Mwigulu anasema hakuna Mtanzania atagongewa mlango alipe Deni la Taifa, kwani tozo maana yake nini?

Dr. Madelu anadhani hatujui kwamba hizi tozo wanazokamuliwa wananchi ni kutokana na nchi kulemewa na mzigo wa ulipaji madeni, asitake kutufanya mazwazwa.......
 
Waziri angetumia muda mwingi kuelezea Ni namna gani tutapunguza Deni la nje na sio kauli za kitoto Kama Hilo.
 
NCHI NGUMU SANA HII NA INA VIONGOZI WAGUMU PIA
 
Dr. Mwigulu amejipambanua haswa Leo kwa kusifu na kusema

-katika Marais wanaoongoza kuombwa ziara huko duniani Dr. Samia anaongoza.
  • Deni la Taifa lipo 18.5% ambalo ni dogo na linaifanya Tz kukopesheka.
  • World Bank huitolea mifano Tz kuwa tupo vizuri nchi jirani watuige.
  • ukomo wa kukopa ni Hadi 52% kwa hiyo TZ Bado sana huwezi kutulinganisha na Kenya, Uganda.

Hayo ni machache tu aliyosema mchumi wetu Dr. Mwigulu Leo asubuhi kwenye mahojiano na Clouds
 
Hata Mimi nilishangaa pia, madeni ya private sectors yanajumuishwa kwenye deni ta Taifa.
Mfano tigo wakope , lakini deni lake lijumuishwe kwenye deni la Taifa, maana ake wa TZ tutakuja kulilipa SS😰😰🤷
 

Hao waendesha kipindi nao hovyo kabisa! Mtu anaongea ujinga wao hawaoni na wala hawana maswali ya kumbananisha nayo.
 
Huyu ndo alimshauri mama Machinga wanunue EFD?
 
Mwana Propaganda yupo kwenye Propaganda unategemea nini ?

 
Huyu jamaa,huwa anaongea,akifikiri wabongo wote ni wajinga kama yeye,
Kama hatulipi wananchi,hizo pesa zitalipwa na nani?na mama yake?
Au zitatoka Kenya?mbulu kenge kabisa,
 
Kwa hiyo we ulitaka u-enjoy huduma za serikali bure, utumie mwendokasi, fly-overs Dsm, unasubiri uje uweke tako lako utambae na SGR, bado unasubiri umeme wa bwawa la Nyerere, uendeke kujipiga selfie daraja la Busisi-Kigogo usikatwe kodi wala tozo? Una mjombako Ulaya? Au una shangazi Marekani? Huna hata aibu, kafanye kazi kodi lazima ulipe na tozo km kawa.
 
Mamlaka itengue uteuzi unataka awekwe mjombako? Mwigulu oiga kazi hawa wamezoea vya bure.
 
Ng'wigulu hana akili
 
wa sababu hautatungoa mlango ndiyo uendelee kukopa tu?, leo deni letu ni Trillion 91, Ndugai kuna siku tutamwelewa.
 
Mbona anamdhalilisha Bakhresa?. Kwamba naye ni mmoja waliokopa Trilioni 20?. Sasa Kama Bakhresa kakopa Trilioni moja, Hilo Deni ni la Bakhresa au Tanzania Kama taifa. Na atakaye lipa ni Bakhresa au sisi wa wananchi.
Deni private linalipwa private na deni la serikali ndio linalipwa na serikali
 
Ninachojua mimi ukilipa KODI unagongewa mlango ukikatwa TOZO unagongewa mlango, ukilipa USHURU unagongewa mlango.

Mwigulu haoni hizi tozo au anajizima data.
[emoji2827]
 
Hakuna taifa linaloongozwa bila mikopo kwaiyo Tanzania lazima tukope kwaajili ya maendeleo na uzuri wa Rais Samia Suluhu yeye anakopa kwa uwazi na maendeleo yanaonekana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…