na mimi hataki nikiwaza kumchukua niondoke nae kimya kimya nikaishinae mbali nikiwaza je likitokea lakutokea maana sisi nibinadami unafikiri nani atakuelewa daah kile kipindi nilichopita sitokisahau

Pole Sana Mkuu
 
80% ya vijana wa leo wanalilia haki sawa, tena wanasema kizungu hakina kuoa na kuolewa ila kuoana....hovyo kabisaa

Ila mimi dada yao anawaambia sisi wanawake waafrika na waswahili wa Tanzania tumebarikiwa kwamba tunaolewa tena wasituletee habari za haki sawa.
Kikwetu Mwanaume anaoa na Mwanamke anaolewa! Mwenye maono ya kuoa ni mwanaume na sio mwanamke

Ningekuwa sijaoa ningetuma posa walahi
 
Hakuna Mwanamke ambaye anakubali kuwa Uke Wenza, huo ni ukweli.
Unaongelea Uke Wenza ? unadhani hio ndio modal pekee

Mimi naongelea wife Swap ; Naongelea tamaduni za wamasai mtu akiondoka mwingine kesho akija anaingia hapo; Naongelea kwa mtoto wa kike kuona kwamba kuolewa na mfalme ni dream yake hivyo yupo radhi hata akiwa mke wa mia tano kwamba hicho ndio anachotaka sasa ukisema binti huyu hakubaliani na dream yake (ile status ) nadhani unaangalia mambo nusu nusu na una-generalize mambo
Kwa sababu penye mapenzi lazima Wivu uwepo.
Nimekupa mfano mtu akipenda kitu hadi akiona kwamba huyu mpenzi wangu anatamani pesa na mimi siwezi kumtimizia hivyo anakosa furaha na kukosa kwake furaha na mimi sina furaha bora aende kwa mfalme huko yaani kupata kwake yeye na mimi nimepata furaha yake furaha yangu (unazungumzia vipi scenario hio) au unaangalia maisha kwa your own perspective na unadhani mitizamo yako ni sawa na mwingine ?
Wewe unacholeta sasa ni ubishi, hiyo kuongea mpaka kesho labda utafute MTU mwingine WA kuongea naye.

Kama Kwa Akili yako unaona Watu kuolewa Wawili unadhani Hawana Wivu basi utakuwa huna unachoelewa kuhusu kile ninachozungumzia.
Wivu wa nini na kwenye nini tatizo lako kubwa ni kudhani unavyodhani wewe ndio msaafu wa maisha ya wengine..., mwingine anapenda furaha ya mwenza wake, yaani akiona vile wanavyomtumikia huyo mwenza kwao ndio wamefika..., kwahio na yeye sababu ana ile position ya mama wa nyumba Mkuu.... kwake anafurahia ile heshima anayopewa; mapenzi mwisho wa siku its all in the mind kwahio ni jinsi unavyoji-position au mtizamo wako kwahio kuna culture nyingine the more wake wenza wanavyoongezeka ndio vijakazi / watu wa kumuheshimu mke wa kwanza inavyoongezeka kwahio ile inakuwa kama family hata wivu ukija huenda usiwe wivu wa kupendwa zaidi au ku-share ile love na muhusika bali ikawa fulani ana watoto wengi zaidi kamzalia fulani kuliko mimi (motherly love)

Narudia tena its all in the mind and since people have different perceptions you can never expect to get same outcomes...
 
Ningekuwa sijaoa ningetuma posa walahi

Wacha tubaki hapahapa kuelimisha vijana

Kuna vijana wangu wa karibu 13; yaani familia na marafiki walikua na matarajio ya kuoana last year nikabahati kukutana na 9 Kati yao. Kati ya hao 9 wa kiume walikua 6 wa kike wa 3. Hadi sasa wale vijana wa kiume wameamua kuahirisha harusi ili kujiimarisha kwanza kiuchumi, wale3 wa kike wawili waliolewa na mmoja akavunja mahusiano.

