Mwanangu wa darasa la pili hili swali kakosaje? Au mwalimu ndiye hajielewi?

Yunifomu? Duh
Mwalimu Kaneli aliniandikia vile. Unajua matatizo sio ya walimu ni ya hizi taasisi za Kiswahili zinarahisisha mambo na kuzembea kwenye kukuza lugha. Zinapotosha, unakuta kamusi za siku hizi neno helicopter wanaita "helikopta" eti ndio wametafsiri. Ukichukua TUKI za miaka ya sabini kuna maneno ya ndani kabisa.

Tunatakiwa kuwa na maneno mapya kama chakachua, piga tafu, tarakirishi, sharubati. Sio maneno kama internet ~ intaneti.
 
Oohh
 
Alama ya kosa anaweka kidogooooo....hata hakaonekani vizuri...sijui ndo kubania wino!!!
 
Mwanao yupo sahihi mwalimu ndio kajichanganya, mwalimu alipaswa kuuliza mchezeshaji wa mpira wa miguu anaitwa nani? Ili jibu liwe "mwamuzi"kwa kiswahili. Refarii ni lugha ya kiingereza tunayoitumi kimazoea, ni sawa na mtu anaposema naenda sheli kununua mafuta wakati kituo anachokwenda ni Total au Agip.
 
Jamani Jf ishakuwa dampo kila kitu hapa !!!
 
Jibu ni REFA

Neno mwamuzi limetumika kuuliza swali, kwahiyo huwez kulitumia kujibu swali. Mfundishe mwanao hii kitu isije kumuathiri huko mbele.
tatizo jibu la mwalimu halipo kwenye lugha aliyoitumia kuulizia swali. Tukubaliane tu kwamba Mwalimu alijichanganya kwenye kuunda swali.
 
La pili! Basi kijana wako yupo vizuri, lakini jibu hilo ni kweli kakosea.

Haiwezekani 'structure' ya swali ikatumika kuwa ndiyo jibu la swali hilo hilo....'Mwamuzi' wa michezo halafu jibu liwe 'mwamuzi' hiyo hiyo.
Maswali ya chemsha bongo ndivyo yalivyo.
 
Ulipaswa umuulize mwalimu.

Hata hivyo watoto wadogo huwa wanafundishwa kujibu kile tu alichofundishwa na mwalimu darsani na sio nje ya hapo, kuna vingine vipo kutokana na hadithi au simulizi mbalimbali walizosoma darasani kwenye vutabu vyao(misamiati) so hawatakiwi kujibu tofauti. Anapokwenda level nyingine ndio ubongo unatanuka na kujua namna ya kujibu maswali kwa namna tofautitofauti ambayo huelekea kwenye jibu sahihi.
 
Jibu ni REFA

Neno mwamuzi limetumika kuuliza swali, kwahiyo huwez kulitumia kujibu swali. Mfundishe mwanao hii kitu isije kumuathiri huko mbele.

Refa ni pronunciation na kifupisho cha Neno Referee, Jibu hapo Ni Mwamuzi , dogo alikuwa Sahihi, hakuna neno la kiswahili “Refa” kwenye kamusi
 
Kww hiyo mtoto alikuwa sahihi kabisa. Maana kama mwalimu akisema jibu ni Refarii, hicho siyo kiswahili.

Huyo mtoto yuko sahihi kabisa, Referee ni english, lakini ukiingia google translate inakuletea pia kwa kiswahili "REFARII" yakiwemo na maneno mengine (MWAMUZI na MSULUHISHI) hapa ndio nimegundua REFARII pia ni kiswahili 😄
 
VAR ni aid kwenye maamuzi haitoi maamuzi
 
Mwalimu yuko sahihi kabisa. Mwanao kakosea hapo.
Ila mpe pongezi, yuko vizuri kwa kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…