Mwigulu: Sijawahi kuwasiliana na Dkt. Emmanuel Nchimbi kwa e-mail tangu nizaliwe

Mwigulu: Sijawahi kuwasiliana na Dkt. Emmanuel Nchimbi kwa e-mail tangu nizaliwe

Hivi kuna jambo ulilowahi kulikubali we M. Nchemba? Vipi kuhusu kutema mate ndani ya jengo la bunge? Hilo nalo utalikataa? Utawaambukiza wenzako magonjwa. Hivi kwa nini hamkukamatwa kutokana na hayo mawasiliano hatari kwa usalama wa raia? Mbona Lwakatare alikamatwa haraka,baadaye aibu ikawa juu yako.Ushahidi wa mbinguni uko wapi we mtema mate ovyo?
 
Punguza mapovu we Jangili, Mbeya uliweka makambi ya kigaidi kwa lengo la kuwadhuru CDM, Igunga ulifumaniwa na mke wa mtu kasha ukaendesha mauaji ya kikatili wewe na Ashely, Usa river ulifanya mauaji, Arusha uliandaa mauaji, Ulifadhili matengenezo ya movie ile ya kichina kwa Lwakatare huku ukiratibu mateso ya mwandishi wa habari... Ikiwa kila ulifanyalo linalengo la kuwadhuru binadamu wenzio kwa malengo ya kuidhoofisha CDM jamii ikuelewe vipi? Ikiwa mawasiliano yako wewe na ZOKA, ZITTO, MSANGI yanaashiria maovu unataka sis jamii tukuchukulie vipi? kwani email yako iliyoko kwenye b.card inakunyima kuwa na emails nyingine? Mbona hapa JF una ID kibao?...WEwe si msafi hata kidogo, damu za watu zitakurudi tu! BTW mchumia tumbo first class "tuambie madhara ya kupandisha bei ya umeme kwa uchumi wa nchi? Ni sahihi kwa CCM kupandisha bei ya umeme ili muweze kuwalipa Agreco, IPTL, SONGAS na SYMBION million 700 kila siku?...

...well said!!!
 
Cjawahi kuona ama kusikia nchi yoyote ambayo chama kilichomadarakani, kazi yake ni kuangalia chama kikuu cha Upinzani kinafanya nn..CCM Mnaboa sana ukienda bungeni ooh! Mbowe...ivi zile ahadi mmetekeleza walau hata moja..Siasa za kizamani hizo hazitawasaidia na kama hamujui kipindi hiki cha awamu ya pili ya Kikwete mmesaidia sana kupiga kampeni za cdm
 
ndg wana jf salaam. Nimelazimika kuja hapa kuweka jambo hili sawa. Nimeona uzi unaoongelea kuwa mimi na mhe Nchimbi tumewashitaki vijana hao waliojitaja kwa kuingilia mawasiliano. Naomba kuweka wazi kuwa

1) Sijawahi kuwasiliana na mhe Nchimbi kwa E mail hata siku moja tangu nizaliwe.
2) Sijapeleka lalamiko la mambo hayo polisi wala vyombo vyovyote vya dola wala vya habari
3) E mail ilibandikwa ikionesha mimi nawasiliana na Nchimbi wala sio e mail yangu wala haijawahi kuwa e mail yangu.
4) Sikuwa hata na sababu ya kuwasiliana na Mhe Nchimbi kwa E mail kwakuwa muda mwingi tuko wote bungeni, kwenye vikao vya chama na mjini.
Inawezekana ni kweli vijana hawa wameitwa polisi, basi kama ndivyo, watakuwa wameitwa kwa kutengeneza e mail kwa majina ya viongozi, kutunga ujumbe wao na kutengeneza kama vile viongozi wamewasiliana na kuusambaza kwa lengo baya la kutaka kuchafua taswira za viongozi mbele ya umma. Hii ni tabia mbaya kabisa na vijana wa aina hii ni mizigo kwa Taifa. Naunga mkono polisi wafuatilie uzushi na ujinga huo wa watu kutengeneza e mail bandia, mawasiliano feki na kusambaza kama ndio mawasiliano halali ili umma upokee matope waliopanga kupakazia viongozi. e mail yangu iko kika mahali kwenye business card zangu. Nalaani kitendo chao cha kubandika e mail batili, mawasiliano batili na kusambaza kwenye mitandao, nalaani pia kwa kutokuwa wakweli kama wameitwa kwa kuandaa e mail feki na mawasiliano feki wanakuja huku kuripoti kuwa wameingilia mawasiliano. yapi? Sio e mail yangu, wala sijawahi kuwasiliana na Nchimbi kwa e mail. E mail yangu inafanya academic issues, nawasiliana na supp wangu wa PhD na wanazuoni wengine kwa academic issues. Ben, look at you?




Hapo kwenye Red mbona unaendeleza mambo yako ya kutishia watu?
Mkuu Nchemba kwa post yako hii unafikiri umejitetea na kueleweka, hakika hutaweza kutubu kwa kunyamaza kimya ni lazima ukiri ili usamehewe. Naomba ujuu watanzania wa leo sio wale wa miaka ya 1961 kipindi Inaitwa Tanganyika, na nani asiejua ukaribu wako wewe na Nchimbi? Ila kwa sasa endeleeni na ukaribu wenu kwani hamna tena chemistry maana mkuu wa kaya keshamweka benchi. Ila nakusii my brother Nchemba usije ukaendelea na michezo yako michafu uliokuwa ukiicheza kipindi cha Nchimbi kwani sasa Mkuu wa Kaya ameamua kufanya substustision katika wizara ya mambo ya ndani kwakuwa hajapendezwa na mlichokifanya Olasiti na Soweto Arusha, Ulimboka, Mwangosya.

