Katika hali isiyo ya kawaida Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela amesitisha kufunguliwa kwa shule zote hapo kesho ili waalimu na wanafunzi washiriki kampeni za chama Cha CCM.
Hali hiyo imesababishwa na chama hicho kukosa ushawishi wa watu kuhudhuria mikutano yake bila kulazimishwa na hali imejionyesha pamoja na kutumia wasanii haijasaidia kitu.
Mgombea wa Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu aliingia Mwanza kwa kishindo kikubwa wiki iliyopita na kuvuta umati wa watu ambao wachunguzi wa mambo wanasema huenda ukawa umati mkubwa zaidi kutokea jijini Mwanza.
Wazazi kadhaa wamelaani hatua ya kutumiwa ujumbe mfupi na wakuu wa shule kadhaa wa maandishi unaowataka wasipeleke watoto shule kesho.
Wazazi hao wamesema hiyo ni kinyume na kanuni za Tume ya Uchaguzi na inaonekana waziwazi CCM imeamua kukanyaga sheria hizo.
Hali hiyo imesababishwa na chama hicho kukosa ushawishi wa watu kuhudhuria mikutano yake bila kulazimishwa na hali imejionyesha pamoja na kutumia wasanii haijasaidia kitu.
Mgombea wa Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu aliingia Mwanza kwa kishindo kikubwa wiki iliyopita na kuvuta umati wa watu ambao wachunguzi wa mambo wanasema huenda ukawa umati mkubwa zaidi kutokea jijini Mwanza.
Wazazi kadhaa wamelaani hatua ya kutumiwa ujumbe mfupi na wakuu wa shule kadhaa wa maandishi unaowataka wasipeleke watoto shule kesho.
Wazazi hao wamesema hiyo ni kinyume na kanuni za Tume ya Uchaguzi na inaonekana waziwazi CCM imeamua kukanyaga sheria hizo.