Mwanza: Mmiliki wa mabasi ya J4 aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa aachiwa huru

Afrika jela ni kwa ajili ya watu masikini, ukiona tajiri jela jua kaingia cha kike. Ukitaka kesi yako iende haraka haraka na upate hukumu poa hakikisha upo vizuri mfukoni.
Mambo ya ajabu sana, Yaaan Bora wakoloni, walotuonea tukijua kabisa, ni wakoloni.

Hiii mijitu inayotanguliza matumbo ni ya ajabu sana sana

Ndioo Sababu unakuta Lina mwaka Mmoja TU kazin, tayari limeshajilimbikizia mali nyingi .


Rushwa , Rushwa Rushwa
 
Unajua scenario mpaka akaua hao watu?
Marehemu walimuuzia mzigo wenye carat/quality ndogo wa dhahabu, wakalipwa %, fedha nyingine zikabaki, jamqa kuupeleka sokoni, ndio anagundua tayari ameshawalipa jamaa ela nyingi.

Jamaa nao wanaendelea kumdai, yeye hataki walipa tena fedha iliyobaki maana mzigo quality ilikuwa ndogo. Majibizano ndio hadi kuwaua.
 
Asante haya ndo majibu
 
Boss usiilaumu mahakama kumbuka mahakama inafata ushahidi na utetezi na mwenendo wa kesi kama mwendesha mashtaka akishindwa kuithibitishia mahakama au vifungu vya sheria visipofatwa MTU anatoka tu
Mkuu, ukiua umeua, ukiua ikathibitika umeua, umeua tuu

Ndioo Sababu Hayati Magufuli Kuna wakati alikua mkali sana.


Mtu alishahukumiwa KUNYONGWA, wamekuja kusubiri JPM amekufa, ndo wakaamua kurudi kwenye rufaaa, na ujanaujanja na Rushwa Rushwa kibao ,Leo ameachiwa huru..

Nini Hatima ya Waliouliwa???,
 
Nimekuuliza sio ugomvi !! Wangapi wanaachiwa ? Kuna mengi mzee na kuwekwa jela kwa mda ni kama sheria hata ukiua jambazi unaweza kushikiliwa kwa mda then ndo unaachiwa.

Fuatilia sana izo mambo wengine majambazi.
Majambazi wanatoa pesa wanatoka thus awakomi kuiba,sema tu siku hizi wamekeshwa na teknologia watu awakai na pesa wala kupokea cash,ni online tu.
 
Ki ukweli hili linaskitisha sana na linavunja moto sana

Shida ya hii nchi rushwa iko kila.mahali especially mahakamani .ovyo sana

Bi tozo wala hana habari yupo kwenye hoteli za nyota 5 huko na msururu wa watu kibao huko .

Any way muosha huoshwa

Damu ya mtuu haimwachi mtu salama

Mwenye kutoa hukumu ya haki ni Munguu

Tusubiri tuu mda si mrefu
 
Ukali wake ndio ulikuwa unaingilia majukumu ya mihimili mingine.

Kila muhimili unapaswa kuwa huru usiingiliwe na mwingine.
 
Mtindo wako wa uandishi unafanya jambo la maana kabisa unalotaka kulielezea lipungue nguvu. Je unaweza kuandika kwa mtiririko mzuri ni nini hasa kilitokea na ameachiwa kwenye mazingira gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…