Mwanza: Mmiliki wa mabasi ya J4 aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa aachiwa huru

Mwanza: Mmiliki wa mabasi ya J4 aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa aachiwa huru

Kwa spidi hii ya bwana DPP tegemea yule Mende wa gesi ya mkopo kurudi uraiani January mwakani.

Hivi rushwa wanapokea pesa taslim au benki transfer?
Hizi Rushwa ni sawa na intercontinental ballistic missiles.

Ni za Benki
 
Ingekuwa ni ndugu yangu ameuawa na huyo bwana ningelipa kisasi hadharani kwa risasi za kichwa alafu nisubiri kesi yangu itakavyokuwa
Ningeiomba mahakama itumie kigezo ilichotumia kumwachia huyo bwana watumie hicho hicho kuniachia mimi
Na kama kuna ndugu yake ambaye atakuwa na roho kama yangu aje kufanya nilichofanya kwa ndugu yao na iende hivyo mpaka dunia iishe kama wanaona walichofanya ni sahihi sana
Unaongea tu
 
Muuaji mwingine ni dikteta Putin[emoji16]
Acha ujinga wako, haijalishi nyuma ya mauaji Kuna sababu zipi.

Kuua ni kuua tu .... Kwahiyo siku hizi, mtu akikutendea baya, ni Kuua tu, kwakua nyuma yake una sababu?.
 
Aachiwe tu, hao wanafamilia wachukue kampunga, maisha yaendelee, mtu kaajiri mamia ya watu akae jela kufanya nini? Mtaani yamejaa majitu kama Mdude yanajaza nafasi tu
Mfanyabiashara na Mkurugenzi wa kampuni ya Mabasi ya J4 Express, alidaiwa kuwaua kwa kuwapiga kwa risasi Ally Abeid Mohamed, mkazi wa Igoma na Claud Sikarwanda, mkazi wa Nyasaka Ilemela, Julai 13, 2015, majira ya saa 4:00 usiku, eneo la Nyakato Boma kwenye ofisi na karakana ya magari ya mfanyabiashara huyo.

J4 alitiwa hatiani na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya kukusudia ya Ali Abeid na Claude Sikarwanda, hukumu iliyotolewa Machi 13, 2020 na Jaji Mfawidhi wa Makahama Kuu Mwanza, Sam Rumanyika.

Hata hivyo Mahakama ya Rufaa ilibatilisha adhabu hiyo na kutengua hukumu ya Mahakama Kuu Mwanza,iliagiza kesi hiyo jinai namba 131/2017 isikilizwe upya.

Mahakama imemwachia huru leo, baada ya DPP kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo. Upande wa utetezi mtuhumiwa alitetewa na Wakili Msomi Peter Kibatala.

------


Nyie Mahakama acheni kuona watu ni mbuzi, Acheni Rushwa, Rushwa ni adui wa haki, Rushwa anatesa, Rushwa anaumiza watu

Hivi mtu aliyeua watu wawili kwa risasi , watu wamekufa, wamezikwa , na mmemhukumu kunyongwa hadi kufa, leo hiii kisa rufaa, kwamba meza imepinduka? Mpaka aachiwe huru?

Mbona mnakoswa huruma nyinyi?? Mbona hamuwakumbuki watu walowapoteza wapendwa wao? Tunarudi wapi?

Huu ndo utawala wa Rais Samia, wenye kufuata misingi ya Demokrasia?

Haya basi, jamhuri haina nia ya kuendelea na kesi, mtufufulie ndugu zetu walouawa basi, na sisi tucheze nao, tupige nao stori, likiwashinda hilo, basi tuambiani, walowaua ndugu zetu wawili kwa risasi ni akina nani?.

Mambo ya ajabu kabisa na aibu ilopitiliza.

Mnatanguliza rushwa mpaka kwenye maisha ya watu, kama mlimuhukumu kunyongwa, leo hii inakuaje mnakoswa nia ya kuendelea na kesi? Kwamba hakukutokea tukio la mauaji? Kwamba hamna aliyekufa? Na kama alikufa nani alimuua?? Kama sio Jumanne, ni nani aliwaua?? Kama ni yeye, imekuaje aachiwe huru? Mtufufulie ndugu zetu .


Shame on you!! Rushwa rushwa mpaka mnauza roho za watu??


Wapumbavu kabisa , mlaaniwe na vizazi vyenu, na hizo rushwa mnazokula, pesa hizo ziendelee kuwapa umasikini wa roho na mpoteze heshima mbele ya watu .


Huyu jamaa alihukumiwa hapa !!👇


Leo kaachiwa Huru, ila Polisi wamejifanya kumkamata Tena, ili kupima upepo, ili hali JAMHURI ndio hiyo hiyo Polisi !!
 
Aachiwe tu, hao wanafamilia wachukue kampunga, maisha yaendelee, mtu kaajiri mamia ya watu akae jela kufanya nini? Mtaani yamejaa majitu kama Mdude yanajaza nafasi tu
Akili za UVCCM hizi.
 
