Mwanamke mmoja Iran aamua kuwakera Ma-Ayatollah kwa kutembea na nguo zilizopigwa marufuku mtaani

Mwanamke mmoja Iran aamua kuwakera Ma-Ayatollah kwa kutembea na nguo zilizopigwa marufuku mtaani

sio kweli usitufanye na sisi hatujui kinachoendelea dunian. huyo ni mental stability issues ndio mana hujaona hata kama kapigwa. so bwana yoda una maanishq demoorqsia unayotaka wewe ni kutembea uchi.?
 
Kama alifanya kwa makusudi ili kuchallenge basi anastahili kuuwawa, kama alifanya baada ya kurukwa na akili alistahili kupelekwa hospital, maana mtu mwenye akili timamu hawezi kutembea uchi
Kwanini auwawe wakati alikuwa anaenda Beach kuogelea.
 
Binadamu akishachoka ni habari nyingine kabisa.
 
so bwana yoda una maanishq demoorqsia unayotaka wewe ni kutembea uchi.?
Sio ya kutembea uchi tu, ni ile hata ya wewe Juma ukitaka kuolewa na Juma mwenzako uolewe tu bila kusumbuliwa.
 
Huku kwetu bado tuko na legacy kubwa ya dini za majahazi na meli.
Hata bila dini ambazo hata mimi sizifagilii ila wewe na huyo mwanamke mna matatizo makubwa ya akili.
 
Wanaharakati wa haki za binadamu wameomba mamlaka nchini Iran kumwachilia binti aliyeko kizuizini baada ya kuvua nguo eneo la Chuo Kikuu mjini Tehran, katika kile walichosema ni kupinga sheria za lazima za kuvaa hijab.

Video ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii siku ya Jumamosi ikimuonesha binti huyo akiwa amevaa nguo za ndani na kuketi kwenye ngazi, kisha akaonekana akitembea eneo la chuo hicho cha Kiislamu cha Azad.

Hata hivyo, chuo hicho kimesema binti huyo alikuwa na matatizo ya akili na amepelekwa hospitali ya matatizo ya akili.
 
Mwanamke mmoja wa Irana aliyejulikana kama Ahou Daryaei amezua gumzo Teheran nchini Iran baada ya kutokelezea mtaani akiwa na nguo za beach kupinga ukandamizaji unaofanywa na polisi wa maadili wa nchi hiyo kulazimisha wanawake wavae Hijabu.
View attachment 3142875
Huyo mwanamke amethibitika ni mgonjwa wa akili lakini hata ivyo ameshikiliwa kwa utovu wake wa adabu
 
Amechoka na unyanyasaji uliopo huko. Ameamua liwalo na liwe.

Na utawala wa Iran ukijichanganya kumkamata katika kipindi hiki ambacho kuna fukuto kubwa la Mgogoro kati yake na Israel na Washirika wake, Basi utawala wa huko Iran ujiandae kuangushwa na kuondolewa madarakani. Israel na Marekani wanaweza wakamtumia huyo Mwanamke kama 'Scapegoat' au trigger ya kuweza kuwahamasisha raia wa Iran ili kuukataa utawala uliopo huko Iran, huyo Mwanamke ni kama 'chambo' ili utawala wa Iran 'uingie mkenge' endapo kama utaamua kumkamata na kumtia misukosuko huyo Mwanamke.
Pale wagalatia wanapopongezana
 
Back
Top Bottom