Mwenyekiti Mbowe, kweli Rais Samia amefanya mazuri ila sifa kwake zimezidi!

Mwenyekiti Mbowe, kweli Rais Samia amefanya mazuri ila sifa kwake zimezidi!

Nahisi Mwenyekiti Mbowe amelewa, hii sio sauti yake ya kawaida. Ametumia mkutano huu kujisafisha kuhusu kulamba asali.

Japo Rais Samia Suluhu anafanya vziuri lakini ametumia muda mrefu sana kumsifia.

Is MBOWE OKAY?
View attachment 2490283View attachment 2490284View attachment 2490285View attachment 2490286
Sijaelewa kabisa
Unaposema ametumia muda wake mwingi kuwakaripia viongozi wenzake wa Chadema, nakushangaa, kama wewe ukiona mtu anakusema kwa kitu ambacho hujafanya, mtu anaendeshwa na hisia zake binafsi kukuhumu, na kukuchafua kwa wanachama wako, utakaa kimya?

Kwangu, alichofanya Mbowe ni sahihi kabisa, Lema na wenzake walitakiwa waje na uthibitisho wa vile Mbowe alilambishwa asali, lakini sio mtu upo Canada, kisa unaona mambo hayaendi vile ulivyozoea, ndio uanze kutengeneza hisia zako na kutoa shutuma kwa kiongozi wako, alikosea.

Mimi na wewe hatuwezi kujua secret behind ya kuruhusiwa hii mikutano ya siasa, lakini inawezekana kabisa, hekima na ukimya wa Mbowe, ndivyo vilichangia kumfanya Samia akubaliane nae, lakini kama mihemko ya kina Lema mnayoipenda ndio ingekuwa kwenye meza ya mazungumzo, basi inawezekana kabisa, mpaka leo mambo yangekuwa hayaeleweki...

Mbowe amejua kucheza na akili ya Samia na kushinda mchezo, tuliona vile ukimuendea Samia kwa mihemko nini atakufanya, - ukinipara nakuparua -, mwishowe Mbowe akaenda jela kwa kesi ya kutengenezewa, na hakuna mwanachama wala mpenzi yeyote wa Chadema, aliyefanya chochote ili kumtoa Mbowe gerezani, wakati mwingine acheni akili zifanye kazi, sio maguvu kila wakati!.
Sasa ndio aje atuambie SS matatizo ya chadema,kazingua
 
Endeleeni kupayuka sisi tupo kimataifa zaidi
20230121_190057231.jpg
 
Nahisi Mwenyekiti Mbowe amelewa, hii sio sauti yake ya kawaida. Ametumia mkutano huu kujisafisha kuhusu kulamba asali.

Japo Rais Samia Suluhu anafanya vziuri lakini ametumia muda mrefu sana kumsifia.

Is MBOWE OKAY?
View attachment 2490283View attachment 2490284View attachment 2490285View attachment 2490286
Anna Nkya, kwa tanzania tulivyo, Mbowe ana haki ya kumshukuru Samia. Samia angeliweza kukaza kama magufuli na hakuna cha kumfanya maana Tanzania tu waoga wakubwa, mimi, wewe na yule. Kenya ingelikuwa hakuna haja ya kumsifia maana wana uwezo wa kulazimisha la kisheria wanalotaka kulifanya (kumbuka wakati wa kumwapisha Raila miak hiyo, polisi/serikali walitishia kuwa watafyatua wakidiriki kuja kwenye kuapishwa, walimiminika watu kuzidi ilivyofikiliwa, meaning walikuwa tayari kufa!). Wewe unaweza, tupo hapa na fake IDs. Woga. Hivyo kwa Samia kufungua mikutano, ni vema akashukuliwa! anna
 
..ile kesi ni ya KIJINGA kila mtu aliona.

..binafsi sioni shida kama Mbowe yuko compromised au la.

..jambo la msingi na la kutia moyo ni kwamba Watanzania walio wengi hawako compromised.
Kama Mbowe na Cdm ameshavunjwa nguvu, Ccm wameshapata 'free ride' ya kufanya watakayo hata kuvunja katiba bila kuhojiwa.

Bila kuwepo upinzani wenye nguvu Watz hawatakuwa na uwezo wa kuhoji chochote.
 
Unaposema ametumia muda wake mwingi kuwakaripia viongozi wenzake wa Chadema, nakushangaa, kama wewe ukiona mtu anakusema kwa kitu ambacho hujafanya, mtu anaendeshwa na hisia zake binafsi kukuhumu, na kukuchafua kwa wanachama wako utakaa kimya?

Kwangu, alichofanya Mbowe ni sahihi kabisa, Lema na wenzake walitakiwa waje na uthibitisho wa vile Mbowe alilambishwa asali, lakini sio mtu upo Canada, kisa unaona mambo hayaendi vile ulivyozoea, ndio uanze kutengeneza hisia zako na kutoa shutuma kwa kiongozi wako, alikosea.