Nimekuuliza sio ugomvi !! Wangapi wanaachiwa ? Kuna mengi mzee na kuwekwa jela kwa mda ni kama sheria hata ukiua jambazi unaweza kushikiliwa kwa muda then ndo unaachiwa.

Fuatilia sana hizo mambo wengine majambazi.
Bush lawyer advise.. tikiti maji
 
We mwalimu usitake udharaurike bure.

Mahakamani ni ushahidi usio na mashaka, ukikosea Mahakama ya Rufaa inamuachia mtu
Sijaelewa katika habari ya mtoa hoja, ameachiliwa na mahakama ya rufaa au Dpp kaondoa shauri hilo mahakamani?
 
Mfanyabiashara na Mkurugenzi wa kampuni ya Mabasi ya J4 Express, alidaiwa kuwaua kwa kuwapiga kwa risasi Ally Abeid Mohamed, mkazi wa Igoma na Claud Sikarwanda, mkazi wa Nyasaka Ilemela, Julai 13, 2015, majira ya saa 4:00 usiku, eneo la Nyakato Boma kwenye ofisi na karakana ya magari ya mfanyabiashara huyo.

J4 alitiwa hatiani na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya kukusudia ya Ali Abeid na Claude Sikarwanda, hukumu iliyotolewa Machi 13, 2020 na Jaji Mfawidhi wa Makahama Kuu Mwanza, Sam Rumanyika.

Hata hivyo Mahakama ya Rufaa ilibatilisha adhabu hiyo na kutengua hukumu ya Mahakama Kuu Mwanza,iliagiza kesi hiyo jinai namba 131/2017 isikilizwe upya.

Mahakama imemwachia huru leo, baada ya DPP kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo. Upande wa utetezi mtuhumiwa alitetewa na Wakili Msomi Peter Kibatala.

------


Nyie Mahakama acheni kuona watu ni mbuzi, Acheni Rushwa, Rushwa ni adui wa haki, Rushwa anatesa, Rushwa anaumiza watu

Hivi mtu aliyeua watu wawili kwa risasi , watu wamekufa, wamezikwa , na mmemhukumu kunyongwa hadi kufa, leo hiii kisa rufaa, kwamba meza imepinduka? Mpaka aachiwe huru?

Mbona mnakoswa huruma nyinyi?? Mbona hamuwakumbuki watu walowapoteza wapendwa wao? Tunarudi wapi?

Huu ndo utawala wa Rais Samia, wenye kufuata misingi ya Demokrasia?

Haya basi, jamhuri haina nia ya kuendelea na kesi, mtufufulie ndugu zetu walouawa basi, na sisi tucheze nao, tupige nao stori, likiwashinda hilo, basi tuambiani, walowaua ndugu zetu wawili kwa risasi ni akina nani?.

Mambo ya ajabu kabisa na aibu ilopitiliza.

Mnatanguliza rushwa mpaka kwenye maisha ya watu, kama mlimuhukumu kunyongwa, leo hii inakuaje mnakoswa nia ya kuendelea na kesi? Kwamba hakukutokea tukio la mauaji? Kwamba hamna aliyekufa? Na kama alikufa nani alimuua?? Kama sio Jumanne, ni nani aliwaua?? Kama ni yeye, imekuaje aachiwe huru? Mtufufulie ndugu zetu .


Shame on you!! Rushwa rushwa mpaka mnauza roho za watu??


Wapumbavu kabisa , mlaaniwe na vizazi vyenu, na hizo rushwa mnazokula, pesa hizo ziendelee kuwapa umasikini wa roho na mpoteze heshima mbele ya watu .


Huyu jamaa alihukumiwa hapa !!👇


Leo kaachiwa Huru, ila Polisi wamejifanya kumkamata Tena, ili kupima upepo, ili hali JAMHURI ndio hiyo hiyo Polisi !!

Inatia hasira uchungu ila mwisho wa Siku Mungu mwema mwisho wao utakuwa mbaya sana kama si wao watoto wao
 
Wekeni hukumu hapa tuone ni mazingira gani jamaa kachomoa pini. Inatokea kabisa mzee mmoja aliachiwa huru baada ya kumchapa shaba askari polisi aliekuja mkamata usiku nyumbani kwake amelala na mke wake. Mzee akawaambia polisi wasithubutu kugusa geti, jamaa wakazama ndani kibabe. Akawachapa risasi mmoja akakata moto pale pale.
Mzee alikomaa kwamba hawakuwa polisi ila majambazi,jamhuri inakazania ni polisi,mzee alipigwa kifungo cha maisha badae akachomoa pini huko huko kwa pilato kwa rufaa. Japo mzee alijua kweli ni askari ila akaamua kuwachapa shaba kibabe!
 
Upande wa utetezi mtuhumiwa alitetewa na Wakili Msomi Peter Kibatala.

Kuna watu huwa wanabeza uwezo wa Kibatala kuwa hashindi kesi huyu jamaa ni moto
Kibatala ni Wakili wa Mchongo,anajua kupenyeza rupia Mahakamani,Kama huna pesa hawezi shinda kesi yako!!
 
Back
Top Bottom