Mwl Mwakasege: Niliwahi kutoka nje ya mwili wangu nikaenda Mbinguni na kukutana na Nabii mkubwa, nikamtambua

Mwl Mwakasege: Niliwahi kutoka nje ya mwili wangu nikaenda Mbinguni na kukutana na Nabii mkubwa, nikamtambua

Still more this is a free forum for whoever wants to participate na hizo "siri za Mungu" ndiyo ujinga gani? Mungu anaogopa kitu gani kuweka mambo yake bayana mpaka yawe siri, huu ubishani wa kipuuzi usingekuwepo japo hata achomoze kichwa kutoka kwenye mawingu atusemeshe kuondoa utata ili shetani awe ameishindwa jumla? Kwani akijificha na wengi kwa kutokumuamini wakaenda jahanam(motoni🥺🥺) anapata faida gani?
Hiyo common sense haitumiki kuzijua Siri za Mbinguni.

Kwa hiyo huwezi elewa chochote, Ujinga wako utabakia.

Unahitaji funguo iitwayo Imani kuzijua Siri za Mbinguni na uongozwe na Roho mtakatifu.
 
Salaam, Shalom!!

Akifundisha katika semina jijini Mbeya Jana tarehe 26 January,Mwalimu Christopher Mwakasege amerudia kauli aliyowahi kuitoa kabla.

Amesema, asubuhi, walipokuwa katika bible study ya familia asubuhi ya jumapili hiyo, Mkewe alimuuliza swali kuwa ikitokea ametokewa na YESU atamtambuaje?

Mwalimu Christopher Mwakasege akamjibu Kwa kumkumbusha juu ya siku aliyotoka ndani ya MWILI wake na kwenda Mbinguni, alipofika Mbinguni, alikutana na Nabii Musa yule Nabii wa kale, na alimtambua, akaongeza kusema, Ukiwa katika mwili wa kiroho, huhitaji kutambulishwa sababu Roho inajua yote na kutambua yote yajayo na yaliyokwisha pita.

..... Mwisho wa kunukuu....

Naungana na Mwalimu Christopher Mwakasege juu ya UKWELI wa jambo hili, mbingu IPO na ni halisi, Mimi pia nimewahi kwenda Nchi nzuri sana, mfano wa uzuri wa Nchi Ile hauelezeki, mji huo hakuna jua Wala mwezi, IPO Nuru nzuri sana ambayo macho hayachoki kuitazama,

Nimewahi kuandika pia juu kupewa taarifa juu ya ujio wa Yesu kulinyakua Kanisa Kwa kumwona Yesu akiwa na jeshi la Malaika, amepanda farasi mweupe wakienda Kwa Kasi mawinguni.

Ndipo tujue yafuatayo.

1. Mbingu ni halisi Si hadithi.

2. WATAKATIFU wote wapo Mbinguni, wakifa hawakai kaburini.

3. Mungu yupo na ni MMOJA, na Jina la Mungu huyo mmoja tulilopewa WANADAMU liwezalo kuokoa ni Yesu Kristo/YESHUA HAMASHIACH.

Mungu awabariki.
Huwa najiuliza sisi wengine huwa tunasali vipi mbona hatupati maono. Kuna mwingine utamsikia akisema jana M-ngu alinena na mimi.

Hata gozbert juzi alisema M-ngu alinena naye mpaka wakabishana.
Unawezaje kutofautisha fikra zako za kawaida na sauti ya M-ngu kichwani?
 
Hapana. , Musa alikufa na roho yake iko hapo ikingojea ufufuo au ikingojea siku ya ufufuo.

Mbinguni yupo Bwana Yesu kwenye Bustani kubwa akingojea siku ambayo hata yeye haijui, Mungu Baba atakapomtuma kuja duniani kwa mara ya pili na kuondoka na Musa na Sie Watakatifu wengine.

Upande wa pili Yupo Mungu mwenyewe, mji ambao nguzo zake ni dhahabu hakuna giza, hakuna mchana wala usiku.

Tunaomwamini Mungu hivi vitu tunaoneshwa tukiwa na mwili huu huu.

Mpe Salaam zangu Mwalimu Mwakasege.
Mnaonyeshwa gamboshi nyie....nako waendaji wanasema pako kama ulivyoelezea hapo mbinguni palivyo
 
Huwa najiuliza sisi wengine huwa tunasali vipi mbona hatupati maono. Kuna mwingine utamsikia akisema jana M-ngu alinena na mimi.

Hata gozbert juzi alisema M-ngu alinena naye mpaka wakabishana.
Unawezaje kutofautisha fikra zako za kawaida na sauti ya M-ngu kichwani?
Nyie wengine subirini tu mkawe mabikira 72 upande wapili
 
Mkuu Rabbon , Mbinguni ulivyopaona , ni kweli panafanana kama hii picha ilivyo ?
 

Attachments

  • Screenshot_20250113-221833~2 (5).png
    Screenshot_20250113-221833~2 (5).png
    1.2 MB · Views: 1
Heri wewe mwenye kuandika haya hakika unyakuo ni wakati wowote endelea kuwa safi maana kufumba na kufumbua unyakuo utatokea na watakaobaki duniani ile miaka 7 ya dhiki kuu itaanza rasmi na wapo watakaokuwa wanarudia kusoma tunayonadika hapa mara kwa mara na wataanza kuuliza Rabbon upo wapi, Salari upo wapi na wengine wengi watatajwa lakini watashangaa mbona IDs hizi zimekuwa kimya ndipo watakumbuka tuliyokuwa tunaandika mara kwa mara kilio na kusaga meno kutakuwa kwingi sana.

Ana heri yeye amuaminiye bwana Yesu sasa na kuishi maisha matakatifu kujianda na unyakuo.
Maran-atha.
 
Wanopinga hawajasima maandiko vizuri, hata mtume Paulo alichachuliwaga mbinguni kabla hajafa, kwa hiyo Mtumishi wa Mungu kuchukuliwa kiroho hadi mbinguni sio jambo geni.
 
Salaam, Shalom!!

Akifundisha katika semina jijini Mbeya Jana tarehe 26 January,Mwalimu Christopher Mwakasege amerudia kauli aliyowahi kuitoa kabla.

Amesema, asubuhi, walipokuwa katika bible study ya familia asubuhi ya jumapili hiyo, Mkewe alimuuliza swali kuwa ikitokea ametokewa na YESU atamtambuaje?

Mwalimu Christopher Mwakasege akamjibu Kwa kumkumbusha juu ya siku aliyotoka ndani ya MWILI wake na kwenda Mbinguni, alipofika Mbinguni, alikutana na Nabii Musa yule Nabii wa kale, na alimtambua, akaongeza kusema, Ukiwa katika mwili wa kiroho, huhitaji kutambulishwa sababu Roho inajua yote na kutambua yote yajayo na yaliyokwisha pita.

..... Mwisho wa kunukuu....

Naungana na Mwalimu Christopher Mwakasege juu ya UKWELI wa jambo hili, mbingu IPO na ni halisi, Mimi pia nimewahi kwenda Nchi nzuri sana, mfano wa uzuri wa Nchi Ile hauelezeki, mji huo hakuna jua Wala mwezi, IPO Nuru nzuri sana ambayo macho hayachoki kuitazama,

Nimewahi kuandika pia juu kupewa taarifa juu ya ujio wa Yesu kulinyakua Kanisa Kwa kumwona Yesu akiwa na jeshi la Malaika, amepanda farasi mweupe wakienda Kwa Kasi mawinguni.

Ndipo tujue yafuatayo.

1. Mbingu ni halisi Si hadithi.

2. WATAKATIFU wote wapo Mbinguni, wakifa hawakai kaburini.

3. Mungu yupo na ni MMOJA, na Jina la Mungu huyo mmoja tulilopewa WANADAMU liwezalo kuokoa ni Yesu Kristo/YESHUA HAMASHIACH.

Mungu awabariki.
Bangi mbaya sana
 
Back
Top Bottom