Sikatai mkuu, ila nyuma ya pazia ni lazima ujue jamaa ana kadi ya kijani na pengine ni miongoni mwa wafadhili wakubwa wa chama chao ndomaana wanamkalia kimya. Kinyume na hapo jamaa ni sisimizi tu mbele ya serikali. Anaweza kupotezwa katika mazingira ambayo hata yeye mwenyewe hatoweza kujua amepoteaje poteaje.
Unakumbuka wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, mzee Lowasa alitauminisha kwamba yeye anaijua serikali kindaki ndaki, kwamba ni mtu aliekulia na kuishi kwenye mfumo wa serikali kwa miaka mingi, hivyo hakuna anaweza kumtisha wala kuthubutu kumuibia kura yake hata moja.
Kilichotokea baada ya uchaguzi kila mtu ikiwemo wewe mwenyewe unakijua. Mhe aliishia kuongelea chini chini tu yakaisha bila kuthubutu kufanya lolote. Hii inamaana kuwa serikali ndio inayoamua kukuacha kwa sababu ya faida yao wenyewe, ila wakiamua kukunyea unaweza kutamani bora ungekuwa raia wa Burundi au Congo.