Vijana wengi hawajui ndoa ni jukumu ila wanajua ndoa ni sex na sex kwao ni starehe
 
Wacha tubaki hapahapa kuelimisha vijana

Kuna vijana wangu wa karibu 13; yaani familia na marafiki walikua na matarajio ya kuoana last year nikabahati kukutana na 9 Kati yao. Kati ya hao 9 wa kiume walikua 6 wa kike wa 3. Hadi sasa wale vijana wa kiume wameamua kuahirisha harusi ili kujiimarisha kwanza kiuchumi, wale3 wa kike wawili waliolewa na mmoja akavunja mahusiano.

Vijana wengi hawajui ndoa ni jukumu ila wanajua ndoa ni sex na sex kwao ni starehe

Ni kweli wengi wanajua ndoa ni kufanya ngono muda wote.
Ilhali sivyo, ndoa ni kampani, kusaidiana majukumu.
 
MWANAMKE LAZIMA ABADILI DINI NA IMANI ILI IFANANE NA YAKO NDIPO UMUOE.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Moja ya ishara za awali Kwa Mwanamke anayekupenda na anayeweza kuwa Mkeo ni kukuamini, na kuamini Kwa kile ukifanyacho na kile unachokiamini. Kwa Mwanamke Hisia na Imani vinaenda sambamba. Mwanamke akishakuwa na hisia za upendo na wewe hapo moja Kwa moja atakuwa na Imani na wewe. Atakuamini. Kila unachomwambia Mwanamke anakiamini. Weka akilini hiyo.

Mwanamke akikupenda, atapenda unayoyapenda. Mtazamo wake utabadilika utakuwa Sawa na wako. Ndio maana ni rahisi kumbadilisha Mwanamke hata kama alikuwa ni kahaba lakini akishakupenda atauacha ukahaba wake. Ishu hapo ni hivi, Kwenye Moyo WA Mwanamke kuna Hisia na Imani. Wakati Sisi wanaume Imani Ipo kwenye Ubongo. Yaani hatuwezi kuamini Jambo bila kulitafakari Kutumia ubongo Akili.
Wakati Wanawake hawawezi kukuamini Jambo pasipo kuwa na hisia nalo, yaani kulipenda.

Sasa ili Mwanamke apende Jambo kuna michakato kadha wa kadha. Na yote lazima itimize imagination zake.

Ukiona umemtongoza Mwanamke mkaingia kwenye mahusiano alafu mpaka mnamaliza miezi sita hajataka Kubadili Imani na dini, jua huyo hujamkamata, yaani hujauteka moyo wake. Huyo hakufai. Hakuna mahali mtaenda.

Tena akikuambia wewe ndio umfuate ndio kabisa. Sisi Watibeli na wataalamu WA hayo mambo tunajua kuwa huyo Mwanamke Hakupendi, lakini pia atakupelekesha tuu.
Kingine ni lazima utashindwa kwenye ishu ya malezi. Yaani Watoto lazima wakushinde Kwa sababu tayari ulimshindwa Mama Yao.

Kubaniwa papuchi na kupewa chakula cha Usiku Kwa vipimo litakuwa ni Jambo la kawaida kwako na hautakuwa na chakufanya. Kiufupi utakuwa Dume-jike ambalo limeoa.

Asije akakudanganya MTU kuwa ndoa ya MKE na Mume WA Imani tofauti zinadumu au zinakuwa na Amani, hakuna kitu kama hicho.

Kingine cha muhimu zaidi ni kuwaz kamwe usimwambie Mwanamke abadili dini ili UMUOE. Hilo ni kosa la kiufundi. Mwanamke akishakupenda hatasubiri umwambie abadili Dini. Atabadili mwenyewe tuu Kwa mapenzi na uelewa wake kuhusu dini yako.

Kama hataki Kubadili dini yake Kwa hiyari jua huyo moyo wake haukupendi. Na kamwe hatakutii wala kukusikiliza Ila wewe ndiye utamtii na kumsikiliza. Atakupelekesha vile atakavyo.

Kesi nyingi za wanaowasiliana na Mimi nyingi zipo Kwa wanandoa ambao ni Aidha Mume alibadili dini na kufuata dini ya MKE. Au kila MTU alibaki na Dini yake wakafunga ndoa za bomani(serikalini).
Au mwanaume alitumia nguvu kumbadilisha Mwanamke Imani na Dini.