Pia unakumbuka kipindi cha kampeni za udiwani Arusha? Ulipokuja wewe na wenzako mkafanya kikao mlichozani ni chasiri katika chuo kiitwacho Help To Self Help Project kilichopo Sakina kuelekea Ollmatejoo. Ambacho kikao kilianza saa moja (07:00) jioni mpaka saa saba na robo (01:15) usiku, uku mkiwa umeweka ulinzi mkubwa kuzunguka chuo chote na kukataza watu kutumia barabara za karibu na chuo hicho.

Najua unashangaa kuipata hiii habari kwani mlikuwa mnaamini ilikuwa ni siri ila sio siri tena nikufaamishe. Kama kuna nilichokupakazia au kupotosha sema ili nilete ushaidi kamili.
 
MWIGULU sijawahi kukuamini hata siku moja , hivi kwanini umekuja jf baada ya MZIGO MWENZIO NCHIMBI kupigwa chini wizarani ? Unaogopa nini ?
 
ukisikia Nchemba amepewa uwaziri utajisikieje?

Kwani Uwaziri serikali ya JK inafuata utendaji kazi au uadilifu?

Kama ww ni mtandao na swahiba wake JK tu ndiyo sifa kubwa ya kupata uwaziri serikali hii!Mbona Mulugo bado waziri bana atashindwaje kumpa Mwigulu?
 
Hata mimi nimeshtuka na kushangaa inawezekanaje mpange mipango miovu iliyopelekea kuondoka kwa dr Mvungi halafu mjipeleke wenyewe polisi kisa mmegundulika? Inashangaza lakini kwenye siasa kulla kitu inawezekana. Ila kiukweli hizi siasa za kucheza na maisha ya watu zinaudhi sana. Familia ya Mvungi inachukuliaje tuhuma hizi na je waliotengeza hizo iff did it watakuwa na aibu gani mbele ya wanafamilia? Tunajitambue na kufanya mambo kwa kufikiri.

mkuu kwa wanasiasa kila kitu kinawezekana,japo kiuhalisia inachekesha
 
Mheshimiwa Mwigulu; Jitahidi Kumrudia Mungu wako!! Shutuma Unazotupiwa na kila aliye Mtenda Haki sidhan Kama zitakusaidia Kupata Yaliyo bora!! Duniani tunapita tuu ndugu Yangu!! Pia Nakushauri uwe na upeo wa kufikiria na Kesho!! Yaleo Yamepita!!!
 
Uwii Mungu anajua na nafsi yako.Nenda basi polisi katoe hayo maelezo yako!
 
Wanakuja kukanisha baada ya Mmoja wapo kufukuzwa kazi ya Uwaziri wa mambo ya ndani
 
Mwigulu ni muongo, mzandiki, mnafiki ni mtu asiye aminika kidogo, hafai, hafai , hafai....hata ukimtupa mto wami mamba hawawezi kumla...hafai hata kidogo kuishi na jamii ya watu waungwana na wastaarab.
 
Nadhani ni vema mheshimiwa Nchemba ukatumia muda huu kuwapelekea maji wananchi wa jimbo lako, kusaidia ujenzi wa shule na zahanati kule jimboni kulikoni kuja kulumbana hapa kwa mada zisizo na miguu wala kichwa. Singida ni kati ya mikoa masikini sana ya nchi hii, better use this opportunity to give your voters their long awaited social amenities!
Siku hizi wauaji mnawaita waheshimiwa?...Wanyonyaji mnawaita wawekezaji? Mafisadi mnawaona celebrities? Bei ya umeme inapandishwa 85% kwaajili ya kulipa deni feki mnashangilia? Miaka 50 plus wameshindwa kuwapa wananchi maji, huduma bora za afya, elimu, barabara, maisha bora mwaka huu mmoja uliobakia wataweza? CHAMA CHA MAJANGILI ni majanga kwa WATANZANIA mkuu...
 
Mwigulu wewe ni haini full stop....Na ukweli tumeshaujua..

nakuambia hivi , lazima watatajana tu , we subiri , hatuwezi kuvumilia MTU MMOJA akituharibia amani kwa kisingizio cha kulinda ccm .
 
Siku hizi wauaji mnawaita waheshimiwa?...Wanyonyaji mnawaita wawekezaji? Mafisadi mnawaona celebrities? Bei ya umeme inapandishwa 85% kwaajili ya kulipa deni feki mnashangilia? Miaka 50 plus wameshindwa kuwapa wananchi maji, huduma bora za afya, elimu, barabara, maisha bora mwaka huu mmoja uliobakia wataweza? CHAMA CHA MAJANGILI ni majanga kwa WATANZANIA mkuu...

Sahihi kabisa. Ndio sababu nimemshauri akatatue shida za wapiga kura wake kwa muda mchache uliosalia, aachane na malumbano yanayopoteza muda wa sie walipa kodi.
 
Ben sio mara yangu ya kwanza kufafanua hili. Siku nilipoiona tu niliandika humu na fb kuwa hiyo sio e mail yangu na wala sijawahi kuwasiliana na Mhe Nchimbi kwa e mail. Hapa nimeongelea ya kuwa umeitwa polisi of which nisingeongea kabla hujaitwa. Hizo siasa za kiwango cha chini mno.

Acha kutufanya sisi watoto wadogo, hakuna mahala ulijibu hili swala na by then kila mtu alikungoja kwa hamu kuona response yako lakini hakuna kilichotokea, by the way, huko Police Ben kaulizwa passwords alitoa wapi? so kwa mtu yeyote aliye vizuri upstairs anaelewa kwamba hizo emails ni za kweli na hakuna cha kutengenezwa.
 
Tatizo Mwigulu haji kujibu hoja badalaya hamy d ndo anajibu...

Hizi ID nyingi ni tabu tupu..
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom