Mwigulu: Sijawahi kuwasiliana na Dkt. Emmanuel Nchimbi kwa e-mail tangu nizaliwe

Mwigulu: Sijawahi kuwasiliana na Dkt. Emmanuel Nchimbi kwa e-mail tangu nizaliwe

Nashukuru sana kwa ulicho andika juu yangu, ila ipo siku utajua ukweli juu ya mwigulu na ccm unayoiabudu.
Ungekuja Arusha Ngarenaro ukaulizia Ole Laiz alikuwa ni nani ndani ya ccm watakuambia. Ila baada ya kuujua ukweli sasa ninajua atua ya kuichukua japo njia nilioipitia ya kumjua Mwigulu na ccm ni ngumu ila yote namwachia Mungu.

...aseeh!!

Mkuu funguka...leo kazi moja tu....
 
Hata mimi na-doubt....yaani wewe upoteze mwanao, halafu uwe na ushahidi wa muhusika (ambaye si tu kwamba ameua mwanao bali na wengine pia pamoja na kujeruhi wengine kibao) halafu badala ya kuchukua hatua stahiki (at least utoe ushahidi hata hadharani ikibidi), wewe unaishia kulalamika kwenye mitandao !?

Mmh ya kweli haya?
 
Mkuu kwanini hamkukanusha tangu mwanzo? Ben anasema aliwatumia hadi sms ili mkanushe lakini bado hamkufanya lolote huku habari zikisambaa kwa kasi.

Uzushi wenye tuhuma nzito kama zile si za kukaa kimya na ukimya wenu umefanya wengine tuanze kuamini! Kwanini kanusho liwe sasa?

Mr Benn saanane ni nyoka wa kijani ndani ya majani ya kijani,amechoka kukaa ndani ya majani.
 
Mwigulu utaitumbukiza nchi yetu kwenye machafuko soon. Sielewi ni kwa nini wazee wenye busara ndani ya CCM wanaweza kukuacha ufanye haya unayoyafanya. Pamoja na degree yako na hiyo PHD unayodai unasoma, you are not smart at all. Mipango yako mingi inakwenda ovyo ovyo na kubuma kila leo, lakini CCM wanakuona wewe ni kichwa babu kubwa. Kwa nini imekuchukua muda mrefu kuzijibu hizi tuhuma? Kwa nini haukutoa ufafanuzi mpaka Ben alipoitwa polisi?

In short, wewe ni janga la taifa.

Tiba
 
ndg wana jf salaam. Nimelazimika kuja hapa kuweka jambo hili sawa. Nimeona uzi unaoongelea kuwa mimi na mhe Nchimbi tumewashitaki vijana hao waliojitaja kwa kuingilia mawasiliano. Naomba kuweka wazi kuwa

1) Sijawahi kuwasiliana na mhe Nchimbi kwa E mail hata siku moja tangu nizaliwe.
2) Sijapeleka lalamiko la mambo hayo polisi wala vyombo vyovyote vya dola wala vya habari
3) E mail ilibandikwa ikionesha mimi nawasiliana na Nchimbi wala sio e mail yangu wala haijawahi kuwa e mail yangu.
4) Sikuwa hata na sababu ya kuwasiliana na Mhe Nchimbi kwa E mail kwakuwa muda mwingi tuko wote bungeni, kwenye vikao vya chama na mjini.
Inawezekana ni kweli vijana hawa wameitwa polisi, basi kama ndivyo, watakuwa wameitwa kwa kutengeneza e mail kwa majina ya viongozi, kutunga ujumbe wao na kutengeneza kama vile viongozi wamewasiliana na kuusambaza kwa lengo baya la kutaka kuchafua taswira za viongozi mbele ya umma. Hii ni tabia mbaya kabisa na vijana wa aina hii ni mizigo kwa Taifa. Naunga mkono polisi wafuatilie uzushi na ujinga huo wa watu kutengeneza e mail bandia, mawasiliano feki na kusambaza kama ndio mawasiliano halali ili umma upokee matope waliopanga kupakazia viongozi. e mail yangu iko kika mahali kwenye business card zangu. Nalaani kitendo chao cha kubandika e mail batili, mawasiliano batili na kusambaza kwenye mitandao, nalaani pia kwa kutokuwa wakweli kama wameitwa kwa kuandaa e mail feki na mawasiliano feki wanakuja huku kuripoti kuwa wameingilia mawasiliano. yapi? Sio e mail yangu, wala sijawahi kuwasiliana na Nchimbi kwa e mail. E mail yangu inafanya academic issues, nawasiliana na supp wangu wa PhD na wanazuoni wengine kwa academic issues. Ben, look at you?