Mimi na wewe hatuwezi kujua secret behind ya kuruhusiwa hii mikutano ya siasa, lakini inawezekana kabisa, hekima na ukimya wa Mbowe, ndivyo vilichangia kumfanya Samia akubaliane nae, lakini kama mihemko ya kina Lema mnayoipenda ndio ingekuwa kwenye meza ya mazungumzo, basi inawezekana kabisa, mpaka leo mambo yangekuwa hayaeleweki.

Mbowe amejua kucheza na akili ya Samia na kushinda mchezo, tuliona vile ukimuendea Samia kwa mihemko nini atakufanya, ukinipara nakuparua, mwishowe Mbowe akaenda jela kwa kesi ya kutengenezewa, na hakuna mwanachama wala mpenzi yeyote wa Chadema, aliyefanya chochote kumtoa Mbowe gerezani.
Hapa hapakuwa mahali pake. Huu ni mkutano wa kwanza na angeweza kuutumia kusherehekea matunda ya juhudi zake bila kuwakaripia wanachama na viongozi wenzake ambao hawakukubaliana nae. Hii kuonyesha kukasirishwa sana na maneno ya baadhi ya wanachama imewaonyesha wapi udhaifu wake upo.

Mimi sijawahi kumsikia kiongozi mkuu yeyote wa CDM akimshutumu kuwa amelamba. Hata hivyo ni haki yao kuhoji gharama ya maridhiano hayo. Huyo Lema unaemsema nae amepitia magumu sana katika haya mapambano. Ingawa sio wote waliopoteza mabilioni kama alivyoteza Mbowe wako ambao kwa kiasi fulani wamepoteza kuliko yeye. Watu kama Heche aliyempoteza mdogo wake, watu kama Lissu aliyenusurika kupoteza maisha yake na vijana na wanachama wengi ambao wameumizwa, wamepoteza vibiashara vyao na wengine wametiwa ndani bila kuwa na uhakika wa kutoka mapema kwa sababu hawana majina kama Mbowe.

Unamsema Lema na wenzake na kumpa sifa Mbowe peke yake bila kujiuliza kama CCM wangekubali kuridhia kama pasingekuwa na sauti za wazi za wakina Lema kuwa hawana imani nao kabisa. Mbowe aliongezewa nguvu na uwepo wa wakina Lema kwa sababu CCM walijua dhati kuwa muafaka ungekuwa mgumu kupatikana kama Mbowe angesusa na wangebaki wakina Lema a Antipas. Ni kama vile Martin Luther King Jr. alisaidiwa sana na uwepo wa Malcolm X ambae hakutaka kabisa mazungumzo na mtu mweupe.

Mbowe anataka kuonekana kama Statesman lakini bila street fighters kama Lema, Lissu hata Mdude Chadema ari ya kuzungumza nae ingepungua.

Leo ilikuwa ni siku ya Chadema lakini yeye ameigeuza kwa kiasi fulani kuwa ya CCM. Hamna mtu anaemkataza kumshukuru Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa CCM. Ni jambo la busara kwa kweli. Lakini hapakuwa na haja ya kuwatupa wenzake chini ya basi.

Amandla...
 
Mimi nilikuwa furahisha mwanza mimeondoka mapema kwa uzuni mkubwa.sikuelewa
alichokuwa anaongea mbowe.kama ni laana Tanzania tumelaaniwa.bora mnyika ameongea points.huyu mwamba bora astaafu kabla ya kuua CHAMA.
 
Mimi nilikuwa furahisha mwanza mimeondoka mapema kwa uzuni mkubwa.sikuelewa
alichokuwa anaongea mbowe.kama ni laana Tanzania tumelaaniwa.bora mnyika ameongea points.huyu mwamba bora astaafu kabla ya kuua CHAMA.
Ile kesi ya kupika ilitumika vizuri sana kummaliza na unayoyaona huenda ni masharti ya maridhiano kwamba kuna mipaka imewekwa ni marufuku kuvuka.......poor Mbowe....Poor Tz democracy...😔😔😔.

denooJ zitto junior
 
Kama Mbowe na Cdm ameshavunjwa nguvu, Ccm wameshapata 'free ride' ya kufanya watakayo hata kuvunja katiba bila kuhojiwa.

Bila kuwepo upinzani wenye nguvu Watz hawatakuwa na uwezo wa kuhoji chochote.

..kinachowakosesha raha Ccm ni chama chao kuwa upande tofauti na HAKI.

..hata wakimchukua Mbowe bado machoni mwa Watanzania Ccm ni chama kisichotenda haki.

..kinachoipa nguvu Cdm sio Mbowe, bali hoja wanazozisimamia na kuzipigania.
 
..kinachowakosesha raha Ccm ni chama chao kuwa upande tofauti na HAKI.

..hata wakimchukua Mbowe bado machoni mwa Watanzania Ccm ni chama kisichotenda haki.

..kinachoipa nguvu Cdm sio Mbowe, bali hoja wanazozisimamia na kuzipigania.
Ni kweli mkuu, lakini ni muhimu sana kuwepo chama cha upinzani chenye nguvu hili sio la kupuuza...hasa kwa Tz ya Sasa.

Cdm ndio ilikuwa na ilitakiwa kukamata hiyo nafasi Ila kwa mambo yanavyoenda ni kama vile mpira umesharudi kwa kipa.
 
