Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wa CCM, Dkt. John Magufuli achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kwa muhula wa pili

Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wa CCM, Dkt. John Magufuli achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kwa muhula wa pili

Alichukua fomu?

Alidhamiria kuchukua fomu wakamzuia, walipoona king'ang'anizi wakamtaliki. Hata hivyo JK na Mkapa walikuwa hawapendwi kama Magufuli, hivyo huenda walikuwa na wasiwasi wa kushinda. Je Magufuli aliyeamua kuongoza nchi kwa utafouti, na kusifiwa sana mbele ya cameras anaoogopa nini? Au zile sifa wanazompa hata yeye anajua wanamsanifu?
 
Mleta Hoja Nina swali nataka nikuulize
Je Rais Magufuli amewakataza wengine wasichukue fomu?
 
Mleta Hoja Nina swali nataka nikuulize
Je Rais Magufuli amewakataza wengine wasichukue fomu?

Naum, Mwenyekiti-CCM Magufuli keshawazuia wengine KIMAZINGIRA na KISAIKOLOJIA!!
Hivi kama wewe ni Dikteta na watu wanajua kabisa wakijaribu kukupinga UTAWASHUGULIKIA wafanyeje?
UDIKTETA huminya Demokrasia wakati wowote mahali popote!
Ndicho kinachoendelea ndani ya CCM kwa sasa!
 



Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli amechukua fomu ya kuwania kinyang'anyiro cha Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Magufuli amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally, Makao Makuu ya CCM, Dodoma.


Maendeleo hayana vyama!

2431549_09886.jpg
 



Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli amechukua fomu ya kuwania kinyang'anyiro cha Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Magufuli amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally, Makao Makuu ya CCM, Dodoma.


Maendeleo hayana vyama!

Sasa hizo nderemo na vifijo vya nini wakati Pelepole alisema vitakuwepo tu baada ya mtu kupitishwa na chama hicho? au ndo tayari mambo yamekwisha hivyo?
Je wengine wakifanya hivyo watakutana na rungu au?
 
Hivi imitokea Mh Rais akaweza kutetea kitichake kwamuhula ujao je itakua ndio Awamu ya6 au ndio bado itakua niAwamu ya5?kingine hivi hizi Awamu zinahesabiwaje jenikutokana na Marais waliopo madarakani au nikutokana kimihula...maana ninavyojua Awamu moja inakwisha baada yamiaka5!...tafadhalini wajuvi naombeni kunielewesha ni namna gani hizi Awamu huhesabiwa!
Cc Pascal Mayalla
Cc John the Baptist!
 
Back
Top Bottom