Amejitokeza baada ya kuona Nchimbi kabwagwa kwani misheni yao imebuma. Inabidi asubirie waziri atakeyekuja ili aanze upya. Kazi unayo Mwigulu damu nyingi zinakulilia vp mbona umemwaga Tesha au kampeni zimeisha
 
Sasa ndg yangu Mkuu ya Kaya! unavielelezo vyote khs huyo Jamaa! na mpaka umepoteza mtoto! kwanza pole kwa yt lkn bado huoni 7bu yakuanika kila kitu unachokijua Unasubiri hadi aifute ARUSHA yote kwa milipuko! Ili ubaki ww uanze kusimulia wapi vikao vilikuwa vinafanyika hujui km utakuwa umechelewa sana! Plz km kuna chochote khs mipango OVU ya Ndg NCHEMBA hebu 2pia hapa jukwaani Ukisubiri hadi akanushe huenda naww hatutakusoma tena hapa JF!
 
Tokea ulivyoandaa ile video ya lwakatare ww na Bukoba boy kupeleka youtube cna imani tena na wewe
 
Mkuu kama hayo unayoyasema ni kweli, inabidi uact faster kwani tayari 'umeshablow cover'..........

Ni rahisi sana kumtrace baba wa mtoto aliyefariki kwenye bomu la mkutano wa CDM Arusha...hata mimi nikitaka kulijua hilo naweza kulijuwa kwa muda mfupi tu (kama sikosei alifariki mtoto mmoja tu).......Hivyo kama hayo unayoyasema ni kweli (kwamba ulishiriki kwenye mipango hiyo haramu, na halafu unatamka vile vile kwamba ulipoteza mtoto) ni rahisi watu kukufuatilia na kukudhuru.....

Chukua tahadhari na ikiwezekana mwaga ushahidi mapema kabla hujadhurika !

Mkuu, kuusu kuzurika ilo siliofii sana, na sina hofu juu ya hawa mafedhuli kwani nilisharipoti polisi juu ya usalama wa maisha yangu na kadi yao nilishawarudishia na wanajua mimi ni adui yao na kwaatakayetaka kunifuatilia zaidi asisumbuke kunitafuta kwani mimi ni Mgonbea udiwani mwaka 2010 Arusha kata ya Elerai kwa tiketi ya ccm nilieshindwa katika uchaguzi huo na Bayo aliekuwa mgombea udiwani kwa tiketi ya Chadema Ambae baadae chama kiliwafukuza uanachama na wakapoteza udiwani wao yeye na wenzakae watatu.

Siogopi na wakinizuru najua watakuwa wamezidi kujipalia makaa, kwani hili swala Mbunge wangu G.Lema analijua na nguvu ya uma ipo na itafanya kazi.
 
[h=2] Ben Saanane anavyoteseka na kivuli cha unafiki...[/h]
(mfahamu ben vizuri hapa)

Kama vijana tunaweza tukainuka na kuanza kuporomosha mashtaka na kutaja majina ya watu bila hata facts, basi kazi ipo ndugu zangu.

