Mwingine Auawa; Jeshi la Polisi Fanyeni Uchunguzi na Mtupe Taarifa.

Mwingine Auawa; Jeshi la Polisi Fanyeni Uchunguzi na Mtupe Taarifa.

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
14,747
Reaction score
24,250
20240920_150152.jpg

Pichani ni kijana aitwaye Aziz Alumini Njombi wa huko wilaya Nanyumbu.

Huyu kijana hajihusishi na siasa wala mambo ya uanaharakati na kazi yake ni afisa usafirishaji a.k.a bodaboda.

Mnamo tarehe ya jana yaani 19/9/2024 alitekwa na mtu aliyembeba kama abilia ila inasemekana hakuwa abilia bali mtekaji.

Baadaye usiku wa kuamkia leo watekaji walipiga simu kwa mke wake wakitaka password ya simu ya mumewe.

Ila baadaye hao watekaji walimuua na leo maiti yake imeokotwa.

NB. Jeshi la polisi nchini, kutokana na kadhia hii ya utekaji raia ovyo hata vibaka, majambazi, wezi na kila muarifu wanatumia mbinu ya kuteja na kuua.

Kwa sababu inaonekana tayari ni njia iliyohararishwa wkt si kweli, ikiwa nyie ndiyo wenye jukumu la kuwalinda raia kisheria basi tunaomba ulinzi.

Vinginevyo mruhusu sasa raia wajilinde katika hali yoyote.


CC. Nawasilisha.
 
Simfahamu, Ila nadharia tu bodaboda hawezi kuwa na pesa za kufanya atekwe., Lakini password ya simu haifanyi uweze ku-access miamala. Pia nimesema kama walihitaji sana hayo wangeondoka na pikipiki
Ishia hapo kwenye..."nadhania"...!Itakusaidia.
 
Usafiri wa bodaboda na bajaj upigwe marufuku turudie usafiri wa baiskeli, teksi, hiace na daladala.

Nchi za kusini mwa Afrika wameweza kujizuia kufanya pikipiki au bajaj (vespa) kuwa chombo cha usafiri wa umma na maisha yanaendelea, kwanini Tanzania tunashindwa kuwa kama nchi za Kusini mwa Afrika.
 
“Polisi ni jamii na jamii ni polisi.” tushirikiane na vyombo vya ulinzi na usalama kutoa taarifa na tushirikiane kufichua uovu unaoendelea.
Tutabaki tunailaumu polisi kila siku kwani wao ni wapiga ramli kua fulani leo atauwawa?
Kama n hapana bhasi sisi ndio wenye taarifa na hawa watenda maovu ni wana jamii wenzetu
Inayoharibika ni Tanzania
 
Back
Top Bottom