Mwanamke na mwanaume waliosimamishwa kwenye mkutano na Makonda siyo wanandoa na wala hakuna anayewafahamu. Walitokea wapi?

Mwanamke na mwanaume waliosimamishwa kwenye mkutano na Makonda siyo wanandoa na wala hakuna anayewafahamu. Walitokea wapi?

Yule mama aliyesema ametengana na mme wake na kwamba anakosa pesa ya kula imebainika ni bosheni ya mzee baba kutafuta kick.

Kwanza hawa wafu siyo wenyeji wa kanda ya ziwa, lakini pia yule mwanamke na mwanaume inasemekana walikuwa na usafiri wao kwenye mkutano ila mwanamke akawa anajidai hana pesa ya kula.

Lakini pia ukisikiliza ile clip na kumwangalia mwonekano wa yule mwanamke utabaini ni familia bora na lengo la ile move nikuvuta attention ya watu.

Kwa upande mwingine hata watoto wadogo wanapewa mic wanakuwa tayari wamepangwa. Michezo hii unajiuliza ina manufaa gani kwa Taifa? Tuendelee na sarakasi hizi zisizoleta umeme, maji wala kujenga barabara?

Lakini pia taarifa za msafara wake zinadai amekuja na mbinu baada ya kuona hakuna mwitikio kwenye mikutano ya pangani kuelekea Singida.

Je, kwa drama hizi kwanini mtu smart kama Bashe asikatae kupelekwa kama mzigo? Toka Bashe ameshtukia huu mchezo simu kwenda kwa Mawaziri unazisikia tena?

Nchi haiwezi kuendelea kwa drama......njo na sera za kuinua wanyonge siyo kugawa laki mbili sijui tano mara milioni. Dunia inahitaji brains zakupambana na Micro na Macro economy
Tuna kopi na kupesti kutoka hata kwa akina ze bulldozier🤣
 
Itoshe kusema tu ya kwamba wewe famba..punguani usiokuwa na mbele wala nyuma. Wewe unawajua wale watu? Wao wamesema wametengana..wewe unasema sio kweli..baasi tuambie unachojua huku jf.
Mwenezi kama mwenezi🤣😅
 
Kama watu wanapenda drama, wape wanachotaka ili uvune kukubalika, kura, endelea kula supu, nyama utazikuta chini post 2025!.
P

Ingekuwa hizo drama zinaleta kura, Magufuli alipora uchaguzi wa 2020 kwanini? Maana Magufuli alikuwa ni namba Moja kwa hizo drama.
 
Waliomteua ndio wana matatizo makubwa sana sana, anachokifanya Makonda ni usanii na ulaghai mkubwa, ni utoto na dharau kwa wanaokwenda kumsikiliza
Ni sawa na yule alie kuwa ana jidai kahongwa majogoo barabarani na yeye kumpa zawadi ya mama yake.
Na kuuziwa mahindi ya kuchoma na mtu mwenye bastola kiunoni.
 
Mmeshikwa pabaya na Mheshimiwa Makonda mpaka mmeanza kuweweseka kama wagonjwa .mapokezi makubwa anayuyapata na namna wananchi wanavyo miminika na kufurika kama maji kumewachanganyeni sana wapinzani na wenye chuki binafsi na Mheshimiwa, ambao mlikuwa mnasema anachukiwa na watanzania na hakuna atakaye kuwa anakwenda kwenye mikutano yake.sasa baada ya kuona maelefu kwa Malaki ya watu wanatiririka kukimbilia kumsikiliza Mheshimiwa Makonda mmeanza porojo na blaa blaa za uongo na uzushi.

Kaeni kwa kutulia maana ndio kwanza haya mwaka hajamaliza ofisini .maana yajayo yanafurahisha sana
Hivi mkuu wewe ndiye Etwege kwa Id tofauti? Maana naona ni kama una viasilia kama vyake
 
Unachotakiwa kujua ni kuwa katika Mikutano hiyo Watu hutoka maeneo tofauti ili kwenda kueleza kero zao au hata kusikiliza, kwa hiyo usitegemee kama utamjua kila mtu, kama kwenye Mtaa tu kuna wengine huwezi wajua sembuse kwenye Mkoa.

Kwa Mtu anayefuatilia au kwenda kwenye Mikutano hiyo hawezi kukubaliana na "Uthomaso"wako, hata kama Makonda anamapungufu yake lakini kwa anachokifanya sasa anasitahili pongezi..
Hivi watu wanaoacha shughuli zao na kwenda kumsikiliza Bashite, je wanakuwa ni watu kama wewe mkuu?
 
Hata kama watu hao ni wanandoa kimtazamo tu unawezagundua kuwa kale ka mchezo kalipangwa, hebu tazama baada ya yule mama kujieleza mume alipoitwa haraka akafika na kuanza kujitetea, that was a mission and locally orchestrated, yanataka kurudi yalee ya enzi hizo ni kweli Kuna watu wanashidq zao lakini Kuna drama zinaongezewa
 
Hivi watu wanaoacha shughuli zao na kwenda kumsikiliza Bashite, je wanakuwa ni watu kama wewe mkuu?
Mkuu! Watanzania tuna changamoto nyingi za kimaisha, pale Mtu anapohisi Mtu fulani anaweza kuwa mtatuzi wa changamoto zake ni lazima ataenda tu.
 
Namshauri makoñda awashirikishe akina Gabo, JB Ili kuficha uongo wa wazi hivi kweli kalia njaa ndo apewe milioni 5
 
Ni sawa na yule alie kuwa ana jidai kahongwa majogoo barabarani na yeye kumpa zawadi ya mama yake.
Na kuuziwa mahindi ya kuchoma na mtu mwenye bastola kiunoni.
Huu ni mpango mkakati ambao hautokuwa na tija yoyote kwa CCM kwenye sanduku la kura. Itawabidi watumie mbinu yao ya miaka yote ya wizi na uporaji wa kura na utangazwaji wa matokeo.
 
Mtu asiye na hela ya kula anaonekana hata kwa muonekano, je kwenye huo mikutano wa maigizo huyo mama muonekano wake ni wa kukosa chakula? Je ni kweli Bado Makonda anawapigia simu mawaziri au kero zimeisha? Je huko kigoma kero ya umeme imeisha Hadi Makonda aone kero kubwa iliyobaki ni ndoa ya huyo meneja wa Tanesco?
Hivi kazi ya Katibu Uenezi wa Chama ni zipi labda nisaidie.
Ninavyofahamu kesi za ndoa zinatatuliwa Ustawi wa Jamii.
 
No hizi sio kama zile za tunza za mashosti na mashostito wao kwenye kitchen parties!, hizi ni fedha za kweli zikitoka zimetoka.
P
Kwahiyo viongozi wa CCM wanagawa pesa mabarabarani bila jasho! Hizo pesa ni zake binafsi au za CCM! Huko CCM wanampa pesa za kunigawia mimi nikilia mkutanoni! Unataka kuniaminisha Makonda na CCM wanagawa pesa kwa watu bila watu hao kufanyakazi zaidi ya kulia mikutanoni! Kama hivyo na mimi nitatafuta vijana wa kukimbizana naye mikoani tupate maokoto ya chee, ila ukweli ni siasa za majukwaani ni sawa na filamu za Charie Chaplin.
 
Na hizo drama zipo mpaka huku jf kwenye threads zinazomuhusu makonda,kuna ma agents huku kazi yao ni kuikuza legacy yake na pasipo shaka wanalipwa,huenda anajiandaa kwa 2030
 
Back
Top Bottom