Ufahamu wangu ni kuwa ili tufanikiwe kuwaondoa CCM madarakani lazima tufanye kazi hiyo kama timu moja, mawazo yangu ni kuwa hatutaweza kufikia hatua yoyote ikiwa tutakuwa na vijana wa namna hii.

Vijana wa aina ya Ben Saanane wanaoweza kukaa, kutengeneza mgogoro, kubuni njia za kuuendesha mgogoro, kutafuta suluhu na hatimaye kwenda kuuza huo mgogoro kwa viongozi wengine huku akiamini kuwa anakinusuru chama hakika anakosea sana.

Vijana wa aina ya Saanane ambao kazi yao nikutumia muda na akili zao nyingi kuwarubuni na kuwagombanisha vijana wa chama na viongozi wa chama ni hatari pengine kuliko ukoma.

Kwa kuwa mara kadhaa amekuwa akinitaja kwenye mijadala yake yote. Bila hata kuangalia namna ninavyohusika, na kwa kuwa na leo hii ameamua kunitaja na kunihusisha moja kwa moja, na kwa kuwa viongozi, vijana na wanachama wengi wa chadema wamekuwa wakinihusisha mimi kuwa karibu sana na zitto kabwe. leo nitasema kitu kwenye hili.

1. Naomba niweke wazi hapa leo, kuwa sikuwahi kumfahamu mtu anayeitwa Ben Saa nane kabla mwezi wa nne 2011.
sijawahi kumsikia jina wala kumuona sura yake.(hawezi kubisha kwenye hili)

2. Ben ndiye alikuwa wa kwanza kunipigia simu, kati kati ya kipindi cha kampeni za uchaguzi wa BAVICHA - 2011 mimi nikiwa nagombea uenyekiti na yeye akiwa ni mgombea wa kimkakati(alitumwa na baadhi ya viongozi kuja kuuvuruga uchaguzi-uthibitisho upo) ambapo aliponipigia simu na kunieleza kuwa tuna haja ya kukaa kama wagombea na kuangalia namna tunaweza shiriki salama kwenye huo uchaguzi kwa madai kuwa amepata tetesi makao makuu wanamgombea wao na wanajiandaa kukata majina ya watu, jina lake na langu yakikiwemo. Nilimsikiliza na kumpuuza.

3. Baada ya hapo sijawahi kuwasiliana nae tena ben saa nane, mpaka usiku wa siku jina langu limekatwa na kamati kuu ya chama, tena aliwasiliana na mimi kupitia grayson nyakarungu, aliyekuwa swahiba wake…cha kusikitisha ni kuwa mwana mkakati ben aliwashauri mwampamba, nyakarungu na kisandu kuungana, akanishirikisha na mimi. Huku nikijua dhamira yake kuwa ni unafiki. Nikamsikiliza kwa kuwa sikuwa tena na cha kupoteza (nimeshaenguliwa tayari).

Masikini ya mungu BEN akawahadaa vijana wa watu (Mwampamba na Nyakarungu) wakaenguliwa huku yeye akiwa ni wa kwanza kukiri kuwa wameamua kuongeza nguvu.

4. Unafiki wa Saanane uliendelea siku ya tatu baada ya kuisha kwa uchaguzi wa BAVICHA maana baada ya kukatwa jina langu, wanafiki wengi walifikiri ningetoa tamko la kukipinga chama ama kuhama chama, sikufanya hivyo, kwangu mimi uchaguzi ule haukuwa ligi, ilikuwa ni mechi tu ya kirafiki. Hapo mwenyekiti wa chadema wilaya ya Kibaha akaomba kukutana namimi, nikakubali, nikakutana nae ubungo plaza, tukiwa hapo tulikuwa na mwampamba na nyakarungu, aliposimuliwa saa nane kuwa tunaenda kukutana ubungo Plaza, akaandika humu jamii forums kwa kutumia ID fake yake kuwa tumekutana na mimi nina mpango wa kuhama chama.

Nlimwambia Mwampamba kuwa saa nane ana kazi maalum, mwampamba hakunielewa, akanipinga sana sana sana, naamini leo atanielewa vizuri sasa.

