Mwanamke lazima Abadili Dini na Imani Ili ifanane na yako ndipo umuoe.

Mwanamke lazima Abadili Dini na Imani Ili ifanane na yako ndipo umuoe.

Tunazungumzia Mapenzi na mahusiano ya Ndoa. Wewe unazungumzia MAISHA.
Ni vitu viwili tofauti.
Okay kwahio unazungumzia mapenzi na ndoa ambayo yana Kanuni zake; Je hizo Kanuni ni universal, Sababu ndoa (sheria na mipangilio) ni tofauti kutokana na Jamii moja mpaka nyingine..., Tukija kwenye Mapenzi ni Mtu kupenda kwahio anaweza akafuata Jamii iliyomzunguka inataka afanye nini lakini sio necessarily hayo ni mapenzi yake...

Mfano sio zamani kuna kina mama walitakiwa wawe wanakaa nyumbani na kulea watoto; ingawa kuna jamii za watu wa Ancient Celtic hadi kina mama walikuwa wanakwenda vitani...; kwahio utaona sheria na nafasi ya mtu na mtu katika ndoa katika jamii moja sio necessarily sawa na jamii nyingine, vilevile individually huenda mtu asipende ila akalazimishwa (refer arranged marriages) kwahio huenda ukafurahisha jamii lakini sio nafsi
Maisha ni neno la Jumla ambalo ndani yake kuna mambo mengi.
Alafu Mapenzi na ndoa ni neno mahususi.

Ni Sawa useme Matunda alafu useme Embe.

Maisha hayana Kanuni Kwa sababu ni neno la Jumla lakini vitu vilivyomo ndani ya Maisha ambavyo ni mahususi (specific) vina Kanuni na formula.

Siasa zina Kanuni zake,
Uchumi unakanuni zake
Dini zinakanuni zake
Akili na tabia ya Mwanadamu inakanuni zake.
Mapenzi na ndoa vinakanuni zake.

Maisha hayana Kanuni Kwa sababu yanahusu muunganiko wa specifications zote za yanayomzunguka Mwanadamu.
Nadhani hapo juu nimejibu huwezi kuchukua formula ya gaelic women ukaipeleka kwa persian women katika mahusiano yao..., vilevile hata katika jamii husika tuseme wahindi na arranged marriages (ingawa jamii inataka hivyo na ndio utamaduni wao) lakini bado kuna individuals kutokana na shinikizo hizo na kutokuwa na upendo wanapelekea kujiua au kuishi maisha ya masikitiko na wengine kuchukiana hata kuwekeana sumu....

Like I say..., anything with too many variables can not be constant..., mambo hayo yote sio black or white (there is lot of grey areas and there is exception to the Rule to everything...., '

Life is not mathematics, and few things have only one correct answer' na hapo naweka (Siasa, Uchumi, Dini, Akili na Tabia, Mapenzi na Ndoa)
 
Mwanamke wa leo anayeweza kumkana MUNGU wa imani yake ili aolewe pia kuwa naye makini. Kama unafungwa na dini kaoe wa dini yako.
 
Nao
Sijasoma ndani nimesoma heading ila kwenye heading yakaja maswali yafuatayo....

Hivi aliyesema maisha yana formula (yaani constant unayoweza kuhamisha kutoka kwa huyu kwenda kwa yule ni nani) yaani sababu y = mx + c; kwahio wewe / mtu yoyote ni kupachika hizo variables basi unapata jibu ambalo ni sawa kwa wote ?

Nadhani ukijua kwamba maisha sio black or white na kuna variables kibao; pia kinachofanyika kwako sio lazima kifanyike kwa mwingine utaona kwamba maisha ni simple sana wala hayahitaji complications (to each his / her own); Yaani Maisha yako ni wewe ndio unayajua zaidi kuliko third party yoyote....
Naona umeamua kumaliza kila kitu😍
 
Okay kwahio unazungumzia mapenzi na ndoa ambayo yana Kanuni zake; Je hizo Kanuni ni universal, Sababu ndoa (sheria na mipangilio) ni tofauti kutokana na Jamii moja mpaka nyingine..., Tukija kwenye Mapenzi ni Mtu kupenda kwahio anaweza akafuata Jamii iliyomzunguka inataka afanye nini lakini sio necessarily hayo ni mapenzi yake...