Ile kesi ya kupika ilitumika vizuri sana kummaliza na unayoyaona huenda ni masharti ya maridhiano kwamba kuna mipaka imewekwa ni marufuku kuvuka.......poor Mbowe....Poor Tz democracy...😔😔😔.

denooJ zitto junior

..kesi ya ugaidi hukumu yake ni KIFO.

..waliofuatilia kesi waliridhika kwamba ilikuwa ni mashtaka ya kutunga.

..Jamhuri na Serikali walikosea sana kuwatoa mashahidi wao wote na kila mmoja akionekana kusema uongo.
 
Hapa hapakuwa mahali pake. Huu ni mkutano wa kwanza na angeweza kuutumia kusherehekea matunda ya juhudi zake bila kuwakaripia wanachama na viongozi wenzake ambao hawakukubaliana nae. Hii kuonyesha kukasirishwa sana na maneno ya baadhi ya wanachama imewaonyesha wapi udhaifu wake upo.

Mimi sijawahi kumsikia kiongozi mkuu yeyote wa CDM akimshutumu kuwa amelamba. Hata hivyo ni haki yao kuhoji gharama ya maridhiano hayo. Huyo Lema unaemsema nae amepitia magumu sana katika haya mapambano. Ingawa sio wote waliopoteza mabilioni kama alivyoteza Mbowe wako ambao kwa kiasi fulani wamepoteza kuliko yeye. Watu kama Heche aliyempoteza mdogo wake, watu kama Lissu aliyenusurika kupoteza maisha yake na vijana na wanachama wengi ambao wameumizwa, wamepoteza vibiashara vyao na wengine wametiwa ndani bila kuwa na uhakika wa kutoka mapema kwa sababu hawana majina kama Mbowe.

Unamsema Lema na wenzake na kumpa sifa Mbowe peke yake bila kujiuliza kama CCM wangekubali kuridhia kama pasingekuwa na sauti za wazi za wakina Lema kuwa hawana imani nao kabisa. Mbowe aliongezewa nguvu na uwepo wa wakina Lema kwa sababu CCM walijua dhati kuwa muafaka ungekuwa mgumu kupatikana kama Mbowe angesusa na wangebaki wakina Lema a Antipas. Ni kama vile Martin Luther King Jr. alisaidiwa sana na uwepo wa Malcolm X ambae hakutaka kabisa mazungumzo na mtu mweupe.

Mbowe anataka kuonekana kama Statesman lakini bila street fighters kama Lema, Lissu hata Mdude Chadema ari ya kuzungumza nae ingepungua.

Leo ilikuwa ni siku ya Chadema lakini yeye ameigeuza kwa kiasi fulani kuwa ya CCM. Hamna mtu anaemkataza kumshukuru Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa CCM. Ni jambo la busara kwa kweli. Lakini hapakuwa na haja ya kuwatupa wenzake chini ya basi.

Amandla...

Niwe mkweli, tumuachie Lissu uenyekiti. Nadhani Muda wa Lissu umefika. All in all tumefanikiwa kufanya mkutano mzuri.
 
..kinachowakosesha raha Ccm ni chama chao kuwa upande tofauti na HAKI.

..hata wakimchukua Mbowe bado machoni mwa Watanzania Ccm ni chama kisichotenda haki.

..kinachoipa nguvu Cdm sio Mbowe, bali hoja wanazozisimamia na kuzipigania.
Uko sahihi. Ni kama walivyoondoka wakina Halima watu waliamini kuwa CDM haita recover. Hata Mbowe akiamua kung'atuka na kukaa pembeni wapo watakao endelea kupigania hoja zilizofanya wengi kukikubali chama chao.

Amandla...
 
Mimi nilikuwa furahisha mwanza mimeondoka mapema kwa uzuni mkubwa.sikuelewa
alichokuwa anaongea mbowe.kama ni laana Tanzania tumelaaniwa.bora mnyika ameongea points.huyu mwamba bora astaafu kabla ya kuua CHAMA.

Mbowe analazimisha chama kiende mrengo wake. Lissu na Heche ndio wanafaa kushika gurudumu. Kulikuwa na mengi ya kusema , mfumuko wa Bei, Deni la taifa.
 
Ni kweli mkuu, lakini ni muhimu sana kuwepo chama cha upinzani chenye nguvu hili sio la kupuuza...hasa kwa Tz ya Sasa.

Cdm ndio ilikuwa na ilitakiwa kukamata hiyo nafasi Ila kwa mambo yanavyoenda ni kama vile mpira umesharudi kwa kipa.

..HOJA iko palepale.

..haitaondoka kwa propaganda na janja-janja ya Ccm.

..Ccm wanachofanya ni kudanganya-dangaya lakini wananchi nao wanazidi kuerevuka.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1][emoji1] Mkuu cdm Leo imenitoka rohoni kabisaa.
Mwamba kalamba asali na mbaya zaid kapamda jukwaani akiwa gambe
Chadama na ccm ni [emoji117][emoji90]
 
Back
Top Bottom