5. Kwa kipindi chote hicho saa nane alikuwa anaitisha vikao vya kila aina, saa nane anatukana na kutoa kejeli za kila aina kwa viongozi wa kuu hasa katibu mkuu na mwenyekiti (lengo ni kutaka kluthibitisha kuwa kuna vijana wanawapinga viongozi hawa). Ninataja maeneo machache ambayo saa nane alipenda kuitishia vikao vyake, KWA JOHN FEDHA-KINONDONI, BLUE PEARL HOTEL-UBUNGO PLAZA na LUCH TIME HOTEL-UBUNGO EXTERNAL….naomba nikiri hadharani hapa, si mimi, mwampamba wala Juliana anayemsema aliyewahi kwenda kukutana na saa nane akajinunulia kinywaji wala chakula…kwa saa nane huwa tukifika tunakula, tunakunywa mpaka tunapochoka saa nane yeye hulipia-tukambatiza jina tukamwita manji. (lakini siku zote nimekuwa nikiwaambia wenzangu kuwa kaeni chonjo na huyu jamaa ana kazi maalum---leo wamejionea)

6. kati kati mwaka jana 2011 mwenyekiti wetu wa taifa freeman mbowe alikamatwa kwa kilichodaiwa kutokutii amri ya mahakama hapa napo saa nane akafanya vitu vyake, kama kawaida yake, akawakusanya vijana wake wote ambao yupo nao kwa kazi maalum akaanza kuwajaza ujinga…naomba nikiri tena hapa kuwa usipokuwa makini ni rahisi sana kuingia kwenye kumi na nane za huyu jamaa. Ni lalzima uwe makini kama mchange kumshinda na ndio maana ananichukia sana sana.

Mimi nimefundishwa kuwafahamu wanafiki. Hasa ninapokuwa naongea nao uso kwa macho saa nane kwangu alikuwa mnafiki kwa hiyo sikumpa nafasi hata chembe.

7. katika kipindi chote hiko sijawahi kumsikia mwana mkakati saa nane akiwasema vizuri viongozi wa chadema. Mtu pekee aliyekuwa anamsifia alikuwa ni zitto.

SAA NANE NA ZITTO
Nimeshtushwa sana na maandishi aliyoyaandika Saanane leo, hii inatokana na ama kuchanganyikiwa au kujihami kutokana na kushushuliwa na kuonekana mwongo. Naomba nieleze vizuri hapa.

1. Ben Saanane ndiye alikuwa muitishaji mkuu wa vikao vya hotelini(makutano) akiwa na saa yake ya kurekodi aliyonunuliwa na kiongozi mmoja wa chama kwa kinachoitwa kazi ya ushushu. Yeye ndiy aliyekuwa mwenyekiti wa vikao na mwandishi wa kila kinachosemwa.

2. Ni BEN SAANANE ndiye aliyewashawishi na kuwalazimisha wenzie anaowasema leo ni wasaliti waunde kikundi. Hakuishia hapo, akakitunga mpaka na jina. Kuwa ni ‘’patriotic movement seven’’ na akakifupisha PM7.(V4C-VOICE FOR VOICELESS) Akashawishi kikundi hicho kizunguke nchi nzima kuhamasisha viongozi wa huko kufanya mageuzi ndani ya chama. Saa nane unafiki utakupeleka pabaya.

3. Ni BEN SAANANE ndiye aliyegawa majina ya kuitana miongoni mwa wana kikundi hiko, yeye akajipa jina la COBRA, mimi akanipa MDUDE (kwa kuwa nilikuwa naijua dhamira yake niliendelea kumkeli)

4. Ni BEN SAANANE ndiye aliyeshauri namna ya kuhakikisha kikundi hicho kinapata pesa, wakati mimi nilimpinga ku anzia kuanzisha hiko kikundi mpaka namna ya kukusanya kwake pesa..wakati yeye alikuwa anasisitiza kwenye njia ya kukusanya michango, tena tuwachangishe viongozi wa chama na watu wengine maarufu.