Elewa kuwa, kwenye mapenzi sio lazima uwe na MTU Fulani hasa kama hakupendi.
Elewa kuwa , mapenzi hayalazimishwi.
Elewa kuwa, kila mtu anauhuru wa Kutumia mwili wake. Hivyo usimpangie mkeo au mumeo matumizi ya mwili wake. Bali jipangie mwenyewe. Kama anakupenda basi ataji-commit kwako na sio wewe umlazimishe aji-commit kwako. Ila unaweza kujipangia kuwa huwezi ishi na Mwanamke au Mwanaume aliyeamua kuutumia mwili wake kufanya uasherati na uzinzi.
Hivyo katika mkataba wenu wa mahusiano ya ndoa, uwepo sheria iliyosainiwa au kukubaliana kuwa Kila MTU anauhuru wa Kutumia mwili wake atakavyo pasipo kuingiliwa na mwingine lakini Mimi(unaweza kuwa MKE au Mume) hutoweza kuishi na mtu mchafu (mzinzi na muasherati) hivyo Talaka itatoka ili kumpa MKE/mume Uhuru wa kuutumia mwili wake katika uchafu kadiri ya atakavyo.
Na hakutakuwa na Mijadala wala usuluhishi Kwa sababu ni Jambo lililojulikana mapema.

Hakutakuwa na hiyo nafasi ya kumshauri, kumfundisha mtu mzima aliyeko kwenye ndoa namna ya kuutumia mwili wake. Ila kila litakalofanyika litahesabika kama uamuzi wa Makusudi uliodhamiriwa na Mhusika.

Msamaha WA pekee utatolewa Baada ya Talaka kukabidhiwa. Kila MTU aishi Maisha yake lakini tukiwa tumesameheana. Hizo ni Kanuni za Watibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Ukweli mchungu!
 
Wacha tubaki hapahapa kuelimisha vijana

Kuna vijana wangu wa karibu 13; yaani familia na marafiki walikua na matarajio ya kuoana last year nikabahati kukutana na 9 Kati yao. Kati ya hao 9 wa kiume walikua 6 wa kike wa 3. Hadi sasa wale vijana wa kiume wameamua kuahirisha harusi ili kujiimarisha kwanza kiuchumi, wale3 wa kike wawili waliolewa na mmoja akavunja mahusiano.


Vijana wengi hawajui ndoa ni jukumu ila wanajua ndoa ni sex na sex kwao ni starehe
Kwamba ndoa ni majukumu ya mwanaume kuhudumia na sio ma-partner kushirikiana ili kuendesha jahazi ?

Kwamba usubiri kwanza ujiimarishe ki-uchumi na sio kwamba nyote mlio na uchumi duni muingie kwenye Jahazi na Kujiimarisha nyote na pale mkiwa sawa ndio muwe na familia ? (Sababu kumbuka watoto ndio wanahitaji huduma na wala hawajakuomba uwalete hivyo ukiwaleta gundua unahitaji kuwahudumia) nyie wawili hata mkishindia H2O ni uamuzi wenu...

Tatizo ambalo umeongelea wewe ni kwamba kwa sasa hakuna mapenzi ya kweli bali ni fursa.., Logically usemayo wewe ni kwamba masikini wasioe (kumbe tena unakuta masikini ndio wana familia kubwa hence defying your logic);

Moral of my Rant: Kuanzisha familia lazima muwe mmejipanga (sio ujipange bali mjipange) lakini mkiwa mnapendana na mmeshibana mnaweza kuingia nyote na kusaidiana katika shida zenu...

Hio ndio ndoa in an ideal world; lakini sababu uhalisia ni tofauti basi huwezi kuwalaumu hata vijana wa sasa sababu uhalisia ni tofauti na maisha yao ya sasa ni tofauti na ulivyoishi wewe (huenda wewe ndoa ilidumu sababu ya uvumilivu wako na sio perfection ya mwenza wako)
 
Back
Top Bottom