Mwanza: Mmiliki wa mabasi ya J4 aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa aachiwa huru

Mwanza: Mmiliki wa mabasi ya J4 aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa aachiwa huru

Mbaya nimekumbuka kumbe hukumu ilishapita kabisa 🙄🙄then kaachiwa .
Huyo bwana baada ya mauaji, alihukumiwaga KUNYONGWA Hadi KUFA.

Amekaa Jela wee, mwaka Jana ndo wakaanza habari za Rufaaa zikiingozwa na Kibatala !!.

Leo jamhuri imesema Haina Nia ya kesi, Mahakama imemuachia huru .

Wakati wanatoka tu, Polisi wakawamkata Tena.
 
Nyie Mahakama acheni kuona watu ni mbuzi, Acheni Rushwa, Rushwa ni adui wa haki, Rushwa anatesa, Rushwa anaumiza watu

Hivi mtu aliyeua watu wawili kwa risasi , watu wamekufa, wamezikwa , na mmemhukumu kunyongwa hadi kufa, leo hiii kisa rufaa, kwamba meza imepinduka? Mpaka aachiwe huru?

Mbona mnakoswa huruma nyinyi?? Mbona hamuwakumbuki watu walowapoteza wapendwa wao? Tunarudi wapi?

Huu ndo utawala wa Rais Samia, wenye kufuata misingi ya Demokrasia?

Haya basi, jamhuri haina nia ya kuendelea na kesi, mtufufulie ndugu zetu walouawa basi, na sisi tucheze nao, tupige nao stori, likiwashinda hilo, basi tuambiani, walowaua ndugu zetu wawili kwa risasi ni akina nani?.

Mambo ya ajabu kabisa na aibu ilopitiliza.

Mnatanguliza rushwa mpaka kwenye maisha ya watu, kama mlimuhukumu kunyongwa, leo hii inakuaje mnakoswa nia ya kuendelea na kesi? Kwamba hakukutokea tukio la mauaji? Kwamba hamna aliyekufa? Na kama alikufa nani alimuua?? Kama sio Jumanne, ni nani aliwaua?? Kama ni yeye, imekuaje aachiwe huru? Mtufufulie ndugu zetu .


Shame on you!! Rushwa rushwa mpaka mnauza roho za watu??


Wapumbavu kabisa , mlaaniwe na vizazi vyenu, na hizo rushwa mnazokula, pesa hizo ziendelee kuwapa umasikini wa roho na mpoteze heshima mbele ya watu .


Huyu jamaa alihukumiwa hapa !![emoji116]


Leo kaachiwa Huru, ila Polisi wamejifanya kumkamata Tena, ili kupima upepo, ili hali JAMHURI ndio hiyo hiyo Polisi !!
PUNGUZA UPEPO
HIZI NI ZAMA NYINGINE.

Alihukumiwa kwenye utawala gani?
Unatambua mazingira ya kosa lake?
Unatambua maisha ya wafanyabiashara wa level zake yalikuwaje wakati huo?
Manji UNAMKUMBUKA?
Mo unamkumbua?
Super shem yuko wapi?

Maisha hayako ivo rafiki yangu.
 
Huyo bwana baada ya mauaji, alihukumiwaga KUNYONGWA Hadi KUFA.

Amekaa Jela wee, mwaka Jana ndo wakaanza habari za Rufaaa zikiingozwa na Kibatala !!.

Leo jamhuri imesema Haina Nia ya kesi, Mahakama imemuachia huru .

Wakati wanatoka tu, Polisi wakawamkata Tena.
Watakuja wale jamaa sijui wakili msomi na yeye anaangalia pesa tu.
 
Ndugu yangu,kuna issue nilikuwa napigania...pesa zimenitoka kweli
Majuzi Kati nilikua Kuna Vijana wapatao wanne nmewafikisha Mahakamani


Huwezi amini, Hakimu wa Kesi hiyo, akawa anawapigia simu watuhumiwa anawaambiaje" Huyu Dr kesi yake nyuma yake inawatu wazitk, mkicheza mtapoteaa , Sasa tuongee kiutu uzima".


Fikiria huyo ni Hakimu aliyetakuwa kusimamia haki, ila anataka watuhumiwa, wampe Hela !!.
 
