Uchaguzi 2020 Mwigulu Nchemba: Rais wetu ni Magufuli, waambieni waliowatuma enyi wenye tamaa ya Madaraka

Mkuu Mtingi, asante kuniheshimu na pole kunishangaa.
Uchaguzi ni process iko very transparent tangu mwanzo. Kura zinapigwa kutuoni, zinahesabiwa kituoni na matokeo yanabandikwa kituoni na kila stage kuna mawakala wa vyama na wanasaini..

Hapa nakataa sio Tume Huru bali inaitwa huru. Ukimwita paka sungura haina maana si paka
 
Utakufa na stress acha wivu wa kike!
Kukemea matumizi mabaya ya mali ya umma sio WIVU wa KIKE wewe POYOYO Aka BUMUNDA!! Hata kama Mnalipwa na kutetea UOZO wa Awamu ya 5 muwe mnashirikisha UBONGO baadhi ya HOJA!!
 
Sheria/Taratibu za NEC kwasasa sio lazima wakala asaini form ya matokeo yaani ni Option kusaini.

Hawa jamaa kila siku wanatafuta mbinu za kukarabati Kanuni na Sheria za Uchaguzi ili Wapinzani wasiweze kupumua.....! Kumbuka sekeseke la Marehemu Acqulina......chanzo ilikuwa ni form zinazosainiwa na Mawakala baada ya Mkurugenzi kukataa kuwapa CHADEMA!!
 

Attachments

  • 2431549_09886.jpg
    46.6 KB · Views: 3
Kiherehere cha kukosoa ili kulinda ugali wako kinakutia fedhea mbele za watu. Maana hata huelewi hiyo cloud ilitamkwa wapi.
 
Kwani kuna Muda uliopangwa wa kudai Tume Huru uliowekwa? Tumia akili kidogo tu kufikiri sio unaandika upupu
 
@Mwigulu Nchemba utaacha lini kuiaibisha PhD?
Unasema Kuna tume huru ya uchaguzi kweli!!
Fikiria mbuzi aliowauza mzee wako ili usome matokeo yake ndio haya!!!?

Mwenzako mmoja alishukuru kwa kutolewa jalalani ilihali Ni professor
Mnawafundisha Nini wanaosoma bado?

Mambo yalipokua shwari Membe hakuwahi kuongelea tume huru
Leo yameharibika amekiri mwenyewe hakuna tume huru.

Wanasiasa tupumzisheni TUMEWACHOKA.
 
Aristotle = educated people are wise; I don’t see wisdom from your writings above.

Again: “Tanzania educated people where do you publish your papers?” Beni saanane
 
Yes tunaona kazi nzuri mliyofanya sasa tunaomba tume iwe huru kulingana na kazi nzuri na maendeleo mliyoleta,

Tunamaanisha tume huru kwa maana ya wajumbe wa tume ya uchaguzi wasitokane na uteuzi wa mwenyekiti /mgombea wa chama kinachoshiriki uchaguzi husika ili kuepusha na mazingira ya bias.

Wengine nia yetu ni njema kabisa labda msime kama kuna mabeberu ambayo intellijensia yenu imewaambia wanania ovu kupitia kilio hichi cha tume ila sisi walaa hatuna shida tunataka kushinda na kushindwa kufanyike kwa haki zaidi ya hapo awali.

Tanzania inahitaji tume huru ili tuepushe mauaji kama ya Akwelina aliyeuliwa kwa risasi baada ya msimamizi wa uchaguzi kuficha form za mawakala wa vyama pinzani.
 
Hivi kuna mtanzania anaendaga kuobserve uchaguzi wa Uingereza ?
Mkuu unalinganisha uchaguzi na uchafuzi?.
Observers kuja huku wanagharimikiwa na mabeberu,kwa hiyo wawalipie na Watanzania kwenda kwao sijui kuobserve nini?.
 
Mh. Membe ni mzoefu wa masuala ya kimataifa, ndiyo maana hataki kusimama ktk mila, desturi na utamaduni ambao kwa uzoefu wake anauona umepitwa na wakati. Hata kama alikubaliana na hali hiyo ktk maisha ya ujana wake, haimlazimishi kufanya hivyo ktk maisha yake ya sasa ya kutaka demokrasia pana ndani ya chama chake, ambacho amekitumikia kwa muda mrefu na kwa uaminifu mkubwa.

Katiba ya chama inatoa ruhusa ya watia nia kuingia kwenye kinyang'anyiro, haijalishi uwepo wa "iincumbent office bearer". With due respect to Hon. Nchemba, tena kwa kuzingatia yeye anahitaji sana fadhila za Mwenyekiti Taifa, isiwe sababu ya kuona wanachama wengine wenye msimamo tofauti naye kuwa wanakosea.

Tofauti za kimisimamo ndiyo hukijenga chama na kukifanya vkiwe imara. Tushiindanishe fikra mbadala ili tukapate kujua ipi ni pumba na ipi ni mchele.
 
Yaani muangalizi huyo huyo,mgombea huyo huyo,muhesabu kura huyo huyo na mpanga matokeo huyo huyo
Na huyo huyo akikipa ushindi chama chako na mgombea wako hana tatizo kabisa!!
Tanzania bila unafiki haiwezekani
 
Ni vibaya sana kuongea wakati wa kula,,, wewe kula kimyakimya sio hadi watu tujue... Mpeni sifa mpishi akiwa jikoni sio kwenye dinning table
 
Huyu ndiye waziri wa Katiba na sheria wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania
Mkuu G Sam, unajibainisha kuwa wewe ni bingwa na mtaalamu wa siasa, tusaidie kutambua sifa za kiongozi unayedhani anafaa badala ya kulalamika na kulaumu tu kila mara. Kwa kuwa nchi inaingia kwenye uchaguzi mkuu, ufafanuzi wako utamsaidia mtu kufanya maamuzi yaliyo sahihi. Kwa lugha ya kigeni "informed decision"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…