Mfano sio zamani kuna kina mama walitakiwa wawe wanakaa nyumbani na kulea watoto; ingawa kuna jamii za watu wa Ancient Celtic hadi kina mama walikuwa wanakwenda vitani...; kwahio utaona sheria na nafasi ya mtu na mtu katika ndoa katika jamii moja sio necessarily sawa na jamii nyingine, vilevile individually huenda mtu asipende ila akalazimishwa (refer arranged marriages) kwahio huenda ukafurahisha jamii lakini sio nafsi

Nadhani hapo juu nimejibu huwezi kuchukua formula ya gaelic women ukaipeleka kwa persian women katika mahusiano yao..., vilevile hata katika jamii husika tuseme wahindi na arranged marriages (ingawa jamii inataka hivyo na ndio utamaduni wao) lakini bado kuna individuals kutokana na shinikizo hizo na kutokuwa na upendo wanapelekea kujiua au kuishi maisha ya masikitiko na wengine kuchukiana hata kuwekeana sumu....

Like I say..., anything with too many variables can not be constant..., mambo hayo yote sio black or white (there is lot of grey areas and there is exception to the Rule to everything...., '

Life is not mathematics, and few things have only one correct answer' na hapo naweka (Siasa, Uchumi, Dini, Akili na Tabia, Mapenzi na Ndoa)

Kwenye mapenzi Duniani kote Kanuni ni zilezile.
Kanuni zote zinakuwa na matokeo yanayofanana.
Ukienda Ulaya, ukienda Asia au huku Afrika mapenzi na ndoa Kanuni zake ni zilezile.
Mapenzi yanaongozwa na Kanuni ya Asili na sio sheria za Mila na desturi. Ndoa ndio huongozwa na sheria za Mila na desturi.

Ukishasema Utamaduni hicho ni kipengele kwenye Maisha ambacho nacho kinakanuni zake. Ukisema Wanawake wa kihindi au kigiriki wanalimitiwa na sheria au Mila Fulani, elewa hayo ni mambo ya kitamaduni ambayo yanabadilika Kutokana na nyakati na Zama.
Ila Mapenzi hayabadiliki na Kanuni zake ni zilezile tuu.

Kuhusu kufanya kazi, kufanya kazi kuna Kanuni zake bila kujali kazi hiyo ni Aina ipi. Kazi itahitaji Ujuzi na maarifa sahihi ili lete matokeo chanya hiyo ni Duniani kote. Kuhusu Nani anafanya kazi hiyo Ipo kwenye kipengele cha utamaduni. Iwe ni Mwanaume, Mwanamke Kwa habari za jinsia, au Kijana au Mzee Kwa habari za umri. Lakini Kanuni ya Kazi haiangalii hayo itakachoangalia ni Ujuzi na maarifa.

Maisha hayana Kanuni kutokana kuwa ni muunganiko wa mambo mengi, kama ulivyosema Variables zipo nyingi.
Lakini hizo Variable zina Kanuni na Formula.

Kwa mfano, katika suala la Uzazi katika Sexual Reproduction.
Ni lazima Fertilization itokee Baada ya Mbegu ya mwanaume zinapokutana na Yai la Mwanamke. Hiyo ni Kanuni.
Sasa mwingine atasema mpaka kujamiiana lakini kujamiana sio Kanuni ya kuu Bali kukutana Kwa Mbegu ya kiume na yai la kike. Hiyo ndio Kanuni.

Hivyo Teknolojia inavyokua haiwezi kuvunja Kanuni hiyo, lakini inaweza rahisisha michakato ya kuifikia Kanuni kuu.
 
Mwanamke wa leo anayeweza kumkana MUNGU wa imani yake ili aolewe pia kuwa naye makini. Kama unafungwa na dini kaoe wa dini yako.

Tatizo Vijana hamsomi Kwa ufahamu.
Hata ukioa wa dini yako. Kama hakupendi anaweza akawa na Imani na mitazamo tofauti na yako Kwa kiwango kikubwa Hali itakayomfanya asikuheshimu kama Mume.

