Mzazi alomfikisha Mahakaman Mwl Madrasa Kwa kosa la kuchapa watoto, akemewe popote pale anapoonekana na ikiwezekana Jamii imchukulie hatua

Nani kakwambia madrasa wanafundisha masuala ya waarabu

Uislamu ni dini ya waarabu hata Quran imethibitisha hilo kwenye aya ya 2 ya Surat Yusufu. Inasema hivi

" Hakika Sisi tumemteremshia Mtume wetu haya maneno kwa lugha yenu ya Kiarabu yasomwe na yahifadhiwe, ili muyafahamu.

Pia aya ya 7 ya Surah Ash_shuraa inasema hivi
﴿وَكَذَٰلِكَ أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ قُرْآنًا عَرَبِيًّا لِّتُنذِرَ أُمَّ الْقُرَىٰ وَمَنْ حَوْلَهَا وَتُنذِرَ يَوْمَ الْجَمْعِ لَا رَيْبَ فِيهِ ۚ فَرِيقٌ فِي الْجَنَّةِ وَفَرِيقٌ فِي السَّعِيرِ
[ الشورى: 7]

Na namna hivi tumekufunulia Qur'ani kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Mama wa Miji na walio pembezoni mwake. Na uhadharishe na Siku ya Mkutano, haina shaka hiyo. Kundi moja litakuwa Peponi, na kundi jengine Motoni.​

 
Sir Jeff yule anayelia lia X ndio huyo?
 
Uislamu ni dini ya waarabu hata Quran imethibitisha hilo kwenye Surat Yusufu

" Hakika Sisi tumemteremshia Mtume wetu haya maneno kwa lugha yenu ya Kiarabu yasomwe na yahifadhiwe, ili muyafahamu.
Pamesemwa imeteremshwa kwa lugha ya kiarabu.
Wapi wamesema ni dini ya waarabu
 
Pamesemwa imeteremshwa kwa lugha ya kiarabu.
Wapi wamesema ni dini ya waarabu

Neno lugha yenu linaamisha nini?

Nakuongeza aya ya sura nyingine


ayat 7 from Surah Ash_shuraa
﴿وَكَذَٰلِكَ أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ قُرْآنًا عَرَبِيًّا لِّتُنذِرَ أُمَّ الْقُرَىٰ وَمَنْ حَوْلَهَا وَتُنذِرَ يَوْمَ الْجَمْعِ لَا رَيْبَ فِيهِ ۚ فَرِيقٌ فِي الْجَنَّةِ وَفَرِيقٌ فِي السَّعِيرِ
[ الشورى: 7]

Na namna hivi tumekufunulia Qur'ani kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Mama wa Miji na walio pembezoni mwake. Na uhadharishe na Siku ya Mkutano, haina shaka hiyo. Kundi moja litakuwa Peponi, na kundi jengine Motoni.​

 
Wapi wamesema lugha yenu
 
aya ya 2 ya Surat Yusufu. Inasema hivi

" Hakika Sisi tumemteremshia Mtume wetu haya maneno kwa lugha yenu ya Kiarabu yasomwe na yahifadhiwe, ili muyafahamu
Nani kakufundisha kiarabu au hiyo tafsiri umeitoa wapi
"Qur'anan arabiyya" maana yake ni "ya lugha ya kiarabu" Na si kwa lugha yenu ya kiarabu
 
Ila maostaaadh wanatoa vichapo heavy heavy punda mwenyewe haingii, siku moja nilikua kwenye vibarua vyangu huko Tanga kuna sehemu inaitwa Mwahako,

Majira ya jioni hivi nikawa napita karibu na msikiti aiseee, ostaadh alimwaga bakora kama njugu ni shwaaaaah shwaàaaaaah vitako vya madogo vinatoa miliooo pwaaah pwaaah pwaaaah aisee maostaadh kwa bakora
 
Kwani akimpeleka kuchapwa? Mfundishe mtoto. Mambo yamebadilika sana
 
Nani kakufundisha kiarabu au hiyo tafsiri umeitoa wapi
"Qur'anan arabiyya" maana yake ni "ya lugha ya kiarabu" Na si kwa lugha yenu ya kiarabu
Hii tafsiri ipo kwenye Quran zote zilizotafsiriwa kiswahili.. kama unabisha leta screen shot ya hii aya kutoka kwenye quran yoyote ya kiswahili tuone kama hakuna neno lugha yenu ya kiarabu

 
Huyo Mzazi kakosa akili unawaza nini hadi umpeleke mwanao Madrsa !.
Dunia ya leo ni sayansi na technology unawezaje kumpotezea mwanao muda wa kwenda kusoma masuala ya waarabu.
Sayansi na teknologia bila kumjua Mungu haitakusaidia chichote. Mnaona jamii za hao waliopiga hatua kimaendeleo zinavyoporomoka kimaadili. Ndo mtaletewa ushoga mtasema "tumepokea"
 
H
Mtaani kwetu wengi ni waislamu
Watoto wanatoka shule saa 11 au 12 wanakula wanaenda madrasa kurudi saa 4 usiku. Kesho tena wanaamka saa 11 ili saa 12 wawe shule.
Hilo linafanyika na ni kawaida kwenye shule za bweni watoto kurudi darasani baada ya mlo wa jioni mpaka saa 4 ucku. Mbona hujalipigia kelele? Kwa vile ni secular? Tatizo la wao kurudi shule mda huo linasababishwa a mfumo wa upande wa pili ulioingizwa mashuleni ili watoto wa kiislamu wasipate kuhudhuria masomo ya kiimani! Ni mpango wenu huo. Kawaida muda rasmi ulioruhusiwa kutoa wanafunzi kurudi nyumbani na wizara ni saa nane na nusu. Nani aliyeongeza muda? Ni upande wa pili hasa shule za mrengo huo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…