Alafu jamaa analeta habari za scenarios hapaa.

Watu wanahukumiwa kunyongwa kisa wamechoma mwizi mtaani aloiba Kuku akawapikie wanawe.

Alafu aliyeua watu Kwa makusudi anaachiwa??


Aibu aibu aibu ..

ANGEKUWEPO HAYATI MAGUFULI, HUU UJINGA USINGETOKEA KAMWE.
Sure thing, chini ya Magu haya maujinga yasingetokea. Aisee nimechefukwa sana
 
Mtu alishahukumiwa KUNYONGWA, wamekuja kusubiri JPM amekufa, ndo wakaamua kurudi kwenye rufaaa, na ujanaujanja na Rushwa Rushwa kibao ,Leo ameachiwa huru..
BADO SIJAELEWA

Mshtakiwa - at this point muuaji, msubiri kunyongwa, condemned, KONDEM - kakata rufaa.

Ina maana kesi anaeileta mahakamani ni KONDEM

Serikali itasemaje haina nia ya kuendelea na kesi, wakati kesi kaianzisha KONDEM ????
 
Wewe ni bure kabisa. Siyo kila kuua kunafanya mtu anyongwe au hata afungwe. Kuna watu wanaua na kuiachiwa, tena wengi tu. Inategemea na mazingira yaliyofanya waue. Kosa lako kubwa wewe unalaani bila kuonyesha marehemu waliuawa kwenye mazingira gani na ni kwa nini. Inawezekana kweli kuwa kuna rushwa imetumika lakini uandishi wako na uking'ang'anizi wako wa kusema kuua ni kuua tu bila kujali mazingira ndiyo kunakuangusha.
Inawezekana hii kesi inamuhusu sana, kwa hiyo hawezi kuwa objective.

Anaandika kwa hisia kali na mihemuko.
 
Majuzi Kati nilikua Kuna Vijana wapatao wanne nmewafikisha Mahakamani


Huwezi amini, Hakimu wa Kesi hiyo, akawa anawapigia simu watuhumiwa anawaambiaje" Huyu Dr kesi yake nyuma yake inawatu wazitk, mkicheza mtapoteaa , Sasa tuongee kiutu uzima".


Fikiria huyo ni Hakimu aliyetakuwa kusimamia haki, ila anataka watuhumiwa, wampe Hela !!.
Tena rushwa ni wazwaz
 
Sasa kama imeamuliwa kuwa kesi ianze kusikilizwa upya kutokana na kasoro zilizo onekana tatizo liko wapi? hakuna cha rushwa wala harufu ya rushwa.

ila kama hakuwa na hatia basi ni bora angeachiwa tu huru, kwa nini ateseke tena kuanza kusikiliza kesi upya kwa uzembe wa upande mwengine?!
 
Huyo bwana baada ya mauaji, alihukumiwaga KUNYONGWA Hadi KUFA.

Amekaa Jela wee, mwaka Jana ndo wakaanza habari za Rufaaa zikiingozwa na Kibatala !!.

Leo jamhuri imesema Haina Nia ya kesi, Mahakama imemuachia huru .

Wakati wanatoka tu, Polisi wakawamkata Tena.
Kama alishahukumiwa basi inamaanisha kesi ilishaisha. Na kama kesi ilishaisha basi mwendesha mashtaka hawezi kusema tena ''hana nia ya kuendelea na kesi''. Inaonekana alikata rufaa na akashinda lakini siyo kweli kuwa mwendesha mashtaka amesema hana nia ya kuendelea na mshtaka.
 
Ingekuwa ni ndugu yangu ameuawa na huyo bwana ningelipa kisasi hadharani kwa risasi za kichwa alafu nisubiri kesi yangu itakavyokuwa
Ningeiomba mahakama itumie kigezo ilichotumia kumwachia huyo bwana watumie hicho hicho kuniachia mimi
Na kama kuna ndugu yake ambaye atakuwa na roho kama yangu aje kufanya nilichofanya kwa ndugu yao na iende hivyo mpaka dunia iishe kama wanaona walichofanya ni sahihi sana
 
Back
Top Bottom