5. Akiwa mkweli atakumbuka na kukiri kuwa nilimwambia kuanzisha kikundi hicho ni sawa na kuanzisha chama ndani ya chama, aliumizwa na misimamo yangu sana.

6. Ni BEN SAANANE ndiy aliyekuwa anasisitiza tuombe kukutana na zitto kabwe ili tumuombe ufadhili wa kufadhili kikundi chetu kilichoasisiwa na SAANANE na akanipa jukumu la kuhakikisha ninamwambia na kumshawishi zitto tukutane nae tufanye nae kikao, sababu yake kubwa ni kwamba Zitto ni rafiki yangu sana na itakuwa rahisi kumpata. Hapa tulirumbana sana, mimi nilielewa dhamira yake na nikiri leo hadharani kuwa nilimshauri zitto asikubali kukutana na kikundi hiki, na niukamwambia kabisa kuwa lengo la kikundi hiki ni kuthibitisha makundi ndani ya chama.-leo yametimia.

7. Ni SAANANE aliyewaapia kujito a kwenye kikundi alichokianzisha mwenyewe kwa sababu ya kutokumpata zitto kwenye kikao, siku ambayo saa nane alipendekeza zitto tukutane naye zitto alikwenda marekani kuzindua tawi la chadema, ni saa nane ndiye aliyenilaumu sana kuwa kwa nini sikumuarifu kuwa zitto hatokuwepo, nilimjibu sio wajibu wangu kuwaambia watu kuwa zitto yupo ama hayupo.

8. Ni Saanane huyu huyu mnafiki tuliyerumbana naye hasa mimi nay eye juu ya namna ya kumshirikisha zitto kwenye michango ya kikundi chake cha PM7. Naomba ninukuu mabishano yetu..mimi ‘’ kama swala ni kukusanya pesa, kwanini tumfuate Zitto kwanza na sio mtu mwengine yeyote’’?...saa nane..’’kwa sababu zitto ni kijana na ana mitazamo chanya kwa vijana wenzie na pia tunafanana nayo mitazamo hiyo sio kamakina mnyika wao status quo’’…mimi..’’kama Zitto tumemwomba tuonane naye na amesafiri bila kutujibu hauoni kuwa anatuudharau, kwanini tujipeleke kwa zitto tunayemnung’unikia kila leo?’’..saa nane.. ’’ hapana ni lazima atusaidie, zitto kwa vyovyote lazima agombee uenyekiti, na hatuwezi fanya hii kazi tukamfungulia milango bila nay eye kutoka jasho lake, ni lazima atupe pesa’’….mimi sasa kwanini tunakataa wenzetu kutumiwa halafu na sisi tunajitumikisha wenyewe kwa zitto?’’…saa nane..’’Mchange, hakuna jinsi tunaweza acha mshirikisha zitto, mwisho wa siku zitto atakuwa beneficiary kwenye huu mpango’’… …………………ukifuatilia kwa makini mazungumzo yetu ambayo kwa bahati nzuri nimeyarekodi kuanzia siku ya kwanza mpaka ya mwisho utaweza kumuelewa SAANANE kuwa alikuwa na kazi maalum.

Niseme hapa kuwa wote kwa pamoja, saa nane na zitto kila mmoja ameniambia kwa mdomo wake kuwa hawajawahi kuonana uso kwa macho, zitto yeye anasema kuwa anaweza akakutana leo na saa nane barabarani na akapishana nae bila kumfahamu.

Wote kwa pamoja wameniambia kuwa mawasiliano yao huwa ni kwa simu hasa SMS na mara chache kwa emails.