Nazungumzia Mwanamke akikupenda, sijui Kwa nini Watu siku hizi hamsomi vitu Kwa ufahamu
 
Tatizo Vijana hamsomi Kwa ufahamu.
Hata ukioa wa dini yako. Kama hakupendi anaweza akawa na Imani na mitazamo tofauti na yako Kwa kiwango kikubwa Hali itakayomfanya asikuheshimu kama Mume.

Nazungumzia Mwanamke akikupenda, sijui Kwa nini Watu siku hizi hamsomi vitu Kwa ufahamu
Tatizo JF watu mna assumption sana. Hapo unaweza kuta upo kwenye 30's ila ushaweka assumptions zako na unaweza dharau maoni ya mtu mwenye ndoa ya zaidi ya 20 yrs.

Anyway, Dini haijawahi kuyashinda mapenzi ndo maana nakwambia mwanamke anayeikana imani yake ili aolewe uwe makini naye, mapenzi huisha na kubaki kiapo cha ndoa. Elewa maana ya kuwa makini naye.
 
Tatizo JF watu mna assumption sana. Hapo unaweza kuta upo kwenye 30's ila ushaweka assumptions zako na unaweza dharau maoni ya mtu mwenye ndoa ya zaidi ya 20 yrs.

Anyway, Dini haijawahi kuyashinda mapenzi ndo maana nakwambia mwanamke anayeikana imani yake ili aolewe uwe makini naye, mapenzi huisha na kubaki kiapo cha ndoa. Elewa maana ya kuwa makini naye.

Vizuri, kumbe unaelewa kuwa Dini haijawahi yashinda mapenzi Kwa sababu mapenzi yananguvu. Sasa kipi unakataa kuwa Mwanamke akikupenda lazima abadili Dini? Au huelewi unachoandika na ulichokisoma?

Mapenzi yalianza Kabla ya Dini.
Mapenzi ndio yaliyoumba Imani. Mapenzi ni Upendo. Upendo ndio umeumba Imani.

Mapenzi yanaisha pale baadhi ya Kanuni zikivunjwa kama kukosa uaminifu, kutokujali, ubinafsi n.k. hizo ni Kanuni.

Kiapo cha ndoa hakina lolote la kufanya katika mapenzi, Kwa sababu yapo mabilioni ya Waliooana na hawana hicho kiapo cha Ndoa.

Mapenzi yakishakufa tafsiri yake hakuna ndoa Hapo. Mapenzi ndio ndoa yenyewe.

Kuhusu umri Hilo TOA Shaka.
MTU anaweza kuwa alienda kufungishwa ndoa lakini asiwe ndani ya Ndoa. Alafu kuna MTU anandoa lakini hajawahi kufungishwa Ndoa. Ambapo Watu huita anaishi kinyumba.

Unaweza ukadhani upo ndoani Kwa miaka 20 ilhali haujawahi kuwa ndoani Kwa miaka Mitano. Yaani Mkeo/Mumeo hakupendi.

Dini unafundishwa lakini mapenzi haufundishwi. Mapenzi unajikuta unapenda tuu.
 
Vizuri, kumbe unaelewa kuwa Dini haijawahi yashinda mapenzi Kwa sababu mapenzi yananguvu. Sasa kipi unakataa kuwa Mwanamke akikupenda lazima abadili Dini? Au huelewi unachoandika na ulichokisoma?
Nimesema kwa wanawake wa kileo akiikataa imani yake ili umuoe kijana kuwa naye makini. Kwanini unaasume kuwa kwa kusema hivyo nimepingana na hoja yako? Au hoja yako imejikita kuwa ukishapendwa ukose umakini?
Mapenzi yalianza Kabla ya Dini.
Mapenzi ndio yaliyoumba Imani. Mapenzi ni Upendo. Upendo ndio umeumba Imani.
Sipingi
Mapenzi yanaisha pale baadhi ya Kanuni zikivunjwa kama kukosa uaminifu, kutokujali, ubinafsi n.k. hizo ni Kanuni.

Kiapo cha ndoa hakina lolote la kufanya katika mapenzi, Kwa sababu yapo mabilioni ya Waliooana na hawana hicho kiapo cha Ndoa.

Mapenzi yakishakufa tafsiri yake hakuna ndoa Hapo. Mapenzi ndio ndoa yenyewe.

Kuhusu umri Hilo TOA Shaka.
MTU anaweza kuwa alienda kufungishwa ndoa lakini asiwe ndani ya Ndoa. Alafu kuna MTU anandoa lakini hajawahi kufungishwa Ndoa. Ambapo Watu huita anaishi kinyumba.

Unaweza ukadhani upo ndoani Kwa miaka 20 ilhali haujawahi kuwa ndoani Kwa miaka Mitano. Yaani Mkeo/Mumeo hakupendi.

Dini unafundishwa lakini mapenzi haufundishwi. Mapenzi unajikuta unapenda tuu.
Sawa.
 
Nimesema kwa wanawake wa kileo akiikataa imani yake ili umuoe kijana kuwa naye makini. Kwanini unaasume kuwa kwa kusema hivyo nimepingana na hoja yako? Au hoja yako imejikita kuwa ukishapendwa ukose umakini?

Sipingi

Sawa.

Vizuri kabisa Mkuu.

Hapo unamaanisha kuwa, upendo wa mabinti wa kileo ni wakutia Shaka, hivyo Vijana wasipumbazike.
Hapo upo sahihi Kabisa

Kwamba Binti anaweza kuzuga anakupenda, kisha anabadili dini yake anafuata yako kumbe anakuchota.

Umakini ni muhimu Sana
 
Kwenye mapenzi Duniani kote Kanuni ni zilezile.
Kanuni zote zinakuwa na matokeo yanayofanana.
Ukienda Ulaya, ukienda Asia au huku Afrika mapenzi na ndoa Kanuni zake ni zilezile.
Mapenzi yanaongozwa na Kanuni ya Asili na sio sheria za Mila na desturi. Ndoa ndio huongozwa na sheria za Mila na desturi.
Naona hapa umeamua tuzunguke bila kujua tunaongelea nini Labda nikuulize mapenzi ni nini na Kanuni ni nini ? Kama wote tunapenda sawa si wote tungekuwa tunampenda mmoja na kuchukia wengine wote.. Ndio maana nikasema people are different thus unpredictability in outcomes - Kutokana na kwamba The players are different huwezi kutegemea same outcome hata kama kwenye mpira unategemea mtu akipata pasi apige golini ili afunge mwingine atataka apige chenga au atoe pasi au sehemu ya kutoa pasi sababu ni selfish atapiga ili afunge
Ukishasema Utamaduni hicho ni kipengele kwenye Maisha ambacho nacho kinakanuni zake. Ukisema Wanawake wa kihindi au kigiriki wanalimitiwa na sheria au Mila Fulani, elewa hayo ni mambo ya kitamaduni ambayo yanabadilika Kutokana na nyakati na Zama.
Ila Mapenzi hayabadiliki na Kanuni zake ni zilezile tuu.
Mapenzi / Kupenda hakubadiliki ila kupenda kwa huyu ni tofauti na yule; kupenda its all chemistry and its in the brain unaweza ukai-break down to the atomic level ila point yangu kubwa ni kwamba hata kitu kilekile mnaweza mkakiangalia watu kumi, kila mtu akawa na perspective yake..., things are not that simple kutokana na kwamba Binadamu ni complex na tuna-different perception; tena ukiongelea utamaduni na sheria hapo mara nyingi ni shinikizo la wengi ambapo katika individual level huenda ikapingana na hao wengi
Kuhusu kufanya kazi, kufanya kazi kuna Kanuni zake bila kujali kazi hiyo ni Aina ipi. Kazi itahitaji Ujuzi na maarifa sahihi ili lete matokeo chanya hiyo ni Duniani kote. Kuhusu Nani anafanya kazi hiyo Ipo kwenye kipengele cha utamaduni. Iwe ni Mwanaume, Mwanamke Kwa habari za jinsia, au Kijana au Mzee Kwa habari za umri. Lakini Kanuni ya Kazi haiangalii hayo itakachoangalia ni Ujuzi na maarifa.
Ujuzi na maarifa ? Nyenzo je ? Unaweza ukawa na ujuzi na maarifa ila hauna nyenzo wala nguvu (kwa sentensi hio tu nimeamua ku-prove kwako kwamba there is always exception to the rule.....
Maisha hayana Kanuni kutokana kuwa ni muunganiko wa mambo mengi, kama ulivyosema Variables zipo nyingi.
Lakini hizo Variable zina Kanuni na Formula.
Unapomuongelea Binadamu ambaye ni complex huwezi kuhakikisha reaction yake itakuwa sawa na haitakuwa sawa akikutana na reactants tofauti, just because yeye kama yeye ni tofauti hivyo reaction yake ni tofauti kulingana na mazingira (hizo sio kama keki ukikoroga mchanyato ukaweka kwenye oven baada ya muda utatoa kitu kitamu) hata keki kuna ambazo zitaungua na nyingine kuwa kavu (kulingana na moto ulizi-affect vipi)
Kwa mfano, katika suala la Uzazi katika Sexual Reproduction.
Ni lazima Fertilization itokee Baada ya Mbegu ya mwanaume zinapokutana na Yai la Mwanamke. Hiyo ni Kanuni.
Nope sio lazima itokee kuna happenstances kibao zinaweza kufanyika na hilo lisitokee...,,
Sasa mwingine atasema mpaka kujamiiana lakini kujamiana sio Kanuni ya kuu Bali kukutana Kwa Mbegu ya kiume na yai la kike. Hiyo ndio Kanuni.

