Mwenendo wa utalii nchini: Waziri Kigwangalla aonyesha kukata tamaa

Mwenendo wa utalii nchini: Waziri Kigwangalla aonyesha kukata tamaa

Hakuna jinsi tourism itarudi mapema. Bora tungekubali yaishe. Tutaje namba hata za uongo afu tuzipunguze. Tungeaminika
Kweli mkuu. HAWA ZERO BRAIN WANASEMA TANZANIA NZIMA INA WAGONJWA 4 TU...UONGO KAMA HUU HATA MWANANGU WA DARASA LA KWANZA B HAWEZI KUAMINI SEMBUSE WAZUNGU!
 
Waache propaganda mfu za kudanganya watu kwenye tv eti kuna watalii wamekuja kwa ndege wakati flight karibu zote duniani zimefungwa.

Dunia iko kwenye janga kubwa namna hii lakini wao wako busy kudanganya wananchi as if wakidanganya mapato yataongezeka.

Serikali zinazoishi kwa propaganda mfu namna hii huwa zimejaa mbumbumbu na wasiyo na maarifa yoyote yakuikwambua nchi kutoka kwenye matatizo.

Uongozi awamu hii spectrum yake ni ndogo sana, wanataaluma zao ila wako Kama picha tu, brains zao sioni zikitumika kwa faida. Mnahemishiwa kwa taaluma ila hamheshimiwi kwa mawazo na maoni ya uendeshaji.

Mimi hata uniteue ntakupa maoni yangu hata kama ikibidi tutofautiane na sitayatoa kwa dharau, bali hekima , busara na bila woga na ntakuwa mnyenyekevu, na ukitaka nikupishe nakupisha pia na sitabwatuka Kama Nape.
 
Haya kuna mwenzenu humu amekata tamaa japo alitoa hadi video na kuhamasisha.
Mwenzio anawasanifu wamarekani wanavyong'ang'ania kuwa hospitali zimejaa wagonjwa wa corona
Atakata tamaa vipi wakati midege inapisha kia kumwaga watalii
 
Mimi sio nabii ila Magu atasoma hii msg ya jamaa kwa jicho la tatu. Na kitakachofuata....... Mi simo
 
Mwenzio anawasanifu wamarekani wanavyong'ang'ania kuwa hospitali zimejaa wagonjwa wa corona
Atakata tamaa vipi wakati midege inapisha kia kumwaga watalii
hahahah hiyo midege unayozungumzia labda unamaanisha mbayu-wayu.

Mataga mliona zeru-zeru wawili Airport mkafanya sherehe eti watalii wamemwagika Tz 🤣🤣🤣
 
Kweli mkuu. HAWA ZERO BRAIN WANASEMA TANZANIA NZIMA INA WAGONJWA 4 TU...UONGO KAMA HUU HATA MWANANGU WA DARASA LA KWANZA B HAWEZI KUAMINI SEMBUSE WAZUNGU!
Mpuuzi wewe, unaendelea kushabikia ujinga NYUMBU wewe, kwenu kunawaliokufa ama wapo walio na Corona?, Unataka namba iwe kubwa kutoka wapi ikiwa wewe Huna maambukizi,
 
Nyie MATAGA mkipewa mbinu ya kupambana na majanga makubwa mnaleta jeuri na kibri siyo?
Haya kuna mwenzenu humu amekata tamaa japo alitoa hadi video na kuhamasisha.

View attachment 1469976

Halafu na nyie watu wa I.T ndiyo nini kutujazia mazagazaga hivyo mezani? Hamjui kuwa yanaonekana kwenye video?
View attachment 1469977
Mimi sioni kosa la waziri biashara ya Utalii ita pick up pole pole huwezi kutegemea kesho watalii wajae Tanzania dunia siyo Tanzania peke yake kuna nchi zingine pia zinaangalia soko hilo hilo.

Cha kufanya kwanza ni kuondoa hofu kwa watalii kwamba Tanzania si salama alafu ni kuwashawishi kupitia vivutio vyetu kwamba watafaidi kile wanachotarajia kutoka kwetu value for money.

Tusiogope mbuga zetu haziozi, fukwe tuzitunze, tamaduni tuzifufue ningependa kuona ikulu ya Dodoma ikiwa na jengo la Tembe jee unakumbuka nyumba za wagogo? Pale mlangoni askari wanaopokea wageni wavae zile shuka za wagogo na katambuga. Tuharakishe SGR ianze kazi na ikiwezekana tujenge SGR nyingine Dar, Tanga, Moshi, Arusha mpaka Musoma watalii watasafiri kwa urahisi na kwa bei nafuu, watakuja kwa wingi tu.

Tufufue utalii wa uvuvi deep sea fishing hasa Baracuda kule Mafia na Pemba, kuna soko kubwa sana hasa kutoka ujerumani na watalii wa deep sea fishing huwa wanakaa muda mrefu mpaka mwezi mmoja. Tungalie uwezekano wa kuanzisha utalii wa retired na senior citizens kule Lushoto kuna hali ya hewa nzuri, utulivu na usalama.

Ile kauli ya waziri Kigangwala kuweka Cable cars mlima Kilimanjaro ilikuwa kosa la jinai. Hizo cable cars apeleke Usambara Mountains kule aweke vivutio mlimani ajenge restaurants, Casinos, night clubs atavutia watalii wengi. Siwezi kuongea yote kwa leo.
 
Mi naona wala hajakata tamaa ila hii taarifa ndio uzushi kujaribu kumkatisha tamaa. Ni mapema sana kupima matokeo ya juhudi za kurejesha utalii. Huko kwenye source ya watalii penyewe hapajatulia kwa corona wala kiuchumi.

Jitihada zitalipa tu. Wale jirani tuliokwisha wapiku kwa utalii ndio wanaleta hila kipindi hiki kutumia corona watudidimize ila tushaamka sana hawana ujanja tena.
 
Asisingie travel advisory,bali akiri tu hali ya kiuchumi duniani ni mbaya na hata hao watalii hivi sasa hali zao sio nzuri sana mbali na hofu ya hili gonjwa popote duniani.
 
Kingwangala awasikilize watu wa TATO wale ndio ma expert ukijifanya mjuaji lazima ukwame
Sasa wana fungua utalii wakati operators hawana booking hata moja. Hotel hazina booking wana tuonyesha maigizo ati watalii wame ingia.. Tanzania tuna ongoza kwa maigizo.
 
Back
Top Bottom