Na moja kati ya malalamiko aliyokuwa ananipa saa nane nimpe zitto ni kuwa..
1.kwa nini hapokei simu za wapiganaji wake akiwemo yeye?...
2..kwanini anakuwa na mpiganaji kama saa nane na hataki kuonna nae….
3…kwanini hataki kukifadhili kikundi cha PM7. a.K.a V4C(VOICE FOR VOICELESS)?

Kwa mtiririko wa matukio ulivyo, na kwa jinsi SAA NANE alivyoandika mashtaka yake dhidi ya zitto huku akizani anamchafua, hakika amejidharirisha sana.

Mtu mmoja mpinzani mkubwa sana wa zitto amenitumia sms kwenye facebook, ananiambia JF vipi maana COMPUTER YANGU HAIFUNGUI..huyu nae ni mjinga sababu anashabikia ujinga.

Kumshambulia zitto kwa mashtaka ya uwongo namna hii kuna mfanya zitto awe na nafasi ya kuonekana anasingiziwa mamba mengi sana hasa ndani ya chama.

Kwa mimi ninayemfahamu Saanane nje na ndani, na ninayefahamiana na kufanya kazi na Zitto, kwa mashtaka haya ya uwongo, basi hakika nitazidi kumuamini Zitto.

Nitazidi kuamini kuwa Zitto amesingiziwa mambo mengi sana ndani na nje ya chama, ninazidi kumuamini na kumtia moyo kwamba hizi ni hatua za mwisho za watu wanaokupinga, wakishindwa kukupinga kwa facts, watakupinga kwa uwongo…saa nane amekubali kutumika vibaya kwa kisingizio cha kuwa anakilinda chama na viongozi wake.

Napata mashaka kama anakielewa anachokisema, huwezi kumtenganisha zitto na uongozi wa chama. Zitto ni naibu katibu mkuu wa chama, hivyo sio rahisi kumchafua zitto ukaacha kukichafua chama.

Nimemwona saa nane anajitetea kutishiwa kuuawa, saa nane, ZITTO akiwa na mimi amenusurika kuuawa kwa ajali ya gari hivi karibuni tukitokea morogoro kwenda iringa(siku ya kumbukumbu ya kifo cha mwalimu nyerere) baada ya wapinzani wake ndani ya chama kwenda kufungua nati za tairi la nyuma ili afe, kweli zitto ameaga kwao, kweli zitto hataweza kufa kwa mipango ya mungu, hatukufika mbali tuliushtukia mchezo tukarudi morogoro mjini na zitto akaendelea na retreat yao mpaka kesho yake tukarudi dar wala hakuitangaza hii sababu aliwadharau na mbinu dhaifu.

Sio rahisi kuitoa roho ya mwanadamu mwenzio, sio rahisi kumuua zitto kama mlivyojaribu mara kadhaa na timu yenu ..

Nasikitika sana kama vijana sasa tunaeza kusimama kidete na kuandika uwongo na kuutetea bila hata woga kama ndugu yangu Saanane.

Hasira yako ya mimi kukushtukia na kuwaambia kina Mwampamba na Juliana kuwa wewe kila siku una warekodi na kwenda kuuza habari kwa kiongozi mmoja wa juu ambaye humtumia HAWARA WAKE kutuma SMS za matusi kwa watu, isiwe sababu ya kuanza kuwachafua watu ndugu yangu.

Mchafue Zitto kama unahisi una sababu ya kufanya hivyo kwa mambo ambayo una ushahidi nayo.

SAANANE acha tabia ya KUBUNI MGOGORO, KUUANZISHA, KUUENDELEZA, NA KISHA KUUTUMIA KAMA CHANZO CHAKO CHA KUPATA PESA.

SAA NANE, Waislam wanasema sifa za mnafiki tatu (ayatul munafiq thalasa).
1. akiongea huongea uwongo..
2..akiaminiwa hajiaminishi/hudhiaki..na ..
3..akiahidi hatimizi..​

Ipo siku huyo saananee atakimbia kivuli chake.
 
Mkuu naanza kukuamini sasa.....chukua tu tahadhari......