Hivyo Teknolojia inavyokua haiwezi kuvunja Kanuni hiyo, lakini inaweza rahisisha michakato ya kuifikia Kanuni kuu.
Have you seen researches ambazo unfertilized egg inatoa embryo..., Au kwa plants grafting and the likes...; au cheki hii research

 
Vizuri kabisa Mkuu.

Hapo unamaanisha kuwa, upendo wa mabinti wa kileo ni wakutia Shaka, hivyo Vijana wasipumbazike.
Hapo upo sahihi Kabisa

Kwamba Binti anaweza kuzuga anakupenda, kisha anabadili dini yake anafuata yako kumbe anakuchota.

Umakini ni muhimu Sana
Kabisa boss.
 
Naona hapa umeamua tuzunguke bila kujua tunaongelea nini Labda nikuulize mapenzi ni nini na Kanuni ni nini ? Kama wote tunapenda sawa si wote tungekuwa tunampenda mmoja na kuchukia wengine wote.. Ndio maana nikasema people are different thus unpredictability in outcomes - Kutokana na kwamba The players are different huwezi kutegemea same outcome hata kama kwenye mpira unategemea mtu akipata pasi apige golini ili afunge mwingine atataka apige chenga au atoe pasi au sehemu ya kutoa pasi sababu ni selfish atapiga ili afunge

Mapenzi / Kupenda hakubadiliki ila kupenda kwa huyu ni tofauti na yule; kupenda its all chemistry and its in the brain unaweza ukai-break down to the atomic level ila point yangu kubwa ni kwamba hata kitu kilekile mnaweza mkakiangalia watu kumi, kila mtu akawa na perspective yake..., things are not that simple kutokana na kwamba Binadamu ni complex na tuna-different perception; tena ukiongelea utamaduni na sheria hapo mara nyingi ni shinikizo la wengi ambapo katika individual level huenda ikapingana na hao wengi

Ujuzi na maarifa ? Nyenzo je ? Unaweza ukawa na ujuzi na maarifa ila hauna nyenzo wala nguvu (kwa sentensi hio tu nimeamua ku-prove kwako kwamba there is always exception to the rule.....

Unapomuongelea Binadamu ambaye ni complex huwezi kuhakikisha reaction yake itakuwa sawa na haitakuwa sawa akikutana na reactants tofauti, just because yeye kama yeye ni tofauti hivyo reaction yake ni tofauti kulingana na mazingira (hizo sio kama keki ukikoroga mchanyato ukaweka kwenye oven baada ya muda utatoa kitu kitamu) hata keki kuna ambazo zitaungua na nyingine kuwa kavu (kulingana na moto ulizi-affect vipi)

Nope sio lazima itokee kuna happenstances kibao zinaweza kufanyika na hilo lisitokee...,,

Have you seen researches ambazo unfertilized egg inatoa embryo..., Au kwa plants grafting and the likes...; au cheki hii research


Watu kuwa tofauti hakuyafanyi Kanuni za mapenzi kuwa Tofauti,
Mapenzi bila kujali Watu wapo tofauti yanahitaji, Kujali, kuthamini, kuvutiwa, kujitoa n.k. mapenzi yanaongozwa na Kanuni kinzani ya Wivu. Wanadamu wote wanawivu linapokuja suala la mapenzi licha ya kuwa Binadamu kuna baadhi ya ishu tunatofautiana.

