Mwisho wa Tanzania Pride: JWTZ wadhalilishwa kusubirishwa mpakani huko Rwanda

Mwisho wa Tanzania Pride: JWTZ wadhalilishwa kusubirishwa mpakani huko Rwanda

Kweli nimeuzwa na video ya Kanali wetu wa JWTz huko DRC akisachiwa na kujisalimisha kwenye Polisi wa Rwanda. kikosi kilichopelekwa kupambana na M23 wote wanapaswa kuvuliwa vyeo wawe private
Yule sio kanali ni Captain ( nyota 3 kama sikosei).

All in All inasikitisha sana
 
Mama Samia kadhalilisha jeshi letu kwa kukoswa msimamo.Kwaachia Rwanda na Uganda kujidai Congo,,kweli Jeshi letu limedhslilishwa.Yaani na vifaa vyetu wamenyanganywa na M23 na sasa wanavitumia kupambana na Serikali ya Thsishekedi

Rwanda na Uganda ni ndugu zetu kuliko Kongo .

Tanzania Kupambana na Rwanda na Uganda ni upunguani .

Ndani ya Jeshi na wanasiasa wanyarwanda wamejaa ndani ya vyombo vya dola na serikali .Sasa tutapambana vipi na ndugu zetu . Wahaya kibao wanaasili ya Uganda na Kinyarwanda na wapo ndani ya mifumo ya serikali .

Kifupi Vurugu za Kongo zitaisha endapo Fisadi Tshesekedi atatolewa madarakani na kufikishwa mahakamani kwa ufisadi na kuchochea mauaji ya kikabila ya wananchi wasio na hatia .
 
Rwanda na Uganda ni ndugu zetu kuliko Kongo .

Tanzania Kupambana na Rwanda na Uganda ni upunguani .

Ndani ya Jeshi na wanasiasa wanyarwanda wamejaa ndani ya vyombo vya dola na serikali .Sasa tutapambana vipi na ndugu zetu . Wahaya kibao wanaasili ya Uganda na Kinyarwanda na wapo ndani ya mifumo ya serikali .

Kifupi Vurugu za Kongo zitaisha endapo Fisadi Tshesekedi atatolewa madarakani na kufikishwa mahakamani kwa ufisadi na kuchochea mauaji ya kikabila ya wananchi wasio na hatia .
Ndugu zako ndo wanateka na kuua wanajeshi wako?
 
Mki tukuta ata na leso ya baka baka mna tuogesha matope leo mnapigwa Search na polisi teh teh 😅😅kagame ana lipiza kwa dharau kubwa sanaaa
Tatizo safari hii Kagame ameshindwa kidiplomasia hana chake ndio maana anafanya propaganda hizo hana lake anajivimbisha ila debe tupu huyo Kagame wenu.
 
Yule sio kanali ni Captain ( nyota 3 kama sikosei).

All in All inasikitisha sana
Wametudhalilisha Sana kwa kweli.

Lakini sisi Wananchi tulikuwa tunashauri Sana humu mtandaoni kwamba Wanajeshi wa nchi yetu warudi nyumbani ili waje kuimarisha ulinzi kwenye mipaka ya nchi yetu, Watawala wamekuwa wakaidi juu ya suala hili.
Matokeo yake sasa ndio haya tunayoyaona hivi Sasa.
 
Kweli nimeuzwa na video ya Kanali wetu wa JWTz huko DRC akisachiwa na kujisalimisha kwenye Polisi wa Rwanda. kikosi kilichopelekwa kupambana na M23 wote wanapaswa kuvuliwa vyeo wawe private
Yani unashauri wapewe adhabu? Duh! Hivi ungekuwa ni wewe huyo kanali wa JWTZ ungefanyaje? Mkuu; Kwenye vita , ukushawekwa chini ya Ulinzi (au Ukishatekwa)au ukijisalimisha hauna budi kutii masharti bila shuruti.Tofauti na hapo unalambwa kichwa. Halafu inafaa ujue kwamba hakuna kikosi cha JWTZ kilichopelekwa kupambana na M23 bali kikosi cha JWTZ kilichopelekwa huko DRC kilienda kujiunga na vikosi vingine vya SADC kulinda amani DRC kwa hiyo sio kupambana na M23. Kama walinzi wa Amani walishindwa jukumu hilo hadi baadhi yao wakauawa, wakatekwa au kujeruhiwa hiyo ni issue nyingine. Ndo mana wakaondolewa (kupitia Rwanda) ili wapishe au watoe nafasi mtanange uendelee "bila kuwekewa kiwingu na SADC" baina ya hao M23+Allies na majeshi ya DRC + Burundi.
 
SAHVI TUNA JESHI LA WANASIASA NA CYO YA WANANCHI.JESHI LA WANANCHI LIMESHAFARIKI KITAMBO.MAZISHI IMEFANYIKIA KWENYE VIWANJA VYA SIASA IBADA ILIONGOZWA NA PASTERI WA CCM
Hakuna nchi itapeleka jeshi lake imara na kuhatarisha maisha ya vikosi vyake imara kisa tu vimaneno vya pride za wananchi zimetikiswa nchi nyingi huangazia maslahi mapana ya muda mrefu na hisia za mpito ndani ya dk 3 hadi 4 zimepita wala haviwashughulishi.
 
Wametudhalilisha Sana kwa kweli.

Lakini sisi Wananchi tulikuwa tunashauri Sana humu mtandaoni kwamba Wanajeshi wa nchi yetu warudi nyumbani ili waje kuimarisha ulinzi kwenye mipaka ya nchi yetu, Watawala wamekuwa wakaidi juu ya suala hili.
Matokeo yake sasa ndio haya tunayoyaona hivi Sasa.
Video iko wapi
 
Video mjongeo inayotrend Tiktok na X ikionyesha jinsi wanajeshi wa Tanzania walivyokuwa wakikaguliwa kwenye mpaka wa Rwanda na Congo wakati wakurudi Tanzania wakitokea kwenye misheni ya kulinda amani Goma.

Video hii inaendelea kusambaa kwa kasi mitandaoni huku M23 wakiitumia katika propaganda, hapo chini ni baadhi ya komenti za Raia wa Warwanda baada ya video hiyo kusambaa mitandaoni .


View: https://x.com/MAbdallaziz/status/1896163224720150659?t=KA_WkcfDRFXYeznPESOPMQ&s=19
 

Attachments

  • Screenshot_20250302_204237_X.jpg
    Screenshot_20250302_204237_X.jpg
    249.5 KB · Views: 1
  • Screenshot_20250302_204200_X.jpg
    Screenshot_20250302_204200_X.jpg
    249.3 KB · Views: 1
Tatizo safari hii Kagame ameshindwa kidiplomasia hana chake ndio maana anafanya propaganda hizo hana lake anajivimbisha ila debe tupu huyo Kagame wenu.

uko uchi sana tu haujui tu, kuna msemo mfalme/malkia akikaa uchi (labda) bila ya kujua utamwambia ajifunike au utamwacha?
 
Wangewezaje kukwepa kutumia mpaka wa Rwanda wakati hao Wanajeshi walikuwa MATEKA wa M23?

Hivi mfungwa anaweza kujichagulia gereza??
Wamejipeleka kutekwa.

JWTZ walikua na nafasi ya kuwa na plan nzuri kama escape plan badala ya kujisalimisha kwa M23 kama njia ya kurudi Tanzania.


JWTZ Wajitathmini
 
uko uchi sana tu haujui tu, kuna msemo mfalme/malkia akikaa uchi (labda) bila ya kujua utamwambia ajifunike au utamwacha?
Hivyo vimaneno tu vya kitaaa havitukoseshi usingizi kwamba tuanze kukimbizana na kichaaa si tunaonekana wote vichaa .
 
Ukienda mission kama hizo ambazo zinakuwa chini ya mwamvuli wa shirika au jumuiya fulani unabii utii masharti fulani ya kidiplomasia kuepusha migogoro zaidi ya kivita.

Hao walienda kama walinda amani Congo na sio kupigana vita na Rwanda, japo Rwanda kaonyesha chokochoko kutokana na maslahi anayoyapata kutokana na mgogoro wa DRC hivyo hao TPDF hawahusiki ndio maana wamepitia Rwanda na kukaguliwa kama exit point ila kama ingekuwa ni kinyume na hapo na wangekuwa ndani ya Rwanda wanapigana hapo hilo zoezi lisingewezekana bali sasa Rwanda angekuwa anashikilia askari wa TPDF kama mateka wa kivita.
Hakuna cha kulinda amani.
 
Kama unakubaliana na huyo jamaa kwamba suala linalojadiliwa ni matokeo ya Jeshi kuwa kibaraka wa ccm basi wote ninyi ni wapumbavu. Hata rais angekuwa kutoka CDM bado Jeshi lingekuwepo Congo. Huko ccm kuna nani anayefahamu kinachoendelea Congo zaidi ya Jeshi linavyofahamu?
Jeshi la CCM ukweli ndio huo na utabaki hivyo.
 
Back
Top Bottom