mshamba_hachekwi
JF-Expert Member
- Mar 3, 2023
- 20,704
- 66,337
Mwanamke huyu hapa (anaitwa Alvera) amesema anajuta sana kuwakataa wanaume wote waliotaka kumuoa akiwa kijana, sasa ana miaka 56, hawezi tena kuolewa na amekuwa mpweke sana.
Amedai kwamba alikua akiogopa atabebeshwa mimba na kuachwa, lakini sasa amepata matatizo ya kiafya, na amekuwa mlemavu, anatamani angekua na familia ya kumfariji.
Kuna mwanaume mmoja aliyetaka kumuoa kipindi cha nyuma, Alvera amesema sasa yuko tayari amlipe pesa ili mradi tu akubali kumuoa.
Kwa kuwa sasa anapendezwa na wanaume, wanaendelea kumwambia kwamba wakati wake umepita na kwamba wanataka wanawake wachanga na wenye uwezo wa kuolewa. Anaishi mwenyewe kabisa kwa sasa, na kampani aliyonayo ni redio yake ya analogi.
Majuto ni mjukuu.
Amedai kwamba alikua akiogopa atabebeshwa mimba na kuachwa, lakini sasa amepata matatizo ya kiafya, na amekuwa mlemavu, anatamani angekua na familia ya kumfariji.
Kuna mwanaume mmoja aliyetaka kumuoa kipindi cha nyuma, Alvera amesema sasa yuko tayari amlipe pesa ili mradi tu akubali kumuoa.
Kwa kuwa sasa anapendezwa na wanaume, wanaendelea kumwambia kwamba wakati wake umepita na kwamba wanataka wanawake wachanga na wenye uwezo wa kuolewa. Anaishi mwenyewe kabisa kwa sasa, na kampani aliyonayo ni redio yake ya analogi.
Majuto ni mjukuu.