Kuhusu hizo Kanuni za mapenzi, sasa itategemea na tamaduni husika jinsi ya kuzitekeleza.
Mfano, Mwanamke wa Kikurya ili ajue unamjali basi sharti umpige. Wakati Mwanamke wa jamii zingine ukimpiga atajua haumpendi.
Sasa wewe unajadili hiyo tofauti ya mchakato wa kujali badala kuangalia dhamira ya mchakato ni kuonyesha Kujali. Nafikiri wewe unajadili zaidi Reactions kuliko lengo au chanzo cha hiyo reaction.

Mfano mwingine, MTU anaweza akafumania Mkewe au mumewe lakini mmoja akaua na mwingine asiue. Lakini Wote Wataumia(Wivu) lakini reaction zao zitakuwa tofauti Kutokana na sababu zingine ambazo zipo katika vipengele vingine labda vya Afya ya Akili, vyakula MTU anavyopendekea Kula au unywaji ambavyo huathiri tezi na homoni zinazozalishwa mwilini.

Utofauti wa Watu hauvunji Kanuni au formula.
Ila unaweza kuathiri mchakato(reactions) wa kudhihirisha Kanuni au formula Fulani.

Kwa mfano, Ukichukua Watu Wawili ambao wanapenda Gari Aina ya V8 nyeusi kama wapendavyo au kama walivyochagua, ukawaletea Kwa pamoja, mmoja anaweza kushangilia huku akikukumbatia, mwingine anaweza akalia huku akiwa haamini. Wote wamefurahi lakini reactions ni tofauti.

Ukimfanyia MTU Jambo zuri na analolipenda lazima atafurahi. Lakini kwenye kuonyesha furaha ndipo Watu wanapishana, ndio hizo reactions unazozisema.

Ndio maana Sheria za nchi hutungwa Kwa kuangalia Kanuni za vitu mahususi na sio reactions za Watu Kutokana na utofauti wao.
Wataangalia zaidi intention, dhamiri kulingana na reactions MTU alizofanya.

Kwa mfano, Mtu ameua. Hapo watataka vithibitisho vya kuonyesha Fulani ameua, kisha wataangalia sababu ya yeye kuua, hapo ndio itakuja kaua bila kukusudia au kakusudia. Kote Huko wanaendeshwa na formula au Kanuni Fulani.

Chukua MKE au Mpenzi wa mtu uone nini kitatokea, jibu ni kuwa Wivu na maumivu ya mapenzi lazima yatokee, hiyo ni Kwa binadamu wote. Kuhusu reactions ndio huwa tofauti lakini Kanuni na formula ni Ileile.
 
MWANAMKE LAZIMA ABADILI DINI NA IMANI ILI IFANANE NA YAKO NDIPO UMUOE.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Moja ya ishara za awali Kwa Mwanamke anayekupenda na anayeweza kuwa Mkeo ni kukuamini, na kuamini Kwa kile ukifanyacho na kile unachokiamini. Kwa Mwanamke Hisia na Imani vinaenda sambamba. Mwanamke akishakuwa na hisia za upendo na wewe hapo moja Kwa moja atakuwa na Imani na wewe. Atakuamini. Kila unachomwambia Mwanamke anakiamini. Weka akilini hiyo.

Mwanamke akikupenda, atapenda unayoyapenda. Mtazamo wake utabadilika utakuwa Sawa na wako. Ndio maana ni rahisi kumbadilisha Mwanamke hata kama alikuwa ni kahaba lakini akishakupenda atauacha ukahaba wake. Ishu hapo ni hivi, Kwenye Moyo WA Mwanamke kuna Hisia na Imani. Wakati Sisi wanaume Imani Ipo kwenye Ubongo. Yaani hatuwezi kuamini Jambo bila kulitafakari Kutumia ubongo Akili.
Wakati Wanawake hawawezi kukuamini Jambo pasipo kuwa na hisia nalo, yaani kulipenda.

Sasa ili Mwanamke apende Jambo kuna michakato kadha wa kadha. Na yote lazima itimize imagination zake.

