Mwanza: Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mbowe na wenzake wanyakuliwa na Polisi usiku wa manane, haijulikani wako kituo gani

Mwanza: Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mbowe na wenzake wanyakuliwa na Polisi usiku wa manane, haijulikani wako kituo gani

View attachment 1861764

View attachment 1861765
View attachment 1861766

Usiku majira ya saa tisa, Polisi walivamia Hoteli aliyokuwa amefikia Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na wageni wengine pamoja na wenyeji wao.

Waliochukuliwa:
1. Freeman Mbowe
2. John Pambalu
3. John Heche
4. Rose Mayemba
5. Masenya(Mwenyekiti BAVICHA Ilemela)
6. Steven Odipo
7. Dr. Rwaitama
8. Seti (Dereva kanda ya Victoria)
9. Apollo (Afisa Habari Taifa)
10. Frank Novatus (CHASO)
11. Mwakiaba (Mwenyekiti Nyamagana)
12. Benja (BAVICHA Kinondoni)

Mpaka sasa haijajulikana wamechukuliwa kwa kosa gani.

=====

My Take.
Uonevu, uvunjifu wa haki za kiraia, kutoheshimu katiba ya nchi unaendelea kwa kasi katika serikali ya Samia Suluhu Hassan.
Anyway, Aluta continua, uonevu huu utaisha oneday, dawa tutaipata tu.

Nimkumbusha Samia kuwa alikuwepo mtu katika nchi hii anaitwa Magufuli, tulimuita Chuma, Jiwe—Leo yuko wapi?

====

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)

Taarifa Kwa UMMA

Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe..Freeman Mbowe alivamiwa na Jeshi la Polisi hotelini alipokuwa ( Kingdom Hotel) majira ya saa nane na nusu usiku na kumkamata pamoja na viongozi wengine waliokuwa naye.

Viongozi wengine walipelekwa Kituo cha Kati cha Polisi Mwanza,Ila Mwenyekiti Mbowe haijulikani alipelekwa wapi na mpaka Muda huu hakuna taarifa zozote za mahali alipo.
Waliokamatwa ni wafuatao;

1. Mhe .Freeman Mbow
2. Mhe.John Pambalu
3. Mhe. John Heche
4.Mhe. Rose mayemba
5. Masenya( Mwenyekiti Bavicha ilemela)
6. Steven Odipo
7.Dr. Azavel Lwaitama
8. Seti ( Dereva Kanda ya Victoria)
9. Apolinary Appolo (Afisa habari Taifa)
10. Frank Novatus (Chaso Mwanza)
11. Mwakiaba (Mwenyekiti Nyamagana)
12. Benjamin Kambarage ( M.kiti Bavicha kinondoni)

Tunalitaka Jeshi la Polisi kujitokeza na kusema alipo Mwenyekiti wa Taifa na sababu za kumkamata zilikuwa nini.

Tunalaani ukandamizaji huu wa Haki za Watanzania Kwa nguvu zote , na hizi NI dalili za wazi kuwa Udikteta uliokuwepo enzi za utawala wa Rais Magufuli bado unaendelea .

Tutatoa taarifa kadiri ya Muda na jinsi tutakavyozipokea .

====

UPDATES:

=====

Jeshi la polisi mkoani Mwanza limefunga barabara ya Bwiru maarufu kona ya Bwiru jirani na ukumbi uliopangwa kufanyia kongamano la Chadema la kudai Katiba, hakuna kinachoendelea kwa sasa polisi wametanda barabara nzima wakiwa na magari na silaha za moto
Msipende kukuza vitu, mbona hawa watuhumiwa walikuja kwangu na tukanywa chai wote kabla ya kupewa vichapo?
 
Mdude mdomo wake mchafu umefanya watawala wakaanza kuwa madikteta tena

Hali ya uhuru ilikua isharudi vizuri tu yule mdude akamtukana na kumkejeli mama,

Mama ashakasirika ameamua kuwabadilikia

Asante sana mdude mdomo wako umetufanya turudi zama za mwendazake za kuonewa.
 
Acheni kuipa katiba majukumu yasiyo yake Africa shida sio katiba ila ni umaskini uliokithiri mno, mbona nchi yetu Ina sera nzuri na Bado hazitekelezeki pia, hata katiba hii tunaona magufuli alikuwa ana vunja katiba waziwazi na hakuna aliyekuwa ana mwambia lolote. Tanzania needs more than constitutional kututoa kwenye huu umaskini wetu, mbona south Wana katiba nzuri kweli wamebaki kuandamana na kuiba plus uhalifu na weusi umaskini wao umebaki palepale
Unafikiri majukumu au umuhimu wa katiba ni nini hasa?

Sera ni kauli za ujumla zinahitaji commitment na rasilimali kutekelezeka. Kama hakuna namna ya kuwabana wahusika serikalini mtaendelea kupigwa blabla wakati rasilimali wanazielekeza kwingine kwenye maslahi yao hasa.

Bila shaka unajua duniani kote hasa kwenye nchi zenye kuzingatia demokrasia, viongozi wakuu kuanzia Rais huapishwa kulinda katiba kabla hawajakabidhiwa madaraka na wakikiuka vipengele vya katiba hufunguliwa mashtaka hata kuondolewa ofisini kwa njia mbalimbali kwa mujibu wa katiba zao.

Uko sahihi kabisa, Magufuli alikuwa akivunja katiba waziwazi na hakukuwa na mwenye ubavu wa kumuuliza kitu kwa sababu kwa mujibu wa katiba tuliyo nayo amri ya Rais haihojiwi; inatekelezwa tu - ana absolute power. Ukienda kinyume na matakwa yake anaweza kukuchukulia hatua yoyote hata kinyume cha sheria na asiulizwe. Hilo ndilo tatizo kubwa sana la kujadiliwa.

Kwa katiba ya Afrika ya Kusini, Rais mstaafu Zuma yuko jela kwa mujibu wa sheria na bado anakabiliwa na kesi nzito ya ufisadi. Wafuasi wake walioandamana na kuiba wamedhibitiwa na vyombo vya dola na wengi wako ndani wanasubiri hatua za kisheria. Chama tawala cha ANC kinahaha jinsi ya kushughulikia umasikini wa weusi wengi na ufisadi wa viongozi wao serikalini.

Kinahojiwa waziwazi na vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi. Hiyo ndiyo katiba makini. Ya Tanzania kila kitu kiko chini ya Rais na kinategemea utashi, fadhila na huruma yake. Vyombo vya habari vinaelekezwa na Ikulu mambo ya kutangazwa na yasiyotakiwa. Rais asipokuwa mtu wa maana nchi inaenda mrama na hakuna wa kumfanya kitu.
 
YAERCTR.jpg
 
Ni kosa kukusanyika na kufanya makongamano ya Chadema,Huko Mwanza na kwingineko walikamatwa watu wengi kwa kuvunja sheria.

Mahakama ndio chombo cha kutafsiri sheria,Je ni lini watu hawa wasioitakia nchi yetu iwe na Amani watafikishwa Mahakamani?

Nguvu ikitumika kubwa vivyo hivo na haki itendeke.
 
Back
Top Bottom