Mkuu, kuusu kuzurika ilo siliofii sana, na sina hofu juu ya hawa mafedhuli kwani nilisharipoti polisi juu ya usalama wa maisha yangu na kadi yao nilishawarudishia na wanajua mimi ni adui yao na kwaatakayetaka kunifuatilia zaidi asisumbuke kunitafuta kwani mimi ni Mgonbea udiwani mwaka 2010 Arusha kata ya Elerai kwa tiketi ya ccm nilieshindwa katika uchaguzi huo na Bayo aliekuwa mgombea udiwani kwa tiketi ya Chadema Ambae baadae chama kiliwafukuza uanachama na wakapoteza udiwani wao yeye na wenzakae watatu.

Siogopi na wakinizuru najua watakuwa wamezidi kujipalia makaa, kwani hili swala Mbunge wangu G.Lema analijua na nguvu ya uma ipo na itafanya kazi.
 
Mkuu, kuusu kuzurika ilo siliofii sana, na sina hofu juu ya hawa mafedhuli kwani nilisharipoti polisi juu ya usalama wa maisha yangu na kadi yao nilishawarudishia na wanajua mimi ni adui yao na kwaatakayetaka kunifuatilia zaidi asisumbuke kunitafuta kwani mimi ni Mgonbea udiwani mwaka 2010 Arusha kata ya Elerai kwa tiketi ya ccm nilieshindwa katika uchaguzi huo na Bayo aliekuwa mgombea udiwani kwa tiketi ya Chadema Ambae baadae chama kiliwafukuza uanachama na wakapoteza udiwani wao yeye na wenzakae watatu.

Siogopi na wakinizuru najua watakuwa wamezidi kujipalia makaa, kwani hili swala Mbunge wangu G.Lema analijua na nguvu ya uma ipo na itafanya kazi.

Mkuu funguka zaidi, umma utakuwa nyuma yako kama ukieleza kinagaubaga nini kilitokea Arusha...
 
mwigulu utaitumbukiza nchi yetu kwenye machafuko soon. Sielewi ni kwa nini wazee wenye busara ndani ya ccm wanaweza kukuacha ufanye haya unayoyafanya. Pamoja na degree yako na hiyo phd unayodai unasoma, you are not smart at all. Mipango yako mingi inakwenda ovyo ovyo na kubuma kila leo, lakini ccm wanakuona wewe ni kichwa babu kubwa. Kwa nini imekuchukua muda mrefu kuzijibu hizi tuhuma? Kwa nini haukutoa ufafanuzi mpaka ben alipoitwa polisi?

In short, wewe ni janga la taifa.

Tiba

....rip ccm
 
Mkuu, kuusu kuzurika ilo siliofii sana, na sina hofu juu ya hawa mafedhuli kwani nilisharipoti polisi juu ya usalama wa maisha yangu na kadi yao nilishawarudishia na wanajua mimi ni adui yao na kwaatakayetaka kunifuatilia zaidi asisumbuke kunitafuta kwani mimi ni Mgonbea udiwani mwaka 2010 Arusha kata ya Elerai kwa tiketi ya ccm nilieshindwa katika uchaguzi huo na Bayo aliekuwa mgombea udiwani kwa tiketi ya Chadema Ambae baadae chama kiliwafukuza uanachama na wakapoteza udiwani wao yeye na wenzakae watatu.

Siogopi na wakinizuru najua watakuwa wamezidi kujipalia makaa, kwani hili swala Mbunge wangu G.Lema analijua na nguvu ya uma ipo na itafanya kazi.

Aisee huyu jamaa ana habari nzuri kwa maslahi ya taifa, jumlisha na yule aliyepelekwa na Lema bungeni..
Tafadhari, toeni taarifa hapa au kwingineko kwa maslahi mapana ya taifa.. weka habari hapa ili kesho kila mtanzania aisome magazetini..
 
Back
Top Bottom