Ukiona umemtongoza Mwanamke mkaingia kwenye mahusiano alafu mpaka mnamaliza miezi sita hajataka Kubadili Imani na dini, jua huyo hujamkamata, yaani hujauteka moyo wake. Huyo hakufai. Hakuna mahali mtaenda.

Tena akikuambia wewe ndio umfuate ndio kabisa. Sisi Watibeli na wataalamu WA hayo mambo tunajua kuwa huyo Mwanamke Hakupendi, lakini pia atakupelekesha tuu.
Kingine ni lazima utashindwa kwenye ishu ya malezi. Yaani Watoto lazima wakushinde Kwa sababu tayari ulimshindwa Mama Yao.

Kubaniwa papuchi na kupewa chakula cha Usiku Kwa vipimo litakuwa ni Jambo la kawaida kwako na hautakuwa na chakufanya. Kiufupi utakuwa Dume-jike ambalo limeoa.

Asije akakudanganya MTU kuwa ndoa ya MKE na Mume WA Imani tofauti zinadumu au zinakuwa na Amani, hakuna kitu kama hicho.

Kingine cha muhimu zaidi ni kuwaz kamwe usimwambie Mwanamke abadili dini ili UMUOE. Hilo ni kosa la kiufundi. Mwanamke akishakupenda hatasubiri umwambie abadili Dini. Atabadili mwenyewe tuu Kwa mapenzi na uelewa wake kuhusu dini yako.

Kama hataki Kubadili dini yake Kwa hiyari jua huyo moyo wake haukupendi. Na kamwe hatakutii wala kukusikiliza Ila wewe ndiye utamtii na kumsikiliza. Atakupelekesha vile atakavyo.

Kesi nyingi za wanaowasiliana na Mimi nyingi zipo Kwa wanandoa ambao ni Aidha Mume alibadili dini na kufuata dini ya MKE. Au kila MTU alibaki na Dini yake wakafunga ndoa za bomani(serikalini).
Au mwanaume alitumia nguvu kumbadilisha Mwanamke Imani na Dini.

Elewa kuwa, kwenye mapenzi sio lazima uwe na MTU Fulani hasa kama hakupendi.
Elewa kuwa , mapenzi hayalazimishwi.
Elewa kuwa, kila mtu anauhuru wa Kutumia mwili wake. Hivyo usimpangie mkeo au mumeo matumizi ya mwili wake. Bali jipangie mwenyewe. Kama anakupenda basi ataji-commit kwako na sio wewe umlazimishe aji-commit kwako. Ila unaweza kujipangia kuwa huwezi ishi na Mwanamke au Mwanaume aliyeamua kuutumia mwili wake kufanya uasherati na uzinzi.
Hivyo katika mkataba wenu wa mahusiano ya ndoa, uwepo sheria iliyosainiwa au kukubaliana kuwa Kila MTU anauhuru wa Kutumia mwili wake atakavyo pasipo kuingiliwa na mwingine lakini Mimi(unaweza kuwa MKE au Mume) hutoweza kuishi na mtu mchafu (mzinzi na muasherati) hivyo Talaka itatoka ili kumpa MKE/mume Uhuru wa kuutumia mwili wake katika uchafu kadiri ya atakavyo.
Na hakutakuwa na Mijadala wala usuluhishi Kwa sababu ni Jambo lililojulikana mapema.

Hakutakuwa na hiyo nafasi ya kumshauri, kumfundisha mtu mzima aliyeko kwenye ndoa namna ya kuutumia mwili wake. Ila kila litakalofanyika litahesabika kama uamuzi wa Makusudi uliodhamiriwa na Mhusika.

Msamaha WA pekee utatolewa Baada ya Talaka kukabidhiwa. Kila MTU aishi Maisha yake lakini tukiwa tumesameheana. Hizo ni Kanuni za Watibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam

Robert Heriel
Kuna mahali Barnababoy amekukosea☺☺☺
 
Mimi ni Taikon Master.
Kutoka Nyota ya Tibeli.
Multi-talented, Gifted.
Psychology + Sociology hapa ndio nyumbani kwao Mkuu
Nakubali sana Mastaa😀..... Bila shaka A. K. A the Father Sigmund Freud Unampata sana mkuu tuendelee kushare madini ya ki-psychology binafsi huwa Naamini ni moja ya Fani nyeti sana duniani hii
 
Back
Top Bottom